Kagonga boda, kakimbia kisha kadakwa

Kagonga boda, kakimbia kisha kadakwa

Hapo wengi wanaongozwa na hasira za maisha na siyo kwa sababu ya ajali iliyotokea. Vijana wengi wenye maisha ya kuunga-unga wamejawa na chuki kwa wenye afadhali ya maisha. Nchi yenye vijana wengi wasio na ajira kama Tanzania, huwa inakuwa kama petrol inayosubiri moto.

Sahihi Kabisa.
Wanakutafutia sababu ya kukutia hasara hiyo ndio furaha yao
 
Hata angesimama ingekuwa hivyo hivyo bodaboda huwa akili hawana

USSR
Angalau wewe umeona. Kuna hasira sana na chanzo ni unemployment ya wale wanaomaliza vyuo wakitegemea kazi ila hawazipati. Hata 29/10 ilikuwa hivi hivi.

Hii inatokana na ukweli kuwa Watanzania (Wazazi na Watoto wao) kug'ang'ani dhana potofu kuwa ajira ipo Serikalini.

Pili wale walioajiriwa Serikalini wanaonesha mfano mbaya wa ufisadi, hiyo nayo ni pulling factor etc

Mtu akijiajiri, bado anaona yupo unemployed (bado yupo kijiweni akisaka ajira za Serikalini). Ila la kushangaza akina Prof Mkumbo badala ya kushughulikia masuala haya, wapo kuhangaika na Chadema with Cheap politics - atu utawala hauonjwi kama uji!!!!!
Na mbaya zaidi huwa wana imani potofu kwamba kila mwenye gari ni mtumishi wa kwenye mfumo hawajui kuwa kuna wengine wanapambana kivyao tu hadi wanatoboa.
Inapotokea ajali akili yako inavurugwa na inakuwa ngumu sana kupata maamuzi sahihi maana linakuwa ni jambo la haraka either ubaki au ukimbie kabla watu hawajaitana.
Kama umegonga mpita njia au mwrndesha bodaboda inatakiwa akili itulie sana kufanya maamuzi na kabla ya kufanya maamuzi angalia kwanza hali halisi ya huyo uliyemgonga kama amepata majeraha lakini hajafa mbebe umpakie kwenye gari yako chap na umuwahishe hospital ukishamfikisha hospital ili aanze tiba hapo kidogo hasira zao zitapungua watakuona muungwana.
Lakini kama huyo mtu uliyemgonga ameshakufa hapo hauna kitu cha kuwashawishi ili wakuelewe ndio maana huyo jamaa akajaribu kukimbia ili kujinusuru,hata angebaki isingesaidia kitu
 
Wamemkuta jamaa hana chuma cha mzungu wangemwagwa watu ubongo hapo mbaya sana hii
Mmmh kuna mdosi ilimkuta hiyo man akatoa kweli chuma tena yeye aligonga watatu na alikuwa #Mike alichofanyiwa acha kabisa kimsingi sijui wapi tunaelekea. Angalia hapo kuna mama baada ya kuona kioo kimeshushwa tu bila woga yeye mwenyewe alirudi nyuma akajua watu wapo serious.
 
Hii nchi kuna tatizo watu wana hasira sana, dispute kama hii inaweza kuwa solved bila violence… Nyie tusijifanye hatuoni, kuna tatizo kubwa sana.

Ni kama nchi imetoboka.
Hamna cha nchi kutoboka hapo, ni wivu tu na roho mbaya. Bodaboda wao wanavyoendesha kwa fujo utafikiri wanamiliki barabara.
Kuna wengine huwa sijui wanaenda kuoa wale n.k wanakua kama 100 na zaidi, ni fujo, kelele, wanapiga magari etc.
Wengi wao wajinga na bangi tu
 
Hapo wengi wanaongozwa na hasira za maisha na siyo kwa sababu ya ajali iliyotokea. Vijana wengi wenye maisha ya kuunga-unga wamejawa na chuki kwa wenye afadhali ya maisha. Nchi yenye vijana wengi wasio na ajira kama Tanzania, huwa inakuwa kama petrol inayosubiri moto.
Absolutely, hii kitu ipo sana kwenye jamii zetu, mtu akifanikiwa tayari watu wanaanza kumuona kama mtu anayejisikia. Unakuta badala ya kufanya juhudi ufanikiwe unakuwa unatamani mtu aliyepiga step aanguke. Hii ndo roho ya kimasikini, ukichanganya na hasira za ugumu wa maisha 🤣🤣🤣 hata mtu akikuta mbwa barabara anampiga mawe
 
Mjinga wewe hasara zaidi ya roho?
Kwa uendeshaji wa hao bodaboda utakuta huyo marehemu ndiye kajitakia kifo mwenyewe , nimeandika kwa kuzingatia matukio mengi ya aina hii, uzoefu binafsi na matukio ya kila siku nionayo barabarani. Japo siwezi hukumu moja kwa moja kuhusu hili tukio pengine mwenye gari alikuwa na makosa.
 
Was*nge sana,mwenyewe nimekutana na kisanga kama hiki ila mwenye pikipiki wala hakuumia na wala hakudondoka aliyumba tu.

Sikuona sababu ya kusimama palepale kutengeneza foleni, wakadhani nakimbia,wakablock barabara na miluzi kibao.

Mhusika hakuwa boda ni pikipiki binafsi hlf wa kishua siyo njaa njaa,tukaelewana bila hata mie kushuka.

Mabodaboda walikuwa tayari wanavuta milango nishuke,hawakuamini jamaa alipoamua kupotezea na kuondoka bila kuhitaji hata mia.

Ni mwezi huuhuu wa 8.
Wanafanya hivyo nia yao kuiba, hapo wana search kwenye gari wanaiba kila kitu kama ni laptop, simu, fedha n.k.. boda vibaka ndio hupenda sana kufanya hizo vurugu..
 
Angalau wewe umeona. Kuna hasira sana na chanzo ni unemployment ya wale wanaomaliza vyuo wakitegemea kazi ila hawazipati. Hata 29/10 ilikuwa hivi hivi.

Hii inatokana na ukweli kuwa Watanzania (Wazazi na Watoto wao) kug'ang'ani dhana potofu kuwa ajira ipo Serikalini.

Pili wale walioajiriwa Serikalini wanaonesha mfano mbaya wa ufisadi, hiyo nayo ni pulling factor etc

Mtu akijiajiri, bado anaona yupo unemployed (bado yupo kijiweni akisaka ajira za Serikalini). Ila la kushangaza akina Prof Mkumbo badala ya kushughulikia masuala haya, wapo kuhangaika na Chadema with Cheap politics - atu utawala hauonjwi kama uji!!!!!
Hii ni mbaya mkuu!

Tunayetakuwa kumuonea na kummalizia hasira zetu hatumuwezi ndio maana tunamaliziana hasira wenyewe kwa wenyewe.

In a bigger picture, hali si nzuri… basi tu hata serikali yenyewe inapambana kubaki madarakani, watu sio vipaumbele vyao.
 
Back
Top Bottom