NJOMBE: MKOA UNAOKUWA KWA KASI ZAIDI KIUCHUMI TANZANIA
Mkoa wa Njombe Unaweza kuuita Duma wa Tanzania, kutokana na Kasi kubwa ya ukuaji unaofananishwa na nchi za Kusini mashariki ya mbali ya Asia kama Malaysia, Singapore na Taiwan.
Mkoa wa Njombe uchumi umekuwa ukikuwa kwa asilimia 63 katika kipindi Cha miaka minne iliyopita. Sekta zinazokuwa kwa Kasi zaidi ni kilimo Cha Asili Cha mkoa huo kinachohusisha mazao makuu kama Chai, Mahindi, Maharage na Viazi kimekuwa kwa asilimia 15. Pia kilimo Cha misitu na biashara ya mazao ya misitu hasa nguzo na mbao ni mhimili wa uchumi wa mkoa na umeajiri watu wengi.
Biashara ndogo ndogo na za Kati (SMEs) zinaongezeka Sana katika miji ya Njombe, Makambako na Halmashauri ya Njombe DC. Kilimo bustani Cha mboga mboga na matunda kimepata mwamko Mpya na kushuhudia ukuaji wa hali ya juu hasa kilimo Cha matunda aina ya Parachichi ambacho kinawaingizia mamilioni wakulima wa Njombe.
Pato la Njombe (GDP) limefikia shilingi trioni 2.66 na Pato la mtu mmoja mmoja ni Tsh. Milioni 3.3 kwa mwaka. Halmashauri zenye wananchi wenye vipato vya juu ni Makambako (7m), Njombe Mjini (5.6m) na Njombe DC (3.2m). Njombe ndio mkoa wenye maskini wachache zaidi, idadi yao ni watu 110,000 tu.
Hata hivyo Kasi ya ukuaji inatarajia Kuongezeka zaidi kutokana na uwekezaji katika kilimo bustani, chuma, umeme wa Maji, Barabara za lami na reli ya kisasa (SGR) kwenda Mtwara.
Mikoa mingine inayokuwa kwa Kasi ni Pwani, Dodoma, Katavi na Mwanza. Pwani imekuwa kitovu Cha viwanda na Utalii pamoja na biashara na ukuaji wa miji. Dodoma, makao makuu yameongeza idadi ya watu, uwekezaji katika makazi, shughuli za kiserikali, mahoteli na burudani. Katavi, imekuwa kitovu kipya Cha Utalii na biashara katika ukanda wa Ziwa Tanganyika. Ukaribu wake na nchi za DRC na Zambia zimeongeza fursa ya kibiashara. Mwanza inarudi kuwa kitovu Cha biashara katika eneo la maziwa makuu. Pamoja na mambo mengine imechochewa na uwekezaji katika miundombinu hasa uwanja wa ndege, ujenzi wa meli Mpya na ujenzi wa reli ya kisasa, ukuaji wa idadi ya watu na uwekezaji katika viwanda na mahoteli ambapo Pato la mkoa wa Mwanza limefikia takribani trioni 11 kutoka trioni 2.5 miaka michache iliyopita.