Mapank
JF-Expert Member
- Mar 8, 2011
- 4,157
- 6,163
Sijajua Mkuu, Ila bado Ngara itanufaika tu, Kahama watafaidika na shughuli za plant, na kuongeza malori mjiniDah kwa hiyo mapato ya Ngara kagera...yanaenda kuhesabiwa kahama shinyanga?...
Halafu wakitoa takwimu za mikoa yenye GDP kubwa kagera inakuwa haimo..na mkoa unaonekana maskini..
Kwa nini hizo processing plant zisijengwe huko huko ngara?...
Hii kitu ilifanyika kwenye kahawa miaka mingi tu...soko na mnada wake unakuwa moshi na mapato kuhesabiwa huko Kilimanjaro wakati wakulima wako kagera...
Pia kwenye sukari ya kagera...mapato na tathmini yake inahesabiwa Dar huko...ndo maana bei ya sukari bado iko juu hata maeneo ya karibu na viwanda...