Kama nikiulizwa kuwa nimeridhika na Utawala wa Rais Samia au ninamkumbuka Hayati Magufuli

Watu wa instagram ,facebook n.k.wanamlilia sana JPM na kumkumbuka,ila humu sijui mnakuwa mmetumwa? ...
Hao wanaomlilia ni ile misukule yake aliyokuwa ameibrain wash na wale walionufaika na utawala wake wa hovyo kama kina Sabaya na makonda.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anamlilia huyo dikiteta aliyekuwa hawezi hata kichagua maneno yakuongea kama raisi wa nchi. Alikuwa anaropoka tu. Mara muhaki na mavi yenu nyumbani!
 
Mleta mada,

Ukitaka ujue ubora na udhaifu wa JPM na Mamá Samia basi ingekupasa urejee changamoto tulizokuwa nazo toka awamu ya Kikwete.

**Rejea zile kelele za wananchi tukiongozwa na Chadema juu ya ufisadi wa Serikali ya JK ( skendo za EPA, Richmond, Escrow, ufisadi nssf) matumizi mabovu ya kodi za wananchi (safari za nje ya nchi za viongozi mbalimbali, semina na warsha zenye posho nono nono etc)
, rushwa kila kona, madawa ya kulevya, ujambazi na uporaji silaha kwenye vituo vya polisi, ugaidi wa kibiti mkuranga, ukwepaji kodi bandarini na kwenye biashara, watumishi hewa, huduma mbovu sekta ya afya, ubovu miundombinu ya barabara reli,na mengine kadha wa kadha

Kisha angalia alivyoingia Magufuli madarakani ameweza kushughulikia kwa kiwango gani hizo kero na changamoto zilizokuwa zinaikabili nchi yetu, ndipo utajua Magufuli alipiga kazi au alikuja kuuza sura

Sio unaleta vitu dhaifu dhaifu vya kumlinganisha Magufuli na Mamá Samia eti huruma, hana dharau, hana visasi, anapenda watu,,,, shabaaashhh....!!!

Magufuli hakuja kuuza sura, alikuja kuchapa kazi na kazi imeonekana.
Mtakubali tu kuwa Samia ni raisi bora kuliko Magufuli.

Unawezaje kushabikia utawala wa raisi aliyekuwa analea watu kama Sabaya. Hapana. Labda kama na wewe ulikuwa unanufaika na huo uovu na uhalifu.
 
Mzee yule alifungia vyombo vya habari,alivitisha,alitisha waandishi,alizuia uhuru wa kujadili mambo ya nchi,alizuia Bunge kuonekana live,alitumia mda mwingi wa TBC kujitangaza na kutangaza mambo yake.
Watu wengi hawakuweza kumuua upande wa pili wake.
Alidhalilisha watu wenye mafanikio kama Matajiri,wafanyabiashara wakubwa,wawekezaji,viongozi wastaafu,wafanyakazi,wakulima na wanasiasa wa Upinzani.
Sasa kwa kawaida watu wasio na mafanikio hufurahi Sana wqkiona kuna mtu ana waadhibu sehemu ya watu hao nilowataja hususan Matajiri na watu wenye mafanikio.
Watu wengi wa Insta na huko face book nadhani Wana mitazamo huo wa kufurahia watu wenye mafanikio wakiadhibiwa bila kujali kama wamekosea ama la
 
Wewe hujui kua nchi zote Duniani ziko kwenye constant war? Siku zote nchi ziko vitani.

Wewe vita unajua ni kama vile tulikua tunapigana na Uganda? Hivyo kwako ndio vita pekee ambavyo nchi inapigana? Haya mambo ya usalama wa nchi yako juu yako usiendelee kuyajadili maana huelewi chochote.

Rais ndie mwenye mamlaka ya kulinda nchi, yeye akiona threats za national security ana wajibu wa kulinda nchi kwa namna anavyoona inafaa. Soma basi hata katiba ujue majukumu ya rais.

Lazima ujue kua kuna overt and convert operations, sio kila adui wa nchi lazima apelekwe mahakamani, wengine wanapotezwa tu. Hii ni kwa mataifa yote hata unayoyafikiria ya demokrasia kama Marekani na Uingereza maana watanzania wengi akili ndogo kila kitu kulinganisha na Marekani na Uingereza. Wale hawwkufika hapo kwa hizi akili ndogo zilizopo Tanzania.

Usipende kudanganyika na hadithi za mitaani na ngonjera zisizo na akili.

So I am trying to get you see things differently.
Wewe ni haramia tu kama Sabaya na huyo mwendazake wako unayejaribu kumtetea. Nyinyi mlikuwa mnanufaika na huo uharamia.
 
Tutakuwa na Rais Samia kwa kipindi cha miaka takriban mitano kabla ya Uchaguzi Mkuu kama mambo yakienda hivi bila Mungu kufanya yake. Inshallah naomba asifanye.

Kama nikiulizwa leo hii je unauonaje Utawala wa Samia?
Je, kwa jinsi Samia anavyoongoza unaona ni vema Magufuli angekuwepo?
Unajua katika Maisha huwa kuna wakati huwa tunawakumbuka Marehemu kwa uwezo wao na nafasi zao katika jamii kuanzia ngazi ya familia.

Jibu langu katika maswali hayo ni moja tu.

Ni afadhari mara mia Samia abaki miaka 10 kuliko Miaka mitano ya Magufuli.

Samia na Magufuli ni mbingu na ardhi.

Samia ana utu,ana hofu ya Mungu,hana kiburi,hana dharau,hana chuki,hana visasi,msikivu,hana roho mbaya,ana nidhamu,sio mkatili,ana heshima,ana heshimu wataalamu,viongozi wa dini,wazee na vijana.

Samia mtoto wa mjini hana mambo ya kishamba.

Anaeheshimu wakulima ,wafanyakazi na wafanyabiashara.

Hawazi kupoteza watu,
Ana huruma,hawezi kufurahia kuona mtoto wa mtu akipotezwa kwa sababu ya tofauti za kisiasa.

Hata ukiangalia body language za watu mitaani,Wana amani Sana.

Hana hotuba za vitisho wala dharau.
Ana vijimaneneo vyake tu vya kipwani,au kimamamama lakini sio sio maneno makali.

Kitu pekee kitamharibia Samia kama asipocheza karata zake vizuri ni Kesi ya Mwamba Mbowe tu.

Vyovyote itakavyokua Samia Sio Mkatili.
Hawezi kuruhusu au kufurahia mambo kama yaliyompata Lisu yatokee ndani ya awamu yake,

Hawezi kupanua barabara na asiwalipe wahanga.

Ukweli ni kwamba Kwangu mimi ni bora Samia kuliko Jiwe.

Nchi ilikokuwa inaelekea Ni Mungu tu ndio ajuaye.

Hivi kw mfano mambo haya ya kuogofya na kutisha aliyokuwa akiyafanya Sabaya Intelijensia za akina Sirro hazikuyaona?

Asante kwa bandiko lako.

Umeeleza upande mmoja tu wa chifu Hangaya.
Ni kweli kabisa ana sifa nzuri ambazo umezitaja. Hakuna anayebisha kwa hilo.
Lkn pia unapaswa kutaja upande mwingine wa wasaidizi wake, wafanyakazi wa serikali, vyama pinzani na wananchi kwa ujumla kuakisi sifa anazoonesha mama. Yeye kaonesha sifa nzuri, inapaswa na wengine pia waoneshe sifa zile zile ambazo mama anazo. Kama mama tu ndiye anaonesha sifa njema, lkn upande huu mwingine hauoneshi kuwiwa (kuwa indebted) haitakuwa na maana. Atavunjika moyo. Naye kama binadamu anaweza kubadirika na kuwa tofauti na alivyo sasa. Tusiwe na mtazamo wa kutaka yeye ndiye anayepaswa kuonesha sifa nzuri, lkn upande mwingine hapana.
The late JPM ali behave vile kutokana na aliyoyaona. Aliikuta nchi katika hali ambayo usipokuwa mvumilivu kama yeye, basi lazima ungefanya kama vile. Yeye tumuache, ameshamaliza mwendo wake, mengi tumejifunza kutoka kwake. Ninachoweza kutamatisha nacho ni kuwa, the rest is history, tugange yajayo. Tuepuke kuingia kwenye mtego wa kuwa watumwa na wafungwa wa historia. Hasa historia isiyofaa, inakuwa ni hasara kwetu. Wanasaikologia wanasema hiyo ni sawa na kujipiga vibao shavuni wenyewe. Kusamehe ni faida ya yule anayesamehe zaidi ya yule anayesamehewa.
 
Kama ni kulinganisha mlima na kichuguu, basi Samia ni mlima Kilimanjaro.

Lile zee ilikuwa ni a total waste...

Haijawahi Tanzania kupata Rais wa ovyo kama Mwendazake.

Tunamshukuru Mungu kwa kutunusuru kwenye mikono ile haramu
Mungu siyo bibi yako
 
Ni kweli alikuwa wa kipekee kwa kujigia promo kubwaaaa kwenye mambo ya kawaida kabisa
Alikuwa anapenda sifa za kijinga, waliomjua wakammwagia mapambio tu ili waendelee kuitafuna keki ya Taifa, awamu yake ufisadi ulishamiri sana ila kuhoji ilikuwa marufuku (Ukihoji unaitwa siyo mzalendo, unatumiwa na mabeberu, mpinga maendeleo)! Alikuwa hawapendi wasomi (Japo alijifanya anawapenda kinafiki) na waliomzidi akili za kiuongozi (J. makamba), wengine alikuwa anajisifia kuwa anawaita wapumbavu (Hiyo yote ilikuwa aonekane mbele ya watu wasomi siyo kitu kwake)! Wasomi wengi waligeuka vituko mbele yake, Kabudi alikunywa mikojo kutoka Madagascar mbele ya Camera, Gwajima alikunywa vitu vya ajabu kabisa na kupiga nyungu za hovyo hovyo! Ni majasiri wachache walisimama bila kumlamba miguu or kumpigia mapambio ndani ya chama (Mf. Membe na J. Makamba)
 
Tutakuwa na Rais Samia kwa kipindi cha miaka takriban mitano kabla ya Uchaguzi Mkuu kama mambo yakienda hivi bila Mungu kufanya yake. Inshallah naomba asifanye.

Kama nikiulizwa leo hii je unauonaje Utawala wa Samia?
Je, kwa jinsi Samia anavyoongoza unaona ni vema Magufuli angekuwepo?
Unajua katika Maisha huwa kuna wakati huwa tunawakumbuka Marehemu kwa uwezo wao na nafasi zao katika jamii kuanzia ngazi ya familia.

Jibu langu katika maswali hayo ni moja tu.

Ni afadhari mara mia Samia abaki miaka 10 kuliko Miaka mitano ya Magufuli.

Samia na Magufuli ni mbingu na ardhi.

Samia ana utu,ana hofu ya Mungu,hana kiburi,hana dharau,hana chuki,hana visasi,msikivu,hana roho mbaya,ana nidhamu,sio mkatili,ana heshima,ana heshimu wataalamu,viongozi wa dini,wazee na vijana.

Samia mtoto wa mjini hana mambo ya kishamba.

Anaeheshimu wakulima ,wafanyakazi na wafanyabiashara.

Hawazi kupoteza watu,
Ana huruma,hawezi kufurahia kuona mtoto wa mtu akipotezwa kwa sababu ya tofauti za kisiasa.

Hata ukiangalia body language za watu mitaani,Wana amani Sana.

Hana hotuba za vitisho wala dharau.
Ana vijimaneneo vyake tu vya kipwani,au kimamamama lakini sio sio maneno makali.

Kitu pekee kitamharibia Samia kama asipocheza karata zake vizuri ni Kesi ya Mwamba Mbowe tu.

Vyovyote itakavyokua Samia Sio Mkatili.
Hawezi kuruhusu au kufurahia mambo kama yaliyompata Lisu yatokee ndani ya awamu yake,

Hawezi kupanua barabara na asiwalipe wahanga.

Ukweli ni kwamba Kwangu mimi ni bora Samia kuliko Jiwe.

Nchi ilikokuwa inaelekea Ni Mungu tu ndio ajuaye.

Hivi kw mfano mambo haya ya kuogofya na kutisha aliyokuwa akiyafanya Sabaya Intelijensia za akina Sirro hazikuyaona?
Pumbavu zako,mwanaume wa shoka kumlinganisha na mwanamke ni ufala ,mama atabaki kuwa mama kudekeza watoto,na mtoto hadeki kwa Baba ,utakuwa umekuzwa na mama yako akiwa msimbe,nyanoko!
 
Mleta mada,

Ukitaka ujue ubora na udhaifu wa JPM na Mamá Samia basi ingekupasa urejee changamoto tulizokuwa nazo toka awamu ya Kikwete.

**Rejea zile kelele za wananchi tukiongozwa na Chadema juu ya ufisadi wa Serikali ya JK ( skendo za EPA, Richmond, Escrow, ufisadi nssf) matumizi mabovu ya kodi za wananchi (safari za nje ya nchi za viongozi mbalimbali, semina na warsha zenye posho nono nono etc)
, rushwa kila kona, madawa ya kulevya, ujambazi na uporaji silaha kwenye vituo vya polisi, ugaidi wa kibiti mkuranga, ukwepaji kodi bandarini na kwenye biashara, watumishi hewa, huduma mbovu sekta ya afya, ubovu miundombinu ya barabara reli,na mengine kadha wa kadha

Kisha angalia alivyoingia Magufuli madarakani ameweza kushughulikia kwa kiwango gani hizo kero na changamoto zilizokuwa zinaikabili nchi yetu, ndipo utajua Magufuli alipiga kazi au alikuja kuuza sura

Sio unaleta vitu dhaifu dhaifu vya kumlinganisha Magufuli na Mamá Samia eti huruma, hana dharau, hana visasi, anapenda watu,,,, shabaaashhh....!!!

Magufuli hakuja kuuza sura, alikuja kuchapa kazi na kazi imeonekana.

Caution.

Kazi za serikali “hazionwi” wala kupimwa kwa macho. Anza na ripoti za CAG ndipo utakapoweza kuuona ukweli wa kazi hizo ikiwemo “value for money”. Ndipo utakapoona uwiano halisi kati ya mipango, miradi, gharama, matumizi halisi na matokeo. Nje ya hapo ni porojo.

Nipe bilioni 10 za kodi, najenga kituo cha afya cha kata na kununua ambulance moja ya hiace. Nakuambia “unaona kazi hiyo?”. Utanipigia vigelegele au utaniuliza nimetumia kiasi gani na mpango unahusu vitu gani hasa?
 
Sasa ulitaka aseme msaliti kijeshi hua anachekewa? Umewahi kusikia wapi msaliti kijeshi anabembelezwa? Hata huko Marekani anahukumiwa kifo.

Kwa hiyo unataka msaliti kijeshi asemewa, maneno ya kumfurahisha, kumbembeleza? I thought una hoja kumbe I was wrong, ni utumbo bin uharo.

Msaliti anahukumiwa kifo. Siku hizi ni maisha. Kifo hawakipendi. Rais wa Marekani hapigi talalila. FBI wanafanya yao msaliti anajikuta nyavuni mbele ya vyombo stahiki.

Msaliti gani huyo aliyehukumiwa kifo hapa Tanzania? Rais hawezi kuwa mpayukaji ovyo kiasi kile hadharani. Kama anamjua msaliti aarifu vyombo vya dola kimya kimya vimchukulie hatua za kisheria. Akipatikana na hatia “anyongwe”.

Sio hii kusema ovyo kisha kutuma incompetent assassins wammiminie zaidi ya risasi 30 halafu asurvive kuja kupambana nawe kwenye kinyang’anyiro cha uRais 2020 huku ukimkodolea macho kwa tension. You end up looking ridiculous.
 
Akili za kisukuma gang hizi. Unadhani Mungu anashindwa kumwangamiza shetani? Mbona anamuacha asumbue watu wake? Mungu huyohuyo alimwacha Meko atunyooshe ili apime akili zetu. Alivyoona akili zetu zimekaa kiUtopolo akaona isiwe taabu, akanyoosha mkono wake kutuokoa...

Hakika tumeuona mkono wake Bwana....
Duh. Comment ya wiki hii. Kwa jinsi tulivyo na tulipofikia, kwa kweli tulihitaji “divine intervention” ili kupona kuwa vichaa kabisa.

Yaani nilikua napata pain sana kusikia jirani yangu mwenye PhD ya medicine akiita Covid 19 ugonjwa wa changamoto za kupumua huku akipepesa macho kwa aibu!
 
Twitter na JF huwez AMINI kama nao ni watanzania. Huko FB na Ista ktk comment 1000,hazifiki 20 za kumponda Magufuli. Maoni sahihi na ya watanzania wengi huwez yapata Twitter au JF
Wa JF walisema Lissu atashinda kwa zaidi ya asilimia themanini,hawakujua Watanzania waliowengi hawajawahi kusikia hata JF Nini,kilichooza nafikiri alimusimulia Bibi yake Ikungi.

UN kumuenzi JPM kuliwaumbua, Watanzania kukanyagana wakimuaga lilikuwa pigo jingine.
Hivi huwa mnazungumzia huu Uchaguzi uliopita au mnatania.
Kwa taarifa yako huo Uchaguzi ilikua ni chukizo kwa Mwenyezi Mungu.
Na inawezekana Mungu aliamua kufanya yake baada ya kuona uonevu katika Uchaguzi huo.
Mawazo yako tu,Kama ingekuwa ukifanya uovu kwenye uchaguzi Kagame,Mseveni,hawa wangalikuwa wameshatwaliwa.
Vipi mimba zinazoharibika?
Vipi watoto wanaokufa wakati wa kuzaliwa?
Vipi watoto wadogo wanaokufa wakiwa na miaka 5 kwenda chini?
Walifanya uovu gani?

Vipi mama mkwe wa Mbowe?
Vipi Kaka yake Mbowe?
Walifanya uovu gani hata wakatwaliwa?
Je wewe mwema utaishi milele?

Ukijua wanadamu wote ni udongo ukiondoa wewe peke yako,watarudi kwa udongo hautahangaika kuwahukumu wengine.
 
Watu wa instagram ,facebook n.k.wanamlilia sana JPM na kumkumbuka,ila humu sijui mnakuwa mmetumwa? ...
😀😁😀Binafsi hupenda kujichanganya na watu mitaani na kwenye vyombo vya usafiri vya umma...ninachokisikia huko kinatisha, siwezi kuweka humu
 
Wenzako wameanza kuruka we piga tararira tu JF. Week ijayo wanaenda Glasgow kwenye environmental summit na posho kibao.

Watabebana wizara ya nishati, TPDC, TANESCO, wizara ya mazingira, NEMC na kila taasisi yenye vinasaba na huo mkutano huko Glasgow ‘mama oyee’.

Si ndio nchi mnayoitaka.
 
Pumbavu zako,mwanaume wa shoka kumlinganisha na mwanamke ni ufala ,mama atabaki kuwa mama kudekeza watoto,na mtoto hadeki kwa Baba ,utakuwa umekuzwa na mama yako akiwa msimbe,nyanoko!
Ha ha haawanaume wa Shoka ndiye aliwatengeneza akina Sabaya,Makonda,msiba na wasiojulikana.
Tombanonko ewe.
 
Msaliti anahukumiwa kifo. Siku hizi ni maisha. Kifo hawakipendi. Rais wa Marekani hapigi talalila. FBI wanafanya yao msaliti anajikuta nyavuni mbele ya vyombo stahiki.

Msaliti gani huyo aliyehukumiwa kifo hapa Tanzania? Rais hawezi kuwa mpayukaji ovyo kiasi kile hadharani. Kama anamjua msaliti aarifu vyombo vya dola kimya kimya vimchukulie hatua za kisheria. Akipatikana na hatia “anyongwe”.

Sio hii kusema ovyo kisha kutuma incompetent assassins wammiminie zaidi ya risasi 30 halafu asurvive kuja kupambana nawe kwenye kinyang’anyiro cha uRais 2020 huku ukimkodolea macho kwa tension. You end up looking ridiculous.
Asante Sana mtaalam
 
Caution.

Kazi za serikali “hazionwi” wala kupimwa kwa macho. Anza na ripoti za CAG ndipo utakapoweza kuuona ukweli wa kazi hizo ikiwemo “value for money”. Ndipo utakapoona uwiano halisi kati ya mipango, miradi, gharama, matumizi halisi na matokeo. Nje ya hapo ni porojo.

Nipe bilioni 10 za kodi, najenga kituo cha afya cha kata na kununua ambulance moja ya hiace. Nakuambia “unaona kazi hiyo?”. Utanipigia vigelegele au utaniuliza nimetumia kiasi gani na mpango unahusu vitu gani hasa?
Asante Sana kiongozi.
 
Duh. Comment ya wiki hii. Kwa jinsi tulivyo na tulipofikia, kwa kweli tulihitaji “divine intervention” ili kupona kuwa vichaa kabisa.

Yaani nilikua napata pain sana kusikia jirani yangu mwenye PhD ya medicine akiita Covid 19 ugonjwa wa changamoto za kupumua huku akipepesa macho kwa aibu!
Dah!
 
Back
Top Bottom