Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Manji kanywa sumu?
• Uvumi wamhusisha na hofu ya mahakamani

na Mwandishi wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


HALI ya afya ya mfanyabiashara maarufu nchini anayemiliki Kampuni ya Quality Group ni mbaya kiasi kwamba imewalazimu madaktari waliokuwa wakimtibu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam, kulazimika kumkimbiza Nairobi nchini Kenya kwa matibabu.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka vyanzo vya kuaminika, kwa watu walio karibu na mfanyabiashara huyo na katika Hospitali ya Aga Khan, zinaeleza kwamba, Manji alianza kuugua juzi usiku.

Kwa mujibu wa habari hizo, hali ya Manji ambaye ni mfadhili mkuu wa klabu ya soka ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, ilianza kwa kutapika mfululizo, jambo ambalo lilisababisha wanafamilia na jamaa zake walazimike kumkimbiza katika Hospitali ya Aga Khan wakihofia kwamba huenda alikuwa amekula chakula au kinywaji chenye sumu.

Mtoa habari mmoja aliyezungumza na gazeti hili alisema kwamba, mara baada ya kufikishwa katika hospitali hiyo, usiku wa kuamkia juzi alipelekwa moja kwa moja katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) akiwa katika hali iliyoonyesha kutojitambua.

Jamaa waliompeleka hospitalini hapo waliwaeleza madaktari walioanza kumhudumia kuwa, Manji alianza kutapika mfululizo baada ya kunywa kiasi kikubwa cha kinywaji anachokipenda.

Kwa mujibu wa habari hizo, madaktari waliompima, waligundua kuwa wakati akitapika, kiasi cha mapishi yake kilirudi tumboni na kingine kikaingia mapafuni, hali ambayo ilianza kutishia maisha yake.

Vyanzo vingine vya habari kutoka hospitalini hapo, vililieleza gazeti hili kuwa, madaktari walishangazwa na matapishi ya Manji na kwamba waliamua kuchukua kiasi kwa ajili ya uchunguzi zaidi kabla hawajafikia uamuzi wa kumpeleka Hospitali ya Aga Khan ya Nairobi, nchini Kenya.

Hali hiyo ilisababisha aondolewe hospitalini hapo majira ya saa 12:00 asubuhi jana na kusafirishwa kwa ndege ya kukodi kwenda Nairobi akisindikizwa na ndugu zake wachache.

Vyanzo hivyo vilieleza kuwa akiwa anaanza kupata fahamu, ndugu zake walimwambia wanamhamishia Nairobi kwa matibabu zaidi, Manji alikataa akitaka kuendelea kubaki hospitalini hapo au kurudishwa nyumbani kwake, ndipo madaktari walipotumia akili ya ziada ya kumchoma sindano ya usingizi ili iwe rahisi kufanikisha zoezi la kumhamishia nchini Kenya.

Kabla ya gazeti hili kupata habari hizo jana asubuhi, uvumi ulisambaa sehemu mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam ukihusisha ugonjwa huo wa Manji na matukio ya siku za hivi karibuni ya kufikishwa mahakamani kwa baadhi ya vigogo wakihusishwa na matumizi mabaya ya madaraka.

“Hali ya sasa ni tete bwana, sisi tunasikia jamaa ameingia hofu kiasi cha kuamua kunywa sumu,” alisema mtoa habari mmoja aliyepiga simu katika chumba cha habari cha Tanzania Daima.

Hata hivyo taarifa hizi zilikanushwa vikali na mmoja wa wanasheria wanaofanya kazi na Manji ambaye aliuelezea ugonjwa wake kuwa ni wa kawaida na uliotokana na hitilafu za kitabibu mwilini.

Msaidizi huyo wa Manji ambaye alikiri kusikia maneno mengi kuhusu kuugua kwa bosi wake, alikanusha katakata kuwapo kwa jambo lolote linalomhusisha mfanyabiashara huyo na matukio ya hivi karibuni ya vita dhidi ya ufisadi.

Hii ni mara ya pili katika kipindi kisichozidi mwezi mmoja kwa Manji kuugua na kulazwa katika Hospitali ya Aga Khan na baadaye kupelekwa Nairobi kwa matibabu zaidi.
 
If what is said above is true, i believe this is a good starting point to begin dealing with unscrupulous lawyers who " facilitate" criminal activities such as this ufisadi business. It has become fashionable for lawyers not to mind about ethics in legal practice.They should know that they are not above the law.They are supposed to be amicus curiae and facilitators in compliance with the law!The exhorbitant fees that they charge and collect is not for helping law breakers!

Jamii iwamulike na wao wasifikiri ni untouchables! tuwapembue na wao tujue pumba na mchele! Uwezo wa kusaidia wahalifu kuvunja sheria siyo kigezo cha kuwa mwanasheria mzuri.Ni sawasawa na daktari anayesaidia kuongeza maradhi - kumpa muuaji sumu inayoweza kuua polepole, kutengeneza vimelea vinavyoweza kuleta madhara nakadhalika.Hao wote watahesabiwa ni wauaji japo mmoja ni daktari! samahani kama nitakuwa nimegusa pahala pabaya..ila yote ni katika kurekebishana tu. No offence intended!
 
I can smell fish kwenye hii issue ya Manji kupelekwa Nairobi then tutasikia kenda UK kama sio USA na mwisho kafa. Mazishi tusishangae yakawa India au nje ya bongo tena kwa kuchoma na hakuna watu kuhudhuria isipokuwa wale wa karibu tu kama kwa Balali. Mwenye macho haambiwi .............!!!
 
KAGODA: A tough investigation ahead

-Growing fears of deep cover-up linked to political, financial clout

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam


WITH a fresh probe already underway into Kagoda Agriculture Limited, investigators are facing an increasingly arduous task in getting to the bottom of the truth behind the dubious company that siphoned more than 40bn/- from the Bank of Tanzania’s external payment arrears (EPA) account, it has been revealed.
Influential people linked to the shell company have so far managed to stifle any meaningful investigation into the firm, thanks to what is described as an intricate web of financial power and political clout.

Although there is overwhelming evidence of conspiracy, fraud and theft by Kagoda, which was first exposed by international auditors from Delloite & Touche and later confirmed via a special audit of the EPA account conducted by Ernst & Young, authorities are yet to file any criminal charges against the company’s promoters.

Well-placed sources say some well-connected members of the local business community, who were the real beneficiaries of the Kagoda funds, have so far managed to deploy their vast network of influence within the government to block the case from going to trial.

So far, prosecutors have filed criminal charges against a total of 20 suspects linked to the EPA embezzlement scandal, including high-profile businessmen Jeetu Patel and Johnson Lukaza.

However, the Kagoda case remains conspicuously missing from the ongoing EPA trials, despite the fact that the company was the single biggest recipient of the loot.

The web of influence wielded by the Kagoda tycoons is believed to have frustrated previous investigations by the EPA scandal probe team led by Attorney General Johnson Mwanyika.

It is understood that evidence gathered by the Mwanyika team failed to convince the Director of Public Prosecutions (DPP), Eliezer Feleshi, to give consent for prosecution of the Kagoda case.

As the new investigation into Kagoda begins, detectives are now expected to turn their attention to an industrial area on the outskirts of Dar es Salaam where the firm’s registered office premises was listed.

According to official government records, Kagoda named its registered office as Plot Number 87 in Kipawa industrial area, Temeke district, Dar es Salaam.

But there is a distinct possibility that this listed office location could be fictitious, much like everything else with this shell company.

Previous attempts by THISDAY to make a physical visit to Kagoda’s listed offices hit a stonewall, as Plot No. 87 could not be physically located nor pinpointed on a map.

One interesting lead that investigators are also in line to follow is the residential address of the company’s listed shareholders - John Kyomuhendo and Francis William.

Records at the Business Registration and Licensing Authority (BRELA) show that both Kyomuhendo and Francis William are residents of Kinondoni in Dar es Salaam.

Kyomuhendo, whose name appears in most of Kagoda’s documents, is said to reside in the Kinondoni Hananasif area, at a house located on plot number 51.

On the other hand, William’s residential address is listed as house/plot number 311313 in the same Kinondoni area.

Sources familiar with the EPA probe say most of the key evidence lies at CRDB Bank Plc, which was used by Kagoda to receive the embezzled funds.

Investigations by THISDAY have already established that Kagoda used a string of bank accounts from various CRDB bank branches in Dar es Salaam to receive payment of the Kagoda funds.

’’The big bosses at CRDB know exactly who withdrew the funds from the Kagoda bank accounts,’’ said another well-placed source.

’’Although banks are required to observe a confidentiality clause with their clients, they are supposed to give full disclosure to the police during criminal investigations,’’ the source added.

Insiders say Kyomuhendo submitted to CRDB Bank a legal document stating that he had transferred power of attorney to a certain individual, giving him (the individual) full authority over the company’s bank accounts.

’’There should be clear and unequivocal records at CRDB Bank showing exactly who withdrew the 40bn/- from Kagoda’s bank accounts. I can assure you neither John Kyomuhendo nor Francis William had access to the money once it was deposited by the BoT in Kagoda’s bank accounts,’’ said a source in the financial sector.

After a long holiday lull, public attention is expected to shift back to the Kisutu Resident Magistrate’s Court in Dar es Salaam from today to watch out for the next move in the EPA trials saga and other cases linked to the anti-grand corruption crusade.
 
Aaaaaaaaaaaaa basi,
Kila tugeuka Kagoda, lakini eti haijulikani ipo wapi, ya nani nk.
Tunaliwa jamani
 
Suala hili la KAGODA kinara wake ni Rostam Aziz ambaye amemtumia Yusuph Manji kurudisha fedha kama ni kweli.Namsihi Rais wetu JK asiogope matokeo hata kama fedha hizo zilitumika kwenye kampeni iliyomuingiza madarakani dawa ni kuwashughulikia wezi hao kwani ukikaribishwa chakula halafu baadaye ukagundua ni cha wizi wewe si mwizi kama utasema ukweli ila ukificha ukweli utakuwa mmoja wa wezi hao.Nchi hii imedidimizwa na inaendelea kudidimizwa na wizi wa aina hii.Kama kiongozi huwezi kusema unafufua uchumi wa Nchi bila kutatua tatizo la wizi wa aina hii.Wezi wote wakamatwe na fedha za hazina ya zirudishwe kwa maendeleo ya wote.Wote wanaohusika na sakata za aina hii wasiruhusiwe kuwa viongozi tena katika Nchi yetu kwani kuna watu wengi waadilifu wanaoweza kuongoza.Wananchi waamuae namna wanavyotaka Nchi yao iongozwe.Wana JF tuendelee kuwaelimisha Watanzania wawe na moyo wa kukomboa Nchi yao kutoka kwenye mikono ya mafia/mafisadi/wakoloni weusi.
 
Kagoda kikaangoni
• Sasa kuhamia bungeni, hotuba ya JK ikijadiliwa

na Salehe Mohamed
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


SAKATA la Kampuni ya Kagoda Agriculture iliyoiba sh bilioni 40 katika Akaunti ya Malipo ya madeni ya Nje (EPA), limechukua sura mpya, baada ya kuwapo kwa taarifa za wanaotajwa kuwa wamiliki wake kuanza kuuza mali zao kwa kile kinachosemekana kutapatapa au kutaka kujificha ili wasikumbane na mkono wa sheria.

Kuhaha kwa wanaotajwa kumiliki Kampuni ya Kagoda kunatokana na kuwapo kwa shinikizo kubwa kutoka kwa wananchi wanaotaka kujua ni nani hasa anamiliki kampuni hiyo, licha ya kuwapo kwa taarifa zisizo rasmi kuwa kuna wamiliki wamepandikizwa ili kuwalinda wamiliki halali ambao inadaiwa ni wafanyabiashara na wanasiasa waliojijengea heshima hapa nchini.

Kwa mujibu wa Chanzo cha habari cha Tanzania Daima Jumapili, hivi sasa sakata hilo linaonekana kuwakera zaidi wamiliki hao ambao hapo awali walikuwa hawajui chochote kuhusu fedha za EPA mpaka pale walipotaarifiwa na kupewa mikakati ya kuiba fedha hizo na wanasiasa wakongwe hapa nchini katika utawala wa Awamu ya Tatu ili ziwasaidie katika mipango yao ya kuusaka uongozi.

Kuna taarifa mmoja wa wamiliki wa Kagoda hivi karibuni alianza kuuza mali zake na kutoa muda maalum kwa watu wanaomdai kwenda katika ofisi zake ili aweze kuwalipa katika hali ambayo ilitafsiriwa na baadhi ya watu kuwa ni kutaka kukimbia mikono ya sheria lakini watu wa usalama katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakichunguza nyendo zake kila kukicha.

Wakati mfanyabiashara huyo akiweweseka kwa kuuza mali zake, mwingine ameanza kuwakaripia na kutoa vitisho kwa baadhi ya watu wenye taarifa za kuhusika kwake na umiliki wa Kagoda ambayo bado haijafikishwa mahakamani licha ya wamiliki wa kampuni nyingine kuburuzwa mahakamani kwa kuiba fedha za EPA.

Mfanyabiashara huyo ambaye pia yupo katika medani za siasa hapa nchini inasemekana ameshaanza kutumia fedha zake kuwapandikiza watu katika sekta mbalimbali nyeti kuwashughulikia viongozi na baadhi ya wafanyabiashara wanaoonekana kulichachamalia suala la Kagoda.

Pamoja na wafanyabiashara hao kila mtu kuhangaika kwa namna yake kupunguza kasi ya kelele za Kagoda, imebainika kuwa hivi sasa kuna kutoelewana kwa kiasi kikubwa baina ya waliotoa mpango wa wizi huo na wafanyabiashara hao kiasi cha kutishiana maisha.

Wafanyabiashara hao wakati sakata la EPA linaanza waliweka wazi kuwa hawatakubali kwenda na maji wakati wao si watu waliopanga wizi huo na pia hawakutumia kiasi hicho cha fedha walichokichota kwa matumizi yao bali waliwasilisha sehemu ya walichokichota kwa wahusika.

Kutokutajwa mpaka hivi sasa kwa wamiliki wa Kagoda na kutofikishwa mahakamani kunaaminika kunatotokana na kuficha siri nzito ambayo kama itawekwa bayana kuna wanasiasa na wafanyabiashara wanaoheshima hapa nchini wataadhirika.

Miongoni mwa mambo yanayozua maswali mengi yasiyo na majibu hivi sasa ni kwa nini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ametumia muda mwingi kuwafikisha mahakamani wamiliki wa Kagoda ilhali wamiliki wa kampuni nyingine walifikishwa mahakamani katika kipindi kifupi baada ya DPP kupata majalada ya EPA kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Wakati hayo yakiendelea kuna baadhi ya wabunge wamedhamiria kuiumbua Kagoda na wanasiasa wenzao bungeni pindi hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa Agosti 21 mwaka huu itakapojadiliwa baada ya kupigwa danadana kwa muda mrefu sasa.

Wabunge hao ambao wameweka bayana kuwa hawaridhishwi na matendo ya baadhi ya wanasiasa wenzao waliopo madarakani na waliomaliza vipindi vyao kwa kutumia vibaya rasilimali za taifa kwa maslahi binafsi.

Wamebainisha kama kuwajibisha kusipoanzia kwa viongozi katu nchi haiwezi kupiga hatua katika mapambano dhidi ya rushwa ambayo kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo inavyoongezeka huku baadhi ya wakionekana kufanya mambo kwa mazoea kuwa wapo katika uongozi.

Wamesema endapo hotuba hiyo ya rais itajadiliwa ndiyo itakuwa changamoto kubwa ya kuwawajibisha mafisadi wote bila kujali mtikisiko utakaotokea ndani ya bunge na taifa kwa ujumla.

“Tabia ya kutishana kuwa Kagoda ni hatari kwa taifa na haipaswi kuguswa imeshapitwa na wakati na kama suala hili litatinga bungeni tutawaumbua wanaohusika kwani tunawajua na mbinu walizozitumia tunazijua,” alisema mbunge mmoja ambaye ni machachari.

Naye Spika wa Bunge, Samuel Sitta, alisema hakuna kitu kitakachoshindikana katika kuijadili hotuba hiyo ya rais na wala hakuna tatizo lolote la kisheria litakalowazuia wabunge kujadili masuala ya EPA, hivyo wasitishike na maneno ya kuwa hawaruhusiwi kujadili kipengele hicho.

Alisema wabunge wanaijadili hotuba nzima ya rais si kipengele kimoja na hata hicho kipengele cha EPA hakimgusi mtu mmoja bali kinazungumzia jambo kwa upana wake kama lilivyozungumziwa na Rais Kikwete.

“Pale tunazungumzia EPA kwa upana siyo fulani kafanya nini au kamshirikisha nani, hili lipo wazi sheria haiwezi kuwabana wabunge wasiijadili hotuba ile,” alisema Sitta.

Alisema mtu yeyote anayeivalia njuga EPA isijadiliwe au kueneza maneno yasiyo sahihi atakuwa hatendi haki kwani kinachojadiliwa bungeni ni hotuba nzima na kila mbunge atakuwa na uamuzi wa kuangalia nini cha kuzungumzia.
 
How BoT failed to probe Kagoda fraud

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam


INTERNAL documents from the Bank of Tanzania show that senior central bank officials failed to institute an investigation against Kagoda Agriculture Limited in 2005 even after the company produced clearly-forged documents to loot billions of shillings from the notorious external payment arrears (EPA) account.

According to latest THISDAY findings, the forged Kagoda documents presented to the BoT included two deeds of assignment that quoted the currency of some old debts owed to German companies dating back to before 1999 in euros instead of deutsche marks.

Germany adopted the euro on January 1, 1999, and was using its own national currency (deutsche marks) before the single European currency was introduced on that date.

The Kagoda forgers used two deeds of assignment signed on October 18, 2005 relating to two German companies - Lindeteves J Export BV and Hoechst - that quoted a total amount of 1,164,402.76 euros.

Although BoT officials correctly established that the quoted currency was false, instead of following up by ordering a probe into Kagoda, the central bank actually helped the dubious company to correct the error so it could benefit from the EPA account funds.

Official BoT documents show that central bank officials wrote to Kagoda Agriculture Limited advising them to correct the currency from euros to deutsche marks.

And incredibly, just two days after being informed by BoT officials that they had used the wrong currency, the Kagoda forgers managed to come up with new deeds of assignment purportedly signed by the German creditor companies in deutsche marks instead of euros.

Investigations by THISDAY have revealed that senior BoT officials, including the then governor Dr Daudi Ballali (now deceased), approved the payments to Kagoda after aiding the company to re-submit the documents in the proper currency.

In 2006, the bank’s then auditors Deloitte & Touche raised audit queries on why a total of 8,196,673,600.53/- had been released to Kagoda even after the currency mix-up had been uncovered.

’’We find it highly unusual and doubtful that a foreign creditor assigning such significant amounts of money would sign off for the wrong currency,’’ said the international auditing company in its audit query to Ballali.

It added: ’’It is also striking that the foreign creditors’ directors allegedly were either still in the country or returned to Tanzania within two days to sign the revised guarantees.’’

Deloitte & Touche advised the BoT to institute a formal investigation into Kagoda and also carry out a search of immigration records to establish whether or not officials of the German creditor companies had really been in the country.

But instead of heeding this advice, Ballali opted to sack Deloitte & Touche as the BoT auditors and proceeded with the highly-dubious payments to Kagoda.

It has been established that a number of officials at different levels within the BoT hierarchy were involved in approving and processing payments amounting to 40bn/- to the Kagoda company.

It is furthermore understood that the involvement of key central bank officials in the fraudulent payments to Kagoda towards the end of 2005 ascended to the top leadership under the then governor, Ballali.

Internal BoT memos show that one of the accused persons in the ongoing EPA embezzlement trials, Imani Mwakosya, was the head of bilateral and commercial debt (BCD) at the BoT during the 133bn/- EPA looting scandal in 2005/06, and personally handled all payments made to Kagoda.

Sources close to the EPA scandal investigation say Mwakosya could turn out to be a ’’star prosecution witness’’ if the government finally decides to prosecute the elusive Kagoda case.

He is one of four senior BoT officials indicted at the Kisutu Resident Magistrate’s Court in Dar es Salaam in connection with the EPA looting scandal. Others are the bank’s former deputy director of the debt department (DDDD), Ms Esther Komu, and two acting company secretaries (lawyers) of the bank, Bosco Ndimbo Kimola and Sophia Joseph Lalika.
 
2009-03-15 14:06:14
Na Salome Kitomary, Moshi

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amesema wahusika halisi wa wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) bado hawajakamatwa na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwakamata wahusika wa kampuni ya Kagoda kwanza kwani ndio waliochota zaidi ya Sh. bilioni 40 mali ya Watanzania.

Mbowe aliyasema hayo jana wakati akiongea na mamia ya wakazi wa Manispaa ya Moshi katika viwanja vya shule ya Msingi Mandaka, wakati wa uzinduzi wa Operesheni Sangara kwa mkoa wa Kilimanjaro itakayodumu kwa siku saba.

Operesheni hiyo ilianza kwa maandamano ya pikipiki, baiskeli na magari katika maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi majira ya saa 6 mchana na kumalizikia katika viwanja hivyo majira ya saa 8 mchana na kufuatiwana hotuba mbalimbali za viongozi waandamizi wa CHADEMA.

Alisema kampuni ya Kagoda imejichotea mabilioni ya fedha lakini hadi sasa wamiliki wake hawafahamiki na hawajachukuliwa hatua yoyote huku wakikingiwa kifua na viongozi mbalimbali wa CCM na serikali na kwamba hadi sasa watuhumiwa wa EPA waliokamatwa ni vidagaa tu.

Mbowe alisema watuhumiwa wa EPA waliopandishwa mahakamani hadi sasa ni kiini macho tu kwani wahusika halisi kama kina Kagoda wameaachwa kana kwamba si wezi na endapo wataendelea kukingiwa kifua ipo siku watawataja hadharani kwani ushahidi wa kutosha wanao.

``Tutahakikisha Rais Kikwete anatueleza wamiliki wa Kagoda na wezi wetu wengine ni kinanani kwani mabilioni ya fedha yamechotwa na hatua hazichukuliwi huku wengine wakijulikana wazi...umaskini wa nchi hii unatokana na viongozi wetu kupenda ubabena kuamini watakaa madarakani milele,`` alisema Mbowe.


Aidha alisema anashangazwa na kauli ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, LutenYusuph Makamba kuwa agenda ya EPA imefungwa na kwamba kamwe haitafungwa mpaka watakapoeleza mmiliki halisi wa Kagoda ni nani na makampuni mengine kama Meremeta,Tangold na Community Import Support na Deep Green .

Alisema kamwe hawataacha kuishutumu serikali ya CCM kwani ndio inalea ufisadi na kuingiza nchi katika mikataba mibovu na wizi wa fedha za umma ambazo zingeweza kuwasaidia wananchi katika afya, maji, elimu na barabara ambazo ni duni sana.

Naye Katibu Mkuu wa CHADEMA Taifa, Dk.Wilbord Slaa aliwashutumu baadhi ya mawaziri na wabunge wa CCM kwa madai ya kuongoza ufisadi ndani ya nchi kwa baadhi kumiliki makampuni ya kitapeli na kujichotea fedha za umma wanavyotaka na kuziweka kwenye akaunti za nje ya nchi.

``Tunamtumia ujumbe Rais Kikwete kuwa raslimali za nchi hii ni mali ya Watanzania wote bila kuwabagua na si CCM pekee na zinapaswa kulindwa vyema na wala hatuombi hisani, wala kumbembeleza yeye ni mtumishi mkuu wa serikali ana wajibu wa kusimamia raslimali zetu na kutuambia wezi wetu ni kina nani,`` alisema Dk. Slaa.


Alisema kamwe hawataacha kupiga kelele hata watishiwe kwani ni wazi kuwa raslimali za nchi hii zinaibwa sana na watu wachache kunufaika huku maelfu ya Watanzania wakiendelea kubaki maskini siku hadi siku nakuahidiwa maisha bora.

Alisema mnamo Agosti Mosi mwaka 2005 majira ya saa 7:45 mchana wakati wa mchakato wa CCM kuteua viongozi wa kuwania nafasi mbalimbali hadi Decemba zilichotwa zaidi ya Sh bilioni 7.5 katika Benki Kuu (BOT) na kupelekwa kwenye benki ya NBC na baada ya nusu saa zilichukuliwa.

Alisema fedha hizo zilipelekwa kwa dola na baadaye kutolewa kama madafu fedha ya Tanzania ambapo kwa mahesabu ya kawaida ni sawa na malori matano ya tani kumi kumi na kwamba si mtanzania wa kawaida anayeweza kuchukua fedha hizo na wahusika wanafahamika lakini wanaendelea kukingiwa kifua bila kufikishwa mahakamani.

Dk. Slaa alisema pia kampuni ya Deep Green nayo ilichota zaidi ya Sh.Bilioni 40 ambazo kwa mahesabu ya haraka zingeweza kuweka maji katika mikoa ya Arusha,Tanga na Kilimanjaro kwa kila kijiji na kata kupata maji ya kutosha.

Alisema kampuni nyingine iliyojichotea fedha kinyemela ni ya Tangold ambayo ilitetewa vikali na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi alilidanganya Bunge kuwa kampuni hiyo ni mali ya serikali ambayo ilifanikiwa kuchota Sh. bilioni 13 fedha za umma kutoka BOT na baada ya kufuatilia hadi kwa Mkurugenzi wa Benki ya Dunia (IMF) alithibitisha kuwa kampuni hiyo ni mali ya mtu binafsi.

Alisema kampuni nyingine ni ile ya Commodity Import Support nayo ni zaidi ya EPA kwani imechota zaidi ya bilioni 500 kutoka BoT na hakuna majibu ya kutosha katika makampuni hayo hewa.

Alisema ni vyema rais akaleta tena wakaguzi wa mahesabu kutoka nje ya nchi ili kuweza kubaini ukweli kwani si EPA pekee yake na kuwa wabunge na mawaziri ambao wana makampuni hewa wanapaswa kuchukuliwa hatua madhubuti.

Operesheni Sangara hiyo inaendelea katika wilaya za Hai, Moshi, Mwanga, Rombo na Same.


SOURCE: Nipashe
 
Mbowe akomalia Kagoda

2009-03-15 14:06:14
Na Salome Kitomary, Moshi

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amesema wahusika halisi wa wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) bado hawajakamatwa na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwakamata wahusika wa kampuni ya Kagoda kwanza kwani ndio waliochota zaidi ya Sh. bilioni 40 mali ya Watanzania.

Alisema fedha hizo zilipelekwa kwa dola na baadaye kutolewa kama madafu fedha ya Tanzania ambapo kwa mahesabu ya kawaida ni sawa na malori matano ya tani kumi kumi na kwamba si mtanzania wa kawaida anayeweza kuchukua fedha hizo na wahusika wanafahamika lakini wanaendelea kukingiwa kifua bila kufikishwa mahakamani.

Dk. Slaa alisema pia kampuni ya Deep Green nayo ilichota zaidi ya Sh.Bilioni 40 ambazo kwa mahesabu ya haraka zingeweza kuweka maji katika mikoa ya Arusha,Tanga na Kilimanjaro kwa kila kijiji na kata kupata maji ya kutosha.

Alisema kampuni nyingine iliyojichotea fedha kinyemela ni ya Tangold ambayo ilitetewa vikali na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi alilidanganya Bunge kuwa kampuni hiyo ni mali ya serikali ambayo ilifanikiwa kuchota Sh. bilioni 13 fedha za umma kutoka BOT na baada ya kufuatilia hadi kwa Mkurugenzi wa Benki ya Dunia (IMF) alithibitisha kuwa kampuni hiyo ni mali ya mtu binafsi.


SOURCE: Nipashe

Hii safi. Kuonesha nini wananchi wangepata, na sasa wanakosa kwa sababu ya haya majangili.
 
Huyu mbowe tatizo lake nikwamba sio mwanasia, sio intellectual, yani kwakweli I fail to see how he can lead a nation. Atakuwa kama JK tuu or worse. We need real opposition lakini naona muelekeo mzuri japokua it will take another 20years or so ila tutakuwa na kitu solid sometime in the not too distant future,ie if the world doesnt end in 2012..lol
 
Huyu mbowe tatizo lake nikwamba sio mwanasia, sio intellectual, yani kwakweli I fail to see how he can lead a nation. Atakuwa kama JK tuu or worse. We need real opposition lakini naona muelekeo mzuri japokua it will take another 20years or so ila tutakuwa na kitu solid sometime in the not too distant future,ie if the world doesnt end in 2012..lol

Kwa nini unadhani Mbowe si mwanasiasa ilihali ni mwana siasa? Kwa nini huyu Mbowe unamfananisha na JK? uoni ni watu wawili tofauti? Malengo yao pia tofauti?
Uoni kwamba JK tangu mwanzo na kwa kweli tangu ule mchakato wa kuchagua rais 1995 alikuwa na hoja ya kufisadi tu? Huwezi kumlinganisha na Mbowe bwana!
 
Kwa nini unadhani Mbowe si mwanasiasa ilihali ni mwana siasa? Kwa nini huyu Mbowe unamfananisha na JK? uoni ni watu wawili tofauti? Malengo yao pia tofauti?
Uoni kwamba JK tangu mwanzo na kwa kweli tangu ule mchakato wa kuchagua rais 1995 alikuwa na hoja ya kufisadi tu? Huwezi kumlinganisha na Mbowe bwana!

Hivi Mbowe amelipa lile deni kwenye mfuko wa pension ya Walalahoi?

Amwachie tu Dr. Slaa aongoze chama vinginevyo huyu CCM wana briefcase yake, siku wakiona anaanza kuwasumbua watafungulia kila mtu aone.
 
Hivi Mbowe amelipa lile deni kwenye mfuko wa pension ya Walalahoi?

Amwachie tu Dr. Slaa aongoze chama vinginevyo huyu CCM wana briefcase yake, siku wakiona anaanza kuwasumbua watafungulia kila mtu aone.

Mkuu mmekaliwa kooni kiasi cha kuanza kupoteza mwelekeo wa Thread kila kitu issue.
 
Huyu mbowe tatizo lake nikwamba sio mwanasia, sio intellectual, yani kwakweli I fail to see how he can lead a nation. Atakuwa kama JK tuu or worse. We need real opposition lakini naona muelekeo mzuri japokua it will take another 20years or so ila tutakuwa na kitu solid sometime in the not too distant future,ie if the world doesnt end in 2012..lol

kinyambiss;

kinyambiss; hapa unatumia nguvu bila maarifa, ni kweli hayo yaliyoijaza nafsi yako yaweza kuwa kweli ila ni lazima tukubali kuwa Mweshiwa Mbowe amejitahidi kuleta dira ya Demekrasia hapa nchini hivyo hatuna budi kumshukuru, tutakuwa wezi wa fadhira kama hatutafanya hivyo.

kinyambiss; mimi huueshimu sana Muda, nadhani ngazi ya juu ya chama wanaelewa wanachokifanya, na sisi tuwe kimya ili siku moja tuone CCM ikitoa kamasi
 
Hivi Mbowe amelipa lile deni kwenye mfuko wa pension ya Walalahoi?

Amwachie tu Dr. Slaa aongoze chama vinginevyo huyu CCM wana briefcase yake, siku wakiona anaanza kuwasumbua watafungulia kila mtu aone.
Mtanzania, ushasema ni deni, kama hajalipa kuna sababu kwa nini hajalipa; hakuiba; that is a difference; he borrowed but others are stealing! Kwani wewe hujwahi kukopa na kushindwa kulipa. Bring something else!
 
Huyu mbowe tatizo lake nikwamba sio mwanasia, sio intellectual, yani kwakweli I fail to see how he can lead a nation. Atakuwa kama JK tuu or worse. We need real opposition lakini naona muelekeo mzuri japokua it will take another 20years or so ila tutakuwa na kitu solid sometime in the not too distant future,ie if the world doesnt end in 2012..lol

We had tried all my friend; the very educated and less educated; I don't understand when you are talking about intellectuals; Mr. Mwinyi ruled this country; and JK is doing it; why you think Mbowe cannot do; from what he is preaching he is better convincing than others; I would better have a CHANGE rather than have the same culprits to rule this country!
 
kinyambiss;

kinyambiss; hapa unatumia nguvu bila maarifa, ni kweli hayo yaliyoijaza nafsi yako yaweza kuwa kweli ila ni lazima tukubali kuwa Mweshiwa Mbowe amejitahidi kuleta dira ya Demekrasia hapa nchini hivyo hatuna budi kumshukuru, tutakuwa wezi wa fadhira kama hatutafanya hivyo.
kinyambiss; mimi huueshimu sana Muda, nadhani ngazi ya juu ya chama wanaelewa wanachokifanya, na sisi tuwe kimya ili siku moja tuone CCM ikitoa kamasi

mwita umesema kweli tupu mkuu, kwakeli Mbowe kajitahidi sana, hasa hasa ukizingatia 'unfair grounds' ambazo siasa za bongo zina endelea ikiwa ni pamoja na limited resources, lakini ameweza kisimamia chama kikaweza himili vishindo na vikumbo vya CCM!

Naamini ni kiongozi mzuri aisee! Kwani katik amazingira haya, kuhakikisha CHADEMA ina simama na kuwa ilivyo sasa, he deserve more...
 
Na Saed Kubenea
MwanaHALISI


MKURUGENZI wa Mashitaka wa Makosa ya Jinai nchini (DPP), Eliezer Feleshi amenukuliwa akisema ameshindwa kufikisha mahakamani wamiliki wa kampuni ya Kagoda Agriculture Limited kwa kuwa hafanyi “kazi kwa shinikizo la wanasiasa.”

Amesema ofisi yake haina ushahidi wa kutosha wa kuwezesha Kagoda kufikishwa mahakamani na kwamba hilo litawezekana iwapo makampuni ya nje yanayodaiwa kuipa kazi Kagoda yatapatikana na kutoa ushahidi.

DPP amesema hawezi kufanya kazi kwa utashi wa kisiasa au wananchi wanavyotaka na kwamba hadi sasa hakuna ushahidi wa kupeleka Kagoda mahakamani.

Alisema atafanya hivyo baada ya kujiridhisha kuwa kuna ushahidi wa kutosha wa kuipeleka Kagoda mahakamani.

Kampuni ya Kagoda ilikwapua zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wiki moja baada ya kusajiliwa.

Kauli ya Feleshi imetolewa ikiwa ni takriban mwaka mmoja tangu Rais Jakaya Kikwete aunde Kamati ya watu watatu kuchunguza wizi katika akaunti ya EPA na miezi mitano baada ya serikali kufikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa.

Kamati ya Rais Kikwete iliongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Johnson Mwanyika na wajumbe wake wengine walikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Edward Hosea na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Saidi Mwema.

Sababu za Feleshi zinaonyesha wazi kuwa ni “mbeleko ya serikali” ya kuibebea Kagoda.

Hoja kwamba DPP hawezi kupeleka Kagoda mahakamani hadi hapo utakapopatikana ushahidi kutoka kwa makampuni ya nje, ni uthibitisho wa kile ambacho wananchi waliona tangu awali, kwamba serikali haina ubavu wa kupeleka Kagoda mahakamani.

Hii ni kwa sababu, katika kesi zote za EPA zilizofunguliwa, hakuna hata mshitakiwa mmoja anayehusishwa na makampuni ya nje ambaye Feleshi anasubiri uthibitisho wake.

Makampuni yote ya nje yanayodaiwa kusaini mikataba ya kuuziana madeni na makampuni ya ndani, hayamo katika kesi zilizofunguliwa na serikali mahakamani.

Kutokana na hali hiyo, kile kinachodaiwa kutafutwa na DPP kwa Kagoda, hakikupewa nafasi kwa makampuni au watu binafsi ambao wameburuzwa mahakamani.

Aidha, Feleshi anajua kuwa hata maodita, kampuni ya Delloite & Toche waliofanya ukaguzi wa hesabu za BoT walishatangaza kwenye vyombo vya habari vya kimataifa kuomba wanaotajwa na Kagoda kuwa waliwapa kazi wajitokeze. Hakuna hata kampuni moja iliyoitikia wito huo.

Si kampuni ya Lindetivs J. Export BV ya Ujerumani wala nyingine yeyote iliyojitokeza. Maodita walithibitishia serikali, pasipo na chembe ya mashaka, kuwa makampuni yaliyotajwa na Kagoda hayapo. Kagoda ilitumia nyaraka za kugushi kujipatia fedha.

Sasa swali ni kwa nini hadi hapo serikali haiwezi kufungua kesi mahakamani dhidi Kagoda kwa kosa la udanganyifu na kujipatia fedha kwa njia ya uwongo?

Je, iwapo makampuni yaliyofanya biashara na Kagoda hayapo na Feleshi anajua kuwa hayawezi kupatikana, kwa nini serikali inaendelea kutumia rasilimali za nchi kwa kuchunguza kitu ambacho hakipo?

Kwa nini Feleshi na wenzake wanadanganya wananchi kwa kusema serikali ina ubavu wa kupeleka mahakamani wamiliki wa Kagoda, wakati ubavu huo haupo?

DPP anasema serikali inachukua tahadhali ili Kagoda isije ikashinda mahakamani na kulazimika kulipwa fidia ya mabilioni ya shilingi kwa kuchafuliwa jina.

Hapa Feleshi amekuwa mpelelezi, mwendesha mashitaka na hakimu. Anataka kusema kuwa ana uhakika serikali itashinda kesi zake zote ilizofungua mahakamani na hivyo haitalipa fidia.

Hili si kweli. Ukweli ni kwamba Feleshi anatumia kisingizio hicho ili kuibeba Kagoda. Ni ukweli usiokuwa na chembe ya mashaka, kwamba ushahidi uliopo kwa Kagoda ndiyo huo huo uliotumika kushitaki makampuni mengine.

Kesi dhidi ya Kagoda haihitaji kuendeshwa na watalaamu kutoka nje. Hakuna asiyefahamu kwamba Kagoda ilitawanya fedha hizo kupitia matawi saba ya Benk ya CRDB jijini Dar es Salaam, na kwamba waliopewa fedha wanajulikana. Hata mahali walipo panafahamika.

Kwamba Kagoda haikuwa na mkataba na makampuni hayo, ni jambo ambalo liko wazi. Kwanza, kwa sababu tayari imethibitika kuwa makampuni hayo hayapo huko yanakotajwa.

Lakini pili, mkataba wa Kagoda una mapungufu mengi ya kisheria ikiwamo usahihishaji uliofanyika ndani ya saa 24, jambo ambalo Kagoda haiwezi kuthibitisha kwamba walisafiri kutoka Tanzania hadi Ujerumani na kurudi nchini kwa muda huo.


Halafu kuna hili la madai ya DPP kukataa kufanya kazi “kwa shinikizo la wanasiasa.”

Ukiangalia kwa makini suala zima la kilichoitwa, “Sakata la EPA,” kazi zote na hatua zote zilichukuliwa baada ya kuwapo shinikizo kutoka kwa wanasiasa, wanaharakati, wananchi na kwa kiwango kikubwa, vyombo vya habari.

Hata mara moja ofisi ya DPP haikuwahi kushinikiza serikali kufanya uchunguzi katika wizi huu. Ni kutokana na shinikizo la wananchi na asasi nyingine za kiraia, Rais Jakaya Kikwete aliunda Kamati ya kuchunguza wizi huu.

Kabla ya wanaharakati kumkalia kooni Kikwete, awali serikali na hata rais mwenyewe alisema, “Fedha za EPA, si za serikali.” Aliingiza hata utani wa “hawa bwana walichomeana utambi.” Tafsiri ya kauli hizo ilikuwa kupoza moto uliokuwa umeanza kuwawakia watuhumiwa.

Hata hivyo, uteuzi wa Feleshi kuwa DPP unafanywa na rais ambaye, katika mazingira ya Tanzania, ni mwanasiasa mkuu anayeongoza chama kilichoko ikulu.

Kutokana na hali hiyo, suala hapa si ushahidi kutokuwapo, kama anavyosema Feleshi, bali serikali haina ubavu wa kupeleka wahusika wa Kagoda mahakamani.

Je, serikali haina andishi la wakili wa Mahakama Kuu, katika kampuni ya mawakili ya Malegesi – Malegesi Law Chambers – ya Dar es Salaam, Bhyidinka Michael Sanze?

Mbona Sanze anasema wazi katika andishi lake kwamba alishuhudia mikataba ya Kagoda ndani ya ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz?

Sanze anasema aliitwa na Malegesi ofisini kwa Rostam Aziz, 50 Milambo. Alipofika aliwakuta Rostam, Peter Noni na Malegesi ambao walimwambia kuwa fedha alizokuwa anashuhudia mikataba yake, zilikuwa zinahitajika kwa ajili ya kugharamia uchaguzi wa mgombea wa CCM mwaka 2005.

Andishi la wakili linaeleza kuwa Rostam Aziz, Peter Noni na Bered Malegesi walimthibitishia Sanze kuwa Rostam alikuwa kwenye kikao ambako rais mstaafu Benjamin Mkapa alitoa maelekezo kwa Gavana Daudi Ballali wa BoT kutoa fedha hizo kwa Rostam kwa ajili ya uchaguzi.


Wakati huo Peter Noni alikuwa Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi katika BoT. Hivi sasa ni Mkurugenzi wa Mipango ya Kimikakati. Ballali alifariki dunia mwaka jana nchini Marekani.

Sanze anasema Malegesi aliishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula kuwa yaliyosemwa na Rostam yalikuwa kweli.

Sasa serikali haina andishi la Sanze? Kama inalo imelifanyia kazi kwa kiasi gani? Je, imewahi kumhoji rais mstaafu Benjamin Mkapa ambaye Sanze anadai kuwa aliambiwa na Rostam kuwa alikuwapo katika kikao kilichopanga mkakati wa kukwapua katika EPA?

Je, DPP anaweza kusema sababu iliyofanya Mkapa asihojiwe? Ni kweli kwamba ushahidi wake haukuhitajika katika kutafuta ukweli juu ya Kagoda, hasa baada ya maodita kujiridhisha kuwa Kagoda ilighushi nyaraka?

Kwa nini Kamati ya Rais haikumuhoji aliyekuwa katibu mkuu wa zamani wa CCM, Phliph Mangula? Ilimwogopa! Au serikali ilidharau maelezo ya Sanze?

Serikali haina andishi la Ballali lenye kufichua kila kitu juu ya ukwapuajia huo na jinsi baadhi ya vigogo walivyoshiriki katika mchezo huo? Kama haina, Feleshi alichukua jukumu gani kuhakikisha Ballali anahojiwa?


Wananchi wanajua mamlaka na madaraka aliyonayo DDP. Lakini inavyoonekana katika hili la Kagoda, DPP ameamua kulimaliza kwa usemi wa Kiswahili, “funika kombe mwanaharamu apite.” Kuna haja ya kufunua kombe ili mwanaharamu aadabishwe.

Kinacholeta faraja ni kwamba wananchi wanaelewa nini kilifanyika na nini kinaendelea kufanyika. Wanajua kupembua, nini mazingaombwe na nini halisi.

Kama Rais Kikwete hajaamua wana-Kagoda kukamatwa, basi na Feleshi anaendelea kuwa likizo. Lakini basi asiendelee kutoa kauli za hadaa hata mahali palipo wazi.

Kagoda haishitakiwi wala kushitakika kwa kuwa inalindwa na wanaoifahamu kampuni na wanaowafahamu walioiunda. Wanawalinda. Feleshi ni kufuli tu.
 
Ashakum si matusi lakini this guy is chatting shit.. Samahanini sana.. Inamaana makampuni ya nje ambayo yalitransfer madeni yao kwa Johnson and all ther rest of waiba peanuts na kina Jetu wametoa ushahidi? Kwanini Kagoda is special!!?! Huu ni ujinga CCM wameiba hela wakazitupa kwenye uchaguzi wao sasa wananmchi wanaambiwa hamna ushahidi? Jamani..
 
Back
Top Bottom