Kanuni za Bunge baadhi zatenguliwa kutokana na Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
KANUNI ZA BUNGE ZATENGULIWA KUPISHA MFUNGO

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetengua Kanuni kwa ajili ya kuruhusu Mfungo wa Mwezi wa Ramadhan ambapo mabadiliko hayo yataendelea hadi mwisho wa mfungo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, George Simbachawene amewasilisha hoja hiyo Bungeni Aprili 5, 2022, ambapo Kanuni ya 34 (2) na 34 (4) ya Kanuni za Kudumu za Bunge zimetenguliwa ili shughuli zimalizike mapema.

Lengo ni kuwaruhusu Waumini wa Dini ya Kiislam kuswali na kufuturu kwa wakati muafaka, hivyo mwisho wa shughuli za Bunge utakuwa saa 12:00 jioni badala ya saa 1:45 Usiku.



Source: TBC
 
Kwa maana hiyo watakuwa wanafanya kazi kwa masaa 6 tu kila siku? Hivyo kwa mshahara wao watakuwa wanalipwa Tsh ngapi kwa kila saa?
 
Kwa akili hizi maendeleo tutayasikia kwenye vyombo vya habari.

Kwa maana nyingine hata malecturer wenye vipindi jioni wahairishe 😂😂

Vipi madaktari nao wakiclaim hoja hiyo? Namna hii ya kutokuelewa dhima ya dini inayumbisha wengi wasio na ufahamu tena ndio msingi wa umaskini kwa jamii nyingi za watu weusi
 
Kwa akili hizi maendeleo tutayasikia kwenye vyombo vya habari.

Kwa maana nyingine hata malecturer wenye vipindi jioni wahairishe 😂😂

Vipi madaktari nao wakiclaim hoja hiyo? Namna hii ya kutokuelewa dhima ya dini inayumbisha wengi wasio na ufahamu tena ndio msingi wa umaskini kwa jamii nyingi za watu weusi
Ujinga jinga tu man
 
Mtu uko pale paspo uhalali na bado unaendaje kufunga na kuwa front kbsa katk swal Kam hili
 
Sasa huu ni ubaguzi wa waziwazi,kwan kwaresma sio mfungo.Au waliokuwa wanafunga sio watanzania..hili liingie kwenye kero ya muungano au jamuhuri (Tanganyika).
 
KANUNI ZA BUNGE ZATENGULIWA KUPISHA MFUNGO

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetengua Kanuni kwa ajili ya kuruhusu Mfungo wa Mwezi wa Ramadhan ambapo mabadiliko hayo yataendelea hadi mwisho wa mfungo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, George Simbachawene amewasilisha hoja hiyo Bungeni Aprili 5, 2022, ambapo Kanuni ya 34 (2) na 34 (4) ya Kanuni za Kudumu za Bunge zimetenguliwa ili shughuli zimalizike mapema.

Lengo ni kuwaruhusu Waumini wa Dini ya Kiislam kuswali na kufuturu kwa wakati muafaka, hivyo mwisho wa shughuli za Bunge utakuwa saa 12:00 jioni badala ya saa 1:45 Usiku.

View attachment 2176672

Source: TBC
Kuna bunge au genge la waharifu tupu
 
Back
Top Bottom