Safari hizo mie huwa nafanya sana, kwa kweli kusini bado sana, kwanza wakisikia umetoka kanda ya ziwa wanakushangaa wanaona unafaiiidi! Wanakuuliza habari za akina brother K waigizaji wa Futuhi, habari za watangazaji wa RFA, Star Tv na kiss FM kama nimewaacha wazima


afu nikirudi nikawasalimie, Last time nilisafiri Makambako to Mwanza nilikuwa nimekaa na Mama mmoja wa Mbeya akawa anasema 'huku kwenu ni pazuri sana, tulikuwa tunapaona kwenye TV kwenye msiba wa Magufuli', nami nikamuambia sasa unajionea live enjoy yourself na kesho yake nikamtembeza maeneo ya Rocky City.