Kama ni kweli na ushahidi upo....

Kama ni kweli na ushahidi upo....

Hii yote inaonyeshwa na mtoa uzi kujitoa ufahamu, niliwahi kuielezea kabla ya hapa na nitajaribu kukuelezea tena kwa sababu sioni sababu ya kupinga a very strong argument toka kwa wachangiaji waliopita na mimi naongezea hoja za msingi ndani ya same argument.

Hapa Tanzania na nchi nyengine nyingi ambazo zinazoitwa zimeendelea, mfumo na taratibu tunaoutumia ie democratic country, ni wa kuiga na tumejikweza nao, una mpaungufu yake na mazuri yake, hii ni topic ya forum nyengine.

Ktk misingi hio ya democrasia na hata kikatiba, kwa sababu vyote viwili vinashabihia kitu kimoja..

Kuna kitu kinaitwa Public office au ofisi za watu, yaani mimi na wewe Nyani, na upande wa pili kuna watumishi au viongozi tuliyowapa dhamana ya kushikilia hizo nafasi, mbele ya KIAPO..

Mathalani wizara na makatibu wake, wakuu wa mikoa, wilaya nk

Na sehemu kubwa kuwa accountable na sifa ya uongozi wa Public office ni kitu kinaitwa transparency au uwazi.

Ndio maana ukienda hata kwenye councils offices, ofisi za madiwani za nchi kama UK na nyengine, cv za hawa madiwani ziko wazi, kuonyesha tunadeal na mtu wa aina gani na muhimu zaidi uwelewa wao kazi, kuchambua mambo, utungaji wa state policy na utendaji na ufutiliaji wa hizo sheria ktk utekelezaji wake.

Sasa tukija kwa Bwana Paul Makonda, yeye ni kiongozi wa mkoa, na sio diwani wa mtaa, ni kiongozi wa Public office yenye kujimuisha watu wasiopungua milioni 8, kwa hio mimi kama mwananchi na mkazi wa Dar, ni haki yangu kumuelewa na kumtambua Paul Makonda ni nani, ametokea wapi, amesoma wapi, amefanya nini ktk Maisha, alimradi full cv, na tafadhali don't get confused na maisha yake binafsi, kama kaoa wapi, anakula nini nk. Hapa kinachtafutwa integrity ya mtu na sio kingine..

Nataka kujua kama mlipa kodi wa jamahuri wa Tanzania na mkaazi wa Dar, kuelewa upeo na uwezo na weledi wa kiongozi wangu, na hio sio kitu cha ajabu.

Au Nyani, huko unakoishi waliokuajiri hawakukuomba uwapatie cv yako? Au it is a walk in job? Na hizo ni private entities wanayohaki ya kuihifadhi cv yako.. sembuse mimi mwananchi ambae ndie muajiri, you seems to be oblivious ya hii fact ndogo tu.

Sasa kwa hili mimi na wewe na wakaazi wa Dar ni waajiri wa Makonda, tunahitajiwa kuelewa hilo wasifu wa Makonda.

Ndio maana ikaitwa ofisi ya uheshimiwa, hatma yake Muheshimiwa sio kwa bahati bali kwa uwazi wake na heshima ya ofisi, yaani Public office, yaani kwa maana sahihi ofisi ya wananchi.

Mbona hili liko simple, serikali a big Public corporate au ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ituweke wazi juu ya hili, kuondoa agitation zetu na wasi wasi wetu.
Lkn kumbuka kuwa huyu ni kiongozi wa kuteuliwa lazima ofosu ya rais iliyomteua na kumweka madarakani hakika inajua cv yake ww kama ukihitaji kupatiwa cv yake nenda kwa aliyrmteua hakika atakupatia cv yake
 
Wanaomtuhumu Makonda walete ushahidi badala ya kumtaka yeye ndio awape ushahidi. Hatutaki hadithi bali nyaraka ....tuhuma mtoe nyie then kudhibitisha iwe mtuhumiwa ....
 
Don't you know that you can illegally own something which is not your!?
Who owns the original certicates then, i mean the real paul Makonda - Where is he and why is he silent if at all it's true he exists
 
Ndugu Nyani Ngabu kinachonisikitisha ni kwanini mnawalaumu hawa "walalamikaji" wa kwenye media badala ya kuwalaumu mamlaka husika polisi na vyombo vingine kwa kukaa kimya na kutokufanya uchunguzi na kuja kuclear doubt au wamuombe Makonda mwenyewe aje afanye clearance kama si kweli:
Hili ni kosa la jinai (uhalifu) kuwa umefanyika kwanini polisi wapo kimya.

I wonder why police need to be moved to take action on this. Tumeona hata practice polisi wetu si lazima wamuvuzishwe popote pale wanapoona pana harufu ya uhalifu huingia hata bila kuambiwa iweje sasa this criminal offense is alleged to be done nao wapo kimya?

Polisi utendaji wao ni tofauti na mahakama tumezoea mahakama wanamsemo kwamba "the court is not your mother cannot give you what you didn't ask" kwamba mahakama ni lazima imuvuzishwe hata jaji akiwa amepata taarifa kuwa kuna mtu ameuawa au umezurumiwa hawezi kujihusisha na hiyo kesi mpaka imeletwa mahakamani na usipoileta shauri yako hiyo ndiyo maana ya "mahakama siyo mama yako haiwezi kukupatia usichokiomba"

Lakini kwa polisi ni tofauti akipata taarifa kuwa kuna mtu ameuawa lazima achunguze haijarishi taarifa hizo ameziona kwenye gazeti, mtandaoni au popote.

Iweje hili swala la Makonda wasubiri mtu akaripoti eti? Hizo taarifa za kiintelejensia zipo wapi?
Mbona linapokuja swala la uchochezi wanafanyia kazi taarifa za mtandaoni? Kwanini?.

Mwisho.
Hii ni kesi ya jinai polisi ndiyo wanatakiwa kuonesha interest mpaka sasa wapo kimya eti wanasubiri taarifa rasmi isipopelekewa hiyo ripoti basi mtuhumiwa aendelee kuenjoy good life in the cape of Good Hope of south Africa?

Na hao waliosimamisha ajira zote wakikagua vyeti nao wanasubiri taarifa rasmi?

Just imagine hizi tetesi zingekuwa juu ya uwepo wa magaidi wa amboni au ujambazi BOT wangebaki ofisini wakisubiri taarifa rasmi?
Ukiona mtu haelewi hata hili nae atakuwa alibashitika katika elimu yake...
 
Lkn kumbuka kuwa huyu ni kiongozi wa kuteuliwa lazima ofosu ya rais iliyomteua na kumweka madarakani hakika inajua cv yake ww kama ukihitaji kupatiwa cv yake nenda kwa aliyrmteua hakika atakupatia cv yake

Mbona unaongelea ndoto za asubuhi Mkuu, jaribu kupitia hio comment yangu tena na tena, wasi wasi wangu bado hujanielewa..

Ulichonijubu sio sehemu ya discussion au tusingefikia hapa tulipo.
 
Wanaomtuhumu Makonda walete ushahidi badala ya kumtaka yeye ndio awape ushahidi. Hatutaki hadithi bali nyaraka ....tuhuma mtoe nyie then kudhibitisha iwe mtuhumiwa ....

Unaelewa misingi ya ufanyaji kazi Public office na moja ya ushahidi, hii nchi inakokwenda ni wewe Mkuu na comment kama hizi ambazo hazina mashiko hata kwa Mungu..
 
Mkuu Nyani Ngabu,mfumo wa kisheria wa nchi yetu ya Tanzania hauruhusu mtu binafsi kumfungulia mwingine,na kuendesha kesi mahakamani,kesi ya jinai. Kinachotakiwa ni kwa mtu mwenye ushahidi dhidi ya jinai ya mwingine kuuwasilisha ushahidi huo kwa mamlaka zinazohusika,mfano polisi au TAKUKURU,ili hatua stahiki zichukukiwe. Mamlaka hizo na nyinginezo,kama Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ndizo zitakazomshtaki mhusika. Ndiyo kusema,wenye kuamua kushtaki au la ni watawala waliopo kwenye mamlaka hizo iwe ushahidi umekabidhiwa au ule walionao wenyewe.
Mtu wa namna yako ndiye niliyekuwa namtaka anitoe uyungi yungi nilionao kichwani juu ya hili.

Hao wanaosema au anaesema kuwa vyeti halisi anavyo mezani kwake au ofisini kwake, kwa nini asiviwasilishe mamlaka husika?!
 
Mbona unaongelea ndoto za asubuhi Mkuu, jaribu kupitia hio comment yangu tena na tena, wasi wasi wangu bado hujanielewa..

Ulichonijubu sio sehemu ya discussion au tusingefikia hapa tulipo.
Itakuwa vzr maana ndoto za asbh ni njema
Lkn mkuu ukisema nimeenda kinyume na kile unachodai ni maada bado pia umetoka nje ya mada ya mleta uzi
Mleta uzi anahitaji uthibitisho kwa wale wanaotoa tuhuma kuhusu elimu ya mpambana na madawa ya kulevya.
 
Who owns the original certicates then, i mean the real paul Makonda - Where is he and why is he silent if at all it's true he exists
Do you really expect me to answer that!!??

That's the puzzle everyone is trying understand. May be Gwajima will come up with answers soon ........ But only if he does not receive an apology!!
 
mkuu hilo tatizo halipo kwa Makonda peke yake wapo wengi hasa wengi waliomaliza kuanzia kidato cha nne chini ya mwaka 2005
sote ni mashahidi katika hili hata mimi mwenyewe nina ndugu yangu ni lecture lakini form one alitumia jina la mtu
ile operation isingevamiwa na siasa ingewatoa wengi madarakani lakini linagusa wengi sana lets keep watching the movie
 
Itakuwa vzr maana ndoto za asbh ni njema
Lkn mkuu ukisema nimeenda kinyume na kile unachodai ni maada bado pia umetoka nje ya mada ya mleta uzi
Mleta uzi anahitaji uthibitisho kwa wale wanaotoa tuhuma kuhusu elimu ya mpambana na madawa ya kulevya.

Mkuu, Moja ya raha ya maongezi nikujiwezesha kwa wa kile anachokiongea mwenzako kukielewa, kwa mtindo wa JamiiForums kusoma na kuelewa kile kilichoandikwa.

Na ndio nakubaliana na wewe, hapa inaongelewa ni ushahidi wa jamhuri juu ya mtuhumiwa.

Na ushahidi wa muajiriwa juu ya muajiri, yaani mimi na wewe aka mwananchi, mlipa kodi Ikiwa ndani ya Dar au mikoani, au kwa msemo sahihi mimi na wewe ndio tunaolipa mishahara, kwa hio jamhuri au kwa kuanzia ofisi ya Mkuu wa Mkoa ndio atupe ushahidi, na sio vice versa.

Naelewa neno Public office au kwa maneno mepesi ofisi ya kwako, yangu na wote sisi humu, hilo neno bado naona linakutatiza.

Nakushauri google it, utapata kufunguka Mkuu , kwa hio kwa comment yako hapo mimi kutoka nje ya mada, mbona nimo at the core of it, kama Dunia na kilichomo ndani yake.

Tutazidi kufahamishana mkuu, ukielewa wewe na mimi basi, taratibu tutaelewana kwa jengine.

Na jengine kwa argument ya kusema mtendaji wa serikali aka Wakuu wa mikoa ambao si wakuchaguliwa yaani wa kuteuliwa na sio accountable kwa anao waongoza yaani sisi wananchi, haina mashiko kwa sababu hapo unaongelea jamhuri yaani serikali kwa ujumla wake, ndio sasa panakua pazuri zaidi, Kwa hio ni amri tu toka juu iende wizara ya elimu, kumlinda mtendaji kwa njia ambayo itutaarifu niyaje.

It sting both ways.. Ndio maana akiwa wazi na sisi kondoo basi tumeridhishwa na mtendaji wetu, tunaangalia mengine muhimu zaidi ya
Haya.
 
Issue hii imenza ku-trend wiki mbili zilizopita, na kuna ushahidi kibao umeshatolewa na akina Mange Ki
Kaka;
Huyo mwanamama ni dummy god kule Instagram!

Sikuwahi kuamini kama Joseph Kibwetere aliwahi kuwaaminisha na kuwafanya watu wakajichoma moto ili waende ''mbinguni'' lakini kinachoendelea kule Instagram nimeanza kuamini kuna uwezekano hata Tanzania kuna watanzania wenye akili na fikra zinazofanana na wafuasi wa Kibwetere.

Huyu dummy god anaweza kuwaambia wafuasi wake ambao ndani yake kuna wahitimu wa UNI wavue nguo na kutembea uchi na watavua nguo na kutembea uchi.

Hakuna umasikini mbaya duniani kama umasikini wa fikra.

Mange Kimambi is a dummy god? you must be kidding me. You may not like her style, but she is smarter and intelligent than you think. The problem is, we are so obsessed with political correctness and lies.
 
98ecbb1a6bff23c44870abba3a00fb07.jpg
Alizaliwa tar.15/02/1981 katika kijiji cha Koromije, wilaya ya Misungwi, mkoa wa Mwanza.
Mbona miaka inapishana? :Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero
 
Back
Top Bottom