Heshima kwako Nyumbu,
Mkuu hizi taarifa nilizisikia jana saa moja usiku nilikuwa maeneo ya Soweto napata kinywaji mleta habari alisema aliyepigwa ni kada wa CCM [mwanamke] kwakuwa aliyejeruiwa hakuwa Mama Dr Batilda sikufuatilia sana.Nasikia viongozi wa CCM na CHADEMA walikuwa kituo cha polisi jana usiku kushughulikia dhamana za wapenzi wao waliohusika moja kwa moja na sakata lenyewe.
Naambiwa kada wa CCM alivunjwa meno kadhaa kapelekwa Mt Meru kwa matibabu zaidi na utaratibu wa kupachika meno bandia unaandaliwa baada ya kupona majeraha.
Heshima kwako Gerad2008,
Mkuu tafuta sehemu niliposema Lema hana uhungwaji mkono wewe umesema 85 % sina tatizo hata kidogo tena ungeweza kuongeza 95%,hoja yangu imezungumzia ushiriki wa Lema kwenye tukio la ujambazi uliofanyika mwaka 1998.Mkuu Gerad2008 Mramba kaitia hasara serekali mabilioni ya fedha,serekali hii hii ya Kikwete imempeleka mahakamani usijekushangaa Mramba akashinda ubunge uko Rombo au asiposhinda utashangaa kapata kura nyingi tu.Mambo ya hovyo hovyo sana yanafanyika Tanzania wananchi wanaona ni mambo ya kawaida.
Usihangae na Ngongo anachuki binafsi na Lema angalia post zake zote hakuna jema kwa Lema ana jaribu kumnadi Lyimo wa TLP lakini Ngongo amengudua jamaa hauziki hata kwenye ukweli unaomhusu Lema anaupindisha mfano Arusha Lema anakubalika kuliko mgobea yoyote kwa nafasi ya ubunge lakini Ngongo atakwambia Lyimo ndiyo anaekubalika hasa sombetini ambako kuna wapinga kura wapatao 30,000 lakini cha ajabu Lyimo akifanya mkutano watu 60 ni mbinde kuwapata na subiri siku lema akitangazwa kuwa mbunge wa Arusha mjini sijui atakuja na pumba gani?Mkuu Ngongo,
Mbona unatuchanganya sana na upenzi wako kwa Dk Batilda?
Kama kuna ushahidi kiasi hicho kuhusu Lema, ni kwanini hajapelekwa polisi mpaka sasa?
Mie ninavyojua angeshaswekwa rumande haraka ili apishe Dk Batilda awe mbunge. Kuna nguvu kubwa ya Lowasa na JK katika kampeni za Dk Batilda, hivyo wasingeshindwa kusweka rumande Lema ili kipenzi chao apite. Leo hii tunashuhudia matiumizi makubwa ya pesa hapo Arusha ili tu Batilda apite, kwanini wasimkamate Lema na kumweka ndani mchezo uishe?
Jibu ni moja: Tuhuma hizo ni za kupikwa na hazina msingi wowote. Baada ya uchaguzi hutazisikia tena!
Kama ni kweli hiyo ndiyo dawa yao. Ukiwapeleka polisi wataachiwa wale. Sasa unaniletea fedha ya kununua utashi wangu na hekima niliyo nayo unifanye zuzu nitakufanyaje? Mimi nakudunda tu na 31.10.2010 nakunyima kura pia. Unakuwa na fimbo ya kwanza ya kumwonyesha mume wako na familia wakuuguze majeraha ya pili kuwaonyesha watanzania kwamba tumechoka na CCM na mambo yao yote
Haki inapokosekana uvumiliv hutoweka, amani pia hutoweka
Chonde chonde jihadharini na vurugu ili wasipate kisingizio
Na palipo amani (kama Tanzania) uharibifu huwa mkubwa sana
Chonde chonde jihadharini na vurugu ili wasipate kisingizio
nilijionea mwenyewe ushabiki usio na staha... arusha imekua kama kempu mbaya kweli!!! Jazba imeanza kutawala na hicho ndicho hasa ccm wanakitaka, very unfortunately wapinzani wameshindwa kusoma alama za nyakati
Heshima kwako Acid,
Mkuu mwendo wa kampeni Arusha ukiachiwa uendelee hakika Tarime nyingine itazaliwa Tanzania kwasababu ya upuuzi wa watu wachache sana.
kuna taarifa kwamba mgombea ubunge kwa tiketi ya ccm jimbo la arusha mjini amepigwa na wananci wenye hasira baada ya kuonekana akifanya vitendo vinavyoashiria rushwa maqeneo ya fire arusaha, ambako kimsingi ndiko alikozaliwa. Taarifa hii imepatikana kwa kupigiwa simu na mdau aliyepo arusha na ambaye pia ni kada wa ccm.
Tunaomba akina ngongo na paka jimmy watutaarifu zaid kuhusu tukio zima, maana nasikia hata gari yake imeharinbiwa na tayari taarifa ziko polisi......
Poleni wote mlioathiriwa na tukio zima