Samson Ernest
JF-Expert Member
- Aug 28, 2014
- 1,118
- 1,565
Kama utabiri utatolewa alafu usitimie huo utabiri bila taarifa za uhakika kutoka kwa Mungu, utakuwa utabiri wa uongo.
Kama kile kimeandikwa kwenye biblia kisiwe kama kilivyosemwa, tutakuwa hatuna haja kuendelea kujivunia neno la Mungu.
Tunajivunia neno la Mungu(biblia) kwa sababu ilituambia mapema yale ambayo tungeyaona waziwazi.
Najua umeona kampeni ya kataa ndoa ikiendeshwa humu kwa nguvu kubwa na kwa ujasiri, na wapo watu wamelipokea hili na kuanza kuliishi.
Napenda uelewe kuwa jambo hili lilionekana mapema litakuwepo, na sasa limekuja na tumeliona humu jamii forum.
1 Timotheo 4
1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;
2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;
3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
Yeyote anayehubiri au kufundisha kuchukia ndoa ya mwanaume na mwanamke hawapaswi kusikilizwa na kuaminiwa.
Mwanaume kuoa mwanamke ni mapenzi ya Mungu jambo hilo liwe kwetu, na sio vinginevyo.
Mungu akubariki sana
Kama kile kimeandikwa kwenye biblia kisiwe kama kilivyosemwa, tutakuwa hatuna haja kuendelea kujivunia neno la Mungu.
Tunajivunia neno la Mungu(biblia) kwa sababu ilituambia mapema yale ambayo tungeyaona waziwazi.
Najua umeona kampeni ya kataa ndoa ikiendeshwa humu kwa nguvu kubwa na kwa ujasiri, na wapo watu wamelipokea hili na kuanza kuliishi.
Napenda uelewe kuwa jambo hili lilionekana mapema litakuwepo, na sasa limekuja na tumeliona humu jamii forum.
1 Timotheo 4
1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;
2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;
3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
Yeyote anayehubiri au kufundisha kuchukia ndoa ya mwanaume na mwanamke hawapaswi kusikilizwa na kuaminiwa.
Mwanaume kuoa mwanamke ni mapenzi ya Mungu jambo hilo liwe kwetu, na sio vinginevyo.
Mungu akubariki sana