Kahama VS Njombe/Mafinga

Kahama VS Njombe/Mafinga

Simjui Sasa choice na fallacy wapi na wapi we Jamaa.Wacha umbea na uchonganishi.
Kula dozi yako
JamiiForums-2010797655.jpg
 
#IceFmHabari
Wafanyabiashara ambao watapisha ujenzi wa soko kuu mjini Makambako wilayani Njombe ambao unatarajia kuanza mwakani 2024 wameiomba Halmashauri kuwahamishia kwenye maeneo rafiki kulingana na biashara zao ili kuwaepusha na hasara wanayoweza kuipata.

Wakizungumza wakati wa mkutano na Mbunge wa jimbo Deo Sangaambao umefanyika standi ya zamani mjini Makambako, wamesema halmashauri inatakiwa kuhakikisha wafanyabiashara wanahamishiwa eneo moja ili wasiwapoteze wateja wao.

wafanyabiashara hao wamesema pindi ujenzi wa soko utakapo kamilika wanatakiwa kurejeshwa kwenye maeneo yao badala ya kupewa kipaumbele watu wengine.

Aidha mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara mkoa wa Njombe na Nyanda za juu Kusini Siphael Msigala amewataka wafanyabiashara kuendelea kutoa maoni yao ya wapi wanataka waende ili waendelee kufanya biashara zao pindi soko linajengwa badala ya kuhama Makambako.

Akizungumza katika mkutano huo Mbunge Deo Sanga amesema jimbo lake katika mwaka wa fedha 2024-2025 limetengewa fedha zaidi ya bilioni 12 kwaajili ya kuanza ujenzi wa soko la kisasa na standi ya mabasi na kueleza kuwa utekelezaji wake utaanza mwakani 2024.

Na @cleefmlelwah ✍🏾

#Miaka10YaIceFmRadio_Waleteee
1689225519270.jpg
 
Back
Top Bottom