Kidono/Kinkuti ni kitu gani?

Kidono/Kinkuti ni kitu gani?

Unapafaham kibirizi. Gungu. Kichwere ndio wanaongoza kua na vitu hivyo.
IMG_20170129_180829.jpg
Kibirizi hapo mkuu
 
Mmhh ngoja nitakufanyia ww mwenyewe ngoja nikusanye vyombo hutachomoka

Weeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.....usijaribu ht kwa bahati mbaya.

Watu wa huko nasikia ni wabishi hatari.mimi mwenyewe ninakaubishi kwa mbaaaaali hii ni kwa sababu ya kimo sasa ukiningezea na wako wa asili kabisa tangu enzi na enzi si nitachomoka mizizi ya kichwa!!aku sitaki mimi
 
Kaka mi ninavyo vyote nisaidieni namna ya kuondokana navyo wakuu.

Sio siri hua unafikia wakati mie najiogopa aseee, hua nikifika ugenini najikuta nakua mnyonge, sijichanganyi mahala panapoweza kunipa changamoto, yamenifanywa nikaachishwa mafunzo ya jeshi nateseka sana

Heeee kumbe kuna side effects..uwiii mondray acha tu.nimegair
 
Mkuu mimi nimeshuhudia, kusimuliwa pia kufundishwa hizo mambo sometimes ni mbaya sanah hasa ukizidisha aina ya dawa. Kuna zingine hutakiwi kukaa sehem zenye watu ikiwa full moon maana wengine hubadurika na kua viumbe vya ajabu.

 
Kidono ni Dawa ambayo imetengenezwa kwa mchanganyiko wa vitu mbalimbali (sitavitaja hapa) . Inaweza kukukinga na kitu chenyekuweza kujeruhi eg. Upanga, kisu, rungu, fimbo, chupa n.k.
Kidono kimetofautiana kidogo. Kuna ambacho unachanjwa kwa wembe au Majani makali na Kidono cha kunywa na soda. Ukichanjwa kwa wembe ni wembe pekee utakao weza kukukata lkn ukichanjwa kwa kutumia jani huwezi kujeruhiwa na kitu.
Wanakuchanja ukiwa umekalia baadhi ya vitu vinavyoweza kjeruhi. Pia ukipata kilicho imara hata risasi haiingii mwilini.

KINKUTI.
Hii ni dawa inayoweza kukupatia nguvu za ziada katika kupambana. Ukichanja kinkuti unauwezo wa kuumka mwili wako na ukawa unauwezo wa kupiga hata wanajeshi 100. Hua hakituliziki kirahisi.

MASHARITI YAKE.
Ukiwa na kidono ukijikata au kujipiga na kitu utaumia. Pia ukimruhusu mtu akupige utaumia.
KINKUTI kinafanya kazi mpaka ukiwa na hasira za kuchokozwa ukichokza basi hakifanyi kazi.
Vyote hivyo vinapatikana Kigoma na Congo
"....ukiwa umekalia baadhi ya vitu vinavyoweza kukudhulu.."
Nimepata shida kuviwaza! Sijui chupa, kisu au bunduki,chui, nyoka!
 
Dah kipindi kile cha Ukoloni hii sayansi haikuwepo mbona tumenyanyasika kwa mababu zetu kufungwa minyororo kirahisi na kupelekwa utumwani!!?
Ilikuwepo lakini haikuonyesha mafanikio babu MAJI MAJI WAR wazee wetu walipotea sana kwa kuamini hizi mambo! Sasa kama mtu unaamini kidono kwanini usimwamini na Mungu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom