Kahama VS Njombe/Mafinga

Kahama VS Njombe/Mafinga

Tumefanya Kikao Kizuri kati yetu Viongozi wa Mkoa wa Njombe( RC na RAS) Pamoja na viongozi wa TAZARA na Taasisi ya Wataalamu wabobezi wa usafirishaji - Chaterd Institute of Logistic and Transport( CILT) Tumekubaliana kwa Pamoja kwamba tuwape kazi ya kufanya upembuzi wa mradi wa uanzishwaji na ujenzi wa Bandari ya Nchi Kavu eneo la Makambako-Itakayotoa huduma muhimu za kiuwekezaji ili kuwezesha ufanisi wa usafirishaji kwa bidhaa zinazozalishwa ndani ya mkoa wa Njombe (Chai,Parachichi,Ngano,na bidhaa zote za Mbao) Multfunctional Dry Port with EPZ Flavour(uwepo wa Bandari hii utaisaidia sii tu Njombe bali nchi katika usafirishaji wa baadhi ya mazao ya kilimo,kama chai,Parachichi,nk-ambayo yamekuwa yakitumia zaidi bandari ya Mombasa kuliko Bandari yetu.Eneo hili tutawaalika wawekezaji katika Smart Containers,Timber treatment Plant,na wawekezaji wengine kwa kadri fursa zitakavyotambuliwa,tutaandaa pia eneo maalumu kwa ajili ya ubebaji wa Makaa ya Mawe pale mradi wake utakapokuwa tayari kuanza ili kurahisisha biashara.Naanza kuyaalika Mabenki na Sekta binafsi ya Tanzania na nje ya Tanzania katika fursa hizi.
Pichani ni Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Bi.Judica Omary,Mtendaji Mkuu wa TAZARA Mr.Fuad Abdallah, Viongozi wa CILT-Makamu Mwenyekiti -madame Mtaki,Katibu Mtendaji wa CILT -Mzee Sawaka,Mr.Otieno Igogo Mdau wa Badandari,wadau kutoka Tanzania Shippers Council,Uwakilishi kutoka Shirika la Reli TRC, Mr.Khan mshauri Mwelekezi TAZARA na CILT. Karibuni.
FB_IMG_16811912351126463.jpg
FB_IMG_16763637887038480.jpg
Soma HiYo nime copy na ku pest mzee
FB_IMG_16676312485395943.jpg
 
NJOMBE: MKOA UNAOKUWA KWA KASI ZAIDI KIUCHUMI TANZANIA

Mkoa wa Njombe Unaweza kuuita Duma wa Tanzania, kutokana na Kasi kubwa ya ukuaji unaofananishwa na nchi za Kusini mashariki ya mbali ya Asia kama Malaysia, Singapore na Taiwan.

Mkoa wa Njombe uchumi umekuwa ukikuwa kwa asilimia 63 katika kipindi Cha miaka minne iliyopita. Sekta zinazokuwa kwa Kasi zaidi ni kilimo Cha Asili Cha mkoa huo kinachohusisha mazao makuu kama Chai, Mahindi, Maharage na Viazi kimekuwa kwa asilimia 15. Pia kilimo Cha misitu na biashara ya mazao ya misitu hasa nguzo na mbao ni mhimili wa uchumi wa mkoa na umeajiri watu wengi.

Biashara ndogo ndogo na za Kati (SMEs) zinaongezeka Sana katika miji ya Njombe, Makambako na Halmashauri ya Njombe DC. Kilimo bustani Cha mboga mboga na matunda kimepata mwamko Mpya na kushuhudia ukuaji wa hali ya juu hasa kilimo Cha matunda aina ya Parachichi ambacho kinawaingizia mamilioni wakulima wa Njombe.

Pato la Njombe (GDP) limefikia shilingi trioni 2.66 na Pato la mtu mmoja mmoja ni Tsh. Milioni 3.3 kwa mwaka. Halmashauri zenye wananchi wenye vipato vya juu ni Makambako (7m), Njombe Mjini (5.6m) na Njombe DC (3.2m). Njombe ndio mkoa wenye maskini wachache zaidi, idadi yao ni watu 110,000 tu.

Hata hivyo Kasi ya ukuaji inatarajia Kuongezeka zaidi kutokana na uwekezaji katika kilimo bustani, chuma, umeme wa Maji, Barabara za lami na reli ya kisasa (SGR) kwenda Mtwara.

Mikoa mingine inayokuwa kwa Kasi ni Pwani, Dodoma, Katavi na Mwanza. Pwani imekuwa kitovu Cha viwanda na Utalii pamoja na biashara na ukuaji wa miji. Dodoma, makao makuu yameongeza idadi ya watu, uwekezaji katika makazi, shughuli za kiserikali, mahoteli na burudani. Katavi, imekuwa kitovu kipya Cha Utalii na biashara katika ukanda wa Ziwa Tanganyika. Ukaribu wake na nchi za DRC na Zambia zimeongeza fursa ya kibiashara. Mwanza inarudi kuwa kitovu Cha biashara katika eneo la maziwa makuu. Pamoja na mambo mengine imechochewa na uwekezaji katika miundombinu hasa uwanja wa ndege, ujenzi wa meli Mpya na ujenzi wa reli ya kisasa, ukuaji wa idadi ya watu na uwekezaji katika viwanda na mahoteli ambapo Pato la mkoa wa Mwanza limefikia takribani trioni 11 kutoka trioni 2.5 miaka michache iliyopita.
FB_IMG_16788596363224305.jpg
 
Serikali ina mpango wa kupima na kuwamilikisha ardhi bure kwa wananchi 1000 kutoka mtaa wa Kikula, uliopo kata ya #Makambako na Mtaa wa Sekondari kata ya Maguvani katika halmashauri ya mji wa Makambako mkoani #Njombe

Afisa mipango miji kutoka ofisi ya Rais #Ikulu, Henry Mathias Tarimo amesema zoezi hilo litaendeshwa chini ya Mpango wa urasimishaji wa rasilimali,biashara na watu wanyonge #Tanzania (#MKURABITA).

Tarimo amesema katika mpango huo wananchi wa mitaa hiyo watatakiwa kuchangia #fedha kwa ajili ya kupata hati miliki ya maeneo yao pekee huku gharama zote za upimaji zikigharamiwa na MKURABITA ili kuwawezesha kiuchumi.

Claudia Daniel Kipapi ni Afisa ardhi mteule halmashauri ya mji wa Makambako amesema zoezi hilo limeanza tangu mwanzoni mwa mwezi mei na linategemewa kufanyika kwa muda wa miezi miwili.
#kingsfmradio #jisikiemfalme #landownership #land #governmentsupports landdisputes
FB_IMG_16780706519420939.jpg
 
MTAKA AHIMIZA FURSA ZAIDI ZA UWEKEZAJI MAKAMBAKO KUPITIA TAZARA
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mh. Anthon Mtaka amehimiza uwekezaji zaidi Mkoani Njombe kwa kuwa Mkoa huo una fursa nyingi za kilimo na biashara.

Mtaka aliyasema hayo wakati wa mazungumzo na Meneja Mkuu wa TAZARA Tanzania Bw. Fuad Abdallah alipotembelea ofisi za mamlaka zilizopo Dar es Salaam mapema wiki hii akielezea namna ambavyo reli ya TAZARA ilivyo na fursa nyingi zinazoweza kusaidia katika kuvutia uwekezaji nchini kupitia Makambako.

Alizitaja fursa nyingi za kilimo na biashara zilizopo Mkoani Njombe kuwa ni pamoja na uzalishaji wa Mbao, Kilimo cha Chai, Parachichi, Ngano , Viazi na Mahindi.

Naye Bw. Fuad Abdallah alisema kuwa Mji wa Makambako ni eneo muhimu kwa shughuli usafirishaji kwa kuwa Makambako inaunganishwa na reli ya TAZARA inayosafirisha mizigo mbalimbali kuelekea kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi kupitia bandari ya Dar es Salaam ambayo ni lango muhimu la biashara nchini.


Kwa sasa Njombe ina fursa nyingi za kibiashara
FB_IMG_16811912351126463.jpg
FB_IMG_16811912351126463.jpg
 
TANGAZO,, naomba watu wote wa lake zone tustmie Jiji la mwanza kushindanisha na mbeya ni kjizalilisha sana na kuzalilisha hadhi ya Jiji la MWANZA,

Mwanza ni second city after Dar,hivo heshima wakuu naomba tutumie mikoa kama kagera,shy,simiyu,mara,na Geita kushindanisha na kusini ila tustumie mwanza kabisa.

Asanteni sana
 
TANGAZO,, naomba watu wote wa lake zone tustmie Jiji la mwanza kushindanisha na mbeya ni kjizalilisha sana na kuzalilisha hadhi ya Jiji la MWANZA,

Mwanza ni second city after Dar,hivo heshima wakuu naomba tutumie mikoa kama kagera,shy,simiyu,mara,na Geita kushindanisha na kusini ila tustumie mwanza kabisa.

Asanteni sana
Tulishaacha muda sana kamanda.
 
Back
Top Bottom