Kanda ya Ziwa, naja kwenu...

Wakuu mlio Mwanza, Kagera na Mara, nitakuwa maeneo haya karibuni. Ningependa kuonana na walio tayari ili tubadilishane mawazo na kusikia kutoka kwenu. Baada ya safari hii nitaelekea Mbeya na Ruvuma.

Hii ni kuweza kuonana na wadau wa JF na kubadilishana nao mawazo, kuwasaidia wenye kuhitaji msaada (kiufundi) na zaidi kuweza kufahamiana na kushauriana namna ya kuipeleka JF kwenye hatua nyingine.

Same Place,Same people we havent catch up for while mkuu.....Kama itakuwa Oct...basi tutakutana...Tai Five Panakuhusu.
 
Duh mkuu am touched.., Hongera sana kwa kufanya kazi nzuri na kulifanya jamvi letu liwe makini sana..., cha maana ni kutoa taarifa mapema kabla ya safari ili wadau wajue na kuweza kuhakikisha kwamba hawakosi kuwepo...

"Alone we can do so little, together we can do so much".... Hellen Keller
 
Mkubwa Maxence Melo.

Bahati mbaya ulipokuja Arusha nilikuwa nje ya mkoa wa Arusha naomba ukipata nafasi urudi tena.


Mkuu,

Kwa Dar hatujawahi kupanga kukutana. Tumekuwa tukikutana na wadau katika mazingira ya kawaida na kwenye events za kijamii, itabidi tuandae mkutano mmoja wa pamoja ambapo nasisitiza, ID za JF hazina umuhimu kusemwa labda mtu afanye hivyo kwa hiari yake.

All we need ni maoni ya wadau na kuyaweka kwny utekelezaji.

Nilipokutana na wadau huko Arusha tuliyoongelea asilimia kubwa (over 80%) yameshafanyiwa kazi na huenda ndiyo yametufikisha hapa
 
Back
Top Bottom