cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 112,159
- 181,307
Basi sawaaBasi kazi ninayo
Basi sawaaBasi kazi ninayo
Shukrani.
Mimi sio mtaalam lakini najua....Nami natamani sana waje wataalam watuambie haya mambo
🙏🙏Kila nchi inautaratibu wake katika utengenezaji wa fedha zake mfano tuzungumzie Marekani coz ndo fedha yake utumika Kwa wingi duniani kule kuna taasisi inaitwa Bureau of Engravin printing (BEP) hii ni taasisi inayoshugulikia uchapishaji na usambazaji wa fedha ya Marekani kuna viwanda viwili ndani ya Marekani kimoja kipo fort Worth TEXAS na Kingine kipo nje kidogo ya jiji Washington karibu na yaliyokuwa makao makuu ya kampuni na viwanda vya kutengeneza ndege vya Boeing Everett Washington bt now Boeing makao makuu wameanishia north riverside illinois Chicago hapo ndo sehemu zinapochapishwa fedha za marekani na ulinzi wa hapo kiwandani ni mkubwa sana mfanyakazi aruhusiwi kutoka hata na kipande cha karatasi ingawa kipindi cha nyuma kuna mfanyakazi mmoja alishawahi kuiba fedha Kwa kujiwekea POP na alikuwa mjamzito so hakuwa anapita kwenye scanner kutokana na hali yake so akawa anafanyiwa ukaguzi wa kupapaswa kumbe alikuwa anazisokomeza ndani ya POP lililokuwa kwenye mguu wake
Bt duniani kuna makampuni yanayotengeneza fedha mengi yako nchi za ujerumani UK na Swiss bt yanakuwa controlled by Government so kama nchi inataka kutengeneza fedha zake wanatangaza tender za makampuni yana shindana ya mshindi anapata tenda ya kutengeneza malipo mnalipa Kwa dollars coz fedha nayo ni bidhaa inauzwa kama zilivyo bidhaa nyingine
Kwa Tanzania fedha zetu tunazitengenezea Germany na kusafiliswa kwenye containers mpaka kwenye port zetu then utaratibu wa custom ufanyika kuzitoa ni kama mizigo mengine inavyotolewa bt mzigo huu ni HVC high value cargo na ulinzi wake ni mkubwa sana kumbuka duniani kinacholindwa si fedha bt ni makaratasi ya kutengeneza fedha kwani tofauti ya fedha bandia na halali ni karatasi tu bt kila kitu vinaweza kufafana
Madini ya nguvumkuu MC7 kwanza si kweli hata kidogo kuwa zebki au mercury inatumiwa kutengeneza fedha materials yanayotumika kutengeneza fedha ni
1 cotton fiber 80-99%
2 wood fiber 1-3%
3 titanium white 2-3.5%
4 polyamide epichlorohydrin 2-3.5%
5 aluminium chloride
6 melamine,formal dehyde resin , na animal grue
so unaweza kujiuliza kama material ya kutengeneza fedha yanajulikana why majangili wanatengeneza counterfeit money?? jibu ni kwamba unaweza kujua material ya kutengeneza kitu husijue formula ya utengenezaji sasa formula ya jinsi ya kuchanganya hizo kunaitaji natural resources ,critical moments in time and human engineer hv nyote ndo vinafanya tuweze kuyatumia haya makaratasi yenye thamani kuhusu mercury hizi mala nyingi hutumika kwa kazi zingine hasa migodini
Shule kubwa sana hiikila nchi ina kitu kinaitwa money policy act MPA huu ndo mwongozo wa central bank zote duniani ikiongozwa na WB mfumo huu ndo unawaongoza katika ku supply and monitoring currently so kuhusu ni kiasi gani wanachapisha inategemea na maitaji ya nchi husika kuna msemo wa kibiashara unasema ukitaka kukipandisha kitu thamani kifanye kuwa adimu pia ukitaka kukishusha kitu thamani basi kifanye kipatikane kwa wepesi so chaguo ni lako kuchapisha tuuuuu au kuchapisha pale inapoitajika
kwa wenzetu yani federal reserve bank and bank of England pia na bank of Canada hawa ndo wanacontrol karibu institutions zote za fedha ikiwamo WB na IMF so ni kama money policy act wanazizibiti wao
lakini thamani ya fedha hawapangi wao kama ingekuwa hvyo basi dollar ndo ingekuwa na thamani kuliko zote bt kuna fedha za nchi zingine zimeizd thaman usd mfano Swiss fanc pound na dinar ya Oman
pia wenzetu wana mfumo mzuri mfano marekani kiwanda cha kutengeneza fedha cha fort Worth cha TX na cha Washington cha tour and visitor centre kwa pamoja vinauwezo wa kutengeneza kiasi cha dollar million 28 par hour na pia wameweka expire date ya ela yao ili kuweza kujua ni kiasi gani cha fedha kipo katika mzunguko duniani na pia kudhibiti mijitu inayoficha ela kwenye masandarusi na ndoo coz ikifika mda fedha inaexpire so ikiexpire mkononi mwako itakuwa ni taratasi tu coz huwezi kufanya manunuz yeyote popote pale kwani itakuwa imeondolewa kwenye mzunguko nadhani ni miaka 10 wao hawasuhili mpaka ela ichanike au kuchakaa kama tunavyofanya ss