Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,931
- 31,176
Hayo si maneno yangu,ni maneno ya Wakili Msomi ingawa lipo katazo la Mh wa mjengoni kwamba tusitumie maneno wakili Msomi.
Ikiwa kesi ya Mh Mbowe ni nyepesi kuliko ya kibaka aliyekwapua simu Kariakoo kwanini Serekali kupitia ofisi ya DPP isiiondoe kukwepa kuaibika siku za usoni ?.
Nimemsikiliza Wakili Msomi vizuri kwamba sasa Mh Mbowe anakaa sehemu mmoja na wafungwa wanaosubiri kunyongwa.Nabaki kushangaa kwanini Wakuu wa mamlaka nchi wanapenda kuipaka serekali yetu tukufu matope pasipo sababu za msingi.Jambo hili likipelekwa Mahakamani Serekali itasema nini sababu za kumfanyia mtu ambaye bado hajahukumiwa vitimbi vya aina hii.
Sasa naanza kuamini kuna watu ndani ya Serekali hii ya awamu ya sita wanafanya kila lililo ndani ya uwezo wao kuonyesha serekali ya awamu ya tano ilikuwa na nafuu kubwa ukilinganisha na hii ya sasa.
Ikiwa kesi ya Mh Mbowe ni nyepesi kuliko ya kibaka aliyekwapua simu Kariakoo kwanini Serekali kupitia ofisi ya DPP isiiondoe kukwepa kuaibika siku za usoni ?.
Nimemsikiliza Wakili Msomi vizuri kwamba sasa Mh Mbowe anakaa sehemu mmoja na wafungwa wanaosubiri kunyongwa.Nabaki kushangaa kwanini Wakuu wa mamlaka nchi wanapenda kuipaka serekali yetu tukufu matope pasipo sababu za msingi.Jambo hili likipelekwa Mahakamani Serekali itasema nini sababu za kumfanyia mtu ambaye bado hajahukumiwa vitimbi vya aina hii.
Sasa naanza kuamini kuna watu ndani ya Serekali hii ya awamu ya sita wanafanya kila lililo ndani ya uwezo wao kuonyesha serekali ya awamu ya tano ilikuwa na nafuu kubwa ukilinganisha na hii ya sasa.