Karibuni Ruangwa

Karibuni Ruangwa

Tatizo mikoa ya kusini ina laana na uchawi umezidi,mnarogana sana,hayo unayoita maendeleo ukicompare na maeneo mengine ni takataka tu,kusini haitakuja kuendelea kamwe
We bhana acha uongo wako! Huko kwingine wapi wakati Tanzania kila unakoenda ni umaskini mtupu na ushirikina?!
 
Nilienda Rwangwa mwaka juzi 2019 kwenda kuishi kufanya miradi Nia kufungua huduma za uwakala na kuuza simu za mikononi. Nilikuwa nimekaa kwa wakala napiga nae story. aisee ruangwa shambani sio pa kwenda kuish wala kuwekeza utaua mtaji wako idadi ya watu waishio mjini ni ndogo sana.Bado sana pa kupapa sifa izo.
 
Mwaka huu nilikuwa na NGO moja ambayo nilizunguka nayo Jimbo la Mchinga (Mabebery yameshanusa gesi). Katika safari zetu tukafika kijiji kimoja kinaitwa Rutamba. Nikiwa pale nikabahatika kufika hadi kwa Mzee Membe kwa sababu sio mbali na Rutamba ingawaje kule kwa Membe hakukuwa kwenye mpango wetu. Nilitamani sana nifike hadi Ruangwa manake nilioneshwa barabara ya Ruangwa lakini inaonekana barabara ile gari nyingi hazifiki Ruangwa. Je, hivi sasa kuna magari ya kufika Ruangwa? Naulizia hivyo kwa sababu kuna kitu nimekipenda pale Rutamba na nina mpango mwaka huu wakati wa likizo niende tena pale. Ningefurahi sana nikikamilisha mishe mishe zangu pale Rutamba, basi niende hadi Ruangwa ili nako nikacheki fursa
Kimekuvutia nini maporini huko..mbali nahuduma za jamii na miundombinu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nilienda Rwangwa mwaka juzi 2019 kwenda kuishi kufanya miradi Nia kufungua huduma za uwakala na kuuza simu za mikononi. Nilikuwa nimekaa kwa wakala napiga nae story. aisee ruangwa shambani sio pa kwenda kuish wala kuwekeza utaua mtaji wako idadi ya watu waishio mjini ni ndogo sana.Bado sana pa kupapa sifa izo.
Kusini sehemu ya kuishi na kufanya biashara ni mtwarana masasi..wilaya zilizobaki ni mashambani tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kati ya viongozi wakubwa wa nchi hii wanaoongoza kutotendea Haki Jimbo analotoka basi MEMBE anaongoza.
Tatizo Membe ni mbinafsi kupindukia, yaani kama Jiwe tu! Focus ya Membe haikuwa Jimbo lote la Mtama bali kijijini kwao tu!! Mwaka jana nilikuwa na NGO moja ambayo tulizunguka vijiji kadhaa vya Jimbo la Mchinga. Katika huo mzunguko, tukafika kijiji kimoja kinaitwa Rutamba ambacho ni very close ni kijiji cha Rondo Chiponda anachotoka Membe. Nikaona kabla hatujarudi town, wacha niende nikaone kijijini kwa Membe. Ambacho niligundua hapo Rutamba ni kijiji kikubwa maradufu na pamechangamka sana kulinganisha na anakotoka Membe. Lakini cha ajabu, hapo Rondo, nikakuta Membe kapiga lami hadi mitaani, kajenga hiki na kile eti lengo lake ilikuwa apafanye wilaya!! Kama utakumbuka, Magufuli alipoenda Mtama, akaitangaza Mtama kwamba wilaya, ikiwa na lengo na la kuzima ndoto za Membe ambazo alikusudia kama angeukwaa urais! Kwahiyo Membe asingeiendeleza Mtama kwa ujumla kwa sababu alitaka Rondo ndo isha-shine ili ahalalishe kuwa wilaya kama Magu alivyokuwa amehalalisha Chato kuwa mkoa!
 
Kimekuvutia nini maporini huko..mbali nahuduma za jamii na miundombinu.

#MaendeleoHayanaChama
Hapo Rutamba umeshawahi kufika? Mimi nimezunguka vijiji vingi na NGO yetu lakini Rutamba inavipita vijiji vingi hata vya hiyo mikoa mingine kwahiyo unanishangaza unaposema "porini huko" manake kama kile kijiji ni porini basi vijiji vingi Tanzania ni porini!
 
Mwaka huu nilikuwa na NGO moja ambayo nilizunguka nayo Jimbo la Mchinga (Mabebery yameshanusa gesi). Katika safari zetu tukafika kijiji kimoja kinaitwa Rutamba. Nikiwa pale nikabahatika kufika hadi kwa Mzee Membe kwa sababu sio mbali na Rutamba ingawaje kule kwa Membe hakukuwa kwenye mpango wetu. Nilitamani sana nifike hadi Ruangwa manake nilioneshwa barabara ya Ruangwa lakini inaonekana barabara ile gari nyingi hazifiki Ruangwa. Je, hivi sasa kuna magari ya kufika Ruangwa? Naulizia hivyo kwa sababu kuna kitu nimekipenda pale Rutamba na nina mpango mwaka huu wakati wa likizo niende tena pale. Ningefurahi sana nikikamilisha mishe mishe zangu pale Rutamba, basi niende hadi Ruangwa ili nako nikacheki fursa
Aiseh mkuu iyo barabara haina michongo pesa , hipo locally na kama inamichongo bas madiwan wa rondo na kata jirani na ruangwa wazembe ,
 
Aiseh mkuu iyo barabara haina michongo pesa , hipo locally na kama inamichongo bas madiwan wa rondo na kata jirani na ruangwa wazembe ,
Ile barabara nimeambiwa sio ya halmashauri bali ni ya TANROADS! Hata hapo Rutamba nilipofika nimekuta nyumba nyingi zimevunjwa lakini hakuna ujenzi wowote!

NB: Rondo ni jimbo tofauti na Jimbo ambalo mimi nilipita.
 
Kati ya viongozi wakubwa wa nchi hii wanaoongoza kutotendea Haki Jimbo analotoka basi MEMBE anaongoza.

Mpaka anastaafu ubungena kuamua kugombea Urais Jimbo la mtama liko hovyo pamoja na jina kubwa la viongozi iliyowazalisha kuanzia aliyepita (MEMBE ) na hata huyu wa sasa Nape hakuna cha maana alichofanya Hadi sasa..Mtama sijui wanafeli wapi asee

Hongera Wana Ruangwa Kwa maendeleo

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Waache uchawi ili wageni waje kuchangamana mji na kuleta maendeleo mambo yatasonga
 
Watu wanaponda sana humu ila mi nabaki kuwacheka tu.Nimezunguka mikoa mingi sana maisha wanayoishi na hali ya kiuchumi kiujumla ktk sehemu nyingi hazina tofauti na maisha ya LINDI,kibaya zaidi sasa watu wao ni washamba sana hata matumizi ya hela hawajui wao kila kitu kwao ni kigeni.Jamani nendeni kanda ya ziwa huko mkakutane na wasukuma wana hela lakini wanalala chini, pia hela zao huweka ndani tu hawapeleki bank ili zikafanye mzunguko,nyumba zao sasa za tope..

Nendeni nyanda za juu kusini huko mkakutane na maskini wa kifipa,kinyakyusa,wasafwa...

Magharibi huko;mkakutane na waha maisha magumu,barabara mbovu,ngonja ngunja(vumbi la udongo mwekundu) basi taabu tu wanachojua wao ni ubishi,kuhama kwenda mikoa ya jirani na majungu

Haya tuje kanda ya kati hapa ndio aibu tupu wilaya na vijiji vya Singida wanaishi maisha magumu,maji ya taabu,mzunguko wa hela ni mdogo pia kuna baadhi ya wilaya hazina hata stendi za magari za maana.

Dom;hapa jangwani raia wanaishi maisha magumu sana,Kondoa,chemba..kuna ukame sana hakuna fursa hata maendeleo hakuna.Chakula chao kikuu ni ugali maziwa.Kwa uchawi hapa ndio pake.


Hii nchi tupo sawa tu kwenye suala la uduni wa maendeleo ila humu jf watu mnajipaisha tu.Bora hata Ruangwa wana madini,wanalima mashamba ya ufuta,wana viunga vya minazi.Hivi vyote vinachangia mzunguko wa fedha na huleta maendeleo, na ukikamilika ule mradi wa gesi asilia haki ya nani Lindi yote kwa ujumla inaenda kuwa Paris ya Bongo.
 
Watu wanaponda sana humu ila mi nabaki kuwacheka tu.Nimezunguka mikoa mingi sana maisha wanayoishi na hali ya kiuchumi kiujumla ktk sehemu nyingi hazina tofauti na maisha ya LINDI,kibaya zaidi sasa watu wao ni washamba sana hata matumizi ya hela hawajui wao kila kitu kwao ni kigeni.Jamani nendeni kanda ya ziwa huko mkakutane na wasukuma wana hela lakini wanalala chini, pia hela zao huweka ndani tu hawapeleki bank ili zikafanye mzunguko,nyumba zao sasa za tope..

Nendeni nyanda za juu kusini huko mkakutane na maskini wa kifipa,kinyakyusa,wasafwa...

Magharibi huko;mkakutane na waha maisha magumu,barabara mbovu,ngonja ngunja(vumbi la udongo mwekundu) basi taabu tu wanachojua wao ni ubishi,kuhama kwenda mikoa ya jirani na majungu

Haya tuje kanda ya kati hapa ndio aibu tupu wilaya na vijiji vya Singida wanaishi maisha magumu,maji ya taabu,mzunguko wa hela ni mdogo pia kuna baadhi ya wilaya hazina hata stendi za magari za maana.

Dom;hapa jangwani raia wanaishi maisha magumu sana,Kondoa,chemba..kuna ukame sana hakuna fursa hata maendeleo hakuna.Chakula chao kikuu ni ugali maziwa.Kwa uchawi hapa ndio pake.


Hii nchi tupo sawa tu kwenye suala la uduni wa maendeleo ila humu jf watu mnajipaisha tu.Bora hata Ruangwa wana madini,wanalima mashamba ya ufuta,wana viunga vya minazi.Hivi vyote vinachangia mzunguko wa fedha na huleta maendeleo, na ukikamilika ule mradi wa gesi asilia haki ya nani Lindi yote kwa ujumla inaenda kuwa Paris ya Bongo.
Tema mate chini..eti vijiji vya kusini ulinganishe na vijiji vya kaskazini..utakua hauko sawa wewe..

#MaendeleoHayanaChama
 
Watu wanaponda sana humu ila mi nabaki kuwacheka tu.Nimezunguka mikoa mingi sana maisha wanayoishi na hali ya kiuchumi kiujumla ktk sehemu nyingi hazina tofauti na maisha ya LINDI,kibaya zaidi sasa watu wao ni washamba sana hata matumizi ya hela hawajui wao kila kitu kwao ni kigeni.Jamani nendeni kanda ya ziwa huko mkakutane na wasukuma wana hela lakini wanalala chini, pia hela zao huweka ndani tu hawapeleki bank ili zikafanye mzunguko,nyumba zao sasa za tope..

Nendeni nyanda za juu kusini huko mkakutane na maskini wa kifipa,kinyakyusa,wasafwa...

Magharibi huko;mkakutane na waha maisha magumu,barabara mbovu,ngonja ngunja(vumbi la udongo mwekundu) basi taabu tu wanachojua wao ni ubishi,kuhama kwenda mikoa ya jirani na majungu

Haya tuje kanda ya kati hapa ndio aibu tupu wilaya na vijiji vya Singida wanaishi maisha magumu,maji ya taabu,mzunguko wa hela ni mdogo pia kuna baadhi ya wilaya hazina hata stendi za magari za maana.

Dom;hapa jangwani raia wanaishi maisha magumu sana,Kondoa,chemba..kuna ukame sana hakuna fursa hata maendeleo hakuna.Chakula chao kikuu ni ugali maziwa.Kwa uchawi hapa ndio pake.


Hii nchi tupo sawa tu kwenye suala la uduni wa maendeleo ila humu jf watu mnajipaisha tu.Bora hata Ruangwa wana madini,wanalima mashamba ya ufuta,wana viunga vya minazi.Hivi vyote vinachangia mzunguko wa fedha na huleta maendeleo, na ukikamilika ule mradi wa gesi asilia haki ya nani Lindi yote kwa ujumla inaenda kuwa Paris ya Bongo.
Yaani vijiji vya unyakyusa ndio ufananishe na vya kusini wewe ebu ona aibu. Wanyakyusa wanaumasikini gani na wasafwa wa kufananisha na kusini uko kwenu au umeadosiwa
 
Tema mate chini..eti vijiji vya kusini ulinganishe na vijiji vya kaskazini..utakua hauko sawa wewe..

#MaendeleoHayanaChama
Pitia bandiko langu sijaidadavua mikoa ya kaskazini naiheshimu sana.Mikoa ya kaskazini hata kama hamna bichi,ila nimevutiwa sana na aina yenu ya maisha na kile kipepo fulani hivi kinanishawishi nihamie huko.
 
Yaani vijiji vya unyakyusa ndio ufananishe na vya kusini wewe ebu ona aibu. Wanyakyusa wanaumasikini gani na wasafwa wa kufananisha na kusini uko kwenu au umeadosiwa
Nimewahi kuishi huko.
 
Pitia bandiko langu sijaidadavua mikoa ya kaskazini naiheshimu sana.Mikoa ya kaskazini hata kama hamna bichi,ila nimevutiwa sana na aina yenu ya maisha na kile kipepo fulani hivi kinanishawishi nihamie huko.
Hamna lolote hata huko Kaskazini! Sema baadhi ya sehemu za Mkoa wa Kilimanjaro ndo afadhali zina unafuu! Unapotaja kaskazini huwezi kuacha kutaja Arusha! Pamoja na kelele nyingi za watu wa Arusha ambazo kelelele nyingi ni za Wachaga, lakini Arusha inaishia pale pale Arusha mjini na baadhi ya miji midogo michache! Ukienda huko vijijini umasaini nako ni umaskini mtupu! Hakuna cha maana wanachojivunia zaidi ya ng'ombe zilizokondeana huku wenyewe wakiishi kwenye nyumba mbovu ajabu! Unapotaja mikoa ya kaskazini huwezi kuiacha Manyara ambayo nayo ni umaskini mtupu!! Hizi kelele za hapa ni za kujikweza tu na nyingi ni Wachaga ndio wanaojiona wao ndo matajiri sana ingawaje ukweli ni majority na wenyewe ni maskini tu ingawaje wamejitahidi kutokomeza nyumba za majani huko vijijini!

Binafsi mtu hanidanganyi! Sehemu ambayo nilikuwa sijafika ni mikoa ya kusini na mwaka jana ndo nikapata hiyo fursa. Nilichokiona kule wala hakina tofauti na mikoa mingi ya Tanzania. Hawa wanaoponda usikute hata Kibiti hawakujui! Lakini kingine nilichogundua kuhusu mikoa ya kusini, hawa watu hawajajaaliwa sana hali ya hewa nzuri kama ilivyo mikoa ya kanda ya juu kusini au mikoa ya kaskazini magharibi! Kwa mfano hicho kijiji nilichokitaja, nimekuta shughuli kubwa inayofanywa na vijana ni kilimo cha nyanya, na zinawaingiza pesa kweli kweli! Hata hivyo, ukifika huko wanakulima nyanya, ukiangalia udongo wake unaweza kusema ni sementi iliyogandishwa kiasi kwamba kama ni mwaka wa jua kali, kilimo chake ni shughuli mzito kweli kweli. Hali hiyo ni tofauti kabisa na sehemu kama Morogoro ambako nako tulienda! Ukienda mahali kama Ifakara au Kilombero, unaweza kulima hata ekari 5 kwa urahisi kabisa lakini sio kwenye mfinyanzi nilioukuta kwenye kile kijiji!
 
Yaani vijiji vya unyakyusa ndio ufananishe na vya kusini wewe ebu ona aibu. Wanyakyusa wanaumasikini gani na wasafwa wa kufananisha na kusini uko kwenu au umeadosiwa
Kwahiyo Wanyakyusa na wenyewe ni matajiri sio?! Ina maana hao matajiri wanabaki huko huko vijijini ama wapo wapi hasa?! Nauliza kwa sababu hawa Wanyakyusa tulionao mijini wala hawana tofauti yoyote na Watanzania wengine!!! Ngoja niache unafiki! Hata Wanyakyusa hamna utajiri wowote zaidi ya utajiri wa vyakula!! Na huo utajiri wa vyakula unatokana na rehemu zake tu Baba Aliye Mbinguni baada ya kuijaalia mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuwa na hali ya hewa na udongo mzuri! Watu wa kusini hawana neema hii ya hali ya hewa na udongo mzuri lakini bado ndo hao hao wanaoliingizia taifa pesa nyingi zaidi za kigeni kupitia korosho na hata mbaazi na ufuta!!
 
Back
Top Bottom