Kampuni za Kitapeli Tanzania (Scam companies)

BANDOKITITA

JF-Expert Member
Oct 4, 2022
1,177
2,281
Kuna maswali mengi fikirishi juu ya uchipukaji huu wa kampuni za kitapeli (Scam companies) hapa Tanzania. Kampuni hizi ni pyramid/ponzi schemes na zimekuwa zikiwaumiza Watanzania sana, na pesa inayopatikana baada ya kukusanya kwa raia huenda kwenye mzunguko wa pesa nchini isivyo kihalali.

Kwa uchache zimekuwepo kampuni kama D9, SCATEC, KALYNDA, KIJIJI (tena hii imeanza juzi tu rarehe 29/09/2022 jijini Dar es Salaam) na nyinginezo nyingi. Hii ya KALYNDA ndio imezima juzi na kuwaacha watu na vilio.

Maswali ya kujiuliza:
1) Hivi serikali haijui uwepo wa uhuni huu hapa nchini? Nchi nyingi hasa Ulaya na Amerika walishapiga marufuku huu utapeli, maana unarudisha nyuma maendeleo ya watu wake.

2) Kama serikali inajua, je, imebariki Tanzania kuwa shamba la bibi? Yeyote toka nje au ndani anaweza kufanya atakavyo hata kuumiza raia kiuchumi pasipo kuguswa?

3) Kinachofanywa na hizi kampuni ni "ULAGHAI", je, serikali imeruhusu kitendo hiki ilihali ikijua kitendo cha utakatishaji fedha kinaua uchumi wa nchi?

4) Kama serikali haijaruhusu uhuni huu, je, hawa wenye kampuni wameizidi serikali akili na hivyo haina cha kuwafanya? Je, kati ya kampuni hizi na serikali nani ana mkono mrefu?

5) Je, serikali inapata mapato kutokana na kampuni hizi, kama inapata basi inajua kinachoendelea, kwa nini haichukui hatua?

6) Kampuni hizi zimekuwa zinatumia hadi vyombo vya habari vya humu ndani kama redio na TV mfano KALYNDA E-commerce imetumia redio nyingi tu na TV kama ITV. Je, serikali inaweza kusema haijui kinachoendelea?

7) Kwanini kampuni hizi zimeibuka kwa wingi wakati huu na wala sio hapo kabla? Huko nyuma zilikuja kadhaa na baadhi kuchukuliwa hatua na serikali. Mfano mzuri ni DESI. Kwanini sasa hatua hizo hatuzioni au ndio tuseme serikali haina taarifa?

NB:
a) Watu wamekuwa wakiwachukulia wanaoweka pesa kama wajinga na wapenda vya bure (mtelezo). Lakini ukweli ni kuwa wanaoingia katika mtego huu wa kitapeli wengine ni wasomi tena wenye elimu ya chuo kikuu. Hapa tukubali/tukatae tatizo hili linasabsishwa na hali ngumu ya maisha ya wananchi. Hivyo mtu anatafuta njia yoyote iwe halali/haramu kwa nia ya kujipatia kipato.

b) Tusiwanyooshee vidole wale wanaopigwa na hizi kampuni, kuna watu wengi wamelizwa kwenye biashara, ununuzi wa viwanja, nyumba, n.k, je hao nao ni wajinga?

c) Serikali ichukue hatua za haraka kunusuru watu wake na uchumi wa nchi. Iwakamate wamiliki wa kampuni hizi wasukumwe ndani na baadae mahakamani.

d) Kuwe na adhabu kali kwa wamiliki wa kampuni hizi za kitapeli, ikiwezekana adhabu iwe kunyongwa maana hata wao wamekuwa wanasababisha vifo ya mshituko wa moyo kwa ndugu zetu wanaowekeza pesa zao.

e) Serikali ikague kwa kina vibali vya wageni wanaokuja nchini kwa lengo la kufanya biashara, maana wengi wa watu wenye kampuni hizi watoka nje ya nchi hasa Nigeria na kwingineko.
 
Watu wanajiunga bila kuihusisha serikali wakipigwa wanaihusisha. Kampuni zinasajiliwa kwa ajili ya kazi nyingine wakishasajiliwa wanaanzisha wizi huu. Cha muhimu ni jamii kujua namna ya kujiepusha na aina hii ya utapeli. Wanapoingia na kutoa vitita vyao hakuna anaelalamika au kutoa report kwa mamlaka na BOT. Wakilisha ndio wanakuja mbio.
 
Serikali isimamie na upuuzi wenu,iko siku utalaumu Serikali kuingia kati ukinyimwa unyumba
 
huu wizi umekuwa ukifanyika kwa mtindo unaofanana, kwa nini mtu ujiingize kwenye shughuli hiyo
kabla ya kalynda, watu waliibiwa na idea debator na humu jf ilipigiwa upatu.
idea debater inafanana kila kitu na hiyo kalynda.
Pamoja na maangalizo kutolewa humu ila watu wanajiunga wanasema wanatake risk halafu bado unailaumu serikali
Pitia huu uzi uone: Niulize chochote kuhusu Kalynda E-commerce

Ipunguzie majukumu serikali maana ponzi scheme inafamika kirahisi tu
 
Na Watu wanashawishika vipi na kuingiza hela huko? hili ndio swali huwa najiuliza.

Ila kwa Taifa linaloamini ushirikina na miujiza hayo yanawezekana tu.

mimi sijawahi kujiingiza huko maana huwa najiuliza swali moja tu, "kwa nini Mtu au Watu wanipe pesa mimi kirahisi tu?" Mimi nitamuelewa Mtu akiniambia njoo ulime hili shamba nikulipe lakini sio eti lete mia tano upate elfu moja...yeye anaitoa wapi hiyo mia tano...na kwa nini asibaki nayo yeye akupe wewe?.
 
NCHI HII INA WAJINGA WENGI SANA

ACHA WAPIGWE TU,MAANA WAKIAMBIWA HAWASIKI

ova
 
Hakuna chombo cha habari kimetumika kuwa makini ni account fake ile ya ITV zipo kibao mpaka za Facebook ,twitter na Instagram ambazo ni fake zipo za It,tbc, millardayo kuwa makini na msipende kitonga
 
Hakuna chombi cha habari kimetumika kuwa makini ni account fake ile ya ITV zipo kibao mpaka za Facebook ,twitter na Instagram ambazo ni fake zipo za It,tbc, millardayo kuwa makini na msipende kitonga
Ni jukumu la serikali kulinda raia wake, werevu na wajinga. Serikali haiwezi kuachia matapeli wabuni mbinu na kufanya lolote watakalo eti kwa sababu ni jukumu la raia kujiongoza.
 
Ni jukumu la serikali kulinda raia wake, werevu na wajinga. Serikali haiwezi kuachia matapeli wabuni mbinu na kufanya lolote watakalo eti kwa sababu ni jukumu la raia kujiongoza.
Nchi Kama Iran wamekamata wale promoter hapa bongo wapo kibao na wanawaangalia kama iyo kampuni Kuna jamaa kule twitter anaitangaza na kuingia kifua ni tapeli amejipa jina la mshauri serikali na kaweka bendera kabisa kumdanganya watu huyu ni WA kushughulikia kabisa.
 

Attachments

  • Screenshot_20221009-121606.png
    Screenshot_20221009-121606.png
    238 KB · Views: 20
  • Screenshot_20221009-121620.png
    Screenshot_20221009-121620.png
    131.8 KB · Views: 18
BOT walishasema zamani sana kuhusu aina hii ya biashara ya utapeli mtandaoni. Yaani mnajiunga uchochoro ni huko halafu mnakuja kulalamika hadharani baada ya kuigwa. Who to blame zaidi ya udhaifu wenu wa kutaka pesa za miujiza?
 
Back
Top Bottom