Mwalo Chibya
JF-Expert Member
- Dec 18, 2019
- 1,350
- 1,005
Shida ya mkoa wa Shinyanga ni moja ,wilaya zilizoendelea vizuri ni mbili tu yaani Shinyanga Manispaa na Kahama Manispaa wilaya zilizobaki zipo nyuma sanaGeita inaizidi Hadi Shy Sasa unashangaa nini?
Uzuri wa Mkoa wa Geita una wilaya tano zimepiga hatua kimaendeleo ya watu na zina fursa nzuri kwa mtu anayetafuta maisha, ( mbogwe, bukombe, Geita DC, Chato na Geita MC). Kwenye haya maeneo kuna pesa
Mkoa wa Mwanza huwa naona unashikiliwa na wilaya tatu tu, Mwanza jiji, Ilemela na Sengerema ndio sehemu zenye fursa nyingi za kiuchumi, kwa wilaya kama Misungwi, ukerewe, Kwimba na magu huwa naona ni setbacks kwa mkoa wa Mwanza ndio zenye maskini wengi na fursa chache na huwa zinachangia sana negatively kwenye data za uchumi kwa mkoa wa Mwanza
Ukiniambia nichague mkoa wa kutaftia pesa kanda ya ziwa chaguo langu kwa sasa litakuwa Geita, Na Geita inapokea wahamiaji wengi sana wanaofata fursa za pesa na kama itabaki hivi mpaka census ijayo Mkoa wa Geita unaweza kuongoza kwa population kwa kanda ya ziwa