Kagera, Ngara: Shule ya Keza yataka kufungwa kwa kukosa vyoo. Ilijengwa 1945

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,818
11,993
Shule ya Singi Keza Wilayani Ngara, hatihati kufungwa kwa Ukosefu wa Vyoo unaopelekea mazingira ya shule kuwa Magumu Kufundisha na kujifunzia.

Mbunge wa Jimbo la Ngara Ndaisaba George Ruhoro, ametoa Mil 3 kutengeneza vyoo vya dharura ili Shule isifungwe. Ruhoro amesema shule ni ya miaka mingi kwani imejengwa kipindi cha vita ya pili ya Dunia hivyo imechoka inahitaji ukarabati mkubwa sio wa vyoo tu.




==========
KAGERA: SHULE YA MSINGI HAINA VYOO
Wanafunzi na Walimu wa Shule ya Msingi Keza iliyopo Wilayani Ngara wapo kwenye hatari ya kupata magonjwa kutokana na uhaba wa huduma hizo.

Baada ya kipande cha video kusambaa mitandaoni ikiwaonesha Wanafunzi na Walimu wakilalamikia hali ya shule hiyo, Mbunge wa Jimbo la Ngara, Ndaisaba George Ruhoro amesema “Nilifika shuleni nikatoa Tsh. Milioni 3 ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo ambayo ilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya dharura na Ths. Milioni 15 ya vyanzo vya ndani vya Halmashauri.”

Ameongeza kuwa tayari ujenzi unaendelea na kuongeza “Shule ya Keza ilijengwa Mwaka 1945 wakati wa Vita vya Dunia, miundombinu inatakiwa kufanyiwa maboresho.”
 
Fedha za uviko na tozo ; tulijenga vyoo na madarasa.

Vyoo vyenyewe ndio kama hivyo.
 
Yaani hii nchi vipaumbele vya serikali havipo sawa.

Kujenga hivyo vyoo na kutoa million 5 Kwa goli kipi cha maana?

Halafu majinga yanashangilia eti Mama anaupiga mwingi Mara ooh kazi iendelee.

Kazi gani sasa, upumbavu mtupu
 
Shule za Wazungu

Wakija watetezi wa haya mambo ya choo, Watadai oh hatujui kujenga vyoo... oh ..vina uhatarishi na afya n.k ....wakati wanasahau hiyo teknolojia walileta wazungu.... Leo hii wanavikana, ati wamesahau vyoo vyao vya kuchutama.


Nyakati hizo 19 kweusi unadungua misituni, maisha yanaendelea(as part of the ecosystem) bila shuruti na Wasomi walikuwa kede-kede....


Leo hii huko katika nchi zinazodaiwa kuendelea, wanachota mavi na kuyarudisha mashambani! Reverse engineering! na bado watadai hakuna cha kuigiza huku

....cha kushangaza lakini, shule hiyo ipo kwenye eneo lililozalisha Madaktari wa kila aina ya Taaluma! Ila choo kalas!
 
Nchi yetu mambo mengine ya kijinga, wazazi nao inatakiwa wawajibike....kama unaona mwanao anasoma kwenye mazingira ya hatari na kuna kuanzia Kijiji,kata,tarafa mpaka wilaya lakini watu wanataka kila kitu Serikali ifanye, watoto ni wenu,wanapata magonjwa wao........Tz tunapenda michango ya kula kula tu kama Harusi ila kila kitu tunataka Serikali ifanye........
 
Nchi yetu mambo mengine ya kijinga, wazazi nao inatakiwa wawajibike....kama unaona mwanao anasoma kwenye mazingira ya hatari na kuna kuanzia Kijiji,kata,tarafa mpaka wilaya lakini watu wanataka kila kitu Serikali ifanye, watoto ni wenu,wanapata magonjwa wao........Tz tunapenda michango ya kula kula tu kama Harusi ila kila kitu tunataka Serikali ifanye........
Umesahau ile wazazi waliyomuita fundi maiko akatengeneza vyoo km 6 hivi vimefuatana Ila baadae wakabaini kwa jinsi vilivyojengwa watoto wakiingia wengi basi wote watazama ndio Serikali ikaingilia kati, nimesahau mkoa gani Ila wananchi wanajitoa, lindi wanafunzi hawana madarasa wazazi wamejenga madarasa ya miti watoto wasome pia walikua hawana kituo cha wamama kujifungua wakajenga cha miti

Ushaelewa au bado? Serikali inatajwa maana inakusanya KODI kutoka kwa hao hao wananchi alafu unawaambia wananchi washughulike wenyewe Kodi yao inaenda wapi?
 
Umesahau ile wazazi waliyomuita fundi maiko akatengeneza vyoo km 6 hivi vimefuatana Ila baadae wakabaini kwa jinsi vilivyojengwa watoto wakiingia wengi basi wote watazama ndio Serikali ikaingilia kati, nimesahau mkoa gani Ila wananchi wanajitoa, lindi wanafunzi hawana madarasa wazazi wamejenga madarasa ya miti watoto wasome pia walikua hawana kituo cha wamama kujifungua wakajenga cha miti

Ushaelewa au bado? Serikali inatajwa maana inakusanya KODI kutoka kwa hao hao wananchi alafu unawaambia wananchi washughulike wenyewe Kodi yao inaenda wapi?
Kama kujenga vyoo wameshindwa acha wafunge shule tu Kwa upuuzi huo
 
Shule ya Singi Keza Wilayani Ngara, hatihati kufungwa kwa Ukosefu wa Vyoo unaopelekea mazingira ya shule kuwa Magumu Kufundisha na kujifunzia.

Mbunge wa Jimbo la Ngara Ndaisaba George Ruhoro, ametoa Mil 3 kutengeneza vyoo vya dharura ili Shule isifungwe. Ruhoro amesema shule ni ya miaka mingi kwani imejengwa kipindi cha vita ya pili ya Dunia hivyo imechoka inahitaji ukarabati mkubwa sio wa vyoo tu.

KAGERA: SHULE YA MSINGI HAINA VYOO
Wanafunzi na Walimu wa Shule ya Msingi Keza iliyopo Wilayani Ngara wapo kwenye hatari ya kupata magonjwa kutokana na uhaba wa huduma hizo.

Baada ya kipande cha video kusambaa mitandaoni ikiwaonesha Wanafunzi na Walimu wakilalamikia hali ya shule hiyo, Mbunge wa Jimbo la Ngara, Ndaisaba George Ruhoro amesema “Nilifika shuleni nikatoa Tsh. Milioni 3 ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo ambayo ilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya dharura na Ths. Milioni 15 ya vyanzo vya ndani vya Halmashauri.”

Ameongeza kuwa tayari ujenzi unaendelea na kuongeza “Shule ya Keza ilijengwa Mwaka 1945 wakati wa Vita vya Dunia, miundombinu inatakiwa kufanyiwa maboresho.”
Wazazi wa keza wanasubiri kujengewa vyoo vya Shule ya msingi
 
Back
Top Bottom