Nimeitoa huko kwa mdadisi na aliyekuwa mshiriki wa ujenzi wa katiba ya kenya,
::::::::::::::::::::::::::::::
KENYA INATEKETEA KISA KATIBA MPYA: NI FURSA NA SOMO KWA TANZANIA
Ni dhahiri polisi wa kawaida wamezidiwa. Sasa jeshi limelazimika kuingia kupambana na wanaojiita GenZ.
Bahati niliteuliwa kama mshauri Kwa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Cha Kenya (COTU -K) anachoongoza Brother Francis Atwoli. Ni wakati wa mchakato wa kutunga kilichoitwa katiba mpya. Wafanyakazi walishirikishwa vya kutosha. Hivyo ITUC na ILO wakanipa kibarua Cha kushauri. Vikao vingi tulifanya pale Mombasa.
Nilipopitia rasimu nilistaajabu kuona mambo ya hovyo ndani ya rasimu. Nitapitia machache:
1. Pendekezo kwamba kima cha chini cha mshahara (minimum living wage) kitamkwe kwenye katiba. Wenyewe wakidhani ni jambo zuri mno mshahara wa kima cha chini kulindwa kikatiba. Niliwaeleza huu ni ujinga. Mshahara ni suala la "econometrics". Sio a political issue.
Kenya kuna taasisi maalum ya kupendekeza mishahara, isyo kwamba imetajwa kwenye katiba.
Huyu anayesema hivi ni nani?
2. Majaji wasailiwe na wananchi kabla ya kuajiriwa kupitia runinga. Wao wakiamini kuwa itazuia majaji kula rushwa au kuendelea serikali. Niliwaeleza upumbavu uliopo. Kwanza jaji hapimwi Kwa kigezo kimoja tu. Pili itawezekana vipi raia ambaye hata kuhesabu mpaka 5 hawezi amsaili jaji? Je baada ya kumsaili nani ataamua huyu aajiriwe yule ailsiajiriwe? n.k.
Kenya majaji hawafanyiwi usaili na Raia.
3. Uhuru wa kuandamana na kukusanyika usio na masharti. Niliwaelez
View attachment 3397462a Nini kitatokea uhuru aina hii ukitolewa na katiba. Ndicho kinatokea Sasa.
Masharti ya mikusanyiko huwa yapo tu. Ikiwemon kuandamana.
Suala la maandamano kugeuka vurugu ni suala jingine
4. Kuwe na wabunge wanaowakilisha wafanyakazi. Hili niliwarejesha Kwa Uganda, Tanzania, Cameroon na Cote D'Ivoire. Wafanyakazi huko walikuwa wanadai ubunge huo ufutwe hauwasaidii. Tanzania tulifanikiaa kujiondoa kwenye jumuia za chama na ndio JUWATA ikafa ikaja TFTU, baadae OTTU na Sasa TUCTA. Wafanyakazi walikuja kugundua wawakilishi wao walijali matumbo Yao. Pia ukitoka uamuzi unaowaumiza wanashindwa kupinga Kwa kuwa wawakilishi wao walishiriki kutoa uamuzi.
Hata TZ muna wabunge wanachukua fomu za viti maalum huko CCM kuwa wana wakilisha wafanyakazi, ila kiuhalisia wanapigania MATUMBO yao tu.
5. Kuruhusu maofisa na watendaji kushitakiwa binafsi hata wanapofanya kosa wakati wanatekeleza majukumu waliyopewa na katiba.
Kwanini ufanye kosa, au ufanye kazi kinyume na taratibu ulizopewa.
Kinachotokea Kenya ni matokeo ya LAWLESSNESS.
Kama watu hawawezi kuzungumza au kwutafita haki mahakamani, watajichukulia sheria mkononi.
Niliwaambia hii itafanya watumishi wa serikali haswa wa vyombo vya Dola kuzembea. Ndio maana Sasa unaona kisichana kinatikisa makalio mbele ya askari mwenye rungu na bunduki. Watumishi aina hii wanatakiwa waadhibiwe na mahakama ya kijeshi tu.
Kama unafikiri kila tatizo linatatuliwa kwa nguvu, huna akili.
Mwaka 2007 Kenya walikifa zaidi ya watu 1,000 na watu walishtakiwa.
Dunia siyo ya bibi yako.
Ukiua watu 200 tu, funia inakuingilia kati.
AFrika siyo Israel kwamba uuwe watu uangaliwe tu.
Nimetaja mifano michache lakini kusema kweli katiba ya Kenya ni mbovu mno na ndio chanzo cha haya machafuko . Wanatuambia ni katiba nzuri tuiige hawajui wasemalo. Nao Wana mawazo na matendo ya kina Shakira, Boniface Mwangi, Martha Karua, Kalonzo na Odinga.
Kafiba ya Kenya ni mbovu kwenye gharama za ue deshaji wa serikali tu.
Serikali ya kenya ni kubwa sana na wanalipana sana pesa za umma.
Kuvurugika nchi ndio wanapata maslahi Yao
Tukatae. Tusiichezee katiba. Tusifanye reforms kwa mashinikizo.
Mwisho: nyumba ya jirani ikungua wee Jenga nyingi. Wapangaji wapo. Hakuna mtalii ataenda Kenya sasa. Wawekezaji wanaanza kuhama. Huu ndio muda wetu kuchangamka.
Halafu tuimarishe ulinzi mpakani. Wakimbizi wako njiani wanakuja.
Mwishoooo: tuendelee kudhibiti wakorofi wetu kwa nguvu na ari mpya. Bora walie sasa kuliko kuacha waanze kuchoma majengo na mali za watu
Nakazia tuwachape viboko tu,wanaojibidisha kutupeleka katika majanga ya aina hii,si kila jambo nilakuiga.
Amani ya nchi hailindwi kwa Mabomu na BUNDUKI.
Amani inalindwa kwa MAZUNGUMZO, HAKI, KUHESHIMU TARATIBU TUKIZOJIWEKEA.
Leo wanansiasa wakitaka kufanya mkutano mtaani ni VITA, bungeni kuna Spika wa Ikulu watu hawaongei, MAHAKAMANI haki hakuna.
Amnai huwa inavurugika katika mazingira kama hayo.
Watu wanakata tamaa, hawaoni sehemu ya kupata haki.
Inakuwa vita sasa.
Mtu akama SATIVA unadhani anaweza kwenda wapi kupata haki???
Imagine watu wenye vinyongo kama SATIVA, LISSU, NDUGU wa Ally kibao wakifika hata 1,000 tu???