Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Kero hizi zimetolewa mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda mara baada ya kufika katika kijiji hicho na kusikiliza kero za Wananchi ambapo wamesema changamoto ya migongano ya Wakulima na Wafugaji bado ni tatizo katika maisha yao ya kila siku huku huduma ya umeme katika makazi yao ikiendelea kukatwa kila wakati pasipo taarifa.
Kaimu Mkurugenzi katika Halmashauri ya Nsimbo, Adolf Semindu amesema changamoto ya huduma ya umeme inasababishwa na matumizi ya jenereta huku Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf akisisitiza upendo katika matumizi ya ardhi ili kuondoa mgongano wa Wakulima na Wafugaji.
Aidha, Jamila amewataka Wakulima na Wafugaji kufanya shughuli za kisasa zaidi ili kuondokana na mwingiliano usio na tija katika maisha yao.