Kama huku ndiyo kufa basi ni hatari

Kama huku ndiyo kufa basi ni hatari

Kwahiyo ulitibiwa au baada ya kuzunguka ndo ikawa pona yako? Baada ya kuzinduka na tumbo likapona?
 
Ilikuwa Alhamisi ya last week nilikuwa nasikia maumivu ya tumbo sana. Familia yangu wakanikimbiza hospitali maana hali yangu ilikuwa siyo nzuri, ndugu na jamaa walikuwa wanasubiri majibu kutoka kwa docters tu maana nilikuwa na hali mbaya.

Nilifika hospitali kwa bahati mbaya kama maelezo yao walivyonisimulia kuwa nilikufa kabisa wakanifunika na shuka. Sasa kilichonishangaza mimi kipindi nipo kitandani pale mimi nilihisi kuwa nimelala, yaani nimepumzika maana akili yangu bado ilikuwa inafanya kazi kabisa.

Nilikuwa nasikia vilio vya watu na kutambua huyu ni mama yangu, huyu ni fulani, ila kule kuongea au kutikisika na kufungua macho ndiyo nilikuwa siwezi kabisa.

Kwa maelezo yao walisema nilifanya kitu cha masaa matatu maiti yangu iko tu kitandani, walikuwa wanafanya utaratibu wakunipeleka mochari ndiyo nikafufuka tena.

Mpaka sasa hivi bado najiuliza kumbe mtu akifa akili yake bado inafanyaga kazi? Kweli ninaamini wangenipeleka udongoni ningejua na pelekwa udongoni, maana nilikuwa nafahamu na nilikuwa nasikia watu wanavyo lia.

Kama ndiyo kufa ni Mungu tu mwanadamu hawezi, watu wanazikwa huku wakijua kabisa wanapelekwa udongoni ila nguvu ya kukataa ndiyo hawana!
Walikueleza kwa nini ilichujua masaa matatu bila ya kupelekwa chumba cha maiti? Na je uliamka mwenyewe au nini kilitokea wakajua bado umzima? Maumivu ya tumbo yalipotea aje?
Mtu anapofariki, anayetoa taarifa ya mwisho ya uthibitisho wa kifo ni daktari. Je ilithibitishwa hivyo?
 
Wengi hapa wataona kama utani lakini alichozungumza kiliwahi nitokea kabisa, unasikia lakini huwezi fanya lolote, binafsi nashauri mtu anapozima ghafla kuwepo na subira na mazoezi mengine ya kuuamsha mwili, kwa atleast 6 hours, and then Daktari aje approve mambo mengine, hii kukimbiza kuzika ni mbaya Sana.
Nini kilikutokea kikakufanya usikie bila kuwa na uwezo wa kufanya lolote?

Je uliumwa tumbo kama mleta mada? Au labda ulipata ajali?

Kama ni angalizo unatoa, lazima uelezee na mazingira yaliyosababisha wewe kukutwa na hali hiyo.
 
Guys,Guys omba yasikukute,niliwahi pata ajali mbaya sana aisee nilikuwa katika hali kama hyo,Nasikia kila kitu ila siwezi kufanya chochote Daa...kuna mama mmoja huwa simsahau mpaka leo yaan huyo ndo alikuwa anashindilia kabsa.nanukuu"Jamani huyu tayari tuharakishe tuanze taratibu za mazishi"[emoji23][emoji23][emoji23]
Hayo maneno huyo mama alisema kwenye eneo la ajali? Ama ni baada ya kufikishwa hospital?

Nina imani huyo mama mtakuwa mnafahamiana kama alitaka kuanza taratibu za mazishi.(Hili ni endapo hii siyo chai)

Pia story yako hii, haimaanishi kwamba tayari ulikuwa umeshakufa then ukafufuka.

Kuzungumzia taratibu za mazishi hapo hapo kwenye ajali ni jambo la ajabu sana.😄
 
"Nilifika hospitali kwa bahati mbaya kama maelezo yao walivyonisimulia kuwa nilikufa kabisa wakanifunika na shuka."

Huenda kadanganya, ila hii dunia ina mambo mengi ambayo ni ya ajabu na hatujui ni nn hawa kimetokea pale kinapotokea na unapomsikiliza mtu unaona kabisa huu ni uongo. Tunasahau kuwa hatujui siri zote za huu ulimwengu. Ukikaa na watu wanaofanya huduma za kusafirisha maiti wanasema kuna maiti huwa zinagoma kusafirishwa mpaka mnashusha watu au mtu fulani.
Wanaposema “ulikufa kabisa”, wanamaanisha kwamba ulikata pumzi?
 
Shukuru mungu sana.kule mochwari ungepelekwa usingetoka salama.
Wana RUNGU kubwa kwa ajili ya marehemu wabishi.daktari amethibitisha umekufa afu uamkie monchwari unapewa moja la utosi unatulia.
Muulize yule JR atakwambia
Nmecheka sana kichaa angu 😂😂😂
 
Umewahi kufa? Katika nadharia ya Kisayansi ndo tunasema hivi ulivyosema ila uhalisia halisi hatujui. Huenda maiti huko kaburini roho zao zinapiga story na zinaona yote ila hazina mlango wa kufikia walio hai. Hakuna binadamu aliye hai anaweza thibitisha hili. Tena angalau wale ambao walishakuwa mahututi sana wanaweza sema, na near death experience ukizisikiliza wapo wanaokiri walijua kila kitu kinachoendelea.
Hao wa “near death” walikuwa “resuscitated”?
 
Umewahi kufa? Katika nadharia ya Kisayansi ndo tunasema hivi ulivyosema ila uhalisia halisi hatujui. Huenda maiti huko kaburini roho zao zinapiga story na zinaona yote ila hazina mlango wa kufikia walio hai. Hakuna binadamu aliye hai anaweza thibitisha hili. Tena angalau wale ambao walishakuwa mahututi sana wanaweza sema, na near death experience ukizisikiliza wapo wanaokiri walijua kila kitu kinachoendelea.
Mimi sijawahi kufa ndugu yangu, ila wewe ndiye, uliewahi kufa siyo.

Kwahiyo jamaa alikufa kidini, alikufa kwa kufuata dini gani, je wasiamini dini yeyote inakuwaje.
 
Ilikuwa Alhamisi ya last week nilikuwa nasikia maumivu ya tumbo sana. Familia yangu wakanikimbiza hospitali maana hali yangu ilikuwa siyo nzuri, ndugu na jamaa walikuwa wanasubiri majibu kutoka kwa docters tu maana nilikuwa na hali mbaya.

Nilifika hospitali kwa bahati mbaya kama maelezo yao walivyonisimulia kuwa nilikufa kabisa wakanifunika na shuka. Sasa kilichonishangaza mimi kipindi nipo kitandani pale mimi nilihisi kuwa nimelala, yaani nimepumzika maana akili yangu bado ilikuwa inafanya kazi kabisa.

Nilikuwa nasikia vilio vya watu na kutambua huyu ni mama yangu, huyu ni fulani, ila kule kuongea au kutikisika na kufungua macho ndiyo nilikuwa siwezi kabisa.

Kwa maelezo yao walisema nilifanya kitu cha masaa matatu maiti yangu iko tu kitandani, walikuwa wanafanya utaratibu wakunipeleka mochari ndiyo nikafufuka tena.

Mpaka sasa hivi bado najiuliza kumbe mtu akifa akili yake bado inafanyaga kazi? Kweli ninaamini wangenipeleka udongoni ningejua na pelekwa udongoni, maana nilikuwa nafahamu na nilikuwa nasikia watu wanavyo lia.

Kama ndiyo kufa ni Mungu tu mwanadamu hawezi, watu wanazikwa huku wakijua kabisa wanapelekwa udongoni ila nguvu ya kukataa ndiyo hawana!
Ulaya mtu hatangazwi kafa hadi Dr ampime na kuthibitisha kuwa amekufa. Dr anatumia chombo cha kusikiliza mapigo ya moyo ndipo atasema mtu yuko hai ama la. Kwako nina imani ulipoteza fahamu tu
 
Ilikuwa Alhamisi ya last week nilikuwa nasikia maumivu ya tumbo sana. Familia yangu wakanikimbiza hospitali maana hali yangu ilikuwa siyo nzuri, ndugu na jamaa walikuwa wanasubiri majibu kutoka kwa docters tu maana nilikuwa na hali mbaya.

Nilifika hospitali kwa bahati mbaya kama maelezo yao walivyonisimulia kuwa nilikufa kabisa wakanifunika na shuka. Sasa kilichonishangaza mimi kipindi nipo kitandani pale mimi nilihisi kuwa nimelala, yaani nimepumzika maana akili yangu bado ilikuwa inafanya kazi kabisa.

Nilikuwa nasikia vilio vya watu na kutambua huyu ni mama yangu, huyu ni fulani, ila kule kuongea au kutikisika na kufungua macho ndiyo nilikuwa siwezi kabisa.

Kwa maelezo yao walisema nilifanya kitu cha masaa matatu maiti yangu iko tu kitandani, walikuwa wanafanya utaratibu wakunipeleka mochari ndiyo nikafufuka tena.

Mpaka sasa hivi bado najiuliza kumbe mtu akifa akili yake bado inafanyaga kazi? Kweli ninaamini wangenipeleka udongoni ningejua na pelekwa udongoni, maana nilikuwa nafahamu na nilikuwa nasikia watu wanavyo lia.

Kama ndiyo kufa ni Mungu tu mwanadamu hawezi, watu wanazikwa huku wakijua kabisa wanapelekwa udongoni ila nguvu ya kukataa ndiyo hawana!
Roho huwa haifi, unaokufa ni mwili tu
 
Ulaya mtu hatangazwi kafa hadi Dr ampime na kuthibitisha kuwa amekufa. Dr anatumia chombo cha kusikiliza mapigo ya moyo ndipo atasema mtu yuko hai ama la. Kwako nina imani ulipoteza fahamu tu
Moyo unaweza kusimama ila mtu bado akawa hajafa mpaka ubongo ufe(brain dead)
 
Mimi sijawahi kufa ndugu yangu, ila wewe ndiye, uliewahi kufa siyo.

Kwahiyo jamaa alikufa kidini, alikufa kwa kufuata dini gani, je wasiamini dini yeyote inakuwaje.
Boss, Nilichosema ni hakuna aliyehai anayejua pasipo shaka ukifa nn kinatokea. Sijasimama na watu wa dini au wapagani.
 
Hayo ni mambo ya kiimani, Kisayansi hakuna kitu Roho.
Kuna mambo Sayansi haijaweza kuthibitisha pasipo shaka ndo maana imani zipo. Binadamu si mwanasansi au mwanadini, hakuna anayejua siri ya kifo. Wote tunaamini na kuassume tu.
 
Kuna mambo Sayansi haijaweza kuthibitisha pasipo shaka ndo maana imani zipo. Binadamu si mwanasansi au mwanadini, hakuna anayejua siri ya kifo. Wote tunaamini na kuassume tu.
Labda utaniona mimi, sina imani, ila mada iko mbali na dini, Wachangiaji ni watu wote bila kujali imani zao.

Je unaweza kumdhitishia mwana sayansi, sehemu ilipo roho ya mwanadamu.
 
Kifo kifo kifo hakina huruma Kuna baazi ya shuhuda zinasema mgonjwa alipo karibia kukata Roho aliwekwa katika kasha la kioo ambacho kinaonyesha kila kitu na likiwa limefungwa haliingizi hewa hazikupita dk Kazaa mtu huyu alikukuruka na kukata moto lakini kioo kilipasuka ile design paaa''
 
Back
Top Bottom