Katavi: DC Mpanda aagiza mwekezaji kurudisha mto

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,462
Wananchi wa Kijiji cha Mtisi kilichopo Kata ya Sitalike, Halmashauri ya Ndimbo Mkoani Katavi wamedai kukerwa na mwekezaji aliyewekeza katika machimbo yaliyo katika kijiji hicho ambapo mwekezaji huyo amehamisha mto ili shughuli yake iende kadri anavyotaka.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf amemtaka mwekezaji huyo ndani ya siku saba awe amesimamisha shughuli zake katika eneo hilo la Mto Mtisi ambapo mto huo ndio tegemeo la Wananchi hao.

Mbali na hayo Jamila amewataka Watumishi wa Halmashauri ya Nsimbo kufanya kazi kwa kuzingatia hitaji la Wananchi ili kuepuka migogoro.
 
Back
Top Bottom