hata vitabu vitakatifu vinatoa onyo ama amri kwa waja wa mwenyezi mungu kwamba usitamani mali ya jirani yako.
Hivi karibuni kumetokea wanaccm kuzungumza sana ama kwa maneno mengine wanachonga sana juu chadema.
Tabia hii ya ccm ni sawa kabisa na usemi ule wa kawaida usemao nyani haoni ku...e kwa sababu tukizungumzia ccm kama nyumba ndio inayovuja kutokana au na uchakavu wa bati au vigae na kwamba kuta sasa zimeanza kulowa maji ya mvua na karibia zitadondoka moja baada ya nyingine.
Hebu tujikumbushe baadhi ya kutu zilizo tafuna paa ya ccm.
Mosi je,kwa nini hawa maccm hawazungumzi habari ya ufisadi wa serhkali?
Pili je,kwa nini ccm hawazungumzi lote juu za ujangiri?
Tatu,kwanini hawazungumzii rushwa iliyokutu sugu kwenye bati la nyumba ccm?
Nne je,kwa nini hawaccm hawazungumzii juu ya madawa ya kulivya yaliyokutu kali kwa bati la nyumba ccm?
Tano je,kwa nini hawa ccm hayazungumzii juu ya usaliti wa wanachama wao kama nape na sita waliotaka kuanzisha ccj?
Sita je,kwa nini ccm hawazungumzii wanachama wao wanao pigiana debe la urais kinyume na katiba ya ccm?hapa angalau john komba atakuwa shahidi.
Saba je,kwa nini ccm yana ufyata kuongelea dukuduku juu ya chama chao na kumalizia dukuduku zao kwa chadema?chadema kimewafanye nyie ccm?
Nane, je kwa nini hawa ccm hayazungumzii ju ya upatikanaji wa katiba bora nchini?
Tisa, jekwa hawa ccm hawazungumzii juu ya uchina kukabidhiwa nchi hii kwa mgongo wa urafiki wa kihistori na kwa mafuta ya mkoloni mamboleo?
Kumi,je kwa nini ccm hawazungumzii juu ya mafisadi kupewa madaraka mapya?turejee kamati ya bunge ya bajeti.
Ccm acheni kutumia muda vibaya kwa kuiota chadema,chama ambacho hakipo madarakani kinawatoa roho? Kwa nini hamzungumzi vyama vingine vya siasa zaidi ya chadema?mmekomaa na chadema tu?
Hii ni fedheha kwenu kwa maana chadema mumekipatia promo vya kutosha,mnatumia kumchonganisha mwigamba na zito eti ni mamluki,mbinu hizi mlizitumia miaka ile,kamwe hazitafua dafu kwa chama mithiri ya mti wa mpingo"chadema".
Mwigamba na zito ni makamanda wa chadema,yaliyotekea kwenye nyumba yetu ya chadema ni tobo kwenye bati,hivo tunatoa bati lilitoboka na kuweka jipya na katu hatuwezi kusubiri kuu kumea kwenye paa la nyumba yetu chadema.yote haya yata imarisha chadema kwa kuwa ni chama cha wajanja.
Kelele za mbwa hazimnyimi mwenye nyumba kulala usingizi,na nyegere haachi kelele hata akishiba.