Kampeni Kupinga 'chenji' ya fedha za Radar wasipewe tena Serikali

WanaJF tuache kulalamika tuchukue hatua! Fedha za radar serikali inazotaka irudishiwe ni dhuluma tupu! Tuandike emails, sms , piga simu hata kwa kiswahili kupinga serikali isipewe fedha ilizoitoa kwa ufisadi. Hapa nimeweka anwani za BAE wanashughulikia namna fedha hizo zinaweza kurejeshwa kwa wananchi wa Tanzania ili ziwanufaishe. Andika kwa mfano: Mimi ni mtanzania napinga sina imani na serikali kufanya matumizi bora tafadhali fedha hizi zirudishiwe umma kupitia NGOs Lindsay Walls, BAE SystemsTel: +44 (0)1252 383074 Mob: +44 (0)7793427582Lindsay.walls@baesystems.comLeonie Foster, BAE SystemsTel: +44 (0)1252 383777 Mob: +44 (0)7540 630168
NGO gani???? NGO's ndo immune kwa corruption???? Acheni kuandika email na kupiga simu bila uhakika wa hili.Mimi naandika watujengee Power plants iongezee kilowats gridi ya taifa tuachane na mchezo wa kukatakata umeme.
 
Nimewapigia BAE System leo kutaka kujua kama wanapokea hizi emails. Nimeongea na Leonie Foster na amesema wamepokea simu toka kwa Watanzania kuhusiana na hili suala la malipo. Ila ameshauri watu wamtumie zaidi emails kwa sababu itakuwa ni vizuri zaidi kwake kurekodi. Kwa wale waliompigia Lindsay Walls, watagundua kuwa simu ilienda moja kwa moja kwenye voicemail. Leonie Foster ameniambia yuko likizo ya wiki mbili na atarudi Jumatatu.

Nimemwuliza sasa itakuwaje kwa vile watu wengi wameshamtumia emails na tunataka zisomwe na kuchukuliwa hatua haraka iwezekanavyo. Ameshauri tumtumie yeye hizo email kupitia Leonie.foster@baesystems.com . Kwa wale ambao tayari wameshatuma kupitia Lindsay.walls@baesystems.com, ameshauri kuwa wazitume tena kwake kupitia Leonie.foster@baesystems.com ili zirekorekodiwe mapema iwezekanavyo.

Nimemwambia kuwa kitendo cha Watanzania kuwaunga mkono hizo peza zilipwe kupitia NGOs badala ya serikali, haina maana kuwa tunaunga mkono kitendo cha BAE Systems kuwahonga viongozi wetu kwenye ile issue ya Radar. We do not condone their corrupt action hata kidogo. Ila hatuoni sababu ya mhongaji (BAE Systems) kuzirudisha pesa kupitia kwa mhongwaji (serikali ya Tanzania). Nimeweleza kuwa mpaka sasa hivi hakuna taratibu za maana za kisheria zilizochukuliwa na serikali ya Tanzania juu ya wale waliotutumbukiza kwenye hili tatizo. Kwa mantiki hiyo hatuoni sababu ya pesa hizo kupewa serikali ambayo imeshindwa hata kuwachukulia wahusika hataua za kisheria.

Kwa hiyo, kwa wale ambao bado, hawajatuma email watume kupitia Leonie.foster@baesystems.com. Kwa wale ambao wameshatuma kupitia Lindsay.walls@baesystems.com ili email zishughulikiwe mapema watume tena kupitia Leonie.foster@baesystems.com. Kwa wale Watanzania ambao wapo UK, wanaweza pia kuwaandikia MPs wao. Nimemwandikia pia Mh. Clare Short ambaye alipinga sana uuzaji wa ile Radar wakati akiwa UK's Secretary for International Development. Unaweza kumwandikia hapa: http://www.clareshort.co.uk/

Unaweza kutumia barua pepe hapa chini.

Email: Leonie.foster@baesystems.com


Re: The Settlement of the £29.5 Million to Tanzanian People


Dear Leonie Foster,

I understand that BAE Systems has formed an advisory board on Tanzania chaired by Lord Cairns in line with the settlement agreement with the UK 's Serious Fraud Office (SFO), approved by the UK's High Court in December 2010. As part of the settlement BAE Systems agreed to pay the sum of £29.5 million for the benefit of the people of Tanzania.

I am aware that a group of Tanzania all party parliamentarians have visited Britain to press for the payment of the settlement of 29.5 million pounds through the Tanzania's Government rather than Non- Governmental Organizations (NGOs).

As a Tanzanian citizen, I am monitoring the situation very closely and I want to express my strong support to BAE System for its decision to return the money to the Tanzanian people through NGO's instead of the same tainted corrupt Tanzanian Government officials. Please bear in mind that this all party parliamentarians visit in Britain is costing us already.

Thank you for your cooperation.

Your sincerely,

Taja jina lako,
 
Good! Huu siyo msaada ambao wanaweza kuuchezea na kuweka masharti wanavyotaka wao. Hizi ni kodi zetu!

Mbona hamkuzifuatilia tangu mliposikia kuwa mmeibiwa? Kwanza wakamateni walioiba pesa hizo ndipo uwe na ujasiri wa kudai hizi. Hata soni hamna? Du! Kazi kweli kweli
 
jamani hizi fedha hazitoshi kamradi ka umeme katakako punguza mgao? Naona fedha hizi kwenda kwenye mradi utakaosimamiwa na wenyewe ni bora zaidi kuliko hata kuzipa NGO maana nazo nyingi ni vichaka.

Nitatuma email soon!
 
naamini ulimwengu unaangalia uwezo wetu wa kuelewa na kudai,
hili swala la rada lingekuwa nchi nyingine tungekuwa tumeshasikia mambo mengi.
inakuwaje mbona tupo kimya sana,naomba viongozi wa upinzani tangazeni maandamano nchi nzima,
serikali ya uingereza ipo tayari kutusaidia,ni swala la kuandamana mpaka kwenye ubalozi wa uingereza,
tumeacha mpaka wale wezi wemeenda uingereza jana kudai hela wakati ndo wao wenyewe walifanya vile
jamani tutazidi kudharauliwa tusipokuwa na uwezo wa kulinda mali zetu wenyewe,
 
Hamna kitu kama hicho, fedha zile ni za serikali ya Tanzania, ni lazima zirudi kwenye mikono ya serikali, kama serikali ikizifanyia ufisadi hilo ni suala lingine, lakini kwanza zirudi serikalini hiyo ni hatua ya kwanza. BAE hawana mamlaka na fedha hizo, kwanza hata BAE ni wezi, sasa vipi fedha zetu tumwachie mwizi tena? heri zirudi serikalini na serikali izifisadi kuliko kuwaachia BAE wafanye wanavyotaka kuhusu fedha zetu. Hata kama serikali yetu ni fisadi hizi fedha ni mali yake, na zinapaswa zirudi serikalini kama zilivyo, kama zikitumika kulipana posho hilo ni suala lingine ila zirudi serikalini.
 
kama hizo pesa haiwezekani kwenda kwenye NGOs basi bora tupatiwe Watanzania wenyewe hata kama tutapata senti tano tano kila mtu sawa,lakini serikali hii hii iliyoyafanya hayo yote irejeshewe,HAPANA jamani.
 
WanaJF tuache kulalamika tuchukue hatua! Fedha za radar serikali inazotaka irudishiwe ni dhuluma tupu! Tuandike emails, sms , piga simu hata kwa kiswahili kupinga serikali isipewe fedha ilizoitoa kwa ufisadi. Hapa nimeweka anwani za BAE wanashughulikia namna fedha hizo zinaweza kurejeshwa kwa wananchi wa Tanzania ili ziwanufaishe. Andika kwa mfano: Mimi ni mtanzania napinga sina imani na serikali kufanya matumizi bora tafadhali fedha hizi zirudishiwe umma kupitia NGOs

Lindsay Walls, BAE Systems
Tel: +44 (0)1252 383074 Mob: +44 (0)7793427582
Lindsay.walls@baesystems.com
Leonie Foster, BAE Systems
Tel: +44 (0)1252 383777 Mob: +44 (0)7540 630168
Leonie.foster@baesystems.com

Hakuna ubishi kwamba baadhi ya Wizara,Idara za Serikali na Halmashauri zimekuwa na matumizi mbaya ya fedha (ushahidi ni ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali); wala hakuna ubishi kwamba tatizo la wizi wa fedha za RADAR ulikuwa engineered na baadhi ya watumishi wa Serikali....

l
akini ukweli huo haufuti ukweli kwamba Serikali imefanya na inaendelea kufanya mambo mengi ya msingi- hatuwezi kudai hatuzioni shule zilizojengwa, wala hatuwezi kudai hatuoni barabara zinazojengwa, na wala hatuwezi kukana kwamba watoto wetu wengi hivi sasa wanasoma elimu ya juu. Pamoja kazi kuwa inayofanywa na Serikali, bado mahitaji ya fedha ni mengi kuliko uwezo uliopo....hivyo, kama ipo fedha ya Serikali mahala fulani, shurti irudi serikalini ili shughuli ziendeleee...

Kuendesha pertition kwamba BAE wasirejeshe pesa serikalini ni kukosa ufahamu na UZALENDO.
Kampuni ya BAE mnayoiandikia, wala haina moral authority ya kuwa muamuzi wa kwamba fedha ziende wapi, zitumike vipi. Wao ndio walihusika na wizi huo in the first place. Hata kisa cha Out of Court Settlement, ni sehemu ya kukubali kwao, kushirikiana na baadhi ya watu wetu wasio waaminifu kuwaibia mamilioni ya wananchi wetu walio masikini mijini na vijijini. BAE hawakutuibia watanzania peke yetu, waliwaibia wamarekani pia ndio maana wamewarejeshea pesa zao pia (kwenye serikali ya Marekani, na sio NGO).Kama unafuatilia vizuri suala la BAE utabaini kwamba wenzetu waingereza wameweka UZALENDO MBELE. Kumalizwa kwa shauri lile nje ya mahakama, limezingatia maslahi ya wananchi wa Uingereza, ambao wanapata ajira pale BAE, na ambao wananufaika na huduma za serikali zinazotolewa kutokana na kodi inayolipwa na BAE..... Kwa hiyo, wamekuwa tayari kufunika kombe, MWANAHARAMU apite katika issue hiiii....Wametambua MAKOSA YA WATU WAO WACHACHE (maofisa wasio waaminifu) hayafuti MASLAHI YA WENGi.

Mimi nadhani Watanzania tunalo la kujifunza hapa.....HASIRA zetu kwa Watendaji wachache wasio waaminifu.....zisifanye tufanya pertition ya kutodai pesa zetu ambazo wauguzi kule kwetu Peramiho, Waalimu kule Muleba, Mabwana shamba kule Mangaka...wanazihitaji sana kwa ajili ya kufanikisha shughuli zao.


Kwanini kutoa pesa hizo kwa charity sio jambo la kuungwa mkono? Charity nyingi zinajulikana kwa kuwa na very high administrative and operation costs. Almost 42% ya pesa wanayopewa ya msaada inatumika kwenye shughuli za uendeshaji ikiwa ni pamoja na malipo ya mishahara, posho kubwa kwa watendaji kwenye organizations hizo; na kwakuwa wao ni watu wa nje....wanapokwenda mahala on the ground, mara nyingi hawapati value for money services.....nyingi zinakuwa inflated......daftari ambalo linauzwa shs 100, wao watalinunua kwa shs 300. Na mara nyingi hupendelea kufanya manunuzi kwenye nchi zao ili kukuza uchumi wao (pesa ibakie nyumbani)....leo hii daftari ambalo nyumbani linauzwa kwa Shs 400 pale TAHAFIF, UK linauzwa Pence 80 ambayo ni sawa na Shs 2000....hapo haujaweka gharama za kusafirisha.....unadhani tutapata kitu kweli hapo? Haya sio maneno yangu tizameni wenyewe kwenye sites zifuatazo muone jinsi charities zinavyotumia pesa: http://www.mainstreet.com/article/moneyinvesting/news/20-worst-charities-america na http://www.mainstreet.com/article/smart-spending/15-highet-paid-charity-ceos


Mie ningewaelewa wale wanaojenga hoja kwamba fedha hizo zipelekwe serikalini kupitia DFID; ambao hivi sasa wanaratibu misaada ya uingereza serikalini ambayo ni mara 4 ya fedha hizo za RADAR wanazitoa kila mwaka. Serikali inachotakiwa ni kuonyesha plan ya matumizi, na DFID watathibitisha matumizi hayo kwa WANANCHI (na sio BAE ambao ndio wezi wetu) TUEPUKANE KUWA NA MENTALITY ZA KUTAWALIWA NA KUTOJIAMINI
 
Nami pia nimetuma email, and I am going to convice other at least 5 fellow Tanzanians to send emails to BAE Systems. Lets join hands on this ans I KNOW WE CAN. AMANDLAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA!!!!!
 
Kaandamane na familia yako sebuleni kwenu! Issue iko clear hapa kwamba fedha zile ni za serikali wewe unazungumzia kumaliza visigino kwa kuandamana. Ili upate nini?
 
lakini ukweli huo haufuti ukweli kwamba Serikali imefanya na inaendelea kufanya mambo mengi ya msingi- hatuwezi kudai hatuzioni shule zilizojengwa, wala hatuwezi kudai hatuoni barabara zinazojengwa, na wala hatuwezi kukana kwamba watoto wetu wengi hivi sasa wanasoma elimu ya juu. Pamoja kazi kuwa inayofanywa na Serikali, bado mahitaji ya fedha ni mengi kuliko uwezo uliopo....hivyo, kama ipo fedha ya Serikali mahala fulani, shurti irudi serikalini ili shughuli ziendeleee...


Shule zilizojengwa ambazo mpaka leo miaka 50 bado wanafunzi wanakaa chini, Shule ambazo hakuna mtoto wa kigogo anayesoma, shule ambazo hazina vitabu, shule ambazo hazina maabara? Hizi ndo wewe unaziita shule?

Barabara zinazojengwa ambazo baada ya miezi mitatu zinaanza kuwa na mahandaki? Barabara ambazo baada ya miezi 6 unaona lami inahamia upande mmoja wa barabara. Hizi ndo barabara unazozisema?

Watoto wetu wengi hivi sasa wanasoma elimu ya juu? Hawa watoto ambao kila leo unaona wanagoma kwa kuomba waongezewe posho ya chakula? Hawa ambao wanapelekwa kusoma bila kutengewa fedha kwa ajili ya kufanya mazoezi ya vitendo?

Haya ndo unayaita mambo makubwa Serikali imeyafanya? Hebu acha upumbavu wewe! Kwani ni nani aliyekua tayari kudai fedha hizo ndani ya Serikalini? Kama ni hivyo mbona hakuna mtu yeyote aliyechukuliwa hatua kutokana na wizi huo? Kama ni hivyo ujasiri wa kwenda kudai hizo fedha unatoka wapi hivi sasa?

Wana JF wenzangu, tusikatishwe tamaa na vibaraka kama hawa. Tutume kwa wingi sana email ili kupinga fedha hizo kuletwa kwa hawa manyang'au wakubwa wanaoendelea kutunyonya.
 
I know tumewashika pabaya! hhahahahh! The money doesn't belong to the government, it belongs to Tanzanians! We want it refunded to them, the government has lost moral authority to administer it. Why are you then crying if our efforts are useless?

If you think I am crying, then it is because you are wasting our time telling you that you are going to meet a brick wall. It makes me so astounded to see that people can be captives of the modern day slavery and yet this country has spent a fortune to educate them with a view to emancipating them from all forms of mental slavery. These masters of your own cannot be left to dictate terms on where and how our hard earned money should channeled and spent! At least not now!
 
Hakuna ubishi kwamba baadhi ya Wizara,Idara za Serikali na Halmashauri zimekuwa na matumizi mbaya ya fedha (ushahidi ni ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali); wala hakuna ubishi kwamba tatizo la wizi wa fedha za RADAR ulikuwa engineered na baadhi ya watumishi wa Serikali....


So far serikali imechukua hatua gani dhidi ya watumishi wahusika? At least BAE System imekiri, lakini serikali yetu mpaka leo, haisemi chochote. Imesubiri kutafuniwa kila kitu then, inataka tuu kuja kumeza. Kama kweli serikali yetu imekuwa ilichukia ile rushwa, it should have taken action long time ago.

akini ukweli huo haufuti ukweli kwamba Serikali imefanya na inaendelea kufanya mambo mengi ya msingi- hatuwezi kudai hatuzioni shule zilizojengwa, wala hatuwezi kudai hatuoni barabara zinazojengwa, na wala hatuwezi kukana kwamba watoto wetu wengi hivi sasa wanasoma elimu ya juu. Pamoja kazi kuwa inayofanywa na Serikali, bado mahitaji ya fedha ni mengi kuliko uwezo uliopo....hivyo, kama ipo fedha ya Serikali mahala fulani, shurti irudi serikalini ili shughuli ziendeleee...


hapa umeandika kama kiongozi fulani wa serikali. Completely hypocrite. Kama mahitaji ya fedha ni mengi kuliko uwezo uliopo, surely kungekuwa hakuna haja ya kuwapa wabunge posho kubwa kiasi hicho. Au basi serikali ingeridhia haja ya kupunguza posho ili kukidhi mahitaji.

Kuendesha pertition kwamba BAE wasirejeshe pesa serikalini ni kukosa ufahamu na UZALENDO.
Kampuni ya BAE mnayoiandikia, wala haina moral authority ya kuwa muamuzi wa kwamba fedha ziende wapi, zitumike vipi. Wao ndio walihusika na wizi huo in the first place. Hata kisa cha Out of Court Settlement, ni sehemu ya kukubali kwao, kushirikiana na baadhi ya watu wetu wasio waaminifu kuwaibia mamilioni ya wananchi wetu walio masikini mijini na vijijini. BAE hawakutuibia watanzania peke yetu, waliwaibia wamarekani pia ndio maana wamewarejeshea pesa zao pia (kwenye serikali ya Marekani, na sio NGO).Kama unafuatilia vizuri suala la BAE utabaini kwamba wenzetu waingereza wameweka UZALENDO MBELE. Kumalizwa kwa shauri lile nje ya mahakama, limezingatia maslahi ya wananchi wa Uingereza, ambao wanapata ajira pale BAE, na ambao wananufaika na huduma za serikali zinazotolewa kutokana na kodi inayolipwa na BAE..... Kwa hiyo, wamekuwa tayari kufunika kombe, MWANAHARAMU apite katika issue hiiii....Wametambua MAKOSA YA WATU WAO WACHACHE (maofisa wasio waaminifu) hayafuti MASLAHI YA WENGi.


BAE Systems na serikali wote wala rushwa. Kama BAE Systems haina moral authority, how come serikali inatoa its morak authority wapi? BAE and serilali both walihusika na na wizi. Kumbuka anayetoa and anayepokea rushwa wote ni wala rushwa. Unakubali kuwa wananchi ndio waliibiwa hizo fedha, basi warudishiwe. Wao ndio victims hapa na sio serikali, simply because serikali ilijihusisha kwenye huo wizi pamoja na kuwa wananchi walipinga sana hili.

Mimi nadhani Watanzania tunalo la kujifunza hapa.....HASIRA zetu kwa Watendaji wachache wasio waaminifu.....zisifanye tufanya pertition ya kutodai pesa zetu ambazo wauguzi kule kwetu Peramiho, Waalimu kule Muleba, Mabwana shamba kule Mangaka...wanazihitaji sana kwa ajili ya kufanikisha shughuli zao.

Usilingalishe Marekani na Tanzania kabisa. Serikali ya Marekani ilichukua hatua kwa wale waliohusika. Tanzania imefanya nini mpaka sasa? Maerkani ilijihusisha tokea mwanzo wa uchunguzi wa hili suala. Serikali ya Tanzania haikufanya hivyo. Wamesubiri kila kitu kimetafuniwa ndio wanataka kuja kumeza wakati wahusika wanatesa tuu mitaani. How ridiculous is this. Kuhusu suala la UK kuweka uzalendo mbele wrong plus wrong does not make it right. Kama UK wametumia upumbavu wao kuwakinga wahusika, basi na sisi tufuatte huo ujinga? I don't think so.

Kwanini kutoa pesa hizo kwa charity sio jambo la kuungwa mkono? Charity nyingi zinajulikana kwa kuwa na very high administrative and operation costs. Almost 42% ya pesa wanayopewa ya msaada inatumika kwenye shughuli za uendeshaji ikiwa ni pamoja na malipo ya mishahara, posho kubwa kwa watendaji kwenye organizations hizo; na kwakuwa wao ni watu wa nje....wanapokwenda mahala on the ground, mara nyingi hawapati value for money services.....nyingi zinakuwa inflated......daftari ambalo linauzwa shs 100, wao watalinunua kwa shs 300. Na mara nyingi hupendelea kufanya manunuzi kwenye nchi zao ili kukuza uchumi wao (pesa ibakie nyumbani)....leo hii daftari ambalo nyumbani linauzwa kwa Shs 400 pale TAHAFIF, UK linauzwa Pence 80 ambayo ni sawa na Shs 2000....hapo haujaweka gharama za kusafirisha.....unadhani tutapata kitu kweli hapo? Haya sio maneno yangu tizameni wenyewe kwenye sites zifuatazo muone jinsi charities zinavyotumia pesa: http://www.mainstreet.com/article/moneyinvesting/news/20-worst-charities-america na http://www.mainstreet.com/article/smart-spending/15-highet-paid-charity-ceos


Same kwa serikali ya Tanzania. Wote tunajua hilo. Angalia tayari wameshaanzisha tume ya kudeal na hii issue. Wameenda UK ku negotiate. All these involve very high and unnecessary costs. Pia Tanzania tunalipa posho kubwa kwa watendaji, na wananchi hawapati value for the money services unayozungumzia.

Mie ningewaelewa wale wanaojenga hoja kwamba fedha hizo zipelekwe serikalini kupitia DFID; ambao hivi sasa wanaratibu misaada ya uingereza serikalini ambayo ni mara 4 ya fedha hizo za RADAR wanazitoa kila mwaka. Serikali inachotakiwa ni kuonyesha plan ya matumizi, na DFID watathibitisha matumizi hayo kwa WANANCHI (na sio BAE ambao ndio wezi wetu) TUEPUKANE KUWA NA MENTALITY ZA KUTAWALIWA NA KUTOJIAMINI

Inawezekana ukawa na point hapa lakini sidhani kama serikali ya UK itataka kujihusisha kwenye hili suala. After all, serikali yetu haja put forward plan yoyoye. Nisingekuwa na tatizo pesa zilipwe serikalini kama, serikali ilikuwa imechukua hatua kwa wahusika. So far hakuna cha maana kilichofanyika juu ya wale watumishi waliotufikisha hapa. Hata wakati uchunguzi unafanyanyika serikali yetu haikutaka kujihusisha kusaidia uchunguzi. Serikali iwachukulie hatua watumishi waliohusika kwanza.
 
Nimeshangazwa na mawaziri kwenda moja kwa moja majuu kudai hizo fedha, kwanza wanajilipa posho na per diem kitu ambacho kinaongezea machungu nchi, kwa kuwa kuna barozi anaye wakilisha TZ kwa nini asishughulike akiwa huko fedha zirejeshwe bila kuongeza gharama za mawaziri kufunga safari na kula per diem?
YALE YALE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! YA POSHO ZA KUFUNDISHWA KUJIKINGA NA UKIMWI
 
Hili ni jambo jema sana
Tutatuma ujumbe kwa njia ya e mail na kuwahamasisha wengine wengi katika mitandao tofauti
 
Nimetuma email sasa hivi. Nimewaandikia marafiki zangu wanane nao watume! Hawa wanaosema tunakosa uzalendo mimi macho _mdiliko nawaambia hivi: wakati wenu wa kuishi kwa kulamba vidonda kaa nzi unawadia!!!
 
WanaJF tuache kulalamika tuchukue hatua! Fedha za radar serikali inazotaka irudishiwe ni dhuluma tupu! Tuandike emails, sms , piga simu hata kwa kiswahili kupinga serikali isipewe fedha ilizoitoa kwa ufisadi. Hapa nimeweka anwani za BAE wanashughulikia namna fedha hizo zinaweza kurejeshwa kwa wananchi wa Tanzania ili ziwanufaishe. Andika kwa mfano: Mimi ni mtanzania napinga sina imani na serikali kufanya matumizi bora tafadhali fedha hizi zirudishiwe umma kupitia NGOs

Lindsay Walls, BAE Systems
Tel: +44 (0)1252 383074 Mob: +44 (0)7793427582
Lindsay.walls@baesystems.com
Leonie Foster, BAE Systems
Tel: +44 (0)1252 383777 Mob: +44 (0)7540 630168
Leonie.foster@baesystems.com

Nitakuwa radical kidogo.Frankly sioni jinsi fedha hizo zinavyoweza kumsaidia Mtanzania wa kawaida hata kama zikija.Mafisadi watazifisadi tu.Kwa hiyo afadhali serikali isipewe tukose wote.
 
Serikali ya JK haiwezi kuaminiwa kusimamia fedha za walipa kodi wa Tanzania. Zile pesa za EPA walidai zinarudishwa TIB na sasa hazijulikani ziliko. Kwa nini wapewe hizi tena? Watanzania tupinge kwa umoja wetu hizi pesa zirudishwe nchini LAKINI kupitia NGOs na si kwa manyang'au wa JK.
 
WanaJF tuache kulalamika tuchukue hatua! Fedha za radar serikali inazotaka irudishiwe ni dhuluma tupu! Tuandike emails, sms , piga simu hata kwa kiswahili kupinga serikali isipewe fedha ilizoitoa kwa ufisadi. Hapa nimeweka anwani za BAE wanashughulikia namna fedha hizo zinaweza kurejeshwa kwa wananchi wa Tanzania ili ziwanufaishe. Andika kwa mfano: Mimi ni mtanzania napinga sina imani na serikali kufanya matumizi bora tafadhali fedha hizi zirudishiwe umma kupitia NGOs

Lindsay Walls, BAE Systems
Tel: +44 (0)1252 383074 Mob: +44 (0)7793427582
Lindsay.walls@baesystems.com
Leonie Foster, BAE Systems
Tel: +44 (0)1252 383777 Mob: +44 (0)7540 630168
Leonie.foster@baesystems.com


nonononooo tumeshatuma email nyingi sana,tufanye jambo la muhimu tuandamane kuelekea ubalozi wa uingereza kushinikiza,habari zikifika kule watatusikiliza
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom