Kama sio tajiri na huna asset, kusomesha watoto shule za gharama ni ujinga unaongeza umaskini kwenye ukoo

FRESHMAN

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
8,822
33,532
Habari wadau..

January imeisha .. wazazi wengi walikuwa wanalalamika school fees tatizo.

Kwa maoni yangu kama mtu huna mali za kutosha, huna kampuni ya kueleweka wala huna mtaji wa kutosha... baba mzazi wewe mwenyewe unategemea ajira za laki nane ama milioni moja, kusomesha watoto wako shule za gharama sio jambo zuri.

Hakuna CEO Mtanzania ambaye ameajiriwa ambaye hayupo kwenye kampuni ya baba yake kama Mo, ambaye amesoma international schools, ama shule za bei nafuu za kiingereza ambazo tunaita english medium... tukumbuke english medium zipo Tanzania miaka kibao kama IST, Arusha school ama Olimpio.

Kuna CEO wengi wazawa kama Dada CEO wa NMB Ruth Zaipuna ama wa CRDB Majid Nsekela na ceo wengine wengi hawajapita Olimpio wala Arusha schools enzi zao ambazo walikuwa wanasoma msingi, hizo olimpio na arusha school zilikuwepo tayari ila wala hawakusoma hizo shule na leo wamepata nafasi kubwa kwa uwezo wao binafsi wa kazi..

Mzazi ambaye huna hela za kutosha peleka mwanao shule za serikali kisha msimamie mwanao vizuri, kila siku mfatilie. Hela ya ada ya kulipa Tusiime nunua asset unazozimudu mwanao zitamsaidia kuliko kumlipia ada mamilioni.
 
Mimi namtazamo mwingine japo sitofauti sana na wewe, mimi naona ni vyema kipindi hichi wazazi wenye kipato cha kawaida wakawa na malengo ya kuja kuwekeza zaidi kwa watoto wao kwenye elimu ya juu huku chini hakuna haja sana sababu watoto wanaishia kujua lugha tu.
 
Mimi namtazamo mwingine japo sitofauti sana na wewe mimi naona ni vyema kipindi hichi wazazi wenye kipato cha kawaida wakawa na malengo ya kuja kuwekeza zaidi kwa watoto wao kwenye elimu ya juu huku chini hakuna haja sana sababu watoto wanaishia kujua lugha tu

True.. mtu analipa milioni 3 ama nne kwa mwaka ili mwanae ajue kiingereza tu. Huku sylabus anayofundishwa mwanae wa tusiime ni ile ile ambayo wa elimu bure anafundishwa. Tofauti ni lugha tu.

Tatizo la elimu yetu ni sylabus. Jaribu kuwaza hiyo milion 3 kila mwaka mnunulie kiwanja ndani ya miaka 7 atakuwa na asset kiasi gani huyo mtoto.

Mtoto atakuwa na uhakika wa kupata elimu ya juu ama basic need hata kama mzazi umefariki.
 
True.. mtu analipa milioni 3 ama nne kwa mwaka ili mwanae ajue kiingereza tu... huku sylabus anayofundishwa mwanae wa tusiime ni ile ile ambayo wa elimu bure anafundishwa. Tofauti ni lugha tu.

Tatizo la elimu yetu ni sylabus.. jaribu kuwaza hiyo milion 3 kila mwaka mnunulie kiwanja ndani ya miaka 7 atakuwa na asset kiasi gani huyo mtoto.

Mtoto atakuwa na uhakika wa kupata elimu ya juu ama basic need hata kama mzazi umefariki.
Mh!
Umechomoa ubongo au?
 
Mimi namtazamo mwingine japo sitofauti sana na wewe mimi naona ni vyema kipindi hichi wazazi wenye kipato cha kawaida wakawa na malengo ya kuja kuwekeza zaidi kwa watoto wao kwenye elimu ya juu huku chini hakuna haja sana sababu watoto wanaishia kujua lugha tu
Hivi huu msemo Wa eti watoto wanaosoma shule za academies sijui private school eti wanaishia kujua lugha tu, mi natofautiana na wewe mkuu, Kijana wangu yuko std seven hizo shule, sikifichi anawa challenge hata majamaa waliosoma hizo ma A level za kata na wanamkubali mbaya.
 
True.. mtu analipa milioni 3 ama nne kwa mwaka ili mwanae ajue kiingereza tu... huku sylabus anayofundishwa mwanae wa tusiime ni ile ile ambayo wa elimu bure anafundishwa. Tofauti ni lugha tu.

Tatizo la elimu yetu ni sylabus.. jaribu kuwaza hiyo milion 3 kila mwaka mnunulie kiwanja ndani ya miaka 7 atakuwa na asset kiasi gani huyo mtoto.

Mtoto atakuwa na uhakika wa kupata elimu ya juu ama basic need hata kama mzazi umefariki...
Mkuu samahani lakini, kwani unaishi mjini au kijijini?
 
Kama una asset na una mashaka na uwezo wa mwanao darasani mpeleke internal school maana ukimpeleka za kawaida utajilaumu baadae, lakini pia Kama una muamini mwanao yuko vizuri darasani Basi huna haja ya kuhangaika na internatn school, una mboost na tuite na paper kibao inatosha. Mwisho wa siku wote watakutana kwenye korido za versity.
 
Kama una asset na una mashaka na uwezo wa mwanao darasani mpeleke internal school,maana ukimpeleka za kawaida utajilaumu baadae,lakini pia Kama una muamini mwanao yuko vizuri darasani Basi huna haja ya kuhangaika na internatn school,una mboost na tuite na paper kibao inatosha.mwisho wa siku wote watakutana kwenye korido za versity.

Una point kubwa sana ila umeenda nje ya uzi upande wa asset

Je kama huna asset? Uzi umeongelea wenye asset ama wasio na asset?
 
Sehemu tulipowezwa ni hapa..

Mtoto wako, anakuja kuishi Tanzania hiii hiii unahangaika awe mzungu..hahaha.. na anafundishwa matatizo ya kizungu, kwa lugha ya kizungu..akitoka huko ameshakuwa mzungu anakuja kwa watanzania mtaani anaanza moja.. :)

Na cha kufurahisha ni sisi wazazi ndio tunakuwa tumewanunulia watoto wetu hiyo delay huku mtaani. Elimu tuliyomnunulia ndio imekuwa kikwazo..

Bora kila mwaka ungekuwa unamnunulia mtoto ng'ombe nne.. anasoma shule ya laki tano kwa Temu.. akija kumaliza shule anakuwa na ng'ombe 68, ukiweka kuzaa na kufa hakosi ng'ombe 100 kwenye kipindi cha miaka 16 ya kusomea elimu.

Na elimu yenyewe ndio imekuwa uchuro uchoro mtupu
 
Back
Top Bottom