Kabla yakuingia kwenye haya mambo watu watafute ushauri wa kisheria. Tafuta wakili akushauri kitaalam kabisa lipa gharama z ushauri alafu kajilipue. Yakibumburuka wewe rudi kamalizane na wakili wako aliyekupa huo ushauri.
Ni rahisi ila ghali, ukija kwetu na sisi tutakupa gharama kubwa ya ushauri, alafu baadae hatutakushauri uingine kwenye.hio biashara, kama ukiingia uingie ukiwa unafahamu kuwa hatutahusika tena maana tulikupa.ushauri usiingie.
Kabla hujaingia kwenye hizo fursa jaribu kufuatilia yafuatayo:
1. Kama ni kampuni usajili wa BRELA hapa fanya Official search kabisa utalipa (20k)
2. Fuatilia TRA rekodi yao
3. Fuatilia TIC kama ni uwekezaji
4. Fuatilia BOT kama ni fedha
5. Angalia sheria zinazosimamia mambo wanayofanya hao watu, je wameendana na takwa la sheria husika?
6. Soma makubaliano yenu vizuri na uyaelewe
7. Kwa Apps soma terms, conditions na privacy policy vizuri na uielewe
8. Fuatilia, fuatilia, fuatilia
Mfano mdogo unaoendana na namba 5 hapo juu ni hii Kalynda, wanachofanya.ni jinai kwenye sheria ya makosa ya kimtandao Tz na bado watu wameingia kushiriki jinai, moja kwa moja unaona kabisa hii kampuni sio, sababu huwezi ruhusiwa kufanya jinai.
Jambo lingine ni vipi data za watu zinalindwa na hiyo Kalynda, sababu wanatumia data hizo.hizo kufanya watu.waamini bidhaa inauza (uongo/utapeli) wakati mtu ameweka tu comment na nyota tano kwenye bidhaa

yaani na atakayenunua.hiyo bidhaa naye kaibiwa, kwa maana rahisi watu woote wanaofanya hiyo Kalynda nao ni waalifu maana wameshiriki ualifu.
Siku yakibumburuka wataambiwa wameshiriki uhalifu chini ya sheria ya makosa ya.kimtandao, sheria.ya utakatishaji fedha, kanuni ya adhabu na sheria ya kupambana na magenge ya uhujumu uchumi


, alafu wataambiwa achaneni na hii mambo kabla hatujawashtaki. Watarudi makwao na vilio.