Kibanda: Kinana ni Kimbunga

Najua rafiki yangu kibanda wewe si mfuasi wa chama chochote lakin kwa stahili hii ya kuondoka kwa muajir ya kutafuta bif si nzuri,kwan ungesema mapema mapungufu ya upizan sio jana nimekuona na rostam sijui ndio unakamilisha mipango ya kwenda habari c0,unatoka na makala za bif tunajua njaa tu ndio inayosumbua
 
Tusubiri fainali 2015
fikiria watz wote tunaji-tune kuwa 2015 ndio final, kuwa hakuna nchi baada ya hapo!? Imeandikwa wapi kuwa ujinga huu, unafiki huu, kutowajibika kwa watawala, rushwa iliyokithiri, incompetence ya watz nk vinaishia hapo!?
Surely, there is nothing wrong with this country called Tanzania but I guess there is something wrong with the people residing in, for sure!! ...na ndio maana wengine wakija hapa wanamake fortune wakati sisi tukikalia mchanga kwenye shule zetu
 
haya ndo yale anayayaongelea kibanda kwani viongozi na pro CDM mnakera sana pale ukweli ukisemwa juu yenu kwanini kama kweli mnajiamini mnapenda kusifiwa kila siku? kukosolewa na kuambiwa uwezo wa adui yako ni njia moja wapo ya kuweza kujipanga kwaajili ya mapambano,au ndo yale mkishapigwa chini 2015 mrudi na kutuambia wamechakachua? jua uwezo wa adui yako.So mlitaka aandike Kinana ni kilaza then mfurahi na kusherekea kutumia ruzuku hiyo ni challenge mnatakiwa mlifanyie kazi.

kwa hili Big up Kibanda.

wewe na kibanda akili zenu zinafanana kama si kulingana.

Nimesema hivi na narudia, ccm ilikofikia sasahivi imebakiwa na mbinu moja tu ya kuwabakisha madarakani, ambayo ni kutumia vyombo vya dola, Polisi, usalama wa Taifa na JWTZ. Kama ni kimbunga basi kimbunga pekee kinachoweza kuwakumba na kuwasomba wanamageuzi na wapinzani kwa ujumla ni hivyo vyombo vya dola na si vinginevyo.
 
Ndiyo hivyo tena ukiwa huna misingi inayokuongoza katika uandishi utaandika chochote, na unajiweka katika mazingira ya kutumika na kutumikishwa kwa kujituma au kutumwa, kwa kujua au bila kujua.

Lakini hata hivyo Kibanda hana sababu ya kulalamikia viongozi, wanachama na washabiki wa CHADEMA kwamba hawakubali kukosolewa na kwamba hawana uvumilivu. Viongozi wa CHADEMA wangekuwa hawana uvumilivu isingewezekana yeye kuendelea kuwa Free Media hadi leo. Kipimo cha uvumilivu wa uongozi wa CHADEMA ni yeye kuendelea kuwa katika kampuni anayotaka kuikimbia hadi dakika hii atapoandika makala rasmi ya kumsifia Kinana na kukandia viongozi wa CHADEMA.

Tutashuhudia mengi kuelekea 2015.
 
Amenikumbusha Deodatus Balile aliyehama Freemedia kwenda Habari Corporation kwa style ya Aina yake

-Kujaribu kufananisha harakati hizi na za Mrema ni jaribio la kufifisha nguvu vuguvugu hili

-Kuhusu CHADEMA kukubali kukosolewa hilo naliunga mkono ila sasa si kwastyle anayofanya Kibanda.

-Nilitegemea kwa uzoefu wake aliousema angeweza kuandika kuhusu changamoto za kimfumo na kisera kwa kujikita kwenye itikadi zaidi badala ya kujadili sura za watu na mbinu za ujanja ujanja katika kushinda uchaguzi

-Imagine maandishi kama haya yanatoka kwa Kiongozi wa jukwaa la wahariri.

-Jenerali Ulimwengu inabidi ashirikiane sana na akina Ayoub Ryoba wapike kizazi kipya cha waandishi wenye weledi huko baadae

-Kwa wafuasi na viongozi wa CHADEMA:Tukubali kukosolewa kwa hoja za kujenga na pia tusiache kujibu hoja zinapopindishwa.Pia Mabadiliko ni gharama na katika safari hii wasaliti ni wengi.Tuwapuuze tusonge mbele
 
Acheni kumpa huyu kanjanja umaarufu asio stahili; please ignore him with all the contempt he desreves. anapalilia ukuu wa wilaya; but he is in for a rude shock.

Karibuni tutaona makala zake nyingi zenye titles kama: Kinana dume la mbegu au Kinana mwanaume wa shoka! au Kinana muarobaini wa wapinzani!

Kwa wenye akili wameshaelewa hamasa na motisha Kibanda kuandika makala hizo unatokana na nini! Huyo ni mchumia tumbo mwingine huyo in the making.

Kuna ndugu wa karibu wa huyu jamaa aliwahi kuniambia,kuwa jamaa alimwambia, akiwa kazini anafanya kazi ya mwajri wake na ikaonekana, akiwa nje ya hapo ,hufanya ya huko nje, vinginevyo bila ya hiyvo utakufa njaa.Then akanitajia marafiki zake wakiwemo wakina Zitto,EL...Since then nilipoteza Imani kwa huyu Mwandishi.Hata alipokuja na hii Single..sikuhangaika nae.
 
Huyu bwana mpuuzi kweli,kwa taarifa ni kwamba yuko kwenye payroll ya mafisadi tukianza na Rostam
 
Ametoa tahadhari tujipange kukabiliana nae.anamuelewa vizuri yeye ndio aliyemuoji na kuandika kwenye tanzania daima,KINANA AKIRI MELI ILIOSHIKWA NA MENO YA TEMBO NI YAKWAKE LAKINI HANA HABARI NA MZIGO WA MENO YA TEMBO.
 
ccm ilikofikia imebakiwa na mbinu moja tu ya kuwabakisha madarakani, ambayo ni kutumia vyombo vya dola, Polisi, usalama wa Taifa na JWTZ. Kama ni kimbunga basi kimbunga pekee kinachoweza kuwakumba na kuwasomba wanamageuzi na wapinzani kwa ujumla ni hivyo vyombo vya dola na si vinginevyo.

Hizi ndoto za Kibanda kwamba kinana ni kimbunga wacha aendelee kuota mwenyewe sisi huko tulishaondoka siku nyingi. Huwezi kumfananisha hata kidogo Augustine Mrema na Dr. Slaa, hawa ni watu wawili walio mbali sana kiuwezo na kwa muono. Yeye aendelee tu kula matunda ya kumsafisha Lowasa na sasa kumjenga Kinana kwakuwa si haba anajipatia ujira wake na kuweza kusukuma mbele gurudumu la maisha na familia yake, lakini atambue kitu kimoja kwamba ccm ilipofikia hakuna mganga yeyote anayeweza kuinusuru na anguko kuu mwaka 2015, si kinana wala vinana!!

Ndugu zangu wapenda maendeleo ya TZ tusiwe wepesi kumlaum huyu jamaa lkn kwa mawazo yake iwe tahadhari ya kiutendaji kwa Dr. Slaa kujiweka sawa, kwani ,dharau mwiba mguu huota tende, kusema ccm ilipofikia haiwezi tena kufufuka, lkn tujuwe kuwa wa TZ wengi hawana elimu ya uraia kama ww na mm tulivyo, chamsingi tuwaelimishe wengine zaidi ili kusije kuwa kama ilivyo mkuta rais wa Zambia wakati ule aliposema hakuna wakunizidi mwisho akang'olewa madarakani kirahisi, Kinana inavyooneka kama amekamia kufufua kile kilichoondoka akili mwa wengi kuwa ccm inaweza fanya miujiza katika system hii walionayo ambayo inaonekana wazi ni mbofumbofu.
Siyo vema kumbeza Kibanda lkn tukubali kuwa Simab timu ninayoipenda toka nikiwa mdogo ilijua haiwezi kufikiwa kwa point na watani wetu, lkn watani wakajipanga leo tumepitwa, ni vema tujiweke tayari kukabiliana na haya anayosema Kibanda ili asije sema nilitabiri yamekuwa.
 
Kipimo cha uvumilivu wa uongozi wa CHADEMA ni yeye kuendelea kuwa katika kampuni anayotaka kuikimbia hadi dakika hii atapoandika makala rasmi ya kumsifia Kinana na kukandia viongozi wa CHADEMA.

Tutashuhudia mengi kuelekea 2015.
Kitila, Mimi nakubaliana na Kibanda kuwa Kinana ni kimbunga (ndani ya CCM) ila sikubaliani na mawazo yake kuhusu viongozi na washabiki wa Chadema.

Kwa nini nasema hivyo. Kinana pamoja na tuhuma zake lukuki zinazomwandama ikiwemo hii ya majuzi kuhusu nyara za serikali (ambayo kimsingi amehusishwa nayo siku nyingi) bado anapewa nyazifa kubwa na sifa kedekede na wana CCM kama mazuzu vile. Jee huyo kwao si ni Kimbunga na jabali kweli la kisiasa? Kibanda katika hili naye amewaza kama wawazavyo wanasiasa na washabiki wa CCM kuwa wamepata jabali la kuweza kuwanasua na kifo wakiwa ICU.

Naamini Kibanda hajatumwa na yeyote kuandika hayo ila ametumwa na utashi wa moyo wake na kile anachokiamini. Ameshindwa kujua kuwa sasa hivi hata mtu wa kawaida kabisa asiye mfuatiliaji wa mambo ya uvunguni mwa siasa anajua Kinana ni nani katika ufisadi na ukosefu wa UPENDO kwa jamii ya waTZ.

Jambo moja Kibanda anatakiwa kujua ni kuwa sasa hivi sio 1995 au 2010, maana wakati huo watu hawakujua kuwa Utawala unaondolewa kwa matakwa ya wananchi wanyonge walio wengi. Ila baada ya kuona kuwa imewezekana kwa vigogo kama Gadaffi, Mubarrak na wengineo kama Kenya, Zambia,Malawi nk sasa wao nao wanasema KUMBE TWAWEZA?
 
Kulikuwa na taarifa niliiona humu JF kwamba huyu jamaa anajiandaa kwenda Habari Corp. kum'replace' mhariri sijui anaitwa Bagenda?
 
Kipimo cha uvumilivu wa uongozi wa CHADEMA ni yeye kuendelea kuwa katika kampuni anayotaka kuikimbia hadi dakika hii atapoandika makala rasmi ya kumsifia Kinana na kukandia viongozi wa CHADEMA.

Mkuu Free Media, ni mali ya Chadema.
 
mm Tembo wetu watapona kweli!!!! Kibanda!!!! kumpamba mtu fisadi kama huyu inaonekana na ww upo huko huko


kwa sasa hata usalama wa taifa wakatae ujue CCm kurudi ikulu ni ngumu mno tena sana
 
wewe na kibanda akili zenu zinafanana kama si kulingana.

Nimesema hivi na narudia, ccm ilikofikia sasahivi imebakiwa na mbinu moja tu ya kuwabakisha madarakani, ambayo ni kutumia vyombo vya dola, Polisi, usalama wa Taifa na JWTZ. Kama ni kimbunga basi kimbunga pekee kinachoweza kuwakumba na kuwasomba wanamageuzi na wapinzani kwa ujumla ni hivyo vyombo vya dola na si vinginevyo.
Mwita, na huo ndio ubaya wa viongozi wa vyombo hivyo kuwa wateule wa Rais (ambaye ni mkuu wa CCM pia). Hakuna cha CDF,IGP au wa TISS anayeweza kusimama hadharani na kusema watu wangu wasitumiwe na chama tawala.
Ona hata juzi JK kajisahau na kutoa hadhari kwa CCM hadharani eti "CCM acheni kutumia Polisi kujijenga kisiasa"
Agizo hilo alitakiwa alitoe kwa siri kwa makada wake ila kwa vile kitendo cha kutumia polisi na jeshi(kumbuka Shimbo 2010) kwao si cha siri kimetufumbua zaidi maana Mwenyekiti wao kakiri hadharani matumizi hayo
 
Judas........that what he is...even Jesus was sold in the last moments of his missions.......and yet he won according to his believers
 
Nilichoona kwenye mtiririko wa makala hiyo ni mwandishi kujicifia mwanzo mwisho.. kwa cifa alizojimilikisha kwenye makala yake hii hakupaswa kuwako hapo alipo sasa.. Ushauri wangu kwake awe makini.. Binadamu anaposukumwa na njaa kufanya jambo ambalo ni ovu kwa jamii anaweza kueleweka.. Ila pale anaposukumwa na tamaa kupalilia uovu jamii haitamuelewa hata kidogo.. Kibanda hana njaa.. Napenda sana kuamini hasukumwi na tamaa kuandika alichokiandika..
 
Back
Top Bottom