Kazi za usalama (TISS) mpaka utoe hela?

TISS ya Tanzania hovyoo sana haina maadili wala nidhamu. Nenda 4 Ways Kinondoni uone wanavyogombania malaya. Uchumi, utawala etc they are useless.
Povu ruksaaa
Hivi kugombania Malaya tu ndiyo justification kuwa TISS Agents hawana Maadili?

Je, unajuaje pengine Kuwagombania hao Malaya kuna Kazi Maalum wanaifanya?

au hujui kuwa wapo Agents wengine wa Idara wanajifanya Malaya ili wapate Taarifa muhimu?

Uwezo wako wa Kufikiri ni Kiduchu mno.
 
Jamani mwenye clue na hili tusije kupigwa maana ni mpunga mrefu tunaambiwa tutoe kazi ipatikane.

Je, kuna ukweli?
Hamna kutoa hongo, hii kazi ni ya kipekee, hata huyo aliyekwambia utoe pesa hayupo huko amekuchota tu....
 
Kutoa vitambulisho kwenye baa ni upumbavu.

Ila kwa namna fulani una hoja maana hii idara yetu ya sasa mhhh.

Lakini lazima sote tuamini kuwa wapo maofisa nguli na wale welevu kabisa trust me.
Mapungufu machache ya Kiutendaji hayaepukiki katika Idara ( Taasisi ) yoyote ile kwani hata huko CIA na MOSSAD nako pia kuna 'some rotten Agents' kama waliopo TISS ila haihalalishi kuwa Ofisi nzima na Watendaji wake hawafai.

Tuwe na Heshima kidogo na hii Idara kwani pamoja na kwamba ina Udhaifu wa hapa na pale ( ambao hata hivyo unafanyiwa Kazi na Kudhibitiwa ) ila imefanya Kazi kubwa na bado inaendelea kufanya Kazi kubwa ya Kiusalama ndani na nje ya Tanzania japo tunaweza tusione au tusiligundue hilo.
 
Jamani mwenye clue na hili tusije kupigwa maana ni mpunga mrefu tunaambiwa tutoe kazi ipatikane.

Je, kuna ukweli?
Waliotoa mpunga kisha wakaingia huko ndo wanaoisumbua jamii kwa dirty job sasa
 
Mapungufu machache ya Kiutendaji hayaepukiki katika Idara ( Taasisi ) yoyote ile kwani hata huko CIA na MOSSAD nako pia kuna 'some rotten Agents' kama waliopo TISS ila haihalalishi kuwa Ofisi nzima na Watendaji wake hawafai.

Tuwe na Heshima kidogo na hii Idara kwani pamoja na kwamba ina Udhaifu wa hapa na pale ( ambao hata hivyo unafanyiwa Kazi na Kudhibitiwa ) ila imefanya Kazi kubwa na bado inaendelea kufanya Kazi kubwa ya Kiusalama ndani na nje ya Tanzania japo tunaweza tusione au tusiligundue hilo.
Ila we popoma Kila siku unajinasibu kuwa jasusi la kagame Sasa tiss inakuhusu nini?
 
wengi mbona wameingia kwa rushwa wengi... TISS ,JWTZ au Polisi.
Wengi sana
Ni kweli wapo vijana wengi wameingia JWTZ, TISS, POLICE lakini hiyo michongo ilipitia kwa wakubwa flani maana tatizo unaweza kukutana na tapeli ukaliwa hela na jamaa usimwone tena.
Mie kuna jamaa zangu kama wanne hivi waliingia kwa michongo kipindi cha nyuma tena wawili kati yao hawakuwa hata na vyeti vya secondary waliishiaga form 2 wakaingia mitaani kusaka maisha ila walikuja kupata mchongo wakaingia JKT miaka 2 badae wakaingia JW na baada ya kuhitimu walipangiwa sehemu tofauti mmoja yuko JW walipelekwa Somalia halafu kuna mmoja yuko JW kambi flani halafu wale wawili inasemekana walichukuliwa TISS na sasa kuna mmoja amejenga bonge la jumba kwa wazazi wake
 
Kama huyo mtu unamwamini mpe tu maan sahv jwtz na Tiss wanachukua watu kimyakimya hutokaa uskie wametangaza kama ilivy vitengo vingine mfano mwez ulopita nyuma kuna gazet nliona polisi,magereza,zimamoto na uhamiaji wanataka idad fulan ya watu wajiunge.

Na Hadi leo sijackia kiliendelea nn lakn JWTz na TISs hawakutangaza kabisaaaa na hata wanaoenda kozi uwa kimykimy sana. Cha kukushaur fanya kama unafumba macho tu mpe anachotaka kikubwa umri wako uwe sio juu ya 25 usiwe umeoa/kuolew.

Kingine rekodi safi ya uhalifu na usiwe na makosa kwn naskiaga wanakuchunguza kwanzia chini yaan uliposoma na history yako kubwa zaidi tunza damu yako iwe swafi na swalama.

Asubuh njema

mmpe na namba yako kabisa akutafute! Tapeli mkubwa wewe!
 
TISS ya Tanzania hovyoo sana haina maadili wala nidhamu. Nenda 4 Ways Kinondoni uone wanavyogombania malaya. Uchumi, utawala etc they are useless.
Povu ruksaaa
Ngj niende hapo huenda na connection zipo hko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom