Sijaona sababu yoyote ya kusababisha kutilia shaka utendaji wa Mh. Mbowe katika uongozi wa Chama. Kama ni kufukuza wasaliti ndani ya Chama, hakuna adhabu mbadala kwa wasaliti wa CDM wanaofanya kazi kwa siri na Mzee Wasira, Mwigulu nk. CCM hawajapata kupumua vizuri katika kipindi chote cha uongozi wa Mbowe.
Lakini tumeshuhudia ukali wa Zitto ukipungua kadili siku zilivyokuwa zikiendelea, tena ushahidi kwa mwenyekiti wa CCM kutofanya kampeni kwenye jimbo la Zitto kipindi cha kampeni zote za uchaguzi mkuu, ni tosha kwamba huenda Zitto ni mwenzao. Kama kweli tunatakla nchi ikombolewe, acheni propaganda za kimwigulu kwamba kuna ukanda, ukabila nk.