Mkuu JGG, kwanza naomba nikupongeze kwa kukubali kuwa mkweli, watu wakweli humu jf, wanaokubali ukweli halisi jinsi ulivyo ni wachache, na wewe uu mmoja wao!. Wengi wa member humu, wanaukubali ule ukweli wao tuu, sometimes sio ukweli halisi!.
Naimba kukurekebisha na kukusaidia kidogo ila pia kukuongezea kidogo na ukweli mchungu!.
- Sio kweli kuwa CCM, inahihitaji mbadala!, CCM inatamani kutawala milele, kama hapatokea mbadala, CCM itaendelea kutawala, na kutawala na kutawala!, kwa wale waliotangulia mbele ya haki, na wale watakaotangulia mpaka 2015, kwao CCM imetawala milele yao yote mpaka mwisho wa maisha yao!, na kwa 2015 itaendelea kutawala milele ya wengine wengi!.
- Ili CCM iondoke, lazima kwanza apatikane mbadala na sio lazima Chadema!, ila mpaka hapa tulipofikia, Chadema ndicho chama pekee kimeonyesha dalili ya angalau angalau, lakini tatizo lao ndiolo hilo hili nililowaambia "Hawajajipanga!' japo walikuja juu, facts are facts hazina mjadala, ni ama wajipange, ama 2015 ni CCM tena!.
- Hili za ZZK kuonewa Chadema naomba let me reserve my comments, si umeona juzi baada ya yule "chalii wa kijiweni" kututapikia humu ule utumbo,humu sebuleni, kale "ka kinda ka juzi" nacho kakasupport kuongeza matapishi!, na uha.. kujazia!, una sasa sebule nzima imechafuka!, jee umeona mpaka leo wenye nyumba wamefanya nini?, nilitegemea wakekuja mbia kusafisha matapishi yale!, lakini kila siku wanapita tuu hapo sebuleni kwa kutafuta pa kukanyaga ili wasijichafue na matapishi hayo lakini sio kutasafisha!. Kama matapishi yale yangekuwa ni wa "wapendwa wao" hata kabla wenye nyumba hawajafika, ungeshuhudia "madekio yao humu" jinsi wanakimbizana kugombea kusafisha uchavu ule, na wengine ambao hawana mop, wangekuwa tayari hata kuyafuta kwa ulimi, na hata kama hakuna mahali karibu pa kutupa, wangeamua hata kuyameza matapishi hayo kuliko sebule kuchafuka!. (Hapa ndio nime reserve my comments!, ningeamua kusema!, patakuwa hapatoshi hapa!).
Pasco.