Titus Amigu: Kazi ya mwanaume ni kutafuta

EP cosmetics

JF-Expert Member
Oct 18, 2015
2,469
3,840
KAZI YA WANAUME – KUTAFUTA: Sehemu ya I

Wanasayansi wanasema na ndivyo ilivyokusudiwa na Mungu. Mwanaume Adamu aliwekwa bustanini Edeni ailime na kuitunza (Mwa 2:15). Hata yeye na mkewe Hawa walipochafua uhusiano wao na Mungu aliadhibiwa katika mstari huo huo wa kazi akiambiwa atakula kwa jasho lake hata siku atakaporudia ardhi ambamo kwamo alitwaliwa.

Imeandikwa ifuatavyo: “(Mungu) akamwambia Adamu, ‘Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale, ardhi imelaaniwa (maana yake imekorofishwa katika uhusiano wake na wewe mwanadamu) kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi’” (Mwa 3:17-19).

Mwanamke hakuadhibiwa katika mistari ya utafutaji isipokuwa katika mistari ya ofisi yake ya kuuzaa na kuutunza uhai. Ndipo mintarafu mwanamke tunasoma, “(Mungu) akamwambia mwanamke, ‘Hakika nitakuzidishia uchungu wako na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala’”(Mwa 3:16).

Maelfu ya Tofauti kati ya Wanaume na Wanawake
Kwa namna hii mwanaume ameumbiwa afanye kazi ngumu. Hapa Wamakonde wameshatangulia mbali kimawazo. Wao hujumlisha majukumu na nafasi ya utafutaji ya mwanaume kwa kukubali kwamba ni lazima mwanaume ataabike kwa kazi ngumu kusudi familia yake na jamii yake ikidhi mahitaji yake ya lazima wakisema, “Nnume alage” yaani “mwanaume lazima apate taabu kwa ajili ya kukidhi maisha yake binafsi, maisha ya familia yake na ya jamii yake kwa ujumla.

Kumbe tofauti na mwanamke aliyeumbwa, awe kwa namna ya pekee, mama na afisa wa uhai, mwanaume ameumbwa awe mtafutaji kusudi uhai upate kulishwa na kudumishwa kwa chakula, malazi na mavazi. Hapa ndipo tofauti za sifa na majukumu kati ya wanaume na wanamke zinapoanzia.
Sayansi inatuambia kati ya wanaume na wanawake kuna tofauti zipatazo 6,500. Tofauti hizi zinagawanyika katika mafungu matatu: tofauti za kisifa, tofauti za kitabia na tofauti za kimaumbile.

Je, nielezee zote? Hapana. Nakataa. Sitaki. Mimi si mtumwa wako. Hivi, kwa kukidhi hoja yangu ninayoijenga katika makala hii acha nizidokeze tofauti za kisifa tu.

Ni hivi, kwa vile Mungu anawapenda waja wake wote, wanaume na wanawake, amewapa sifa tofauti kusudi kila jinsia imudu majukumu yake. Sifa za wanaume ni kumi: 1) kutafuta mahitaji, 2) kupambana na kushindana, 3) nguvu nyingi, 4) kutumia akili, 5) kuamua haraka, 6) kubuni zana na mipango, 7) kujikwamua kwenye shida, 8) kujiamini na kutoogopa, 9) kuvutika na wanawake na 10) kuleta furaha.

Kifupi, hizi ndizo sifa 10 za mwanaume naye anasimama kama mwindaji (hunter). Ushahidi wa kwamba mwanaume ameandikiwa moyoni mwake na ameumbwa na Mungu kwa upande wa uwindaji, ni kwamba tangu utotoni yeye huanza kucheza na vitu vya kutafutia mahitaji: manati, ndoana, visu, bunduki na kadhalika.

Kwa upande wao, sifa za wanawake ni kumi na tano: 1) kuupenda, kuuzaa na kuutunza uhai, 2) upole na amani, 3) uvumilivu wa malezi, 4) kuona shida mapema na kusaidia, 5) kufariji na kutuliza, 6) kutamani kupendwa, 7) kusikiliza, 8) kusimulia, 9) kuamini kwa nguvu, 10) kupenda kwa nguvu, 11) kulinganisha mambo katika uzuri, 12) bidii ya kazi nyingi ndogondogo na kusimamia mambo, 13) kuwategemea wengine, 14) kuwateka wengine na 15) kuwastaajabia wengine.

Hizi ndizo sifa 15 za mwanamke naye anasimama kama mtunza kiota (nest keeper). Ushahidi wa kwamba mwanamke ameandikiwa moyoni mwake na ameumbwa na Mungu kwa upande wa utunzaji kiota, ni kwamba tangu utotoni yeye huanza kucheza na vitu vya kulelea uhai: midoli (wanasesere), maji, vyungu, vikombe na kadhalika.

Mungu Hajawahi Kumwonea Mtu
Kwa nini Mungu amewapanga wanadamu kwa namna hii? Jibu ni rahisi: Mungu si mwonevu. Hata siku moja yeye hataki kuwaonea waja wake. Hakika Mungu hajawahi kumtwisha mtu yeyote mzigo wowote pasipo kumwandalia mabega. Ndiyo maana yeye hajawahi kumuumba ndege na kumwamuru aruke angani pasipo kumpa mabawa wala hajawahi kumuumba samaki aogelee majini pasipo kumpa mapezi.

Mwanaume ni Kiongozi wa Maendeleo
Tukubali, tusikubali ipo hivyo na itabaki hivyo. Mungu si mpumbavu kuwatofautisha wanaume na wanawake katika vipengele 6,500. Nisikilize wewe! Kwa sifa yake ya utafutaji mwanaume hatagemewi kupoa, la sivyo atakuwa Marioo. Hali kadhalika kwa sifa yake ya kupambana na kushindana. Kwa sifa yake ya nguvu nyingi, kwa vile alivyo na oksijeni nyingi mwilini mwake, mwanaume hategemewi kulegea legea. Unyoronyoro si uanaume. Badala yake mwanaume anatagemewa afanye kazi ngumu, kama vile za kujenga nyumba kubwa na imara, kulima mashamba makubwa, kuchimba visima virefu, kupasua mbao, kujenga barabara nzuri, kutengeneza samani imara kusudi mwanadamu akae na alale pazuri na kadhalika.

Kwa sifa yake ya kubuni zana na kupanga mipango, mwanaume anategemewa atengeneze zana za kurahisishia kazi na kupanga mipango ya miaka mingi ya usoni. Hapa ndipo wanaume wenzetu wa Ulaya na Asia walipobuni risasi, bunduki na mabomu wakati sisi tukibaki na mikuki, pinde na mishale. Hapa ndipo wenzetu walipobuni baiskeli, pikipiki, treni na ndege, sisi tukibaki kutembea kwa miguu na kujibembeleza kwa hadithi za kuruka kwa nyungo, pembe, mbweha na fisi.

Kwa sifa yake ya kuamua haraka na kujikwamua kwenye matatizo, mwanaume anategemewa kuwa mtatuaji wa shida au matatizo ya jamii kusudi jamii isilimatie kwenye matatizo. Hapa ndipo wanaume wenzetu walipoamua kutufanyiza kazi, kutengeneza matrekta na mitambo na kujikita katika biashara kubwa kubwa, sisi tukibaki na hadithi za kuiba mazao kwa ushirikina na hadithi za chumaulete. Kwa sifa yake ya kujiamini na kutoogopa, mwanaume anategemewa kuondoa woga katika jamii. Hapa ndipo wanaume wenzetu walipoamua kuyavamia mabara ya Afrika, Amerika na Australia pasipo kutuogopa wanaume wenzao. Huko Amerika Wahindi wekundu “wakahanithiwa” kama sisi na huko Australia Aborijini “wakahanithiwa” pia.

Aghalabu, kwa sifa yake ya kuleta furaha, mwanaume anategemewa kuwa chombo cha kukabiliana na huzuni. Hadi hapa, kwa kujumlisha, shida, matatizo, woga na huzuni ni vitu vibaya sana kwa vile huharibu siha, kuzeesha watu mapema na hatimaye kuleta vifo pasipo adabu. Soma YbS 30:21-25. Kama unanibisha mimi basi waulize wanasaikolojia na madaktari wa wanadamu.

Wanaume Wengine Wanajitambua Isipokuwa Waafrika
Wanaume wengine, isipokuwa wa Waafrika, wanajitambua sana ndiyo maana tangu mwanzo hadi leo wamekuwa watafutaji wa mahitaji yao binafsi na ya jamii zao. Wao ni wachakarikaji. Wao ni wawindaji kweli kweli. Wanawinda popote. Ndiyo maana wanawinda hata barani mwetu. Wakiwa wanajitambua hivyo, waligundua tangu mapema kwamba wanaume wa Afrika walikuwa hawajitambui. Waligundua sisi hatuko mbali sana na wanawake. Ndipo wanaume wa mabara mengine wamekuwa “wakituhanithi” wanaume wenzao hapa Afrika. Kumbe sasa uelewe kwa nini historia ya dunia ilikwenda na inakwenda nitakavyokusimulia. Ngoja nikutaliishe katika mambo matano: kuvumbuliwa mabara, biashara ya utumwa, kugawanywa kwa bara la Afrika, ukoloni mkongwe na ukoloni mambo leo.

1. Kuvumbuliwa Mabara
Katika karne ya 15, wanaume wa Ulaya walikwenda safari za mbali na za hatari kutafuta mahitaji kwa ajili ya wake na watoto wao. Walitoka kwenda kuwinda. Hapa wakumbuke akina Christopher Columbus (Mwitaliano wa Genoa 1451 - 1506) na Vasco da Gama (Mreno 1469-1524) waliosafiri mbali na bara lao la Ulaya. Columbus alikwenda bara la Amerika kwa kutumia marekebu yake Santa Maria. Vasco da Gama alikwenda India kutafuta viungo akilizunguka bara letu la Afrika. Wakati hao wakiwinda hivyo, sisi wanaume wa Afrika tulikuwa tunapiga usingizi wa pono. Sana sana, sisi tulikuwa tunawinda kereng’ende, sungura, swala, nyati na ndovu tu. Nakuambia, inayoitwa kazi ya uvumbuzi wa nchi mpya ilikuwa kazi za wanaume (wawindaji) wenzetu, wanaume wa Afrika tukiwa tumelala tu.

Wanawake Wazungu waliambiwa na waume zao watulie majumbani wawalee watoto. Basi, wanaume wakajitosa katika “kulaga” kama Wamakonde wanavyosema. Si haba wakayapata mabara ya Afrika, Amerika ya Kusini na Amerika ya Kaskazini kama mashamba ya bibi. Haya ni mabara waliyoyang’ang’ania kama kupe kwenye shingo za kondoo.

2. Biashara ya Utumwa
Kwa kuwa sisi wanaume wa Afrika tulikuwa hatujitambui kuwa tuna nguvu, wakaja Waarabu na Wazungu kutukamata utumwa, wapate kuzitumia nguvu zetu “kwa che.” Walitufuma wanaume wenzao, na wake zetu na watoto wetu tukiwa na misuli mikubwa lakini pasipo kujitambua. Tukakamtwa na kuuzwa kwenye minada kama wauzwavyo mbuzi, kondoo na ng’ombe. Tukanunulika kwa bei za kutupa kabisa.

Tusisahau, biashara ya kutuuza Waafrika ilidumu karibu miaka 400 (tangu 1526 -1867). Waarabu walitukamata na kutuuza Waafrika tusiopungua milioni 18. Je, humkumbuki mwanaume mmoja aliyeitwa Hamad ibn Muhammad ibn Jum’ah ibn Rajab ibn Muhammad ibn Said al Murjabi (maarufu Tippu Tib) aliyekuwa anawakamata watumwa Kongo na Wanyamwezi wa Tabora na kuwaswaga hadi kuwauza huko Bagamoyo? Mkumbuke basi walau machozi yakikulengalenga. Eti wanaume wenzetu walishindwa kupambana naye.

Baadaye Wazungu (hususan Wareno, Wahispania, Wadachi na Waingereza) wakatukamata na kutuuza huko Amerika ya Kusini na Kaskazini Waafrika tusiopungua milioni 12.5. Inasikitisha sana, katika kutusafirisha tulikufa Waafrika tusiopungua milioni 1.8. Mizigo ya watumwa wapya ilikuwa inafikishwa kwanza huko Rio de Janeiro (Brazili). Hapo ndipo Wazungu walipokuwa wanakuja kutununua kwa jumla au kwa reja reja. Biashara ya utumwa ilikuwa biashara yenye kulipa na kutajirisha sana. Laiti ningelikuwapo enzi hizo na mimi ningeliwauza Waafrika wenzangu kuwakomesha ulofa wao. Hapa niwieni radhi.

Hebu niendelee kusema. Sisi tulikuwa bidhaa kama mbuzi, kondoo, ng’ombe, farasi na punda tu. Ukitaka kujua kwamba, huko Marekani, Wazungu walikuwa wanataka nguvu zetu tu, mkunbuke mtumwa mmoja aliyeitwa Pata Seca. Mtumwa huyu aliyekuwa baunsa mwenye nguvu na umbo kubwa la miraba minne na kimo cha mita 2.14 alikuwa akitunzwa na kulishwa kwa kazi moja tu ya kuwabebesha mimba watumwa wanawake waliokuwa wanaletwa kwake na mabwana zao “kupandishwa” kama vile watu wanavyokwenda kuwapandisha ng’ombe wao majike kwa dume fulani la mbegu.

Pata Seca alikuwa dume la mbegu mwanadamu. Historia inasema, kwa kazi hiyo ya “kuwapanda” watumwa wanawake aliweza kuzaa watoto wanaokadiriwa kutopungua 200. Ndiyo kisa ukiwatazama Wamarekani weusi na watu wengine weusi huko Amerika ya Kusini na Amerika ya Kaskazini wanafanana fanana kwa sababu babu yao ni mmoja, huyo Pata Seca.

3. Kugawanywa kwa Bara la Afrika
Baada ya utumwa, wanaume Wazungu waligawana bara letu kwa rula katika mkutano wao wa miezi mitatu kule mjini Berlin, Ujerumanni. Hapo mwanzoni bara la Afrika lilikuwa limevamiwa na Wazungu pasipo utaratibu. Wanaume Wazungu wakaketi kitako kuweka utaratibu wa kisheria. Ndipo wanaume Wazungu walikusanyika hapo 15.11. 1884 kuanza mkutano wa kuratibu nidhamu ya kulichukua bara letu. Baada ya kughairisha kidogo hapo katikati, wanaume Wazungu walimaliza mkutano wao 25.2.1885.

Kifupi, mkutano huu uliamua kisheria kwamba Afrika inaweza kuchukuliwa na kukaliwa na Wazungu wowote wanaoweza kufanya hivyo. Wakati wote huo sisi wanaume wa Afrika hatukuwa na habari. Yaani, tulikuwa kama ng’ombe wanaopangiwa kutolewa kama mahari wasivyokuwa na habari ya mpango huo wa wanadamu. Mkutano huu uliitishwa na Kansela wa Ujerumani, Otto von Bismarck, kwa maagizo ya Mfalme Leopold II wa Ubelgiji.

Tukijikumbusha, wanaume Wazungu, akina David Livingstone (1813-1873), Henry Morton Stanley (1841-1904) John Hanning Speke (1827-1864), Richard Francis Burton (1821-1890) walishafika kutuchungulia kama Waafrika tulikuwa tumelala. Wanaume hawa walivinjari kila kona ya Afrika kututazama kwa karibu. Ripoti zao ziliwaambia Wazungu kwamba wanaume wa Afrika tulikuwa tumelala wakati huo huo tukiwa tumekalia rasilmali nyingi sana. Sikiliza sasa. Eti walipopita huko na huko waliokota milima, maziwa na mito yetu.

Ndiyo waliokota. Ndiyo maana waliweza kutoa vitu hivyo kama zawadi kwa viongozi wao. Kwa mfano wakipookota Ziwa Nyanza, walilitoa kama zawadi kwa Malkia Victoria (1819 – 1901). Ndiyo kisa Ziwa Nyanza linaitwa Ziwa Viktoria hadi leo. Wanaume wa Kisukuma, Kiluo, Kikuria, Kizanaki, Kiruli, Kihaya, Kihangaza, Kinyambo, Kisubi, Kikerewe, Kijita, Kikara, Kizinza wala hawakuwa na habari kwamba ziwa lao limeokotwa na Wazungu.


Mzee wenu Pd. Titus Amigu
(Itaendelea)
 
KAZI YA WANAUME – KUTAFUTA : Sehemu ya II (inaendelea)

4. Ukoloni Mkongwe
Baada ya kugawana bara letu, ukoloni mkongwe ulianzishwa rasmi. Wanaume wa nchi saba za Ulaya walifika kututawala Waafrika. Walifika wanaume wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji, Hispania, Ureno na Italia. Wanaume hao walifaulu “kutuhanithi” wanaume wenzao. Wengine walipata ardhi yetu kwa shuka kama akina Mangungo wa Msovero, Tanganyika, alivyotoa ardhi. Machifu wetu wengine walitoa ardhi kama bei za vioo vya kujitazamia walivyopewa na Wazungu. Wengine walitoa dhahabu kwa malipo ya sahani, vikombe na sufuria kama mfalme wa Ashanti, Ghana. Wengine walikodisha ardhi kwa vijipesa vichache tu, kama Lobengula alivyokodisha ardhi yote ya Zimbabwe na Zambia (siku hizi), kwa paundi za Uingereza mia moja tu.

Nawakumbusheni. Wanaume wenzetu hao walikuja kuwinda barani Afrika kwa ajili ya jamii zao Ulaya. Hapa napigia mstari. Wakoloni vinara wote walikuwa wanaume si wanawake. Ndipo tunapowasikia akina Karl Peters na wanaume wenzao walivyokuja kuchukua ardhi yetu. Wakati huo wanawake wao walibakizwa majumbani kwao wasubiri nyara watakazoleta waume zao.
Kama unanibisha kwamba haya yote hayakuwa kazi za wanaume, nitajie wanawake walau watatu waliohusika moja kwa moja katika kutukamata utumwa, kupeleleza na kutwaa nchi zetu kama makoloni. Najua huwezi kunitajia wowote maana hizo zote zilikuwa kazi za wanaume wenzetu, wawindaji.

Wanaume wenzetu wachache walishtukia mchezo mbaya wa Wazungu kuja kuwinda barani mwetu. Hawa waliamua kuchukua silaha na kuwapiga Wazungu. Hapa tuwakumbuke akina Al Bashir ibn Salim al Harthi (a.k.a. Abushiri), Chifu Mkwawa, Kinjikitile Ngwale na Wangoni wa Songea. Hawa walitualika wanaume wenzao tuwafukuze Wazungu kwa vita. Kwa bahati mbaya silaha zetu zilipwaya mbele ya silaha za wanaume wenzetu. Wao walikuwa wameshagundua silaha za maana zaidi kuliko zetu. Wao walikuwa na risasi, bunduki na mabomu sisi tungali bado na mikuki, pinde na mishale. Vibaya zaidi, wengine wetu walitumaini vitu dhalili sana, kwa mfano, eti Kinjikitile Ngwale aliamini kwamba maji yangeliyeyusha risasi za moto za Mzungu kwa kusema tu “Maji, maji, maji.”

Kwa kuwa kiteknolojia tulikuwa chini ya wanaume wenzetu, tukafeli sana. Akina Al Bashir ibn Salim al Harthi (a.k.a. Abushiri) walifeli miaka ile ya 1888 - 1889. Akina Chifu Mkwawa, miaka ile 1891-1898, walifeli na Wangoni wapiganaji wa vita vya Majimaji, miaka ile ya 1905-1907, walifeli pia. Hata kule Kenya vipiganaji wa vita vya Mau Mau (1953-1960) walifeli. Ndipo wanaume wa Ulaya wakatutawala kwa raha zao. Makoloni yakageuka vilivyo mashamba ya bibi.

5. Ukoloni Mamboleo
Nchi zetu tulizikomboa kwa namna mbili. Wengine walipata uhuru kwa mazungumzo na wengine kwa mtutu wa bunduki. Wanaume wa Angola, Msumbiji, Namibia, Zimbabwe walivurumisha vita vya ukombozi, wakoloni wakaachia. Hapa ndipo walipoingia wanaume wenzetu, akina Augustino Neto, Samora Machel, Sam Nujoma, Robert Mugabe, Jomo Kenyatta, Julius Nyerere, Kwame Nkurumah, Kenneth Kaunda na Nelson Mandela. Lakini kwa uhuru huu si kwamba wanaume wa Ulaya wameacha kuwinda kwao. Tena sasa si wanaume wale wa Ulaya peke yao wanaowinda barani mwetu. Wamejiunga nao Wachina, Wahindi, Waturuki, Wathailandi, Wabrazili na Warusi.

Aibu tupu. “Kuhanithiwa” kwetu wanaume wa Afrika kunaendelea kwa nguvu lakini kwa kimya kimya. Siku hizi, wanaume wenzetu “wanatunyenga” wanaume wa Afrika, wanawake wetu pamoja na watoto wetu kwa misaada ya kadiri tu. Wanabeba vikubwa vyetu na kuturudishia kiduchu tu. Siku hizi ukoloni wao unaitwa wa kisasa. Unaitwa mamboleo. Taasisi za fedha ulimwenguni zinakadiria Afrika inaibiwa kati ya $ 60 – 88.7 bilioni sawa na 3.7% ya GDP ya Afrika kila mwaka na kinachoingia kama misaada, kwa mwaka, ni kati ya $ 49 – 58 bilioni. Piga hesabu hapa.
Kwa ukoloni mamboleo, wanaume wenzetu wanajipatia kwa bei ya kutupa madini na rasilimali zetu. Vitu hivyo vinachukuliwa kirahisi mno. Zamani wanaume Wazungu walikuja kutafuta mali zetu. Kinyume chake tumerahisisha kunyonywa kwetu kwa kiasi kikubwa. Hatupingi chochote. Siku hizi tunawaendea wenyewe Wazungu, Wamarekani, Wachina na kadhalika na ramani zinazoonesha vizuri madini na rasilimali zetu zipo wapo kuwaalika kusudi waje wachukue wanachotaka kwa masharti nafuu. Eti tunaita biashara ya soko huria na uwekezaji.
Yaani sasa tumewafungulia wenyewe milango yote wakitaka wachukue ardhi yetu. Wakitaka wachukue dhahabu yetu. Wakitaka wachukue almasi zetu. Wakitaka wachukue gesi yetu. Wakitaka wachukue uranium yetu. Wakitaka wachukue nickel yetu na kadhalika. Wamakonde wanaita kinachoendelea sasa “liteka mwene”, yaani mwendo wa kila mtu kujichotea pombe kiasi anachotaka. Ukweli ni kwamba nchi zetu sasa zinashindana kuweka masharti nafuu na mazingira wezeshi ili wageni waje wachukue wanavyotaka. Aibu hii. Uanaume wetu uko wapi? Tutawapata wapi tena akina Mkwawa na akina Jomo Kenyatta watupiganie walau Mau Mau? Vita vya Mau Mau viliwachachafya Waingereza huko Kenya tangu mwaka 1953 hadi mwaka 1960 viliposhindwa vibaya.

Tusikubali Wanaume ni Wanaume Tu
Kutokana na haya unaweza kujua kwa nini hakuna mambo ya 50 – 50 huko Marekani wala Ulaya wala Asia. Je, ulisikia habari za 50 – 50 Marekani licha ya kupata uhuru wao tarehe 4.7. 1776? Je, umewahi kusikia habari hiyo Uingereza? Umewahi kusikia habari hiyo Ujerumani? Umewahi kusikia habari hiyo Ufaransa, Italia, Ureno au Urusi? Mtego huo, Waafrika wenzangu! Wanaume wenzetu wanatutega waone mambo yatakavyotuendea kombo tutakapokubali wanaume kulinganishwa na wanawake. Kwa hakika, wanaume wenzetu wanajua wanaume na wanawake wana sifa tofauti 6,500: wanaume ni wawindaji wakati wanawake ni watunza viota na kwa namna hiyo hawawezi kulinganishwa hasa katika vyombo vya maamuzi na upangaji mipango. Wanaume ni wapangaji na wanawake ni wasimamiaji.
Ndivyo ilivyo na itabaki hivi milele, kwa sababu ni mpango wa Mungu Muumbaji. Narudia. Hiyo habari ya 50 – 50 ni mtego kwetu sisi tusiojitambua. Wanaume wenzetu wanataka kuona tutakavyoanguka kwa ujinga wa kutaka wanaume na wanawake tujisikie tupo sawa katika michakato ya maendeleo. Basi, hapa, akili ya kuambiwa afadhali tuchanganye na yetu mapema kabisa.

Wanaume wa Afrika Siku Hizi Je?
Ni aibu tu. Aibu inaendelea mchana kweupe. Wanaume wa Afrika tunaubananga uanaume wetu. Inaonekana kana kwamba hatuna tena zile sifa kumi za wanaume. Ndiyo kisa tunakubali kulinganishwa na akinamama. Ndiyo maana tunakubali 50-50 ambayo hakuna mahali pengine popote duniani wanaume wenzetu walipokubali. Kwa kisa hiki cha ulofa wetu, siku si nyingi tutafikia mahali pa kuona mwanaume kuolewa ni sawa tu. Siku si nyingi tutafikia pahala pa kuona mwanamke kutuoa ni sawa tu. Na nadhani pale pa kudhani mwanamke anaweza kufanya shughuli zetu tumeshapafikia. Pale mahali pa kuona mwanamke anaweza kuchukua majukumu yetu na yeye kututafutia mahitaji tumejapafikia. Tumeshapafikia maana ingelikuwa hatujapafikia wasingelikuwapo akina Marioo ambao kwa maisha yao wanawategemea mashangingi. Aidha wasingelikuwapo wanaume wa kuolewa.

Katika suala hili la ndoa za watu wa jinsia moja ninaona wanaume weusi wakiolewa na wanaume wa Kizungu. Wala sijapata kuona mwanaume mweusi akimwoa mwanaume Mzungu. Je, wewe umewahi kuona? Sasa maana yake nini hata katika kiroja hiki? Maana yake ni kwamba sisi ndio malofa katika kila hali. Asalale! Lakini hii ni aibu sana.
Sasa hapa hapa ongezea upujufu wa siku hizi ambapo vijana tele wanageuka “akina Marioo.” Vijana wa kiume wanakuwa weroro, wanavishwa, kulishwa na kutunzwa na akina mama. Hawa wanavaa heleni, kusuka nywele na kujipodoa kama akina Asumpta, Fatuma, Magdalena na Habiba. Kwa haya tunaelekea wapi?

Hatima
Sasa tuhitimishe mambo. Kihistoria tunakumbuka jinsi tulivyokamatwa utumwa na kuuzwa na wanaume wenzetu. Tunakumbuka tena Wazungu walivyokuja kututawala katika ukoloni mkongwe. Aidha tunakumbuka jinsi tunavyoendelea kutawaliwa katika mfumo mpya wa ukoloni mamboleo. Kutokana na ukoloni mambo leo, sisi wanaume wa Afrika, na wake zetu na watoto wetu, tumeshindwa kutafuta, badala yake tumekubalishwa mitumba: magari, pikipiki, nguo: suruali, mashati, sketi, blauzi, sidiria, vyupi, viatu, soksi na kadhalika. Uanaume wa kufanya mambo kwa nguvu hatuna tena. Uanaume wa kubuni zana na mipango hatuna tena. Sisi sasa ni wategemezi kama wanawake na watoto wetu tu.

Lakini kinachonikera zaidi ni kwamba wanaume wa Afrika tumeanza kugeukia kulia kama suluhu ya matatizo. Kukemea uchawi, laana, mizimu, majini ni dawa gani? Eti wanaume wazima, mapadre na wanaume waliooa kabisa, tunajiunga kwenye vikundi vya kulia, kwa mfano, Karismatiki tupate kulia hadharani sisi na wake zetu na watoto wetu. Tunalia eti Mungu atusaidie, badala ya sisi kutumia uanaume wetu, na nguvu zetu za musuli na akili kupanga mambo na kufanya kazi. Eti sisi tunadhani suluhu ya matatizo yetu ni kulia na kufanya mikesha isiyokwisha. Tunajenga mustakabali gani kwa watoto wetu wa kiume hapo? Huko siyo kuwafanya walemavu maradufu yetu? Wanaume mbona tunawalemaza warithi wetu? Watoto wetu wa kiume watawezaje kuwa wanaume, waume za watu na baba za watoto wao wenyewe? Afrika vipi? Tunajipeleka wapi wenyewe? Hapo tukiwaona wanapenda kubadili jinsia zao wawe wanawake kabisa tutawashangaa?

Kwa namna hii, kadiri yangu, mustakabali wa bara letu una giza. Kama wanaume wa Afrika hatutajitambua na kuanza kushindana na wanaume wa mabara mengine hakika kabisa tutatawaliwa milele. Tunawasaliti wake zetu na watoto wetu katika kuwaamini wawezekezaji. Hao kamwe hawatakuja kutuletea maendeleo. Wawekezaji ni wawindaji. Ni wanaume. Wanakuja kuwinda katika nchi zetu na bara letu. Wanaume wa Afrika tugutukeni!

Mzee wenu Pd. Titus Amigu

C&P
 
Hakika ni andiko zuri sana,padre kaandika maneno kuntu.Wale wavivu wa kusoma,jitahidini kusoma,ni madini matupu,huyo padre kayaandika.Katusihi tuamke,hasa sisi wanaume.
 
KAZI YA WANAUME – KUTAFUTA : Sehemu ya II (inaendelea)

4. Ukoloni Mkongwe
Baada ya kugawana bara letu, ukoloni mkongwe ulianzishwa rasmi. Wanaume wa nchi saba za Ulaya walifika kututawala Waafrika. Walifika wanaume wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji, Hispania, Ureno na Italia. Wanaume hao walifaulu “kutuhanithi” wanaume wenzao. Wengine walipata ardhi yetu kwa shuka kama akina Mangungo wa Msovero, Tanganyika, alivyotoa ardhi. Machifu wetu wengine walitoa ardhi kama bei za vioo vya kujitazamia walivyopewa na Wazungu. Wengine walitoa dhahabu kwa malipo ya sahani, vikombe na sufuria kama mfalme wa Ashanti, Ghana. Wengine walikodisha ardhi kwa vijipesa vichache tu, kama Lobengula alivyokodisha ardhi yote ya Zimbabwe na Zambia (siku hizi), kwa paundi za Uingereza mia moja tu.

Nawakumbusheni. Wanaume wenzetu hao walikuja kuwinda barani Afrika kwa ajili ya jamii zao Ulaya. Hapa napigia mstari. Wakoloni vinara wote walikuwa wanaume si wanawake. Ndipo tunapowasikia akina Karl Peters na wanaume wenzao walivyokuja kuchukua ardhi yetu. Wakati huo wanawake wao walibakizwa majumbani kwao wasubiri nyara watakazoleta waume zao.
Kama unanibisha kwamba haya yote hayakuwa kazi za wanaume, nitajie wanawake walau watatu waliohusika moja kwa moja katika kutukamata utumwa, kupeleleza na kutwaa nchi zetu kama makoloni. Najua huwezi kunitajia wowote maana hizo zote zilikuwa kazi za wanaume wenzetu, wawindaji.

Wanaume wenzetu wachache walishtukia mchezo mbaya wa Wazungu kuja kuwinda barani mwetu. Hawa waliamua kuchukua silaha na kuwapiga Wazungu. Hapa tuwakumbuke akina Al Bashir ibn Salim al Harthi (a.k.a. Abushiri), Chifu Mkwawa, Kinjikitile Ngwale na Wangoni wa Songea. Hawa walitualika wanaume wenzao tuwafukuze Wazungu kwa vita. Kwa bahati mbaya silaha zetu zilipwaya mbele ya silaha za wanaume wenzetu. Wao walikuwa wameshagundua silaha za maana zaidi kuliko zetu. Wao walikuwa na risasi, bunduki na mabomu sisi tungali bado na mikuki, pinde na mishale. Vibaya zaidi, wengine wetu walitumaini vitu dhalili sana, kwa mfano, eti Kinjikitile Ngwale aliamini kwamba maji yangeliyeyusha risasi za moto za Mzungu kwa kusema tu “Maji, maji, maji.”

Kwa kuwa kiteknolojia tulikuwa chini ya wanaume wenzetu, tukafeli sana. Akina Al Bashir ibn Salim al Harthi (a.k.a. Abushiri) walifeli miaka ile ya 1888 - 1889. Akina Chifu Mkwawa, miaka ile 1891-1898, walifeli na Wangoni wapiganaji wa vita vya Majimaji, miaka ile ya 1905-1907, walifeli pia. Hata kule Kenya vipiganaji wa vita vya Mau Mau (1953-1960) walifeli. Ndipo wanaume wa Ulaya wakatutawala kwa raha zao. Makoloni yakageuka vilivyo mashamba ya bibi.

5. Ukoloni Mamboleo
Nchi zetu tulizikomboa kwa namna mbili. Wengine walipata uhuru kwa mazungumzo na wengine kwa mtutu wa bunduki. Wanaume wa Angola, Msumbiji, Namibia, Zimbabwe walivurumisha vita vya ukombozi, wakoloni wakaachia. Hapa ndipo walipoingia wanaume wenzetu, akina Augustino Neto, Samora Machel, Sam Nujoma, Robert Mugabe, Jomo Kenyatta, Julius Nyerere, Kwame Nkurumah, Kenneth Kaunda na Nelson Mandela. Lakini kwa uhuru huu si kwamba wanaume wa Ulaya wameacha kuwinda kwao. Tena sasa si wanaume wale wa Ulaya peke yao wanaowinda barani mwetu. Wamejiunga nao Wachina, Wahindi, Waturuki, Wathailandi, Wabrazili na Warusi.

Aibu tupu. “Kuhanithiwa” kwetu wanaume wa Afrika kunaendelea kwa nguvu lakini kwa kimya kimya. Siku hizi, wanaume wenzetu “wanatunyenga” wanaume wa Afrika, wanawake wetu pamoja na watoto wetu kwa misaada ya kadiri tu. Wanabeba vikubwa vyetu na kuturudishia kiduchu tu. Siku hizi ukoloni wao unaitwa wa kisasa. Unaitwa mamboleo. Taasisi za fedha ulimwenguni zinakadiria Afrika inaibiwa kati ya $ 60 – 88.7 bilioni sawa na 3.7% ya GDP ya Afrika kila mwaka na kinachoingia kama misaada, kwa mwaka, ni kati ya $ 49 – 58 bilioni. Piga hesabu hapa.
Kwa ukoloni mamboleo, wanaume wenzetu wanajipatia kwa bei ya kutupa madini na rasilimali zetu. Vitu hivyo vinachukuliwa kirahisi mno. Zamani wanaume Wazungu walikuja kutafuta mali zetu. Kinyume chake tumerahisisha kunyonywa kwetu kwa kiasi kikubwa. Hatupingi chochote. Siku hizi tunawaendea wenyewe Wazungu, Wamarekani, Wachina na kadhalika na ramani zinazoonesha vizuri madini na rasilimali zetu zipo wapo kuwaalika kusudi waje wachukue wanachotaka kwa masharti nafuu. Eti tunaita biashara ya soko huria na uwekezaji.
Yaani sasa tumewafungulia wenyewe milango yote wakitaka wachukue ardhi yetu. Wakitaka wachukue dhahabu yetu. Wakitaka wachukue almasi zetu. Wakitaka wachukue gesi yetu. Wakitaka wachukue uranium yetu. Wakitaka wachukue nickel yetu na kadhalika. Wamakonde wanaita kinachoendelea sasa “liteka mwene”, yaani mwendo wa kila mtu kujichotea pombe kiasi anachotaka. Ukweli ni kwamba nchi zetu sasa zinashindana kuweka masharti nafuu na mazingira wezeshi ili wageni waje wachukue wanavyotaka. Aibu hii. Uanaume wetu uko wapi? Tutawapata wapi tena akina Mkwawa na akina Jomo Kenyatta watupiganie walau Mau Mau? Vita vya Mau Mau viliwachachafya Waingereza huko Kenya tangu mwaka 1953 hadi mwaka 1960 viliposhindwa vibaya.

Tusikubali Wanaume ni Wanaume Tu
Kutokana na haya unaweza kujua kwa nini hakuna mambo ya 50 – 50 huko Marekani wala Ulaya wala Asia. Je, ulisikia habari za 50 – 50 Marekani licha ya kupata uhuru wao tarehe 4.7. 1776? Je, umewahi kusikia habari hiyo Uingereza? Umewahi kusikia habari hiyo Ujerumani? Umewahi kusikia habari hiyo Ufaransa, Italia, Ureno au Urusi? Mtego huo, Waafrika wenzangu! Wanaume wenzetu wanatutega waone mambo yatakavyotuendea kombo tutakapokubali wanaume kulinganishwa na wanawake. Kwa hakika, wanaume wenzetu wanajua wanaume na wanawake wana sifa tofauti 6,500: wanaume ni wawindaji wakati wanawake ni watunza viota na kwa namna hiyo hawawezi kulinganishwa hasa katika vyombo vya maamuzi na upangaji mipango. Wanaume ni wapangaji na wanawake ni wasimamiaji.
Ndivyo ilivyo na itabaki hivi milele, kwa sababu ni mpango wa Mungu Muumbaji. Narudia. Hiyo habari ya 50 – 50 ni mtego kwetu sisi tusiojitambua. Wanaume wenzetu wanataka kuona tutakavyoanguka kwa ujinga wa kutaka wanaume na wanawake tujisikie tupo sawa katika michakato ya maendeleo. Basi, hapa, akili ya kuambiwa afadhali tuchanganye na yetu mapema kabisa.

Wanaume wa Afrika Siku Hizi Je?
Ni aibu tu. Aibu inaendelea mchana kweupe. Wanaume wa Afrika tunaubananga uanaume wetu. Inaonekana kana kwamba hatuna tena zile sifa kumi za wanaume. Ndiyo kisa tunakubali kulinganishwa na akinamama. Ndiyo maana tunakubali 50-50 ambayo hakuna mahali pengine popote duniani wanaume wenzetu walipokubali. Kwa kisa hiki cha ulofa wetu, siku si nyingi tutafikia mahali pa kuona mwanaume kuolewa ni sawa tu. Siku si nyingi tutafikia pahala pa kuona mwanamke kutuoa ni sawa tu. Na nadhani pale pa kudhani mwanamke anaweza kufanya shughuli zetu tumeshapafikia. Pale mahali pa kuona mwanamke anaweza kuchukua majukumu yetu na yeye kututafutia mahitaji tumejapafikia. Tumeshapafikia maana ingelikuwa hatujapafikia wasingelikuwapo akina Marioo ambao kwa maisha yao wanawategemea mashangingi. Aidha wasingelikuwapo wanaume wa kuolewa.

Katika suala hili la ndoa za watu wa jinsia moja ninaona wanaume weusi wakiolewa na wanaume wa Kizungu. Wala sijapata kuona mwanaume mweusi akimwoa mwanaume Mzungu. Je, wewe umewahi kuona? Sasa maana yake nini hata katika kiroja hiki? Maana yake ni kwamba sisi ndio malofa katika kila hali. Asalale! Lakini hii ni aibu sana.
Sasa hapa hapa ongezea upujufu wa siku hizi ambapo vijana tele wanageuka “akina Marioo.” Vijana wa kiume wanakuwa weroro, wanavishwa, kulishwa na kutunzwa na akina mama. Hawa wanavaa heleni, kusuka nywele na kujipodoa kama akina Asumpta, Fatuma, Magdalena na Habiba. Kwa haya tunaelekea wapi?

Hatima
Sasa tuhitimishe mambo. Kihistoria tunakumbuka jinsi tulivyokamatwa utumwa na kuuzwa na wanaume wenzetu. Tunakumbuka tena Wazungu walivyokuja kututawala katika ukoloni mkongwe. Aidha tunakumbuka jinsi tunavyoendelea kutawaliwa katika mfumo mpya wa ukoloni mamboleo. Kutokana na ukoloni mambo leo, sisi wanaume wa Afrika, na wake zetu na watoto wetu, tumeshindwa kutafuta, badala yake tumekubalishwa mitumba: magari, pikipiki, nguo: suruali, mashati, sketi, blauzi, sidiria, vyupi, viatu, soksi na kadhalika. Uanaume wa kufanya mambo kwa nguvu hatuna tena. Uanaume wa kubuni zana na mipango hatuna tena. Sisi sasa ni wategemezi kama wanawake na watoto wetu tu.

Lakini kinachonikera zaidi ni kwamba wanaume wa Afrika tumeanza kugeukia kulia kama suluhu ya matatizo. Kukemea uchawi, laana, mizimu, majini ni dawa gani? Eti wanaume wazima, mapadre na wanaume waliooa kabisa, tunajiunga kwenye vikundi vya kulia, kwa mfano, Karismatiki tupate kulia hadharani sisi na wake zetu na watoto wetu. Tunalia eti Mungu atusaidie, badala ya sisi kutumia uanaume wetu, na nguvu zetu za musuli na akili kupanga mambo na kufanya kazi. Eti sisi tunadhani suluhu ya matatizo yetu ni kulia na kufanya mikesha isiyokwisha. Tunajenga mustakabali gani kwa watoto wetu wa kiume hapo? Huko siyo kuwafanya walemavu maradufu yetu? Wanaume mbona tunawalemaza warithi wetu? Watoto wetu wa kiume watawezaje kuwa wanaume, waume za watu na baba za watoto wao wenyewe? Afrika vipi? Tunajipeleka wapi wenyewe? Hapo tukiwaona wanapenda kubadili jinsia zao wawe wanawake kabisa tutawashangaa?

Kwa namna hii, kadiri yangu, mustakabali wa bara letu una giza. Kama wanaume wa Afrika hatutajitambua na kuanza kushindana na wanaume wa mabara mengine hakika kabisa tutatawaliwa milele. Tunawasaliti wake zetu na watoto wetu katika kuwaamini wawezekezaji. Hao kamwe hawatakuja kutuletea maendeleo. Wawekezaji ni wawindaji. Ni wanaume. Wanakuja kuwinda katika nchi zetu na bara letu. Wanaume wa Afrika tugutukeni!

Mzee wenu Pd. Titus Amigu

C&P
Ahsante Mtoto wa Mungu
 
Hakika ni andiko zuri sana,padre kaandika maneno kuntu.Wale wavivu wa kusoma,jitahidini kusoma,ni madini matupu,huyo padre kayaandika.Katusihi tuamke,hasa sisi wanaume.
Padre ni Mwanaume na sista ni Mwanamke

Hapo pakoje kazi padre Mwanaume ni Nini?
 
Padre ni Mwanaume na sista ni Mwanamke

Hapo pakoje kazi padre Mwanaume ni Nini?
Huwa wanakua na job descriptions zao wakati wa upataji wa madaraja yao.
Yeye kaongelea mwanaume wa kwaujumla wake.
 
Huwa wanakua na job descriptions zao wakati wa upataji wa madaraja yao.
Yeye kaongelea mwanaume wa kwaujumla wake.
Kwa hiyo kwenye wanaume Kwa ujumla wao yeye hayumo? Pamoja na kuwa mwanaume?
 
Yumo,yeye ni mmoja wa wanaume wanaojitambua,ndiyomaana katika andiko lake anafumbua macho kwa kile kinachoendelea.
Kwa hiyo kwenye wanaume Kwa ujumla wao yeye hayumo? Pamoja na kuwa mwanaume?
 
KAZI YA WANAUME – KUTAFUTA : Sehemu ya II (inaendelea)

4. Ukoloni Mkongwe
Baada ya kugawana bara letu, ukoloni mkongwe ulianzishwa rasmi. Wanaume wa nchi saba za Ulaya walifika kututawala Waafrika. Walifika wanaume wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji, Hispania, Ureno na Italia. Wanaume hao walifaulu “kutuhanithi” wanaume wenzao. Wengine walipata ardhi yetu kwa shuka kama akina Mangungo wa Msovero, Tanganyika, alivyotoa ardhi. Machifu wetu wengine walitoa ardhi kama bei za vioo vya kujitazamia walivyopewa na Wazungu. Wengine walitoa dhahabu kwa malipo ya sahani, vikombe na sufuria kama mfalme wa Ashanti, Ghana. Wengine walikodisha ardhi kwa vijipesa vichache tu, kama Lobengula alivyokodisha ardhi yote ya Zimbabwe na Zambia (siku hizi), kwa paundi za Uingereza mia moja tu.

Nawakumbusheni. Wanaume wenzetu hao walikuja kuwinda barani Afrika kwa ajili ya jamii zao Ulaya. Hapa napigia mstari. Wakoloni vinara wote walikuwa wanaume si wanawake. Ndipo tunapowasikia akina Karl Peters na wanaume wenzao walivyokuja kuchukua ardhi yetu. Wakati huo wanawake wao walibakizwa majumbani kwao wasubiri nyara watakazoleta waume zao.
Kama unanibisha kwamba haya yote hayakuwa kazi za wanaume, nitajie wanawake walau watatu waliohusika moja kwa moja katika kutukamata utumwa, kupeleleza na kutwaa nchi zetu kama makoloni. Najua huwezi kunitajia wowote maana hizo zote zilikuwa kazi za wanaume wenzetu, wawindaji.

Wanaume wenzetu wachache walishtukia mchezo mbaya wa Wazungu kuja kuwinda barani mwetu. Hawa waliamua kuchukua silaha na kuwapiga Wazungu. Hapa tuwakumbuke akina Al Bashir ibn Salim al Harthi (a.k.a. Abushiri), Chifu Mkwawa, Kinjikitile Ngwale na Wangoni wa Songea. Hawa walitualika wanaume wenzao tuwafukuze Wazungu kwa vita. Kwa bahati mbaya silaha zetu zilipwaya mbele ya silaha za wanaume wenzetu. Wao walikuwa wameshagundua silaha za maana zaidi kuliko zetu. Wao walikuwa na risasi, bunduki na mabomu sisi tungali bado na mikuki, pinde na mishale. Vibaya zaidi, wengine wetu walitumaini vitu dhalili sana, kwa mfano, eti Kinjikitile Ngwale aliamini kwamba maji yangeliyeyusha risasi za moto za Mzungu kwa kusema tu “Maji, maji, maji.”

Kwa kuwa kiteknolojia tulikuwa chini ya wanaume wenzetu, tukafeli sana. Akina Al Bashir ibn Salim al Harthi (a.k.a. Abushiri) walifeli miaka ile ya 1888 - 1889. Akina Chifu Mkwawa, miaka ile 1891-1898, walifeli na Wangoni wapiganaji wa vita vya Majimaji, miaka ile ya 1905-1907, walifeli pia. Hata kule Kenya vipiganaji wa vita vya Mau Mau (1953-1960) walifeli. Ndipo wanaume wa Ulaya wakatutawala kwa raha zao. Makoloni yakageuka vilivyo mashamba ya bibi.

5. Ukoloni Mamboleo
Nchi zetu tulizikomboa kwa namna mbili. Wengine walipata uhuru kwa mazungumzo na wengine kwa mtutu wa bunduki. Wanaume wa Angola, Msumbiji, Namibia, Zimbabwe walivurumisha vita vya ukombozi, wakoloni wakaachia. Hapa ndipo walipoingia wanaume wenzetu, akina Augustino Neto, Samora Machel, Sam Nujoma, Robert Mugabe, Jomo Kenyatta, Julius Nyerere, Kwame Nkurumah, Kenneth Kaunda na Nelson Mandela. Lakini kwa uhuru huu si kwamba wanaume wa Ulaya wameacha kuwinda kwao. Tena sasa si wanaume wale wa Ulaya peke yao wanaowinda barani mwetu. Wamejiunga nao Wachina, Wahindi, Waturuki, Wathailandi, Wabrazili na Warusi.

Aibu tupu. “Kuhanithiwa” kwetu wanaume wa Afrika kunaendelea kwa nguvu lakini kwa kimya kimya. Siku hizi, wanaume wenzetu “wanatunyenga” wanaume wa Afrika, wanawake wetu pamoja na watoto wetu kwa misaada ya kadiri tu. Wanabeba vikubwa vyetu na kuturudishia kiduchu tu. Siku hizi ukoloni wao unaitwa wa kisasa. Unaitwa mamboleo. Taasisi za fedha ulimwenguni zinakadiria Afrika inaibiwa kati ya $ 60 – 88.7 bilioni sawa na 3.7% ya GDP ya Afrika kila mwaka na kinachoingia kama misaada, kwa mwaka, ni kati ya $ 49 – 58 bilioni. Piga hesabu hapa.
Kwa ukoloni mamboleo, wanaume wenzetu wanajipatia kwa bei ya kutupa madini na rasilimali zetu. Vitu hivyo vinachukuliwa kirahisi mno. Zamani wanaume Wazungu walikuja kutafuta mali zetu. Kinyume chake tumerahisisha kunyonywa kwetu kwa kiasi kikubwa. Hatupingi chochote. Siku hizi tunawaendea wenyewe Wazungu, Wamarekani, Wachina na kadhalika na ramani zinazoonesha vizuri madini na rasilimali zetu zipo wapo kuwaalika kusudi waje wachukue wanachotaka kwa masharti nafuu. Eti tunaita biashara ya soko huria na uwekezaji.
Yaani sasa tumewafungulia wenyewe milango yote wakitaka wachukue ardhi yetu. Wakitaka wachukue dhahabu yetu. Wakitaka wachukue almasi zetu. Wakitaka wachukue gesi yetu. Wakitaka wachukue uranium yetu. Wakitaka wachukue nickel yetu na kadhalika. Wamakonde wanaita kinachoendelea sasa “liteka mwene”, yaani mwendo wa kila mtu kujichotea pombe kiasi anachotaka. Ukweli ni kwamba nchi zetu sasa zinashindana kuweka masharti nafuu na mazingira wezeshi ili wageni waje wachukue wanavyotaka. Aibu hii. Uanaume wetu uko wapi? Tutawapata wapi tena akina Mkwawa na akina Jomo Kenyatta watupiganie walau Mau Mau? Vita vya Mau Mau viliwachachafya Waingereza huko Kenya tangu mwaka 1953 hadi mwaka 1960 viliposhindwa vibaya.

Tusikubali Wanaume ni Wanaume Tu
Kutokana na haya unaweza kujua kwa nini hakuna mambo ya 50 – 50 huko Marekani wala Ulaya wala Asia. Je, ulisikia habari za 50 – 50 Marekani licha ya kupata uhuru wao tarehe 4.7. 1776? Je, umewahi kusikia habari hiyo Uingereza? Umewahi kusikia habari hiyo Ujerumani? Umewahi kusikia habari hiyo Ufaransa, Italia, Ureno au Urusi? Mtego huo, Waafrika wenzangu! Wanaume wenzetu wanatutega waone mambo yatakavyotuendea kombo tutakapokubali wanaume kulinganishwa na wanawake. Kwa hakika, wanaume wenzetu wanajua wanaume na wanawake wana sifa tofauti 6,500: wanaume ni wawindaji wakati wanawake ni watunza viota na kwa namna hiyo hawawezi kulinganishwa hasa katika vyombo vya maamuzi na upangaji mipango. Wanaume ni wapangaji na wanawake ni wasimamiaji.
Ndivyo ilivyo na itabaki hivi milele, kwa sababu ni mpango wa Mungu Muumbaji. Narudia. Hiyo habari ya 50 – 50 ni mtego kwetu sisi tusiojitambua. Wanaume wenzetu wanataka kuona tutakavyoanguka kwa ujinga wa kutaka wanaume na wanawake tujisikie tupo sawa katika michakato ya maendeleo. Basi, hapa, akili ya kuambiwa afadhali tuchanganye na yetu mapema kabisa.

Wanaume wa Afrika Siku Hizi Je?
Ni aibu tu. Aibu inaendelea mchana kweupe. Wanaume wa Afrika tunaubananga uanaume wetu. Inaonekana kana kwamba hatuna tena zile sifa kumi za wanaume. Ndiyo kisa tunakubali kulinganishwa na akinamama. Ndiyo maana tunakubali 50-50 ambayo hakuna mahali pengine popote duniani wanaume wenzetu walipokubali. Kwa kisa hiki cha ulofa wetu, siku si nyingi tutafikia mahali pa kuona mwanaume kuolewa ni sawa tu. Siku si nyingi tutafikia pahala pa kuona mwanamke kutuoa ni sawa tu. Na nadhani pale pa kudhani mwanamke anaweza kufanya shughuli zetu tumeshapafikia. Pale mahali pa kuona mwanamke anaweza kuchukua majukumu yetu na yeye kututafutia mahitaji tumejapafikia. Tumeshapafikia maana ingelikuwa hatujapafikia wasingelikuwapo akina Marioo ambao kwa maisha yao wanawategemea mashangingi. Aidha wasingelikuwapo wanaume wa kuolewa.

Katika suala hili la ndoa za watu wa jinsia moja ninaona wanaume weusi wakiolewa na wanaume wa Kizungu. Wala sijapata kuona mwanaume mweusi akimwoa mwanaume Mzungu. Je, wewe umewahi kuona? Sasa maana yake nini hata katika kiroja hiki? Maana yake ni kwamba sisi ndio malofa katika kila hali. Asalale! Lakini hii ni aibu sana.
Sasa hapa hapa ongezea upujufu wa siku hizi ambapo vijana tele wanageuka “akina Marioo.” Vijana wa kiume wanakuwa weroro, wanavishwa, kulishwa na kutunzwa na akina mama. Hawa wanavaa heleni, kusuka nywele na kujipodoa kama akina Asumpta, Fatuma, Magdalena na Habiba. Kwa haya tunaelekea wapi?

Hatima
Sasa tuhitimishe mambo. Kihistoria tunakumbuka jinsi tulivyokamatwa utumwa na kuuzwa na wanaume wenzetu. Tunakumbuka tena Wazungu walivyokuja kututawala katika ukoloni mkongwe. Aidha tunakumbuka jinsi tunavyoendelea kutawaliwa katika mfumo mpya wa ukoloni mamboleo. Kutokana na ukoloni mambo leo, sisi wanaume wa Afrika, na wake zetu na watoto wetu, tumeshindwa kutafuta, badala yake tumekubalishwa mitumba: magari, pikipiki, nguo: suruali, mashati, sketi, blauzi, sidiria, vyupi, viatu, soksi na kadhalika. Uanaume wa kufanya mambo kwa nguvu hatuna tena. Uanaume wa kubuni zana na mipango hatuna tena. Sisi sasa ni wategemezi kama wanawake na watoto wetu tu.

Lakini kinachonikera zaidi ni kwamba wanaume wa Afrika tumeanza kugeukia kulia kama suluhu ya matatizo. Kukemea uchawi, laana, mizimu, majini ni dawa gani? Eti wanaume wazima, mapadre na wanaume waliooa kabisa, tunajiunga kwenye vikundi vya kulia, kwa mfano, Karismatiki tupate kulia hadharani sisi na wake zetu na watoto wetu. Tunalia eti Mungu atusaidie, badala ya sisi kutumia uanaume wetu, na nguvu zetu za musuli na akili kupanga mambo na kufanya kazi. Eti sisi tunadhani suluhu ya matatizo yetu ni kulia na kufanya mikesha isiyokwisha. Tunajenga mustakabali gani kwa watoto wetu wa kiume hapo? Huko siyo kuwafanya walemavu maradufu yetu? Wanaume mbona tunawalemaza warithi wetu? Watoto wetu wa kiume watawezaje kuwa wanaume, waume za watu na baba za watoto wao wenyewe? Afrika vipi? Tunajipeleka wapi wenyewe? Hapo tukiwaona wanapenda kubadili jinsia zao wawe wanawake kabisa tutawashangaa?

Kwa namna hii, kadiri yangu, mustakabali wa bara letu una giza. Kama wanaume wa Afrika hatutajitambua na kuanza kushindana na wanaume wa mabara mengine hakika kabisa tutatawaliwa milele. Tunawasaliti wake zetu na watoto wetu katika kuwaamini wawezekezaji. Hao kamwe hawatakuja kutuletea maendeleo. Wawekezaji ni wawindaji. Ni wanaume. Wanakuja kuwinda katika nchi zetu na bara letu. Wanaume wa Afrika tugutukeni!

Mzee wenu Pd. Titus Amigu

C&P
Ahsante sana sikuwa najua kuwa mwanaume ni HUNTER na mwanamke ni NEST KEEPER
 
Back
Top Bottom