Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Status
Not open for further replies.
Jitahidi kuelezea Zitto atatufanyia nini kwenye haya mageuzi zaidi ya Mbowe siyo blaa blaa za goo goo hapana!! Kitila tueleze na wana JF wengi wa goo goo huyu je ataweza kwa lipi na amefanya lipi ndani ya chama???

Sina uhakika kama ni kazi ya Kitila kuanza kumwaga sera za Zitto kwa niaba yake hapa JF, Zitto ni member hapa kama umeshindwa kumuuliza huko nje, nafikiri unaweza kuelekeza hilo swali kwake hapa JF!

Mimi nilivyomwelewa Kitila ametoa maelezo hapa kulingana na makala ya Kibanda ilivyokuwa imetolewa, na si kwamba amekuja kupiga kampeni hapa vinginevyo basi kila aliyeangainst kibanda anampigia debe Zitto, sio?

hii ni hatari kutoka naibu katibu kuruka mpaka Uenyekiti!

What? nini cha ajabu hapa...kumbe hata uzoefu wa uongozi kny chama anao? Ina maana kwako wewe ungeshangaa sana kumuona mwanachama wa kawaida tu akigombea uenyekiti, sio?.....ulitaka atokee wapi, ili agombee huo wenyekiti ati?
 
Au ndio mbio za kugombea urais 2010?maana traditionally wenyeviti wa chama huwa candidates, hii haitanishangaza nakumbuka huko nyuma huyu jamaa alishasema ndoto zake ni kuwa rais.Kila la heri ila kama Mbowe kamind tutarajie mengi siku za usoni.
 
Cha Msingi ni Kampeni Safi ambazo hazitaacha Vidonda wala Visasi kwa Watakaoshindwa baada ya Uchaguzi. Wote Zitto na Mbowe naamini wana Dhamira Safi hata kama hazifanani! Hatuna Haja ya kuogopa kwamba Fulani aweza kuwa ametumwa ( After all hizi ni Hisia za Wapambe) coz kwa nyakati hizi ngumu sana kwa Mamluki kuambatana na wapiganaji wa Kweli. Chadema chagueni Viongozi then watakaopatikana kama ni Makuwadi watafahamika tu within very short time na hakutakuwa na msalie mtume.

For Now Demekrasia iache ichuke Mkondo wake
 
Au ndio mbio za kugombea urais 2010?maana traditionally wenyeviti wa chama huwa candidates, hii haitanishangaza nakumbuka huko nyuma huyu jamaa alishasema ndoto zake ni kuwa rais.Kila la heri ila kama Mbowe kamind tutarajie mengi siku za usoni.

Hapana Ndugu yangu, 2010 Zitti bado hatakuwa na Sifa za kugombea Urais may 2020
 
Au ndio mbio za kugombea urais 2010?maana traditionally wenyeviti wa chama huwa candidates, hii haitanishangaza nakumbuka huko nyuma huyu jamaa alishasema ndoto zake ni kuwa rais.Kila la heri ila kama Mbowe kamind tutarajie mengi siku za usoni.

Hapana Ndugu yangu, 2010 Zitto bado hatakuwa na Sifa za kugombea Urais may 2020
 
Kitila humu JF wengine hatuna upande sisi kwetu ni Maslahi ya Taifa kwanza. Kitila ulivyomjibu Kibanda ukweli ni kuwa na wewe tulivyokusoma umeegemea Upande wa Zitto au sijui ndo Kampeni sielewi.

Nadhani Kibanda amemchambua Vizuri Mh. Zitto na pia na Mbowe ingawa ya Mbowe hatuna haja nayo kwani amekuwa madarakini miaka mitano tunamjua. Jitahidi kuelezea Zitto atatufanyia nini kwenye haya mageuzi zaidi ya Mbowe siyo blaa blaa za goo goo hapana!! hii ni hatari kutoka naibu katibu kuruka mpaka Uenyekiti! Kitila tueleze na wana JF wengi wa goo goo huyu je ataweza kwa lipi na amefanya lipi ndani ya chama???

Kweli Safari bado ni Ndefu, ulitaka awe kwanza makamu mwenyekiti?
 
Ukiamua kuwa mwanachama wa chama cha siasa basi unapaswa kupita katika misingi inayokiongoza chama husika. Pengine ndugu yangu Omarlyas anataka Zitto awe Mwenyekiti wa chama cha wagombea binafsi ambao hawana itikadi, sera wala mwelekeo mmoja.

Ndiyo maana jana wakati akihojiwa na DW Zitto huyo huyo alifikia hatua ya kusema kwamba yeye anaamini katika ujamaa wakati Mbowe anaamini katika ubepari. Je haoni kwamba chama ambacho kingemfaa ni CCM ambacho hadi leo katika maandishi kinadai ni cha kijamaa japo hakiufuati? Hiki ni kichekesho.

Acha niendelee kulikoroga ilimradi tu nausema ukweli hata kama ukweli huo ni mchungu kiasi gani. Zitto ni rafiki yetu, sawa, ni ndugu yetu, sawa, ni kijana shupavu, sawa, lakini katika hili la uenyekiti wa Chadema, hajapevuka, si kwa sababu ya umri wake kama ilivyopotoshwa na baadhi ya wana JF, bali uchanga wake katika kuzingatia, kuheshimu na kuitekeleza kwa vitendo misingi ya uongozi bora ya ufanyaji kazi wa pamoja, kwa nia moja hata kama ni kwa njia tofauti.
Sasa naanza kukuelewa
 
Kibanda.
Leo uko kimya nasubiri list ya vijana wajinga wa Chadema.
swali la pili jee Gazeti la Tanzania Daima linaendeshwa kwa nguvu za uenyekiti? au ruzuku za chama ni sehemu ya mtaji wa Gazeti?
maneno mazito uliyompa Kitila Mkumbo yameniacha sina mbavu na wenye Chadema yenu.
Kazi yote wanayoifanya kina Kitila Mkumbo ya kuifagilia Chadema hapa JF bado wanaoneka ni Mamluki? kweli tunatakiwa tusiingie kwenye vyama hivi kichwa kichwa bila kufanya tafiti za kutosha.KITILA somo hilo umesoma?jee mtu kama Mkandara ataaminiwa na Chadema kama akijiunga.

Jana nililitaja kundi la 'Vijana Wajinga' kwa majina na wengine wamenijibu kwa sms na simu wakinitaka yaishe kwani wanadai eti tunaelekea kufichua siri nyingi zaidi.

Mbali ya kuwataja wawili kati yao wamejitokeza katika jamvi jana na leo na mmoja nikamjibu. Soma sawasawa kaka. NALIONA ANGUKO LA ZITTO linalokuja. Anguko hilo litakuja akishinda uenyekiti au la, akiwa Chadema au nje ya chama hicho. Tatizo si kama atashinda au la bali ni matokeo ya kuingia kiringeni kwa staili yake ya kuvizia akifunga goli toka nje ya uwanja. Subirini muone.

Tanzania Daima inajiendesha kwa faida kubwa. Haitegemei ruzuku au uenyekiti wa Mbowe. Hata hivyo nguvu ya kambi ya upinzani (demokrasia madhubuti) ni sehemu ya uimara wa Tanzania Daima na uhalali wangu wa kuendelea kuwapo hapa. Sina njaa, sina sababu hata moja ya kujikomba kwa yeyote zaidi ya kusimama katika kile ninachokiamini. Niko tayari kubakia peke yangu kwa kuwa na mtazamo ambao ni unpopular. Tumeona vitu popular nchi hii na vyote mwisho wake vimetuingia nyongo...Mrema...Mkapa (Baada ya kuwa Rais na kabla ya kumaliza muda wake)...Kikwete na sasa Zitto...Tusubiri tuone. Amkeni mashabiki
 
Nd. Kibanda nilishaandika tokea mwanzo kuwa huyu ni muandishi wa Kuogopa kwani ameanzia mbali tokea huko kwa Sitta anakuja kwa Zitto kazi yeye ni kuchafua tu watu . Pia ukijumlisha wajumbe wengi waliochangia humu JF wote wamemponda nadhani hilo ni fundisho arudi shule au abadilishe fani hii anavuruga kama sio kulikoroga.

Ukifuatilia JF Kibanda na Zitto wanatumiwa na RA kwani historia nzima tokea nyuma zinajieleza. (Mungu atatuhukumu kama ni hisia)

Sasa vita hii tulioyo nayo na ambayo tunapaswa kuipigania ni kwa huyu Muhindi RA. Tusiwatukane au kuwakebehi hawa waganga njaa Zitto/Kibanda, CCM - NEC na waandishi uchwara wengi, hapana! vita ya kuipigania na kujikomboa Tanzania ni dhidi ya RA full stop.
.

Duh. Huu mparanganyiko kweli. Zitto na Kibanda wote wanatumiwa na RA! History will judge u wrong and us right. Leo tumetofautiana na Zitto, huyo RA yuko wapi? Ameshindwa kututumia? Wewe margreth ndiye unayechafua watu.

Waganga njaa wengi huwaona wenzao nao ni waganga njaa. Yaani huyo mtu RA is super human anaweza kumtumia yeyote atakaye. Kwa nini sisi tushindwe kumtumia? Vita tunayopaswa kuipigana ni dhidi ya 'ufisadi dola' au 'ufisadi wa kitaasisi' (state corruption au institutional corruption) unaolitafuna taifa letu kwa namna ambayo haipo katika nchi nyingi duniani, ikijengwa katika mfumo wa CCM kuwa chama dola kilichohodhi mamlaka kwa staili ya vyama vya kikomunisti duniani.

Tatizo letu Watanzania wengi ni mabingwa wa kufikiri kwa ndimi zao
 
Jana nililitaja kundi la 'Vijana Wajinga' kwa majina na wengine wamenijibu kwa sms na simu wakinitaka yaishe kwani wanadai eti tunaelekea kufichua siri nyingi zaidi.

Samahani kaka, Mimi ni kijana na rafiki wa Zitto na pia jana nilikupigia simu nikijaribu kutumia busara kuhusu na mwenendo wako hapa.

Naomba unijibu swali moja hapa mbele ya wanajamiiforum. Je na mimi ni mmojawao hao "vijana wajinga"

Nasubiri jibu lako kaka mwerevu..

omarilyas
 
Samahani kaka, Mimi ni kijana na rafiki wa Zitto na pia jana nilikupigia simu nikijaribu kutumia busara kuhusu na mwenendo wako hapa.

Naomba unijibu swali moja hapa mbele ya wanajamiiforum. Je na mimi ni mmojawao hao "vijana wajinga"

Nasubiri jibu lako kaka mwerevu..

omarilyas

Mosi: Wewe ni kijana sawa, wewe ni rafiki wa Zitto ndiyo, lakini je wewe ni mwanachama wa Chadema?

Pili: Ujinga ni nini? Mbona kila mtu ni mjinga katika jambo fulani? Marafiki wa Zitto na vijana wa Chadema wasioliona anguko la Zitto lililo dhahiri ni wajinga wa kutoliona hilo. Au nimekosea? Kunradhi.
 
kibanda ni mtumishi wa mbowe hivyo tusimlaumu sana manake anachokifanya yeye ni kufuata matakwa ya bosi wake.
 
Bila kutokea Migogoro Hamuwezi kujuana vilivyo...zinapoteka kashkash kama hizi ndivyo sura halisi ya tunaowaita "wapambanaji" zinavyojulikana....!!!

Kibanda hivi ilishindikana nini kumuita Zitto pembeni(kisiri) mkadiscuss nae hio mikakati mliyonayo wazee wa "chama" kabla hujaenda Public...? Ulichokifanya japo kwa uoni wako its OK, lkn unapokwenda Public hapo ndipo upolikoroga...!!!

Pia Tatizo la Zitto unapolihamisha kwa vijana wote wa Chadema....huo ndio Mtaji wenu...then unawaitwa Wajinga...is it?..Mtu kama Dr.Kitila unajaribu kuhoji PHD yake...Sijui kama wewe hata "degree" unayo...!!!...kama unaona PHD kazi nyepesi hebu itafute kwanza uone Jasho lake...!!!

Huku ukimponda Kitila Kuhama CCM kuja Chadema kuwa Mamluki...the same mmechukua Selasini na Rwekatare....How then?..!!!..hapa una send message nzito kwa wale ambao walishaanza kujenga Iman ya kuhamia Chadema...wafikirie mara2 kabla ya kuja "kundini"

Kuhusu Uchanga wa Zitto..si uChanga wa Zitto, bali ni Uchanga wa Chadema...!!! Ulitakiwa Ujifunze CUF namna wanavyowaondoa wale wanaowaona ni "Virusi" na huo ndio ukomavu wa Kisiasa....!!!

Wale wanaosema Zitto miezi 3 hajafika Makao Makuu na hataki kukutana naViongozi wakuu....Hili dai kubwa sana...Nakumbuka wakati Prof.Lipumba anaingia buguruni aliwakuta wazee wengi wamejaza ofisini buguruni hawana kazi za kufanya kazi kupiga soga, akawaambia watoke waende kwa wananchi...nyie leo Zitto anakwenda kwa wananchi...mnataka akae ofisini apokee simu...is it?au ndio policy za kusubiri Chopa kuwafikia wananchi...?

By the way nionavyo Ka-Mgogoro ndani ya Chadema either baina ya "Wazee" na "Vijana" au Baina ya "Wasomi wa Hali ya Juu" na Wale walioishia "Vidato/certificate"
 
Kitila humu JF wengine hatuna upande sisi kwetu ni Maslahi ya Taifa kwanza. Kitila ulivyomjibu Kibanda ukweli ni kuwa na wewe tulivyokusoma umeegemea Upande wa Zitto au sijui ndo Kampeni sielewi.

Nadhani Kibanda amemchambua Vizuri Mh. Zitto na pia na Mbowe ingawa ya Mbowe hatuna haja nayo kwani amekuwa madarakini miaka mitano tunamjua. Jitahidi kuelezea Zitto atatufanyia nini kwenye haya mageuzi zaidi ya Mbowe siyo blaa blaa za goo goo hapana!! hii ni hatari kutoka naibu katibu kuruka mpaka Uenyekiti! Kitila tueleze na wana JF wengi wa goo goo huyu je ataweza kwa lipi na amefanya lipi ndani ya chama???

Du hii balaa!Obama nae katoka ubunge hadi uraisi bila kupitia uwaziri leo inakua ajabu Zitto kugombea uenyekiti kisa ni naibu katibu
 
Suala hili la Zitto mimi nililiona la kawaida na linalenga kudumisha demokrasia. Lakini sasa ninaliangalia kwa hisia mbaya. Hii inatokana na habari nilizozipata leo kwamba Mhe. Zitto alimtumia Ndg. Msafiri (Afisa Uchaguzi - CHADEMA) kumchukulia na kurudisha fomu. Wakati Msafiri akifanya shughuli hiyo ndo alikuwa mezani kutoa na kupokea fomu za wagombea. Hali hiyo ililazimu kuondolewa ktk kazi hiyo na kupewa Katibu Mkuu Dr. Slaa.

Sasa, ninaamini kwamba Bw. Msafiri anajua vizuri taratibu na maadili ya uchaguzi kwamba anayesimamia zoezi la uchaguzi hatakiwa ku-base upande wowote wa wagombea au kuwa shabiki wa mgombea mmoja wapo.

Pili naamini kwamba Mhe. Zitto anajua vizuri maadili na taratibu za uchaguzi kwamba hakupaswa kumtumia Afisa uchaguzi kuchukua na kurejesha fomu yake. So, kwanini Zitto na Msafiri walifanya hili? Je, wanataka kuvuruga uchaguzi? au ni utoto wa kisiasa?

Anyway, CHADEMA mnapaswa kupita salama ktk uchaguzi huu, ili kujiandaa vema kwa uchaguzi mwakani. Hivyo, busara kubwa inapaswa kutumika.

Naomba kama inawezekana utuletee kanuni za kuchukua na kurudisha fomu za uongozi ndani ya CHADEMA hapa ili nasi tuone jinsi Zitto alivyokwenda kinyume na taratibu.

Endapo haiwezekani basi tupe maelezo ya ndani yaliyopelekea wewe kufikia hiyo tamati.
 
Jana nililitaja kundi la 'Vijana Wajinga' kwa majina na wengine wamenijibu kwa sms na simu wakinitaka yaishe kwani wanadai eti tunaelekea kufichua siri nyingi zaidi.

Mbali ya kuwataja wawili kati yao wamejitokeza katika jamvi jana na leo na mmoja nikamjibu. Soma sawasawa kaka. NALIONA ANGUKO LA ZITTO linalokuja. Anguko hilo litakuja akishinda uenyekiti au la, akiwa Chadema au nje ya chama hicho. Tatizo si kama atashinda au la bali ni matokeo ya kuingia kiringeni kwa staili yake ya kuvizia akifunga goli toka nje ya uwanja. Subirini muone.

Tanzania Daima inajiendesha kwa faida kubwa. Haitegemei ruzuku au uenyekiti wa Mbowe. Hata hivyo nguvu ya kambi ya upinzani (demokrasia madhubuti) ni sehemu ya uimara wa Tanzania Daima na uhalali wangu wa kuendelea kuwapo hapa. Sina njaa, sina sababu hata moja ya kujikomba kwa yeyote zaidi ya kusimama katika kile ninachokiamini. Niko tayari kubakia peke yangu kwa kuwa na mtazamo ambao ni unpopular. Tumeona vitu popular nchi hii na vyote mwisho wake vimetuingia nyongo...Mrema...Mkapa (Baada ya kuwa Rais na kabla ya kumaliza muda wake)...Kikwete na sasa Zitto...Tusubiri tuone. Amkeni mashabiki

Ulitakiwa kulijua hili mapema kabla hujamwaga pumba zako kwenye TD. Makala yako haikuwa/haina/ na haita kuwa tija yeyote katika ujenzi wa demokrasia katika vyama vya upinzani nchini. If anything imeleta mtafaruku usio na lazima.

Tatizo unamtumikia mtu ulie mzidi kwa shule lakini unakubali kufuata ushauri wake m-bovu muradi upate ugali wako aibu kubwa fani imevamiwa!
 
Pamoja na mapungufu ya Kibanda,
Waanzilishi na wachangiaji wengi wa thread hii ni wale wa chama cha kijani ..............😀
Chadema mpo??????????????????
Mwenye macho na masikio na asikie!
 
FMES,

1. Waambie when they come they better come correct, wasiamshe mizimu ya Bluray kuja ku bulldoze na ku murder machete hoja zisizo afya.

2. Maana tunaweza kwenda kwenye nitty gritty hapa na kuamua kuhamisha lile subatomic particle smasher la CERN kulileta hapa wazee wazima wakajiona kama hawajavaa nguo.

3. Not to say Zitto is infallible -in my book even Benedict XVI, that pontif bishop of Rome and his godhead are not- but when criticizing any person, especially one that is assuming a statesmanlike gravita, you better produce the requisite researched data, not mere politrickin.

- Aaahggggrrr!, I love JF maana kila ukihesabu vichwa ni vigumu kuvimaliza idadi!

Respect.


FMEs!
 
Philosopher mzuri siku zote huyaishi anayoyahubiri,nionavyo ni kwamba Chadema inatekeleza dhana yake ya Demokrasia na Maendeleo kwa vitendo,Zito Kabwe anataka kuwaonyesha Walimwengu kwamba demokrasia inayozungumzwa chadema haipo kinadharia bali kwa matendo dhairi yanayopaswa kuigwa na vyama vingine na vijana wengine wa kitanzania.Binafsi nampongeza Zito kwa kuitendea haki demokrasia.Kiukweli Kwa mtu makini hawezi kuibeza kazi aliyofanya Mbowe katika Chadema,lakini kanuni ya demokrasia inataka uongozi wa kupokezana.Watanzania tutakuwa tunafanya makosa makubwa sana tukianza kumuhukumu Zito kwa umri wake badala ya uwezo wake wa kuongoza.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom