Teslarati
JF-Expert Member
- Nov 21, 2019
- 1,728
- 6,792
Uanaume ni mateso, yaani mababu zetu ndo walifurahia uanaume ila siku hizi ni mateso mara mia.
Nina jamaa yangu aliyumba kdg kiuchumi baada ya kuachishwa kazi miaka minne imepita, jamaa alikuwa ana hela kinoma, mke aliomuoa kwa ndoa ya mapepe mengi akamwomba amfungulie biashara huku yeye anatafuta kazi. Jamaa akauza nyumba moja akampa huyo mwanamke mtaji, mwanamke akaanza kwenda china kununua mizigo na kuuza hapa DSM na mikoani.
Biashara baada ya kuiva, mwanamke akaanza kutembea na vijana wake wa kazini hapo. Jamaa alipojua mwanamke akawa mkali, biashara kila kitu kimeandikwa kwa mwanamke. Mwanamke mwishowe akaondoka jumla nyumbani akaenda kupanga kivyake bila kuachana rasmi. Huko inasemekana akawa anakaa kinyumba na dogo mmoja wa kazini kwake. Kizuri hawakua na mtoto bado.
Biashara ikafeli, inasemekana alidhurumiwa na huyo dogo alokua naye, mwanamke akaanza kutanga tanga tu.
Jamaa si kajitafuta kajipata leo hii anapokea barua eti mke kamfungulia kesi kwamba waliachana ila jamaa hakumpa talaka na gawio lake la mali uthibitisho wa ndoa anao sababu walifunga ndoa ya kanisani.
Msioe msioe msioe. Kwani nini kigumu kukaa na mwanamke ndani bila kumuoa? Kama utalazimika kuoa mpe mwanamke prenup asije kugusa mali zako.
Nina jamaa yangu aliyumba kdg kiuchumi baada ya kuachishwa kazi miaka minne imepita, jamaa alikuwa ana hela kinoma, mke aliomuoa kwa ndoa ya mapepe mengi akamwomba amfungulie biashara huku yeye anatafuta kazi. Jamaa akauza nyumba moja akampa huyo mwanamke mtaji, mwanamke akaanza kwenda china kununua mizigo na kuuza hapa DSM na mikoani.
Biashara baada ya kuiva, mwanamke akaanza kutembea na vijana wake wa kazini hapo. Jamaa alipojua mwanamke akawa mkali, biashara kila kitu kimeandikwa kwa mwanamke. Mwanamke mwishowe akaondoka jumla nyumbani akaenda kupanga kivyake bila kuachana rasmi. Huko inasemekana akawa anakaa kinyumba na dogo mmoja wa kazini kwake. Kizuri hawakua na mtoto bado.
Biashara ikafeli, inasemekana alidhurumiwa na huyo dogo alokua naye, mwanamke akaanza kutanga tanga tu.
Jamaa si kajitafuta kajipata leo hii anapokea barua eti mke kamfungulia kesi kwamba waliachana ila jamaa hakumpa talaka na gawio lake la mali uthibitisho wa ndoa anao sababu walifunga ndoa ya kanisani.
Msioe msioe msioe. Kwani nini kigumu kukaa na mwanamke ndani bila kumuoa? Kama utalazimika kuoa mpe mwanamke prenup asije kugusa mali zako.