Watu wanaponda sana humu ila mi nabaki kuwacheka tu.Nimezunguka mikoa mingi sana maisha wanayoishi na hali ya kiuchumi kiujumla ktk sehemu nyingi hazina tofauti na maisha ya LINDI,kibaya zaidi sasa watu wao ni washamba sana hata matumizi ya hela hawajui wao kila kitu kwao ni kigeni.Jamani nendeni kanda ya ziwa huko mkakutane na wasukuma wana hela lakini wanalala chini, pia hela zao huweka ndani tu hawapeleki bank ili zikafanye mzunguko,nyumba zao sasa za tope..
Nendeni nyanda za juu kusini huko mkakutane na maskini wa kifipa,kinyakyusa,wasafwa...
Magharibi huko;mkakutane na waha maisha magumu,barabara mbovu,ngonja ngunja(vumbi la udongo mwekundu) basi taabu tu wanachojua wao ni ubishi,kuhama kwenda mikoa ya jirani na majungu

Haya tuje kanda ya kati hapa ndio aibu tupu wilaya na vijiji vya Singida wanaishi maisha magumu,maji ya taabu,mzunguko wa hela ni mdogo pia kuna baadhi ya wilaya hazina hata stendi za magari za maana.
Dom;hapa jangwani raia wanaishi maisha magumu sana,Kondoa,chemba..kuna ukame sana hakuna fursa hata maendeleo hakuna.Chakula chao kikuu ni ugali maziwa.Kwa uchawi hapa ndio pake.
Hii nchi tupo sawa tu kwenye suala la uduni wa maendeleo ila humu jf watu mnajipaisha tu.Bora hata Ruangwa wana madini,wanalima mashamba ya ufuta,wana viunga vya minazi.Hivi vyote vinachangia mzunguko wa fedha na huleta maendeleo, na ukikamilika ule mradi wa gesi asilia haki ya nani Lindi yote kwa ujumla inaenda kuwa Paris ya Bongo.