Kama unaamini wanawake hawajui kwamba matokeo ya kukamatwa wakicheat hayalingani kati ya wanaume na wanawake, basi unaidanganya nafsi yako

Six Stars

Member
Dec 8, 2021
14
96
Wanawake ni wenye ujasiri sana. Watadhubutu kukupa changamoto katika maeneo mengi, ili kujaribu jinsi unavyokuwa dhaifu au imara.

Wanajua wanachofanya na watakusukuma hadi kufikia hatua ambapo utaanguka na bado kukataa kuwajibika.

Mwanamke ambaye anafungua miguu yake kwa mwanaume mwingine, anajua matokeo yake ni nini, kama akikamatwa. Ikitokea amekamatika, anajua kabisa mchezo umekwisha.

Lakini bado atatafuta njia ya kuona kama unaweza kumsamehe, ili wakati mwingine anapodanganya tena, atakulaumu wewe kwa hilo.

Hapo wewe ndiye uliyeanguka kwa hila yake. Amekuzidi ujanja. Na haijalishi ana umri gani, hata mabinti wadogo wanajua hili. Ni asili ndani yao, kutenda hivyo.

Tangu kuzaliwa, wanawake wamejitolea maisha yao kuwasoma wanaume. Huku wanaume wakijitolea maisha yao kufanya kitu maishani.

Wanaume wengi huanza kuzingatia wanawake wanapokuwa vijana. Huku wanawake wakijipanga kwa muda mrefu kwa ajili ya wanaume.

Hapo ndipo wanakuwa wenye akili zaidi katika mahusiano na huwa hawana nia ya kuomba msamaha wanapotaka kumove on. Wamejijenga kwa ajili ilo na jinsi wanavyoweza kuvinjari na kuishi katika ulimwengu uliojengwa na wanaume na wenye mfumo dume.

Nasisitiza.
Kama mwanamke anakiri kwako kwamba amekucheat, huyu anakuomba umwache aende. Na ikiwa amebainika bila kujitokeza mwenyewe kukiri, huyu hatatamani kubaki.

Ni wale wasiojua, wakorofi na wenye ukaidi tu ndio wanaotaka kukuendelea kukupima ndio watabaki. Na mara nyingi, wanapata adhabu kwa hilo. Lakini wewe kama mwanaume, hutaweza kukwepa adhabu yake pia. Hivyo ni vyema nyote msijidhuru zaidi, kwani mwisho huwa ni janga.

Kwa hivyo, ukweli kwamba mwanaume ana advantage ya juu akikamatwa amecheat, haimaanishi kwamba mwanaume anapaswa kumkosea heshima mwanamke.

Mwanaume ambaye anakiri kwa hiari kwa mpenzi wake kwamba amemdanganya, ni mjinga na mwanaume dhaifu. Unajua binadamu hawana asili ya kuwa waaminifu kwa mmoja pekee.

Una mwanamke ambaye anajitolea kujizuia tamaa zake za kimapenzi kwa ajili yako, na yote unayoweza kufanya ni kumfanya ahisi kuwa anastahili kupata upendo wako tu na "Kibamia" chako pekee? Unawezaje kufikiri kwamba hataki kujaribu "Kibamia" kingine? Na hasa ikiwa hukumkutana naye akiwa bikira?

Katika kila unachofanya katika mchezo wa mahusiano/ndoa, lazima utumie hekima. Tunapaswa kujifunza jinsi ya kudhibiti tamaa zetu za kibinafsi ili tusije tukaharibu kile ambacho tumejenga. Katika ndoa na wakati mmebarikiwa watoto, wanaume na wanawake wote lazima wawe makini wasivuke mipaka na kuwaadhibu watoto wasio na hatia. Ikiwa wewe ni wa kujaribu sana na hujali, utatia mkwaruzo katika ndoa yako na kuharibu ujumuisho huo ambao Mungu ameuweka kwa mikono yako mwenyewe.

Siyo tu mnapoachana ndipo ndoa yako imeharibika. Wanandoa wanaweza kuendelea kuwa pamoja, lakini wakipitia maisha ya mateso ndani yake. Inakubalika, bado mnaendelea kuwepo katika ndoa hiyo kwa ajili ya watoto wenu. Lakini je, wewe pia haukustahili kuwa na furaha? Hapo ndipo sote tunahitaji kuwa makini.

Kila kitu utakachokumbana nacho katika ndoa, kinaanza katika uhusiano wako.

Vijana wanahitaji kujifunza kwamba hawawezi kula keki yao na kuendelea kuwa nayo. Na hakuna haja ya kutoka na watu wengi kabla ya kupata mwenzi.

Haijalishii ulitumia miaka 5 ukimchumbia mwanaume, Ikiwa utamcheat, na yeye akagundua, jitihada zako zote zimepotea bure.

Usiwe mwathirika katika hadithi yako ya mapenzi.

Mwisho.
 
Tujuane wale ambao hatujali hisia uchwara za hao viumbe.
sisi ambao kazi yetu ni kuwagonga na kuwaacha,
tujuane tafadhali.
 
Back
Top Bottom