Kama kuna Rais anayetafuta legacy ya kudumu asimamie mipango miji

Mwanafalsafa

Platinum Member
Jun 24, 2007
662
851
Akili na ustaarabu unaanzia kwenye mipango miji.

Kama kuna Rais anayetafuta legacy ya kudumu asimamie mipango miji. Mipango miji ni legacy ya milele. Ukishapanga mitaa na barabara zitabaki hivyo milele. Ukishindwa kupanga kuja kurekebisha ni ngumu sana. Gharama yake ni kubwa sana kiasi kwamba huwa haiwezekani. Sasa mtu akija kwenye nchi zetu hizi za Afrika lazima atuone ni wapumbavu tu kama tunashindwa kitu kidogo sana na kisichohitaji akili kubwa cha kupanga miji na kunyosha makazi.

Watu wanaweza wakajenga nyumba za kifukara za mabanda lakini wazjenge katika mitaa iliyonyooka. Siku nchi ikitajirika au wananchi wakitajirika watabomoa vibanda hivyo na kujenga nyumba za kisasa.

Lakini huwezi kujenga barabara na mitaa iliyonyooka na ya kupendeza kama hukupanga mji na kuweka nafasi ya barabara zilizonyooka na zenye nafasi. Utafanya kwa kiasi kidogo tu kwa sababu gharama za kunyoosha mji ambao haujapangiliwa ni kubwa sana.

Tuanzie hapo kwanza ndo maendeleo tutayaona. Kuna faida nyingi sana kiuchumi za kuwa na miji na makazi yaliyopangiliwa. Usambazaji wa huduma na bidhaa unakuwa rahisi. Unaweza ukajenga kwa urahisi mifumo ya kusambaza huduma ambazo zina mchango mkubwa sana katiba pato la taifa kama vile mabomba ya maji, mabomba ya gesi, nyaya za mawasiliano (internet na cable TV), na kurahisha usafirishaji wa bidhaa na hivyo kuchochea biashara kwa njia ya Posta.

Mifano ya maeneo ambayo ni ngumu sana kuja kuyanyoosha ili yaoneshe kuwa hii nchi ina watu wenye akili:

Dar es Salaam


1677310361341.jpeg


Oysterbay (kushoto), Namanga (kulia)

1677310400942.jpeg


Mwanza (Mabatini)

1677310387682.jpeg


ONA NYUMBA ZA KIMASKINI LAKINI ZIMEPANGILIWA ZINAVYOPENDEZA. HAPA HATA NDO UTAJIRI UKIPATIKANA BAADAE NI RAHISI KUPABORESHA PAKAPENDEZA ZAIDI.

Kambi ya Wakimbizi Kasulu (Hii ni kazi ya UN ndo imepanga hiki kijiji cha kimaskini nyumba zimenyooka)

1677310413434.jpeg


Hii ni Nepal, kuna tajiri kajenga nyumba hizi za kimaskini kwa ajili ya watu wa kipato cha chini waweze kuishi vizuri. Ona zinavyopendeza kwa jinsi zilivyopangiliwa:

1677310425438.jpeg

1677310431750.jpeg


KUONESHA NI JINSI GANI WATANZANIA TUKO NYUMA KABISA KATIKA MIPANGO MIJI (YAANI HAIPO KABISA KATIKA AKILI ZETU) ONA HATA MAKABURI YETU YALIVYOKAA SHAGHALABAGHALA.

Haya ni Makaburi ya WaTanzania:

1677309916720.jpeg


1677309924714.jpeg


Linganisha na Makaburi ya watu ambao suala la mipango miji liko kwenye damu zao tayari. Haya ni makaburi ya wazungu na wahindi waliokufa katika vita ya pili ya wazungu (1938-1945), yako Dar es Salaam jirani na Nyumba ya Sanaa.

1677310053033.jpeg


Na haya ni makaburi kutoka nje ya nchi:

1677310078579.jpeg


Mimi nakerekwa sana SANA na serikali yetu jinsi ambavyo inaachia watu wajenge makazi holela holela tu. Serikali inakuwa wapi kutoa amri ya kwamba ni marufuku kujenga eneo lolote ambalo halijaingizwa katika mipango miji?

Katika suala la kuunda utitiri wa Mamlaka (Executive Agecies) kwa nini isiunde Mamlaka moja ambayo kazi yake itakuwa ni moja tu... kuhakikisha hakuna jengo lolote linalojengwa nje ya mpango mji?
 
Mipango miji ilikuwepo tangu ukoloni ila serikali ndio imeziharibu kwa kukosa maarifa maana nikisema kukosa akili ni neno pana

Miji ilikuwa kwenye mipangilio kama ulivyosema ya kuwa hata ziwe za kimasikini lakini zimepangwa

Hata Dar mjini nyumba za udongo zipo na zilikuwepo ila suala linakuja watu wakapewa hela ndefu au wazazi wanapokufa watu wanakuja na kuziuza

Hapo ndio unakuta anatokea tajiri na kuporomosha gorofa na serikali ndio wanaotoa vibali bila kuwa na taaluma ya mipango miji
Drainage systems ni mbovu kwa sababu wamevunja na kuchimbua kila kitu wakati wa ujenzi holela na serikali imekaa kimya

Dar masika bora ukae kijijini kuna hali ya hewa nzuri kuliko kugongana na vinyesi kila kona unayopita

Hivi mnajisikiaje kuona Mavi yanaelea mitaani halafu ndio jiji kuu?

Tanzania nimeona miji miwili tu iliyojengwa kama Glasgow nayo ni Tanga na Urambo
Hizi sehemu zimefanana sana kwani zote 3 nimefika

Barabara zao ni vertical na horizontal na unatembea hadi raha jinsi ilivyopangika

Kama wangedhibiti ujengaji holela au kutoa masharti magumu basi tungekuwa na miji mizuri sana
Screenshot_20230225_075852_Maps.jpg
Screenshot_20230225_075934_Maps.jpg
Screenshot_20230225_080347_Maps.jpg
 
Mimi na kupinga mipango miji sio kipaumbele mimi naomba Raisi atakae weza kusambaza maji safi na salama nchi nzima hasa hasa Dar na Dodoma, huyu ata akibadili katiba atawele mihula mitatu amalizie mradi ntamsupport na hili jambo linawezekana Ziwa Victoria lina maji baridi na ya wakika. Kama unaweza kusafirisha mafuta kitoka Hoima Uganda kwanini km 1600 kwanini usisafirishe maji kutoka shinyanga 900km hadi Pwani.....maji ni kero dar.
 
Hongera Mtoa mada. umegusa eneo muhimu lililo sahaulika.
Mipango Miji ni zoezi linalohitaji Fedha Nyingi ili kulikamilisha, Hii ni Kuanzia Kupanga, Na kutekeleza kile kilichopangwa.

Jambo la Kustaajabisha Katika Vipaumbele vya Serikali,
1. Kilimo
2. Mifugo
3. Afya
4. Elimu
5. Uvuvi
6. Nishati
7. Maji
8. Usafirishaji
9. TEHAMA
10. Utalii, Orodha ni Ndefu
Hata ukitaja Vipaumbele 20, Hutaikuta Ardhi,(Ambayo ndani yake kuna Mipango miji). Mambo yote niliyotajwa hapo juu yanatekelezwa juu ya Ardhi, ambayo Kuipanga sio kipaumbele cha Serikali.

Ndio maana Si ajabu Kukuta tunahangaika Kulipa Fidia Majengo ya watu eti Kupisha Ujenzi wa Barabara, au Ujenzi wa Hospitali n.k

Angalia huu Mfano;
Umezembea Kupanga Ardhi yako,
Afya italeta shida;
kwanza, Utakosa maeneo ya Kujenga vituo vya Afya, Utakosa maeneo ya kutupa taka, taka zikizagaa Magonjwa ya Mlipuko yatazidi (Rejea Kipindupindu na Jiji la Dar), n.k

Migogoro ya Wakulima Na Wafugaji Chanzo, Ardhi haijapangwa, Mkulima Alime wapi, na Mchungaji achunge wapi.

Mifano ni Mingi, Mipango miji ni lazimw iwe kipaumbele, Kwa sababu Shughuli nyingize zote zinatekelezwa katika Ardhi, kwaiyo lazima ipangwe.
 
Swala la mipango miji haliepukiki kama tunataka maendeleo endelevu lakini hapa kwetu limezungukwa na siasa zisizo na nia ya kweli(porojo kwa wapiga kura)
 
Naunga mkono hoja. Ila wakulaumiwa ni kuanzia serikali za mitaa kwa watendaji, wajumbe mpaka kata ,wilaya,mkoa na Tarura na Tanroads.


Mfano barabara ya kawe imeachwa watu wanajenga mpaka barabarani maduka na kubakiza njia ndogo hata waenda kwa miguu wanaweza kugongwa na magari.ile kawe ingepata watendaji wazuri isingefika pale ilipofika yaani lori likipaki kushusha nafaka basi njia nzima inasimama.


Yaangaliwe mawe tu waliozidi wavunjiwe . Tegeta watu wamejenga fremu za biashara wameruka mawe ya viwanja serikali ipo imekaa kimya kama sio jukumu lake kunatakiwa service road zionekane na zipitike wao wamekaa kimya.ukienda njia ya goba kule goba centre fremu zimejaa mpaka barabarani.

Kitu cha kushangaza makaburi yetu yanasikitisha hata malawi na umaskini wote marehemu wanazikwa vizuri kwa mistari kama makaburi ya mashujaa pale nyuma ya gymkhana. Kwanini tusiige wamarekani grave yard zao zimetulia mpaka raha lakini sisi ni uchafu mpaka wa akili.

Huku mitaani kuna vibopa makusudi wanajenga wanafinya barabara na mamalka zipo zimekaa kimya ni kama hawahusiki. Sijui nani katuloga waswahili hata kenya watu wanajenga kwa mpangilio wanafuata ramani na mawe hapa hilo limeshindikana kabisa
 
Mimi na kupinga mipango miji sio kipaumbele mimi naomba Raisi atakae weza kusambaza maji safi na salama nchi nzima hasa hasa Dar na Dodoma, huyu ata akibadili katiba atawele mihula mitatu amalizie mradi ntamsupport na hili jambo linawezekana Ziwa Victoria lina maji baridi na ya wakika. Kama unaweza kusafirisha mafuta kitoka Hoima Uganda kwanini km 1600 kwanini usisafirishe maji kutoka shinyanga 900km hadi Pwani.....maji ni kero dar.
Jinga wewe
 
Wanasiasa uchwara huku hutowaona maana hiyo hauonekani Kwa macho kama madaraja and such upuuzi
 
Mipango Miji ni zoezi linalohitaji Fedha Nyingi ili kulikamilisha, Hii ni Kuanzia Kupanga, Na kutekeleza kile kilichopangwa.
Fedha nyingi ndo shilingi ngapi?

Maono yangu ni serikali ianze kwa kuunda Mamlaka ya Taifa ya Mipango miji, badala ya kuwaacha Halmashauri kila mmoja ajifanyie anavyoona inafaa.

Hiyo ni kama ilivyoundwa TARURA kusimamia barabara ndogo, badala ya kuachia Halmashauri zijifanyie zinavyotaka ambapo kulikuwaga na upuuzi mwingi sana ulikuwa unaendelea katika ujenzi wa barabara ndogo za kwenye halmashauri.

Halafu iweke sheria kwamba ni marufuku kujenga kwenye eneo ambalo halijawekwa kwenye mpango mji.

Kisha serikali ikawa inawahi maeneo ambayo hayajajengeka na kuyapima na kuyawekea ramani.

Kisha Mamlaka ikawa na kazi ya kufuatilia kwamba yeyote anayejenga nie ya mpango mji anazuiwa mapema, na akikaidi anavunjiwa jengo lake.

Mapato ya Mamlaka yatatokana na:
1. Mauzo ya viwanja
2. Kodi ya ardhi
3. Faini kwa wakosefu.
 
Hii itakuwa na ufanisi mkubwa sana
Fedha nyingi ndo shilingi ngapi?

Maono yangu ni serikali ianze kwa kuunda Mamlaka ya Taifa ya Mipango miji, badala ya kuwaacha Halmashauri kila mmoja ajifanyie anavyoona inafaa.

Hiyo ni kama ilivyoundwa TARURA kusimamia barabara ndogo, badala ya kuachia Halmashauri zijifanyie zinavyotaka ambapo kulikuwaga na upuuzi mwingi sana ulikuwa unaendelea katika ujenzi wa barabara ndogo za kwenye halmashauri.

Halafu iweke sheria kwamba ni marufuku kujenga kwenye eneo ambalo halijawekwa kwenye mpango mji.

Kisha serikali ikawa inawahi maeneo ambayo hayajajengeka na kuyapima na kuyawekea ramani.

Kisha Mamlaka ikawa na kazi ya kufuatilia kwamba yeyote anayejenga nie ya mpango mji anazuiwa mapema, na akikaidi anavunjiwa jengo lake.

Mapato ya Mamlaka yatatokana na:
1. Mauzo ya viwanja
2. Kodi ya ardhi
3. Faini kwa wakosefu.
 
Manispaa nyingi sasa hivi ukienda kutaka kiwanja unaelekezwa kwa kampuni binafsi,huwezi pata kiwanja kwa urahisi hata Kama unapesa,utapeli wa ardhi Ni wa kiwango Cha juu sana,wabunge wetu nao vichwani Ni empty containers hawawezi kujadili swala lolote lenye manufaa kwa watu wetu Ni watu wa hovyo wasiojiamini
 
Mipango miji ilikuwepo tangu ukoloni ila serikali ndio imeziharibu kwa kukosa maarifa maana nikisema kukosa akili ni neno pana

Miji ilikuwa kwenye mipangilio kama ulivyosema ya kuwa hata ziwe za kimasikini lakini zimepangwa

Hata Dar mjini nyumba za udongo zipo na zilikuwepo ila suala linakuja watu wakapewa hela ndefu au wazazi wanapokufa watu wanakuja na kuziuza

Hapo ndio unakuta anatokea tajiri na kuporomosha gorofa na serikali ndio wanaotoa vibali bila kuwa na taaluma ya mipango miji
Drainage systems ni mbovu kwa sababu wamevunja na kuchimbua kila kitu wakati wa ujenzi holela na serikali imekaa kimya

Dar masika bora ukae kijijini kuna hali ya hewa nzuri kuliko kugongana na vinyesi kila kona unayopita

Hivi mnajisikiaje kuona Mavi yanaelea mitaani halafu ndio jiji kuu?

Tanzania nimeona miji miwili tu iliyojengwa kama Glasgow nayo ni Tanga na Urambo
Hizi sehemu zimefanana sana kwani zote 3 nimefika

Barabara zao ni vertical na horizontal na unatembea hadi raha jinsi ilivyopangika

Kama wangedhibiti ujengaji holela au kutoa masharti magumu basi tungekuwa na miji mizuri sana View attachment 2529384View attachment 2529385View attachment 2529386
Hii picha ya mwisho wapi?
 
Dodoma wanajitahidi na ni wakali "kweri kweri".

JK alikua na miji yake ya mfano sijui iliishia wapi, mmojawapo ulikua mvomero.

Kwa jinsi miji mingi ilivyo kwa sasa, nguvu isiyokuwa ya kawaida itatakiwa kutumika kuipanga, next to impossible.
 
Back
Top Bottom