Kero: IGP tuondolee Askari wa Usalama Barabarani Tabata, wamekua kero na kusababisha Foleni kwa faida yao.

The Evil Genius

JF-Expert Member
Mar 21, 2014
5,462
17,277
Mimi kama mkazi wa Ukonga, naetumia barabarani ya Tabata naomba kutoa ombi kwa IGP ama mkuu wa usalama wa barabarani mkoa wa Dar es Salaam.

Inajulikana kwamba asubuhi ni muda wa rush hours, watu wanawahi kwenda kwenye shughuli zao za kiuchumi na pia inajulikana setup ya barabara zetu asubuhi gari nyingi zinaelekea upande wa mjini na jioni zinatoka mjini kurudi nyumbani.

Hivyo ni common sense tu kwamba askari wa usalama barabarani kwa asubuhi wasaidie gari zinazoelekea mjini kufika mapema na jioni zinapotoka mjini kufika majumbani mapema.

Cha ajabu askari wa usalama barabarani wa Tabata kila siku sa 12 wako barabarani sio kwa kusaidie gari zipite kwa haraka bali kutengeneza foleni kwa faida yao wenyewe hivyo unakuta barabara ya kutoka mjini kuja Segerea iko tupu, nyeupe lakini barabara ya kwenda mjini imejaa foleni bola sababu za msingi huku askari wakiwa wamejazana barabarani kuanzia magereza hadi barakuda.

Hii foleni hua wanaotengeneza kwa faida yao ili ikitokea umechepuka hata kama mistari ya barabarani inakuruhusu, wanakukamata na kukuandikia faini ya makosa 2 ya matumizi mabaya ya barabara ama uwape kitu kidogo usamehewe.

IGP ama mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Ilala, tupunguzie hawa, wamekua ni kero hasa nyakati za asubuhi.
 
Nadhani huelewi anaewatuma kuja kukusanya hizo pesa ndio hao hao unaowaomba wawaondoe. Impossible.

Unafikiri hao wanajipangia wenyewe muda na sehemu ya kukaa? Hapo wanachukua hizo rushwa lakini kuna percent inapelekwa ngazi za juu, na kama upelekaji wako ukionekana unasuasua basi unahamishiwa Kondoa vijijini, kisha analetwa mwingine atakaepeleka mapato vizuri kwa walio ngazi za juu.
 
Askari nchi nzima wanaenda barabarani wakiwa na malengo binafsi na Kuna commission wanapekeka mahali jion wakitoka barabarani ndo maana imekuwa kwao halali so kama nchi watolewe wote barabarani zifungwe camera

Sent from my CPH2239 using JamiiForums mobile app
 
Askari nchi nzima wanaenda barabarani wakiwa na malengo binafsi na Kuna commission wanapekeka mahali jion wakitoka barabarani ndo maana imekuwa kwao halali so kama nchi watolewe wote barabarani zifungwe camera

Sent from my CPH2239 using JamiiForums mobile app
hiyo kazi inalipa sana aisee
muhimu usiwe na aibu wala maadili, utapiga pesa
kibaha pale jamaa walikuwa wanashindana kujenga
 
Mimi kama mkazi wa Ukonga, naetumia barabarani ya Tabata naomba kutoa ombi kwa IGP ama mkuu wa usalama wa barabarani mkoa wa Dar es Salaam.

Inajulikana kwamba asubuhi ni muda wa rush hours, watu wanawahi kwenda kwenye shughuli zao za kiuchumi na pia inajulikana setup ya barabara zetu asubuhi gari nyingi zinaelekea upande wa mjini na jioni zinatoka mjini kurudi nyumbani.

Hivyo ni common sense tu kwamba askari wa usalama barabarani kwa asubuhi wasaidie gari zinazoelekea mjini kufika mapema na jioni zinapotoka mjini kufika majumbani mapema.

Cha ajabu askari wa usalama barabarani wa Tabata kila siku sa 12 wako barabarani sio kwa kusaidie gari zipite kwa haraka bali kutengeneza foleni kwa faida yao wenyewe hivyo unakuta barabara ya kutoka mjini kuja Segerea iko tupu, nyeupe lakini barabara ya kwenda mjini imejaa foleni bola sababu za msingi huku askari wakiwa wamejazana barabarani kuanzia magereza hadi barakuda.

Hii foleni hua wanaotengeneza kwa faida yao ili ikitokea umechepuka hata kama mistari ya barabarani inakuruhusu, wanakukamata na kukuandikia faini ya makosa 2 ya matumizi mabaya ya barabara ama uwape kitu kidogo usamehewe.

IGP ama mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Ilala, tupunguzie hawa, wamekua ni kero hasa nyakati za asubuhi.
acha wivu na kazi za watu, wache wapige hela
 
Back
Top Bottom