Sophoghani
JF-Expert Member
- Mar 3, 2018
- 395
- 626
Pesa haziingi kwenye mzunguko bila kuwa registered na kuwa halali.... baada ya kutengenezwa lazima BOT wafanye mambo then ziwe halali kutumika....Mkuu umeeleza vyema sana lakini vipi kuhusu uaminifu wa makampuni hayo?
Hayawezi kufanya janja janja ya kutengeneza pesa za ziada na kuziingiza kwenye mzunguko kiaina?!
Najua kuna namba za fedha na ugumu kidogo wa hili ila wanaaminiwa vipi? na kwa nini kusiwe na jinsi ya kutengeneza fedha zetu hapa?
Gusa hapa Vatican Inamiliki Dunia - JamiiForumsHi wana JF,
Nimekuwa nikisikia kuwa pesa ya nchi yoyote ile utengenezwa katika nchi ya Uswisi, lakini katika kujua huko nimekuwa nabaki na maswali mbalimbali juu ya hilo. Maswali hayo ni pamoja na;
(i) Je katika nchi hiyo ni kampuni binafsi au za serikali ndiyo zinahusika kutengeneza?
(ii) Je kampuni hizo zinafanya kazi hiyo kama msaada au ni ki biashara?
(iii) Kama ni ki biashara?, wao wanalipwa nini? pesa hiyo hiyo wanayotengeneza au kitu kingine? kwa maana kama ni pesa hiyo sioni kama wana fanya biashara, nitoe mfano mdogo, chukulia umpe mtu order ya kukutengenenezea mikate, na baada ya kukutengenezea umlipe kiasi fulani cha mikate hiyo, hapo si ni sawa sawa mikate hiyo kakupa bure? n.k
Kwa kutambua JF ni jukwaa lililojaa wataalamu katka nyanja mbalimbali natumaini nitapata majibu kulingana na duku duku hizo.
Nawasilisha.
Lazima kuwe na taasisi zinazo wacontrol sivyo michezo ingekuwa mingi na habari za mapichapichaMkuu umeeleza vyema sana lakini vipi kuhusu uaminifu wa makampuni hayo?
Hayawezi kufanya janja janja ya kutengeneza pesa za ziada na kuziingiza kwenye mzunguko kiaina?!
Najua kuna namba za fedha na ugumu kidogo wa hili ila wanaaminiwa vipi? na kwa nini kusiwe na jinsi ya kutengeneza fedha zetu hapa?
Nimekubali jamaa uko vizuri👏👏👏👏Kujibu swali lako Dr. Duniani kuna taasisi mbili zinazohusika na maswala ya kifedha na uchumi taasisi hzo ni International Monetary Fund (IMF) na World Bank (WB) taasisi hzi zinaongozwa na money policy act (MPA) ndani ya MPA kuna mfumo unaoitwa Global financial system (GFS) mfumo huu unamilikiwa na Rothschild family kumekuwa na fikra ya kuwa Rothschild family ndio wamiliki wa Bank kubwa kubwa ikiwamo WB , IMF na Federal Reserve System japo wengi wanajua ni Federal Reserve bank lakini ukweli ni Federal Reserve System huku bank ikiwa ni Bank of America (FRS ) ni mfumo tu unaoendesha bank hzo ambapo unaendeshwa na sheria ya federal reserve system act ya mwaka 1913
Rothschild si wamiliki wa banks hzo bali wanamiliki mfumo wa GFS unaotumika kwenye banks nying duniani kuelewa vizuri ni kama leo MAX malipo wanamfumo wao wa maxcom mfumo unaotumika kufanya malipo kwa huduma mbalimbali so ndio mfumo wa GFS unavyofanya kazi
Money policy act (MPA) ndio mwongozo wa centro banks zote duniani na kazi ya centro bank duniani ni
1 print money
2 control supply of money
3 Set the Reserve Requirement
4 Influence Interest Rates
5 Engage in Open Market Operations
6 Control inflation
Hii ndio kazi ya CB zote duniani kuhusu kushuka kwa thamani ya fedha au uchumi
Kwanza unatakiwa kujua hakuna mahusiano ya thamani ya fedha na uchumi japo wengi wanajua kuna mahusiano ya vtu hv lakini ukweli ni kwamba hakuna wakati formula ya uchumi wa ndani ni
MV=PY
M=Money suppy
V=Velocity of circulation
P=price level
Y=National income
Wakati formula ya kushusha au kupandisha thamani ya fedha ni vitu hv
1 INFLATION
2 INTREST RATES
3 Current-Account Deficits
4 Public Debt
5 . Terms of Trade
6 . Political Stability and Economic Performance
Kutokana na kutokuwa na mahusiano hayo ndio unaona dola ya US kuna fedha duniani zimeizidi thamani kama Euro,paund,dinar ya oman pia ukiangalia uchumi wa US na uchumi ya Omani ni vichekesho leo kama kungekuwa na mahusiano ya uchumi na thamani ya fedha basi leo fedha ya Japani ,China zingekuwa ni moja ya sarafu zenye nguvu kubwa duniani na USD ndio ingekuwa fedha yenye thamani kuliko zote
Kuna kitu kinaitwa Balance of trade na ambayo mfumo wake ndio unakwenda kwenye mfumo wa uchumi mkuu moja kwa moja yani GDP
GDP = C + I + G (Ex - Im)
C = Consumer spendng
I= Investment spendng
G= Govement spendng
Ex= Export
Im=Import
Sasa kuhusu uchumi wetu Tanganyika na thamani yetu ya fedha kushuka au kuteteleka aidha kuna vitu viwili
1 Wataalamu wetu wameshindwa kutumia maarifa (Ufahamu) wao vizuri (kwani kwa binadamu tuna vitu vitatu
(A) Utashi (B) Akili ( C) Ufahamu
Sasa Akili ni matumizi mazuri ya ufahamu ambao mara nying unapatikana kwa uzoefu au kwa kwenda shule
2 Labda wataalamu wetu hawajui kupigana vita hii ya kiuchumi na kifedha
Duniani kuna vita tatu
1 Vita vya silaha na majeshi
2 Cyber war(Vita vya mifumo ya technologia ya habari na mawasiliano)
3Economic war (Vita vya kiuchumi)
Vita vya kiuchumi ndio vita inayopiganwa sasa duniani kuliko vita vingine vyote unavijua zipo mpaka mbinu za kimafia za kupigana vta hii ya kiuchumi
ambazo zipo njia 6 za kupadisha uchumi na fedha
Matola jibu lako ni wanapokuchejia dola iliyoexpire kwanza unachenjiwa chini ya exchange rate ya siku hyo kama ni dola mia ni sh 200,000 ww kwa fedha yako ya zamani utachengiwa chini ya laki mbili then wanazipeleka Zanzibar fedha za zamani huko wanapewa wageni au wazungu wanaorudi makwao wanarudi nazo US
mwenye swali anaweza uliza kwani JF ndio sehemu pekee ambapo hakuna bodi ya mikopo hapa unapata elimu bure
Mkuu MALCOM LUMUMBA unaweza kujazia nilichosahau kuweka hapa
brazuca Paprika k_dizle Juma chief MNANSO mtimkav Dux_1234 LIKE Niku ADD Kalamu Yangu
Molaro
Halafu kuna mpumbavu mmoja alitaka kufunga JFsNimekubali jamaa uko vizuri👏👏👏👏
Hawa mabeberu kumbe hawakwepeki, bado ndio wanatutengenezea hizi pesa zetu za madafu halafu kila siku tunawananga??kila nchi ina kitu kinaitwa money policy act MPA huu ndo mwongozo wa central bank zote duniani ikiongozwa na WB mfumo huu ndo unawaongoza katika ku supply and monitoring currently so kuhusu ni kiasi gani wanachapisha inategemea na maitaji ya nchi husika kuna msemo wa kibiashara unasema ukitaka kukipandisha kitu thamani kifanye kuwa adimu pia ukitaka kukishusha kitu thamani basi kifanye kipatikane kwa wepesi so chaguo ni lako kuchapisha tuuuuu au kuchapisha pale inapoitajika
kwa wenzetu yani federal reserve bank and bank of England pia na bank of Canada hawa ndo wanacontrol karibu institutions zote za fedha ikiwamo WB na IMF so ni kama money policy act wanazizibiti wao
lakini thamani ya fedha hawapangi wao kama ingekuwa hvyo basi dollar ndo ingekuwa na thamani kuliko zote bt kuna fedha za nchi zingine zimeizd thaman usd mfano Swiss fanc pound na dinar ya Oman
pia wenzetu wana mfumo mzuri mfano marekani kiwanda cha kutengeneza fedha cha fort Worth cha TX na cha Washington cha tour and visitor centre kwa pamoja vinauwezo wa kutengeneza kiasi cha dollar million 28 par hour na pia wameweka expire date ya ela yao ili kuweza kujua ni kiasi gani cha fedha kipo katika mzunguko duniani na pia kudhibiti mijitu inayoficha ela kwenye masandarusi na ndoo coz ikifika mda fedha inaexpire so ikiexpire mkononi mwako itakuwa ni taratasi tu coz huwezi kufanya manunuz yeyote popote pale kwani itakuwa imeondolewa kwenye mzunguko nadhani ni miaka 10 wao hawasuhili mpaka ela ichanike au kuchakaa kama tunavyofanya ss
Asante daudi bilali.
Kumbe kwer upo hai[emoji1]
Ninavyoelewa sio hivyo! Huwezi kuipandisha dhamani fedha kwa kuificha, kinachopandisha dhamani fedha ni jinsi inavyohitajika(demand for money), ili fedha yetu iwe na dhamani, kinachotakiwa ni kuwa na bidhaa nyingi sana zinazouzwa kwa Shilingi, mfano, watalii wakija wengi sana, na tukalazimisha watumie shilingi, au tukiuza sana madini yetu kwa shilingi, mazao yetu kwa shilingi, kwa hivyo vichache tu, utakuta kila mtu anatafuta shilingi, so dhamani yake inaenda juu, fedha ni bidhaa, ikihitajika sana dhamani hupandaduuuh kumbe inamaana pesa mfano za kwetu sisi tunaweza tukacontroll thamani yake ipande au ishuke kwa kuiadimisha mitaani na nchi zingne? au cjamwelewa vizur #izzo!
Mkuu umeeleza vyema sana lakini vipi kuhusu uaminifu wa makampuni hayo?
Hayawezi kufanya janja janja ya kutengeneza pesa za ziada na kuziingiza kwenye mzunguko kiaina?!
Najua kuna namba za fedha na ugumu kidogo wa hili ila wanaaminiwa vipi? na kwa nini kusiwe na jinsi ya kutengeneza fedha zetu hapa?
Mkuu kumbuka hata majangili wanatengeneza fedha na kujaribu kuziingiza kwenye mzunguko hata marekani mpaka Leo wanapambana na kuzuia fedha bandia kuingizwa katika mzunguko wao kazi nyingine ya kikosi cha secret service si kumlinda rais wa marekani peke yake pia na kuhakikisha federal reserved system FRS ya marekani inakuwa safe and secure secret service walisha wai kukamata mabilion ya fedha bandia katika godawn huko Colombia
kama nilivyo sema hapo mwanzo kampuni hizi zote zinakuwa controlled by the government pia kila kampuni inakuwa na material ya utengenezaji wa zile karatasi inakuwa ni top secret au classified kwa kampuni husika na ndo kitu kinachofanya kampuni kupewa tenda kwani isingekuwa hvyo kumbuka kuwa kuna watu wanatengeneza fedha bandia pia utakiwa kujua kinacholindwa si fedha bali makaratasi ya kutengeneza fedha
kuhusu ss kutengeneza fedha zetu hapa tunaweza bt kuna vitu unatakiwa kujiuliza kama tunaweza? ?
1 je thamani ya fedha yetu nani atakuwa anaicontrol kulinganisha na fedha za wenzetu kwani tunaweza kuwa tunaprint tuuuuu mifedha mfano Zimbabwe kuna mpaka noti ya laki moja
2 je tuna technology ya kutengeneza fedha zetu ili watu wasiweze kucopy na kutengeneza zao na kuziingiza kwenye mzunguko
3 maswala ya kifedha duniani yanakuwa controlled by IMF na WB bt kuna nchi hazipo kwenye mfumo wa kinyonyaji wa IMF mfano Iran na china tatizo lake linakuja pale unapotaka kufanya international transaction kwani bank zako zinakuwa hazipo kwenye mifumo ya kibenk zingine mfano ilifikia kipindi ukitaka biashara Iran itakulazimu uende na fedha kwani bank zao zilikuwa hazipo katika mfumo wa mabanki mengine so huwezi kufanya wire transaction
Asante kwa Elimu hii nzuri, lakini iweje nchi zetu zinauwa maskini wakati uchumi unapimwa kwa kiwango cga fedha?? Mfano Rais Magufuli anataka kununua ndege ya bilioni 500 za kitanzania sawa na Usd 20Milioni, kwanini ahangaike kukopa huko nje badala ya kuagiza kampuni yetu ya Ujerumani ikatengeneza bilio 500 za kitanzania tuka exchange into usd tukaagiza ndege yetu kanada bila kukopa kopa na kupiga watu marisasi?
Umeuliza: Kampuni gani inahusika na kutengeneza pesa?
Jibu ni Benki Kuu ya kila nchi. Benki Kuu ya kila nchi ndo inahusika na kutengeneza pesa. Kwa hiyo sio kampuni, bali ni taasisi.
Ila kama msingi wa swali lako ni kutaka kujua kuwa ni kampuni au taasisi zipi zinatengeneza noti na sarafu, majibu ndo kama hayo uliyopewa na wadau huko juu.
Hata hivyo inatakiwa ujue kuwa anayehusika na utengenezaji wa noti na sarafu ni Benki Kuu ya nchi husika. Yeye Benki Kuu ndo ataamua kuwa tenda ya kuchapisha noti au sarafu ampe nani, lakini anayehusika ni Benki Kuu.
Na pia utambue kuwa noti na sarafu ni sehemu tu ya pesa. Lakini pesa yenyewe ni hisabati za kiuchumi. Ni namba inayotengenezwa kwenye computer. Unapoona namba mahali popote pale ujue kuna hisabati imetumika. Kwa hiyo unapoona ile 10,000/- kwenye noti, ni matokeo ya hisabati hayo.
Kwa hiyo kuna hela zinatengenezwa na Benki Kuu, au chini ya usimamizi wa Benki Kuu, lakini haziwekwi katika mfumo wa noti na sarafu. Zinaishia katika mfumo wa kidigitali. Lakini ni pesa halali na zinatumika kununua mali kama nyumba, magari, n.k.
Ninavyojua angola zimbabwe wana mitambo ya kutengeneza hela mizuri tu. Hata tz tunaweza kua na yetu. Ila kutengeneza hela ya nchi kuna mambo makubwa ya viwango na kuaminiana.Pesa ya Tanzania inatengenezwa Ujerumani, kama Sikosei na huwa inatangazwa zabuni na mshindi ndiye anayechukua tenda na malipo ni kama tenda nyingine tu mkuu!!
Ila nasikia pesa ya Marekani inatengenezwa na freemason ingawa sina uhakika sana!!