Kidono/Kinkuti ni kitu gani?

Kidono/Kinkuti ni kitu gani?

Binafsi nahisi nilichanjiwa vitu flani kwenye mikono yangu nilipokuwa mdogo enzi naishi na marehemu babu yangu huko mbinga-nyasa(sasa hivi wilaya ya Nyasa).

maana Nina nguvu zisizo za kawaida hususani mikononi.

hata wafanyakazi wenzangu ninapo peana nao mikono,huwa wananiambia mikono yangu inanguvu sana.

lingine ni kwamba nilipofikisha umri wa utuuzima,familia yangu ilinitahalisha sana kutopigana na mtu yoyote.waliniambia sipaswi kumpiga mtu yoyote hata Kofi.

mara ya mwisho kumpiga mtu ilikuwa wakati nikiwa o-level jitegemee sec miaka kadhaa iliyopita.

alikuwa ni konda wa daladala za kutoka ukonga kwenda kkoo.baada ya mabishano ya hapa na pale na purukushani,nilimpiga ngumi moja nzito eneo la mbavuni.

kwa kilichomtokea konda yule,niliapa kutompiga tena mtu maisha yangu yote.taarifa zilipoifikia familia yangu,nililaumiwa sana.nikakumbushwa kuhusu onyo nililopewa la kutompiga mtu au kutopigana.

Mondray naomba usome maelezo yaliyomo ktk hii post yangu halafu nifafanulie vizuri kunikuhusu.
 
Hiii kitu inatofautiana na jamiii na jamiii katika majina.


Tanga hiyo kitu inaitwa MUKU.

Nimeishuhudia inavyo fanya kazi kwa mtu, na hatua za majaribio niliwahi kuiona. Ina masharti yake, nikipata muda naweza hadithia kidogo
Tanga kuna watu wa kigoma wengi waliopelekwa manamba (kukata mkonge) wakamua kuishi huko hao ndio waliopeleka hiyo taaluma
 
Yeah mkuuu.

Ila the worst ikifika time yako yakurudi vumbuni unapata shida sana.

Unakuta wengine wana fight kuto taka kufa, till wengine huteseka even wengine kuoza wakiwa wanapumua, hiz vitu vina mengi na miiiko mengi.

Kuna baadhi ya miiko au vitu hafanyiwi mtu ambaye hana mtoto,
Lazim huwe na wakiume na kike, ina depend na unatakaje
Ni kweli nimewahi shuhudia mzee mmoja hali hiyo ikimtokea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom