HUO NI USHAMBA WAKO HAYA SOMA HAPO VIWANDA VYA MITI VINAVOZIDI KUONGEZEKA NDANI YA MKOA WA NJOMBE NA VINGI NI AROUND MAKAMBAKO👇👇👇👇
Katibu tawala wa mkoa wa Njombe Judica Omary amesema sekta ya misitu inategemewa mkoani Njombe jambo ambalo limepelekea wawekezaji wengi kuingia kwenye sekta hiyo na kujenga viwanda huku baadhi yao wakifuata sera za uwekezaji na wengine wakionekana kufanya kazi kinyume na utaratibu.
"Hivi viwanda vimeanza kuja kidogokidogo na mpaka sasa hivi vimefikia viwanda 19 vinavyojihusisha na mazao ya Venia na hivi vyote vipo wilaya ya Njombe sasa hivi na kwa ujumla vimeajiri watumishi wa muda 1878"amesema Judica Omary
Baadhi ya wadau walioshiriki kikao hicho akiwemo Meneja wa TRA mkoa wa Njombe Specioza Oule pamoja Daniel Okoka ambaye ni MNEC kutoka mkoa wa Njombe,wametoa wito kwa wawekezaji kuhakikisha wanafuata mikataba ya kikodi pamoja na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii kwenye maeneo yao ya uwekezaji ili kuimarisha uchumi.
#IceFmHabari
#NisikilizeMimi
Na @cleefmlelwah
View: https://www.instagram.com/reel/DJ6cYhttrL0/?igsh=MWN6amRnaHRycWI3bA==