Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,988
Mwisho Mkuu Mwita Maranya,miongoni mwa watu ambao huwa wanaheshimu hoja zao humu ndani Jamvini ni mimi,lakini leo hii nashangaa umekua na jazba sana na Kibanda,au kwa sababu ameigusa CHADEMA?,mbona siku zote za Nyuma ulikuwa mfuasi mkuu a Kibanda hata kama alikuwa ameandika Utumbo katika kuisifia CHADEMA ama kiongozi yoyote wa CHADEMA,hizi hasira zako za leo zinatoka wapi Mkuu?
Ndugu yangu WABHEJASANA kwanza nikushukuru kwa heshima unayonipa, tuendelee kuheshimiana Vivyo hivyo.
Mimi siku zote msimamo wangu uko very clear katika mambo yanayohusiana na chama changu na Taifa langu. Kama mtu anaandika ukweli nitamuunga mkono lakini pia mtu akiandika uongo ama upotoshaji ninamuambia ukweli wake papo hapo. Kwahiyo tunaweza kukubaliana katika jambo moja lakini tukashindwana katika jambo jingine, na hiyo ni hali ya kawaida sana katika maisha, jambo la msingi ni kuhakikisha siku zote tunasimamia ukweli tena ukweli mtupu.
Bahati mbaya sana kibanda anajitahidi sana kutaka kuwapotosha watu kwa kumpamba sana kinana as if ni mtu mpya kutoka sayari nyingine wakati ukweli wa mambo ni kwamba kinana ni miongoni mwa watu walioifikisha kubaya nchi hii, kashfa alizonazo hazimpi nafasi kamwe ya kuwa tishio kwa upinzani nchini, na hasa Chadema ambayo kibanda anajaribu kuionyesha kwamba sasa hatuwezi kufukurukuta kwa uteuzi wa kinana kuwa katibu mkuu wa ccm, kitu ambacho si sahihi hata kidogo, isipokuwa anajaribu kuwajengea wananchi uoga usiokuwa na msingi kwa maslahi yake binafsi na ccm ambao tayari kuna taarifa kwamba wameshamalizana nae, na anajiandaa kuhamia habari corporation ili akawafanyie kazi yao vizuri. Sasa njaa yake asiitumie kuwatia uoga usio na msingi wananchi hasa wapenda mageuzi.
Pia naomba kukufahamisha kwamba sijaandika kwa jazba yoyote isipokuwa nimeandika kwa "tune" ile ile aliyotumia kibanda kutujibu katika makala yake hii. Kama comments zangu zimekustua kwa leo naomba uwe na amani bwana shemeji tuko hapa kubadilishana mawazo kwa njia ya kueleweshana na kukosoana. Na jambo kubwa zaidi ni kuona kwamba nchi hii inapata viongozi makini na mahiri wanaoweza kuwatumikia watanzania wote bila ubaguzi ama kinyongo cha aina yoyote, na hakuna namna ccm inaweza kuwa tegemeo la kuyabadili maisha ya watanzania hawa walio mafukara kwa sababu ya sera mbovu za ccm isipokuwa Chadema pekee ndiyo tegemeo la wananchi kwa sasa.
Last edited by a moderator: