Kibati hakilipi, mnajidanganya

Kibati hakilipi, mnajidanganya

Mnachukua hela zenu mnapeana kwa zamu mi siamini kabisa katika uwekezaji au biashara ya namna hii wa hela wanaofanya watu wengi haswa wanawake (kibati) naona kama kujidanganya vilee.

Kwanini usikae na hiyo hela mwenyewe labda kama ni miezi 3 ukawa umeizalisha zaidi? Ukanunua hiki ukauza hata ukikopesha inalipa kuliko kibati.

Acheni kujidanganya hakuna faida kwenye kibati.

Me naamini wewe kama ww huwezi kujiwekea 5000 kila cku badala yake cku ingine utajipigisha story tu bana ntaweka kesho then kesho ikipita umepitisha..ukiwa na wenzio kuna force ya kufanya lazma utoe na itakufanya ujinyime adi uitoe..mwisho wa cku utapata fungu lako ulilojigangaikia..

We ona ni ujinga wenzio Wanacheza kilo kila week wakiwa watu 30 ana milion 3 yake anafanya jambo la maana we io kilo unaenda inywea weekend..ndio maana mjini hatuishi kuangaliana njiani mkipigiwa honi tu mnavimba mashavu..
 
Linaloongelewa hapa ni kibati, sio upatu wala kikoba. Ninaamini wanaocheza kibati kimewapa faida au manufaa kama baadhi walivyoeleza na kama kuna anayeona havina manufaa, wote hawajatoa ushahidi, basi kila mtu ashikilie msimamo wake, kila mtu ana maisha yake na jinsi ya kuyaendesha.
 
Hiyo tsh.2000 uikusanye mpaka ifike tsh.150000 na shida hii unaweza kweli ,sidhani .
Ila kwa mtindo wa kumchangia mmoja mmoja,inakusanyika vema tu.
Mawazo tu.
Hii kitu haina faida. Hela kuzimudu kwanza lazima uwe na nidhamu ya hela. Lazima ujue kuweka hela. Lazima ujue kutumia hela vizuri.

20 to 80 rule. Asilimia 20 ya matumizi yetu huchukua asilimia 80 ya ujira ama vipato vyetu.

Ukishajua ni wapi unatumia pesa nyingi ktk mahitaji yako, kinachofuata ni kuona ni kwa namna gani unaweza weka control ya matumizi yako ktk hiyo nyanja kuhakikisha unapunguza matumizi ili ukuze ziada utakayo wekeza ktk Biashara ambayo itarudisha Faida.

Hili ndio somo gumu tunalolikimbia kila siku kwa kuendekeza vikoba, saccos, na hata Mabank.

Na wajanja wachache kama Mabenki yanatumia ujinga wetu kutupiga hela.

Hivi hujiulizi kwanini ni lazima ukatwe pesa kuchangia mfuko wa hifadhi ya Jamii? Unaambiwa ni Akiba ya Uzeeni? Hivi unaamini ni kwasababu unapenda sana na Serikali ndio maana ni lazima uchangie?

Akiba ni ya Muhimu sana. Maana ndio pesa ya kuwekeza.

[HASHTAG]#Stuka[/HASHTAG]
 
Ujinga ni pamoja na kuamini unachokijua tu!
Hoja iko hivi:

Mleta mada:
Kibati haina faida.

Wana Kibati:
Kibati inafaida, maana nanihii alijenga nyumba kutokana na kibati

Wana mada:
Hela alizojengea ni za kwake zilizokaa kwa mtu mda mredu bila kuzaa faida,

Wana kibati:
Inawezekana mnapinga kwa sababu mko chini ya umri wa kujua mambo.

Wana mada:
Hakuna umri wa kujua mambo ukampa mtu hela akuhifadhie miezi mitatu bila faida wakati ungezifanyia biashara zingekuwa za kwako na ungekuwa na faida iliyoongezeka.


Hapo mwenye point ni nani?

Good explanation..ingawa hata ww hujui jibu ni nini sababu hujawahi fanya ivyo..try upate jibu lililokua verified na research yako ww mwenyewe..watu wanazalisha biashara mpya kila siku sbb ya hii michezo..
 
Eneo nalofanya shughuli zangu tunafanya haya mambo,tunaita mchezo tupo watu 30 kila wiki tunatoa 50,000/= na kila wiki anatoka mtu na 1,500,000/=zake haijawahitokea siku tukakorofishana huwa tunamaliza na tunaanza tena siku zinasonga..usijidanganye kutengeneza sijui kibubu au kuweka chini ya godoro ndiyo kutakufanya ujiwekee akiba,never huo ni uwongo utaishia kuwa na akiba ya lak1 ndani hotokaa uione akiba yako ya maana.kwa mtu anaekamata hizi hela ndogo ndogo hii michezo wakati mwengine inamsaidia kuinua mtaji wengine hata kwenye ujenzi au ada za watoto inawasaidia sana,kukamata mill1.5 ndani ya miezi 5 sio jambo dogo hata kidogo japo utabaki unadaiwa ila kwa manufaa utakayoyapata akili itachangamka kutafuta pesa ya kulipa ili usitolewe ktk group.
 
Hii kitu haina faida. Hela kuzimudu kwanza lazima uwe na nidhamu ya hela. Lazima ujue kuweka hela. Lazima ujue kutumia hela vizuri.

20 to 80 rule. Asilimia 20 ya matumizi yetu huchukua asilimia 80 ya ujira ama vipato vyetu.

Ukishajua ni wapi unatumia pesa nyingi ktk mahitaji yako, kinachofuata ni kuona ni kwa namna gani unaweza weka control ya matumizi yako ktk hiyo nyanja kuhakikisha unapunguza matumizi ili ukuze ziada utakayo wekeza ktk Biashara ambayo itarudisha Faida.

Hili ndio somo gumu tunalolikimbia kila siku kwa kuendekeza vikoba, saccos, na hata Mabank.

Na wajanja wachache kama Mabenki yanatumia ujinga wetu kutupiga hela.

Hivi hujiulizi kwanini ni lazima ukatwe pesa kuchangia mfuko wa hifadhi ya Jamii? Unaambiwa ni Akiba ya Uzeeni? Hivi unaamini ni kwasababu unapenda sana na Serikali ndio maana ni lazima uchangie?

Akiba ni ya Muhimu sana. Maana ndio pesa ya kuwekeza.

[HASHTAG]#Stuka[/HASHTAG]

Na kweli hili ni somo gumu sana kulielewa..ndio maana unaambiwa mtanzania ukitaka kumficha material muwekee kwenye vitabu..mnashauriwa sana Msome vitabu ili muondoke na dhima kwamba faida ni lazima liwe ongezeko baada ya kutoa matumizi..
 
Hee hee hee kibat tEna c bora tu waje tusaidiane kubet
 
Good explanation..ingawa hata ww hujui jibu ni nini sababu hujawahi fanya ivyo..try upate jibu lililokua verified na research yako ww mwenyewe..watu wanazalisha biashara mpya kila siku sbb ya hii michezo..
〣( ºΔº )〣
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom