Kati ya watu milioni 600 ukabahatika wewe peke yako…………..!

vukani

JF-Expert Member
Dec 30, 2009
245
165
Nimewaza haya nikiwa nje ya Dini kabisa. Hapa nilikuwa naliangalia jambo hili Kisayansi, kwa hiyo kama ukihusisha Dini yako na jambo hili, utatoka nje ya mada.

Nilikuwa najiuliza tu kwamba, sisi wote tulitoka kwa wazazi. Baba alitoa mbegu, ambazo kwa sehemu kubwa ni protini (chakula alacho). Kwa kufanya tendo la ndoa mara moja mwanamme hutoa cc 5 za manii (ujazo wa kijiko kimoja cha chai). Kila cc moja ina mbegu zipatazo milioni 120. Hivyo, cc 5 za manii, zina mbegu zipatazo milioni 600. Kati ya hizi, ni mbegu moja tu inayotakiwa kurutubisha yai ili azaliwe mtoto, ni ajabu eh!

Mbegu moja kati ya mbegu milioni 600. Ni uwiano mbaya sana kama siyo kituko. Yaani hii ni bahati sana, kati ya watu milioni 600 aliowatoa baba ukabahatika wewe peke yako. Mama naye alitoa yai. Kila mwezi hutoa yai moja ambalo likirutubishwa anazaliwa mtoto. Kila mwezi, mwanamke hutoa yai moja, kwa mwaka mmoja hutoa mayai 12. kati ya haya ni mangapi hurutubishwa? Kumbuka, mbegu na yai vilitokana na vyakula ambavyo vilioteshwa au kupandwa kwenye udongo wenye rutuba (mbolea) na maji. Maji na mbolea vilitoka wapi? Ni mzunguko usio na mwisho wala mwanzo……………..
 
Kwa maana nyingine wewe ndo ulikua mjanja , ukatoka speed na ukawa wa kwanza kurutubisha yai.
 
hongera kwa kufikirishaubongo wewe ni great thinker.
sio watu wanajiita gt halafu wanapost utumbo hapa.
 
Thread bora ya siku. Mastaajabu ya uumbaji na hili ndilo linalofanya uhai wa binadamu uzidi kuwa bora na kuwa kitu ambacho hakikutokea kibahatibahati tu.
 
Naomba nikusahihisha, mwanaume hatoi WATU na bado haijaqualify kuwa mbegu. Anachotoa ni 50% ya kile kinabhotengeneza mtoto if u like!

So hiyo manii yenye 0.5 au nusu mbegu 599 zinazokufa hazijawa mtu bila kukutana na kiyai cha mama kinachosubiri kurutubishwa kutengeneza mtoto!

Pointi yako ya how amazing ile mashindano ya kuogelea na hatimaye kispermatozoa kimoja kufanikiwa kurutubisha kijiovum, wanasayansi watatuambia ila l think ni jinsi ya kuhakikisha urutubishaji unatokea, kwani vingi vinakufa hata kabla ya kufikia kijiyai!
 
Mimi ni mmoja kati ya watu nisioamini kuwa kuzaliwa ni bahati,na pia naamini katika mahali kuna uongo mkubwa ni kwenye sayansi!
 
Mimi ni mmoja kati ya watu nisioamini kuwa kuzaliwa ni bahati,na pia naamini katika mahali kuna uongo mkubwa ni kwenye sayansi!

Bahati inayozungumziwa hapa ni ile kati ya mbegu milioni 600 ikaingia yako wewe, suala la sayansi kuwa ni uongo linategemea unafahamu mangapi yanafanyika kutokana hizi facts. umewahi sikia juu ya 'test tube babies'? na je unajua facts zinazotumia kutengeneza hawa watoto?
 
  • Thanks
Reactions: SMU
jukwaa hili linahitaji watu kama wewe tu! FIKRA ZINAZOVUKA MIPAKA....
 
Mkuu umewaza kwa undani sana, ila kuna mambo mengine yako kiimani zaidi ni gumu sana kuyapa maelezo ya kisayansi ya kutosha! Ni kama ilivyo kwa theory ya kuwa binadamu alitoka wapi kisayansi? kwa sokwe? Mbona sokwe wa siku hizi hawabadiliki kuwa binadamu!
By the way nimependa the way ulivyofikiri na kutoa mada yako.
 
Nimewaza haya nikiwa nje ya Dini kabisa. Hapa nilikuwa naliangalia jambo hili Kisayansi, kwa hiyo kama ukihusisha Dini yako na jambo hili, utatoka nje ya mada.

Nilikuwa najiuliza tu kwamba, sisi wote tulitoka kwa wazazi. Baba alitoa mbegu, ambazo kwa sehemu kubwa ni protini (chakula alacho). Kwa kufanya tendo la ndoa mara moja mwanamme hutoa cc 5 za manii (ujazo wa kijiko kimoja cha chai). Kila cc moja ina mbegu zipatazo milioni 120. Hivyo, cc 5 za manii, zina mbegu zipatazo milioni 600. Kati ya hizi, ni mbegu moja tu inayotakiwa kurutubisha yai ili azaliwe mtoto, ni ajabu eh!

Mbegu moja kati ya mbegu milioni 600. Ni uwiano mbaya sana kama siyo kituko. Yaani hii ni bahati sana, kati ya watu milioni 600 aliowatoa baba ukabahatika wewe peke yako. Mama naye alitoa yai. Kila mwezi hutoa yai moja ambalo likirutubishwa anazaliwa mtoto. Kila mwezi, mwanamke hutoa yai moja, kwa mwaka mmoja hutoa mayai 12. kati ya haya ni mangapi hurutubishwa? Kumbuka, mbegu na yai vilitokana na vyakula ambavyo vilioteshwa au kupandwa kwenye udongo wenye rutuba (mbolea) na maji. Maji na mbolea vilitoka wapi? Ni mzunguko usio na mwisho wala mwanzo……………..

Dah! nimekusoma dada
 
Back
Top Bottom