Mfiaukweli
JF-Expert Member
- Aug 30, 2018
- 5,636
- 8,774
Kila kitu unachokisikia kuhusu dini/dhehebu lako, kifanyie kazi. Watu wengi tupo kwenye hizi Imani kwa kuzaliwa , na siyo kwa kujifunza na kuchagua. Na haitatokea zoote zikawa sahihi. Na kwenye familia zetu wanaamini wako sahihi , unapojaribu kuachana na dini ya familia utakiona cha mtema kuni, watakutenga.
Kwa mfano hizi habari za uislam kuanzishwa na Roman catholic zinasikika sana. Tuzifanyie utafiti tujue ukweli na mengine mengi tuyachunguze. Tatizo tunawaamini sana viongozi wetu. Kwanini tusiamini biblia inachosema/korani. Biblia/koran inaweza kuwa inasema kivingine na viongozi wetu wakasema kivingine, na sisi tunawaamini wao na blahblah zao.
Waefeso 4:5 ''Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja''
Mtu yeyote yule ambae leo hii ni Muislamu na anaisoma na kuielewa Qur'an halafu akiamua kusoma Biblia na kulinganisha hivyo vitabu viwili hawezi kuendelea kuwa Muislamu.
Ukitaka kuthibitisha ukweli huu chunguza uone kama mtoto wa Kiislamu (anaetokea kwenye familia ya Kiislamu hasa) anaweza kushika Biblia (e.g. ukimuomba akushikie). Nchi kama Pakistan, Afghanistan, Iran, Saudi Arabia na Indonesia kuonekana umeshika Biblia hadharani ni kosa la jinai.