Kampeni ya Ubunge Arusha Mjini - Batilda Burian Vs Lema

Kampeni ya Ubunge Arusha Mjini - Batilda Burian Vs Lema

KATI YA BATILDA NA LEMA YUPI ATIBUKA KIDEDEA?


  • Total voters
    52
Ngongo na Nyumbu,

Kama hizi taarifa ni za UONGO basi lazima MFUNGIWE MILELE na Computer zenu.

Jana nimeomba Wa 16 afungiwe. Ni ajabu tangu mwanzo nilianza kupata wasiwasi kuwa jamaa ni PANDIKIZI la CCM. Alianza kwa kujifanya ni CHADEMA na Mtetezi wa Slaa ila mwisho, akazidisha Chumvi kwenye Mboga. Wa 16 lazima afungiwe kwa kujiita yeye ni USALAMA WA TAIFA na ikibidi atafutwe hata kama yupo nje ya nchi.

Kama mtu anaandika hana uhakika basi aseme TETESI. Ila Ngongo kidogo ninaweza kuamini kwani amekuwa akisema mengi sana ya kumshambulia mgombea wa Chadema na yanakuja kuandikwa kwenye magazeti. Leo nashangaa kuwa yuko upande wa CHADEMA (kwa huruma tu). Au labda kwa sababu Uchakachuaji wa CCM unaweza kudhuru pia CUF? Maana imesemwa "... Adui wa Adui yako, ni Rafiki."
 
Mwizi ni mwizi tu! Hawapigwi kwa sababu ya vyama vyao ila wanapigwa kwa sababu ni wezi kama wezi wengine.
Wezi wa simu wanapewa kichapo,wakati mwingine hadi kufa je, hawa wezi wa kura wanaotuletea wezi wakubwa kama mafisadi papa tuwafanyeje?Kama TAKUKURU IMESHINDWA au imeingia kwenye mpango...... acha wananchi wachukuwe hatua,ikendelea hivi itakuwa njia rahisi ya kukomesha rushwa wakati wa chaguzi.
 
Kimsingi nilikuwa sijabahatika kupata habari hizi.
Lakini kwa mwendo wa Batilda wa kuhonga, suala kama hilo kutokea si la ajabu!...Hali ni mbaya jamani Arusha!
The thing is hatakiwi Arusha, labda aombe zile karatasi za Tunduma zije kumwokoa...lol!
 
jamani jamani chadema acheni uvurugaji amani, huu ni uongo mwingine tena kama wa drslaa aliozusha na kuaibika kisha kupoteza imani kwa waliompenda uzushi uliokanushwa wa gari la vipodozi kubeba kura,
Hii ilotokea huko Mateves, kwa hiyo waandishi wa hapa jamvini ni wazushi tu wanasikia habari ziszoza kweli na kupublish wengine , themi, wengine olasiiti, jamani msipotoshe watu.

Hili tukio lilikuwa la akina mama wa uwt waliokuwa na vikao vyao wala dr. hakuwepo, na chadema walienda kufanya mkutano wao wa hadhara karibu na hapo yaani walikuwa petrol station na hawakupata watu hata mmoja ila wale waliokuja nao mjini, hii ni mara ya pili kwenda huko na kukosa watu wa kuwasikiliza. Ndipo walipodokezwakuwa hamuwezi kupata watu maana ccm wamo ndani ya ofiici yao wanagawana pesa, kwa ghadhabu vijana hao walivunja mlango wa ofisi hiyo na kuanza kuwapiga kina mama, hao sana kisha kuwaitia polisi na walisachi hiyo gari nakuipiga mawe aina ya vxlandcruiser mali ya uwt makao makuu dsm.
Kufika polisi baada ya uchunguzi ikagundulika ukweli wakaachiwa hao kinamama wakaenda kutibiwa na wanaumwa kweli na wamewekwa ndani watu watatu wa chaga development manifesto.

MY TAKE: HIVI NDIVYO TUNAVYOKUSUDIA MABADILIKO ? MABADILIKO YA KUMWAGA DAMU WALIOKUSUDIA KUMWAGA YAMEENZA KUTAKE CHARGE. UNAPOKUSUDIA KUUWA WENZAKO HAUJUI KAMA WEWE UTAPONA AU UTAKUWA WAPI NA JAMAA ZAKO
 
Kuna taarifa kwamba mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la Arusha mjini amepigwa na wananci wenye hasira baada ya kuonekana akifanya vitendo vinavyoashiria rushwa maqeneo ya Fire Arusaha, ambako kimsingi ndiko alikozaliwa. Taarifa hii imepatikana kwa kupigiwa simu na mdau aliyepo Arusha na ambaye pia ni kada wa CCM.
Tunaomba akina Ngongo na Paka Jimmy watutaarifu zaid kuhusu tukio zima, maana nasikia hata gari yake imeharinbiwa na tayari taarifa ziko polisi......

Poleni wote mlioathiriwa na tukio zima


Twasikia kumbe Jana hapo Arusha Palikuwa na vuta nikuvute pia kuna mahari CCM walienda na walikuwa wanatumia gari la IKULU na hii ilijulikana baada ya dreva huyo kupewa kibano na wakereketwa wa CHADEMA na ndipo dreva akasema kweli hilo gali ni la IKULU na likapelekwa police na huko ndiko lilikwenda kwa Ukaguzi na baadhi ya watu wanasema ilikuwa na vitenge , Tshirt za CCM kwa bahati mbaya hawakufanikiwa kupata PESA na inavyosemekana mpaka tunavyoenda mitamboni hilo gari lipo police hapo kituo cha kati Arusha, Paka Jimmy fuatilia hiyo issue utu updates tafuadhali.


Mei natoa tena angalizo kuwa hizi chaguzi ziishapo hiyo 31/10/2010 zisije zika acha nyuma huku na kujenga matabaka ya hawa ni CHADEMA na hawa ni CCM na hawa ni CUF na ndio Athari nayo iona mbeleni kwa sasa. Maana Ubabe umeisha tanda kwa hali kubwa esp kwa haya majimbo Nyamagan, Iringa mjini, Mbeya Mjini,Arusha Mjini, na Asilimia kubwa ni wale wanao wa support CCM ndio wana toa vitisho kwa hawa wa vyama pinzani huku hawajui wanajia haribia kura
 
Jamii forum mpo juu. nikiwa kama mwanachama mpya ambaye leo hii ndo mara yangu ya kwanza kutoa maoni yangu. ningependa niwashukuru wanachama wenzangu wa jamii forum kwa michango/mawazo yenu mazuri yenye ukweli isipokuwa hao wachache wenye chembembeche za ufisadi wanaopinga siasa za ukweli zinazojionesha wazi.
Nikija kwenye swala la huyu Batilda ana kazi ya ziada ya kufanya kuliokoa jimbo lake kama atathubutu, yeye anafikiri wananchi bado wamelala usingizi wa pono kumbe watu tupo makini tunafuatilia kila jambo kwa ukaribu na kwa kutumia busara. Hongera sana kwa hao wafanyakazi waliomuwekea pozi la kufa mtu na wakimuonesha alama ya vidole viwili wakimaanisha hana chake hivyo ale kona fasta kabla hajageuzwa ndafu wa shughuli. Huo ni mwanzo tu, wananchi tupige kura tumchague yule anayefaa, yule aliyeweza kuwata hadharani mafisadi bila ya kuhofia chochote. Kumbe Tanzania ina vichwa vilivyotulia kama rais wetu mtarajiwa Dr. Slaa.😛ray:​
 
Kimsingi nilikuwa sijabahatika kupata habari hizi.
Lakini kwa mwendo wa Batilda wa kuhonga, suala kama hilo kutokea si la ajabu!...Hali ni mbaya jamani Arusha!
The thing is hatakiwi Arusha, labda aombe zile karatasi za Tunduma zije kumwokoa...lol!

Hapo ndipo nami nashindwa elewa kama hutakiwi why do you force kwa wananchi wasio kutaka je Utafanyanao kazi kivipi?
Na hao Campaigner wake wataka kuniambia hawajui kutizama hali ya kisiasa inavyokwenda au ni njaaa ndio zinawasumbua? Twasikia hadi mgombea Udiwani(CCM) kata fulani maarufu sana hapo Arusha kabla hajaenda kwa jukwaa lazima ashtue bear kadhaaa za kutoa woga? sasa huko tuendako ni kubaya.

Mkia ninao uhofia sana ni huko Arusha maana watu wa huko ukichanganya na waarusha na wameru khaaaaaa mbona baraaaaaaa usipaime

Free Democracy ikifuatwa patakuwa na amani sana hapo angalieni mifani kama hapo kenya mpani karibu sana na arusha 6hrs drive to nairobi walipitia machafuko na wakabadilisha katiba na sasa Katiba inaaanza waengua mmoja baada ya mmoja na ndilo sisi watanzania twatakiwa kufanya mabadiliko bila ya kufanya umwagaji damu au vurugu yeyote hile

 
Mwizi ni mwizi tu! Hawapigwi kwa sababu ya vyama vyao ila wanapigwa kwa sababu ni wezi kama wezi wengine.
Wezi wa simu wanapewa kichapo,wakati mwingine hadi kufa je, hawa wezi wa kura wanaotuletea wezi wakubwa kama mafisadi papa tuwafanyeje?Kama TAKUKURU IMESHINDWA au imeingia kwenye mpango...... acha wananchi wachukuwe hatua,ikendelea hivi itakuwa njia rahisi ya kukomesha rushwa wakati wa chaguzi.

TAKUKURU yaaani sio chombo cha kukiongelea tena hapa wakiitwa kwenda kushika deal ya watu CCM hawaendi hata muwafanyeji ila ya vyama vingine wanakuja faster utadhani wanampeleka mgonjwa ICU Hosea its time you must Gooooooooooo huwezi kazi, Maana hamjajifunza mkajua jinsi ya kuongoza Taasisi hizi katika karne hii ya vyama vingi kabisa

 
regardless ya huyu mama nia yake, siungi mkono kupiga wanawake tena na mawe hasa wakiwa wajawazito... na pia sielewi kimbelembele cha chadema mkoa kutoa tamko maana hapo itathibitisha kwamba ni wao wamefanya

lets not get into the new level ya jungle, we can do better bila kupiga wajawazito

BTW, kitendo kinachoashiria rushwa ni kipi?

Huyo mama ana Mimba? so mtu mwenye Mimba ndo amehalalishiwa kuwapa watu rushwa? mbona mzee sikelewi na kukusoma? Rushwa inabaki kuwa dhambi no matter who is involved, and what thpe of gender was involved.
 
[QUOTE:zubeda]
uzushi mwingine huo!!!! Yaani kwanza unadai kuna taarifa kwamba,,, halafu pili ili kusisitizia uwongo wako unapakazia ati kada wa ccm wa arusha ndie aliekupigia simu na kukupasha hizi!!!
Haya wewe kada wa chadema unashirikiana vipi na kada wa ccm? ......

Kama wanashirikiana wewe kinakuuma nini? Unadhani kutofautiana vyama ndio kuwa maadui? ... grow uP!!

"Tena kupashana habari za kumwaga damu za watu?"

Kwa hiyo ulitaka watu wasijulishwe kuwa kuna tukio kama hilo siyo?

"Jamani sasa na huu uchaguzi heri uishe tu! Maana kila siku tutapashwa uzushi tu, mara utasikia masanduku ya kura yameingizwa toka zambia, mara fulani kafa kumbe yuko hai, mara ccm wameshaiba kura kumbe hata uchaguzi haujafanyika!!! "

kama haya yanakukera sana .. just log out and dont log in mpaka after 31/10 !

"Sasa chadema mukiambiwa kuwa munataka kuleta machafuko nchini kweli munasababu ya kukanusha? Mbona dalili zote zinajitokeza kuwa kila penye fujo na umwagaji damu chadema wanahusika mwaka huu!!!"

Ni kweli, wanahusika kwa sababu ndio walengwa; hope ulisikia kule Tarime, Musoma , mwanza etc ... kote wana CHADEMA walipigwa , where the hell were you?!!

"Mbona hatusikii vyama vingine vikidai kumwaga damu isipokuwa chadema!!! Nani aliewaroga chadema uchaguzi huu!!! Mimi sitashangaa kusikia hivi karibuni kuwa kontena za silaha zimekamatwa bandarini zikiwa na stakabadhi za chama cha siasa!!!"


Mwaka huu tabu tupu; hata vilaza na wenye upupu wote .... ndani ya uwanja.
 
I am not supporter of instant justice!the matter could be reported to police or PCCB by good samaritarians,in steady of taking illegal action, which is offensive!
 
Batilda imetosha haya ona sasa unalazimisha ushindi ambao haupo. HEBU ACHANA NA MAKAMPENI YASIYOKUSAIDIA NA BADALA YAKE ONGEA NA JK AKUANDALIE VITI MAALUM VYA UPINZANI
 
Heshima kwenu,

Gari iliyokamatwa inasadikiwa ni usalama wa taifa [ikulu/ofisi ya waziri mkuu] wahusika walikuwa wanagawa khanga,tshirt,kofia na vipeperushi kwaniaba ya Dr Batilda.CHADEMA wakapigiwa simu walipofika eneo la tukio [Matevesi] wakalizingira gari na kuanza kutoa kichapo cha hatari polisi [FFU]walipofika eneo la tukio walikuta watuhumiwa katika hali mbaya sana.

Kwakuwa gari iliyokamatwa ni mali ya serekali [UWT] nina mashaka sana kama polisi watatenda haki au watakuwa na ubavu wa kuwashitaki wafanyakazi wenzao.Inashangaza sana role ya UWT badala ya kuangalia usalama wa taifa wanafanyakazi ya usalama wa CCM !.
Haya ni matumizi mengine mabaya ya gari la serikali kutumika katika kampeni za chama.
 
Ninaomba utulivu wakati huu Jemadari mkuu wa Chama Chetu ndugu Dk Slaa ambaye ni mtetezi wa watanzania wote anapokaribia kuitwaa dola. Tuache papara najua kama kama umezoea kushinda tu siku ukiona unashindwa lazima umn'gate mtu sikio, kama nadanganya kamuulize Mike Tyson, CCM inageuka tyson muda sii mrefu ila ushindi wa 2005 ulikuwa wa mwisho kabisa katika historia yake.
 
jamani jamani chadema acheni uvurugaji amani, huu ni uongo mwingine tena kama wa drslaa aliozusha na kuaibika kisha kupoteza imani kwa waliompenda uzushi uliokanushwa wa gari la vipodozi kubeba kura,
Hii ilotokea huko Mateves, kwa hiyo waandishi wa hapa jamvini ni wazushi tu wanasikia habari ziszoza kweli na kupublish wengine , themi, wengine olasiiti, jamani msipotoshe watu.

Hili tukio lilikuwa la akina mama wa uwt waliokuwa na vikao vyao wala dr. hakuwepo, na chadema walienda kufanya mkutano wao wa hadhara karibu na hapo yaani walikuwa petrol station na hawakupata watu hata mmoja ila wale waliokuja nao mjini, hii ni mara ya pili kwenda huko na kukosa watu wa kuwasikiliza. Ndipo walipodokezwakuwa hamuwezi kupata watu maana ccm wamo ndani ya ofiici yao wanagawana pesa, kwa ghadhabu vijana hao walivunja mlango wa ofisi hiyo na kuanza kuwapiga kina mama, hao sana kisha kuwaitia polisi na walisachi hiyo gari nakuipiga mawe aina ya vxlandcruiser mali ya uwt makao makuu dsm.
Kufika polisi baada ya uchunguzi ikagundulika ukweli wakaachiwa hao kinamama wakaenda kutibiwa na wanaumwa kweli na wamewekwa ndani watu watatu wa chaga development manifesto.

MY TAKE: HIVI NDIVYO TUNAVYOKUSUDIA MABADILIKO ? MABADILIKO YA KUMWAGA DAMU WALIOKUSUDIA KUMWAGA YAMEENZA KUTAKE CHARGE. UNAPOKUSUDIA KUUWA WENZAKO HAUJUI KAMA WEWE UTAPONA AU UTAKUWA WAPI NA JAMAA ZAKO

Heshima kwako Subira,

Mkuu wangu angalia bandiko langu nimesema bila kukosea sakata lote limeanzia Kata ya Matevesi na chanzo changu cha habari ni sawa na chanzo cha Dr Slaa hakuna uchakachuwaji.Mkuu jana ulikuja na habari za Lema nikakupa ufafanuzi wa kutosha ambao nina hakika ulibaki unashangaa !.
 
Hakuna haja ya kumpiga jamani, wangefuata taratibu tu za kisheria hata kama hatafuatiliwa. Kumchapa lawama zitakwenda kwetu wapinzanimkwamba tumemfanyia fujo na kuwachafua wapenda mabadiliko na maendeleo. Mchapeni kwa kumnyima kura tu!

Huko nyuma sheria zimefuatwa lakini polisi na Takukuru wamekuwa mstari wa mbele kupindisha haki.

NEC haiwezi kumbeba mgombea anayevunja sheria zake za kutopiga kampeni baada ya saa kumi na mbili jioni. Sheriua ni msumeno na inauma pande zote mbili.

Hizo siyo kampeni ila ni mambo yake binafsi tu na hayalindwi na sheria ya uchaguzi kama yalikuwa yanafanyika baada ya muda rasmi uliowekwa na sheria............................
 
Kuna taarifa kwamba mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la Arusha mjini amepigwa na wananci wenye hasira baada ya kuonekana akifanya vitendo vinavyoashiria rushwa maqeneo ya Fire Arusaha, ambako kimsingi ndiko alikozaliwa. Taarifa hii imepatikana kwa kupigiwa simu na mdau aliyepo Arusha na ambaye pia ni kada wa CCM.
Tunaomba akina Ngongo na Paka Jimmy watutaarifu zaid kuhusu tukio zima, maana nasikia hata gari yake imeharinbiwa na tayari taarifa ziko polisi......

Poleni wote mlioathiriwa na tukio zima

Yap, ni kweli hayo yametokea sio fire kama mdau alivyosema ni kata ya olasiti, na gari liko police limevunjwa vioo. Na chadema wako Unga limited leo wanafanya mkutano, mmh ni bado dk chache mkutano uanze, sina uhakika sana kama mh Lema atazungumzia sakata hilo nitawajulisha zaidi wana JE
 
Ngongo na Nyumbu,

Kama hizi taarifa ni za UONGO basi lazima MFUNGIWE MILELE na Computer zenu.

Jana nimeomba Wa 16 afungiwe. Ni ajabu tangu mwanzo nilianza kupata wasiwasi kuwa jamaa ni PANDIKIZI la CCM. Alianza kwa kujifanya ni CHADEMA na Mtetezi wa Slaa ila mwisho, akazidisha Chumvi kwenye Mboga. Wa 16 lazima afungiwe kwa kujiita yeye ni USALAMA WA TAIFA na ikibidi atafutwe hata kama yupo nje ya nchi.

Kama mtu anaandika hana uhakika basi aseme TETESI. Ila Ngongo kidogo ninaweza kuamini kwani amekuwa akisema mengi sana ya kumshambulia mgombea wa Chadema na yanakuja kuandikwa kwenye magazeti. Leo nashangaa kuwa yuko upande wa CHADEMA (kwa huruma tu). Au labda kwa sababu Uchakachuaji wa CCM unaweza kudhuru pia CUF? Maana imesemwa "... Adui wa Adui yako, ni Rafiki."

Heshima kwako Sikonge,

Bahati mbaya umeshindwa kufuatilia mabandiko yangu sawa sawa.Simpingi Lema kwakuwa yuko CHADEMA nampinga kwasababu nayajua madhaifu yake mengi ambayo kwa namna moja yamechangia kurejesha nyuma harakati za mageuzi.

Mkuu Sikonge nikiona jambo baya siwezi kulipindisha kwakuwa nampinga Lema hiyo haitatokea kwangu hata siku moja nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.Mkuu unakumbuka hicho kiapo cha chipkizi enzi hizo?.
 
Huyu mama ni mtoa rushwa mzuri kweli mimi akinipitia nachukua na kura pia simpi, vijana wa arusha kuleni hela zake lakini hukumu yake 31. Oct. Yaani nasikia ana mbinu nyingi sana za kutoa rushwa hata akienda car wash anagawa elfu kumi kumi kwa kila anayemkuta pale halafu akiondoka anawaambia vijana msinisahau siku ya kupiga kura!!! pumbafu elf 10 ni hela kweli ya kununua uhuru wa mtu!!! I hate her.

Uhuru wa mtu haununuliwi kwa pesa, mambo ya kula nyumbu shku moja na kuteseka miaka 5 wakazi wa Arusha sasa basi.
Huyu mama ni mtoa rushwa mzuri kweli mimi akinipitia nachukua na kura pia simpi, vijana wa arusha kuleni hela zake lakini hukumu yake 31. Oct. Yaani nasikia ana mbinu nyingi sana za kutoa rushwa hata akienda car wash anagawa elfu kumi kumi kwa kila anayemkuta pale halafu akiondoka anawaambia vijana msinisahau siku ya kupiga kura!!! pumbafu elf 10 ni hela kweli ya kununua uhuru wa mtu!!! I hate her.

Uhuru wa mtu haununuliwi kwa pesa, mambo ya kula nyumbu siku moja na kuteseka miaka 5 wakazi wa Arusha sasa basi
 
. Mchapeni kwa kumnyima kura tu!
2005, marehemu Juma Akukweti hakushinda uchaguzi kwa kura za wapiga kura,ila alitangazwa mshindi na alikwenda "kuwakoga"wananchi kuwa hawana lolote licha ya wao kumnyima kura,lakini tume ya uchaguzi ndo ilimpa ubunge. Haikupita muda mrefu huyu jamaa akalaaniwa na sasa hatunaye tena (R.I.P). Kuna kila dalili kuwa mdada huyo na yeye huenda akapewa ubunge na tume ya uchaguzi kwa msaada wa chama shirikishi (TAKUKURU) so mpinzani wake ahakikishe hatembei na pesa mfukoni na awe na ulinzi wa kutosha maana inaonesha kuwa ccm "bora wakose urais" kuliko kumpoteza mdada huyo. Alifanya kazi nzuri ktk ishu ya Kabwe Zito.
 
Back
Top Bottom