Nimeisoma makala yangu yote mara mbili mbili na kuihakiki akili yangu na kubaini kwamba pengine kuna aya moja tu ambayo pengine imepotosha dhana nzima iliyokusudiwa.
Hata hivyo ni jambo la kusikitisha kwamba 'The Home of Great Thinkers' inataka kuchafuliwa na Watanzania ambao ni wavivu wa kufikiri na ambao kwao wao furaha ni kuona kukithiri kwa mitikisiko isiyo ya lazima ndani ya vyama vya siasa hususan hivi vichanga vya upinzani.
Ninayo imani kubwa kwa Zitto na pengine ninaujali sana mustakabali wake kuliko ilivyo kwa wengi ambao leo hii wanajifanya wakimtetea na kumpigania kinafiki ili mbele ya safari wapate maneno ya kuinyoshea kidole Chadema, au Mbowe au Zitto.
Sijakatishwa tamaa.
KIBANDA makala yako imesimamia kwa Mbowe hata kama mimi ni mvivu wa kufikiri. umekuwa ukirudia rudia
KIJANA HUYU au
KIJANA HUYO hii kuonesha kuwa
Zitto ni mtoto MDOGO hawezi kitu uenyekiti.
umeenda mbele zaidi kwa kusema kuwa Zitto mentor wake ni Mbowe.hiyo umemvunja kabisa kwani wanachadema wakisoma kama
MENTOR anagombea kwanini tusimpe mentor tumpe mtoto AU kijana mchanga?
Umesema kuwa Chadema chini ya DR.Slaa na Mbowe wameipaisha juu hukusema kuwa Zitto akishirikiana na hao wawili wamekipaisha chama.
Zitto amejiunga Chadema wakati Mbowe akiwa hana madaraka. mara nyingi Zitto katoa kauli humu humu JF kuwa wako watu wengi wamemsaidia kufika hapo alipo fika, amemtaja DR.Salim Ahmed Salim lakini hakuwahi kusema kuwa
MBOWE ni mentor wake.
Gazeti hili unaloliongoza watu wengi wanadhani ni la Chadema wakati ni la Mbowe. hivyo basi naamini kwa vile gazeti hili linatumiwa sana na wanachadema kama John Mnyika alikuwa akiandikia sana, Kitila MKUMBO,Mwanakijiji na wengi wanaodhaniwa ni wapenzi au makada wa Chadema.
kitendo hicho kimepelekea gazeti lako naamini litakuwa likisomwa kwa umakini na matawi Ya Chadema nchi nzima.makala yako akisoma mtu wa Mtwara mwanachadema ambaye ni mjumbe wa Mkutano mkuu wa Chadema tayari umempa jibu kuwa
kura yake aipeleke wapi?
umsema kuwa CCM au Usalama wamekuwa na utaratibu wa kuvuruga vyama ukatoa mifano na
kuhitimisha kuwa Zitto kaingia kwenye mtego huo.
Kibanda kama ni kampeni basi tayari
umemmaliza Zitto.umeshindwa kutaja mapungufu hata kidogo ya Mbowe kama kukataa kulipa madeni ya Nssf ambapo ni doa kwa kiongozi makini, kuendesha zoezi la kuteua wabunge wa viti maluum kupitia Chadema kwa
misingi ya ukabila chini yake Mbowe KAMA mwenyekiti.
Mbowe alishindwa kuweka chombo au baraza la wanawake Chadema wafanye kazi hiyo ya kuchaguana.wakajazwa watu wa familia na wenye mahusiano na mkoa wa Kilimanjaro. ulikuwa na nafasi ya kubalance Story yako.
gazeti hilo hilo ukaweka
READ STORY kuwa Zitto azua mjadala na ukaeleza kuwa wazee wa Chadema wamemuomba Mbowe achukue Fomu ya uenyekiti ili
akivushe chama, maneno hayo yanatafsiri nzito sana kwa mwanachama wa kawaida wa Chadema kuwa
kama wazee wenye chama wamepima na kuona Mbowe anafaa kwanini kura yangu nimpe KIJANA HUYU au
Mwanasiasa Mchanga KWA mujibu wa maneno yako.
pia kama Zitto ni mtu wako wa karibu kwanini usimwite au kumtumia email ukamsikia kabla ya kumchafua kwenye gazeti la Mbowe? ok Mbowe umempigia kampeni kupitia gazeti alilokuajiri jee Zitto akasemee wapi?
Kibanda HUKUMTENDEA HAKI ZITTO.
Andika makala nyingine kusahihisha habari hii kwani ukija kujibu hapa huwezi kupata audence kama uliyonayo kwenye gazeti La Tanzania Daima ambalo kama sikosei ni la pili kwa circulation nyuma ya Mwananchi.Kwenye online lina watu wengi sana hilo unalijua. umemchafua Zitto bwana Kibanda.