Kidono/Kinkuti ni kitu gani?

Kidono/Kinkuti ni kitu gani?

Binafsi nahisi nilichanjiwa vitu flani kwenye mikono yangu nilipokuwa mdogo enzi naishi na marehemu babu yangu huko mbinga-nyasa(sasa hivi wilaya ya Nyasa).

maana Nina nguvu zisizo za kawaida hususani mikononi.

hata wafanyakazi wenzangu ninapo peana nao mikono,huwa wananiambia mikono yangu inanguvu sana.

lingine ni kwamba nilipofikisha umri wa utuuzima,familia yangu ilinitahalisha sana kutopigana na mtu yoyote.waliniambia sipaswi kumpiga mtu yoyote hata Kofi.

mara ya mwisho kumpiga mtu ilikuwa wakati nikiwa o-level jitegemee sec miaka kadhaa iliyopita.

alikuwa ni konda wa daladala za kutoka ukonga kwenda kkoo.baada ya mabishano ya hapa na pale na purukushani,nilimpiga ngumi moja nzito eneo la mbavuni.

kwa kilichomtokea konda yule,niliapa kutompiga tena mtu maisha yangu yote.taarifa zilipoifikia familia yangu,nililaumiwa sana.nikakumbushwa kuhusu onyo nililopewa la kutompiga mtu au kutopigana.
Jitahidi kudhibiti hasira zako na usivunje miiko
 
huwa najitahidi sana mkuu.kuna uwezekano labda babu alinichanjia vitu vinavo jadiliwa na wadau hapa jamvini.

maana babu yangu alikuwa ni mtu mashuhuri aliyeheshimika na kuogopwa sana na jamii yake iliyomzunguka.
Kila kitu ni manuizi tu, ulozi na sanaaaa, ina mbinu na namna nyingi za ku manupulate dawa na tricks.

Inawezekana, maan kuna zingine mtu ukitengeenezewa una ruhusu ziende hata kwa uzao wako, bila hata kuwafanyia dawa
 
Kwani mtu akiwa huko alikofukiwa haendelei na kupumua, kula+++ n.k anakuwa mahututi au anaweza kufa 1 kwa 1 ai inakuaje ? na ni negative impacts zipi Ndg ?
Hawezi kufa. Unakua na mizimu tu.
Negative impact ni.
Kushindwa kujicontroo.
Waweza kuua au kujeruhi then ukafungwa.
Itakubidi sometimes ukae mbali na watu maana wengine ikifikia mwezi mpevu hua sio viumbe wa kawaida.
 
Hawezi kufa. Unakua na mizimu tu.
Negative impact ni.
Kushindwa kujicontroo.
Waweza kuua au kujeruhi then ukafungwa.
Itakubidi sometimes ukae mbali na watu maana wengine ikifikia mwezi mpevu hua sio viumbe wa kawaida.
Kwa hiyo ikifikia mwezi mpevu ndo ratiba ya hiyo kinga kwamba lazima isale au imuendeshe muhusika kufanya vurugu ?
 
Kwa hiyo ikifikia mwezi mpevu ndo ratiba ya hiyo kinga kwamba lazima isale au imuendeshe muhusika kufanya vurugu ?
Mkuu haimuendeshi mtu kufanya vurugu bali akikasirishwa ndio hua hatar.nadhani umeona picha ya hulk ilivyo. Hua hutakiwi kukaa sehem zenye vurugu hata kidogo au kua mkorofi.
MPAKA UKICHOKOZWA
 
Brother Mondray, ina maana mtu akiwa na hiyo kinga ya kiafrika, hata Risasi na mabomu vikitupwa 1 kwa 1 kwa mwenye kings higo, havimuathiri kabisaaaaa au inakuaje Ndg .... .... ...
 
Kidono ni Dawa ambayo imetengenezwa kwa mchanganyiko wa vitu mbalimbali (sitavitaja hapa) . Inaweza kukukinga na kitu chenyekuweza kujeruhi eg. Upanga, kisu, rungu, fimbo, chupa n.k.
Kidono kimetofautiana kidogo. Kuna ambacho unachanjwa kwa wembe au Majani makali na Kidono cha kunywa na soda. Ukichanjwa kwa wembe ni wembe pekee utakao weza kukukata lkn ukichanjwa kwa kutumia jani huwezi kujeruhiwa na kitu.
Wanakuchanja ukiwa umekalia baadhi ya vitu vinavyoweza kjeruhi. Pia ukipata kilicho imara hata risasi haiingii mwilini.

KINKUTI.
Hii ni dawa inayoweza kukupatia nguvu za ziada katika kupambana. Ukichanja kinkuti unauwezo wa kuumka mwili wako na ukawa unauwezo wa kupiga hata wanajeshi 100. Hua hakituliziki kirahisi.

MASHARITI YAKE.
Ukiwa na kidono ukijikata au kujipiga na kitu utaumia. Pia ukimruhusu mtu akupige utaumia.
KINKUTI kinafanya kazi mpaka ukiwa na hasira za kuchokozwa ukichokza basi hakifanyi kazi.
Vyote hivyo vinapatikana Kigoma na Congo
Duh hatari hiyo

Nitakuona mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom