Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Ndugu zangu wapenda maendeleo ya TZ tusiwe wepesi kumlaum huyu jamaa lkn kwa mawazo yake iwe tahadhari ya kiutendaji kwa Dr. Slaa kujiweka sawa, kwani ,dharau mwiba mguu huota tende, kusema ccm ilipofikia haiwezi tena kufufuka, lkn tujuwe kuwa wa TZ wengi hawana elimu ya uraia kama ww na mm tulivyo, chamsingi tuwaelimishe wengine zaidi ili kusije kuwa kama ilivyo mkuta rais wa Zambia wakati ule aliposema hakuna wakunizidi mwisho akang'olewa madarakani kirahisi, Kinana inavyooneka kama amekamia kufufua kile kilichoondoka akili mwa wengi kuwa ccm inaweza fanya miujiza katika system hii walionayo ambayo inaonekana wazi ni mbofumbofu.
Siyo vema kumbeza Kibanda lkn tukubali kuwa Simab timu ninayoipenda toka nikiwa mdogo ilijua haiwezi kufikiwa kwa point na watani wetu, lkn watani wakajipanga leo tumepitwa, ni vema tujiweke tayari kukabiliana na haya anayosema Kibanda ili asije sema nilitabiri yamekuwa.
Hakuna anayepinga kibanda au mtu mwingine yeyote kuwa na maoni ya mawazo yake. Tunachokataa hapa ni upotoshaji unaofanywa kwa makusudi mazima na huyu kibanda kwa malengo yake binafsi.
Nimesema hapo awali kwamba kinachoweza kuwanusuru ccm kubaki madarakani kwa mwaka 2015 ni vyombo vya dola pekee na hakuna kingine. Kinana hana uwezo wowote wa kuihuisha ccm. Umeshafanya tathmini ya ziara alizofanya hivi karibuni mikoa ya Mtwara, Rukwa, Geita na Arusha na kuona muitikio wa wananchi dhidi ya kinana na ccm kwa ujumla?
Kama kweli kinana mwenyewe anajitambua kwamba yeye ni kimbunga cha kuuzoa upinzani na kuufukia shimoni inakuwaje anakwenda mikoani na kukodi wananchi wa kwenda uwanjani kumsikiliza? kimbunga kikivuma si wananchi/ watu wenyewe wanakisikia na kujikusanya? inakuwaje hiki kimbunga cha kinana kisaidiwe kujaza watu uwanja kwa kuwanunua watu kama alivyofanya hivi karibuni Arusha ambako ni "nyumbani" kwao kwa watu kupewa fedha ili wahudhurie mkutano?
Kama mtu anawakosoa viongozi wetu kwa mambo ya ukweli tutakubaliana nae lakini yeyote atakayethubutu kutengeneza kiwanda cha uongo huyo hatutamuacha apite kimya kimya, lazima tutamjibu kwa tune ile ile aliyotumia kuwahadaa wananchi. Imeshafahamika kwamba kibanda yuko njiani kwenda kwa fisadi Rostam sasa kwanini anahangaika kuwachafua viongozi wetu? kwanini asiondoke kwa amani tu? kwani wangapi waliondoka Tanzania daima lakini bado gazeti linazidi kupata mauzo ya juu? Manyerere Jackton na Deodatus Balile kwa kutaja wachache, waliondoka lakini bado Tanzania Daima haikutetereka.