Mbunge Ndaisaba Afunguka Mazito: Miaka 3 ya Rais Samia Ilivyoibadilisha Ngara

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,897
941

MBUNGE NDAISABA AFUNGUKA MAZITO: MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA ILIVYOIBADILISHA NGARA

"Niwaombe wananchi wa Mumilamila kwa Umoja wenu endeleeni kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, endeleeni kumuunga mkono Mbunge Ndaisaba George Ruhoro. Hakika mengi tumeyafanya. Maendeleo ni hatua, hatua moja huanzisha hatua nyingine" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kipenzi cha watanzania amefikisha miaka mitatu tangu aingie madarakani. Wananchi wa Jimbo la Ngara wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Ngara, Ndaisaba George Ruhoro tumeazimia kumpa kura nyingi mwaka 2025, ametufanyia mambo makubwa sisi Wananchi wa Ngara" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara

"Rais Samia ametoa Shilingi Bilioni 100 kwaajili ya ujenzi wa barabara ya lami kutoka Nyakahora mpaka Rusumo katika Jimbo la Ngara, mradi huu umeanza kujengwa na Mkandarasi yupo Site. Ni Mama yetu, kipenzi cha Watanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara

"Rais Samia ametoa zaidi ya Shilingi Bilioni 11 katika kipindi cha miaka mitatu hapa Ngara kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya umeme. Umeme uko unakuja, Mkandarasi yuko site, nguzo zinaendelea kusogea, anatakiwa alete nyaya afunge transformer awashe umeme. Mpaka kufikia mwaka 2025 umeme utakuwa umewaka hapa Mumilamila" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara

"Rais Samia katika kipindi cha miaka mitatu ametoa zaidi ya Shilingi Bilioni 8 kwaajili ya ujenzi wa miradi ya Maji mpaka mradi wa Maji wa Bugarama ni sehemu ya fedha alizotoa Rais. Mradi umejengwa, umekamilika na unatoa Maji" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara

"Mama Samia nilimkimbilia, nikasema watu wa Bushubi, Bugarama, Kihinga na Mumilamila wanapoenda hospitali ya Wilaya wanateseka sana wengine wanafia njiani kwasababu ya umbali mrefu wa kusafiri zaidi ya Kilomita 70. Rais Samia amenipa Bilioni 2 katika ya Bilioni 3 alizoahidi kutoa na Hospitali ya Wilaya inaendelea kujengwa Mbuba" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara

"Barabara ya kutoka Bugarama mpaka Kabanga Nickel (Km 7.9) imetengewa Shilingi Milioni 8.98. Barabara ya kutoka Lunyana - Kihinga - Nyarukubala - Nyarulama imetengewa Shilingi Milioni 27.28. Barabara ya Nyarulama Sokoni - Mukivumu - Mumilamila Centre imetengewa Shilingi Milioni 27.9 kwaajili ya matengenezo" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara
 
Maskini Ngara.

kwa kuwa umeamua kusifia kana kwamba hizo pesa zinatoka mfukoni mwa mtu, basi tueleze pia nani alitoa kiasi gani kujenga barabara ya lami kuelekea nyumbani kwake?

Pia atueleze kuhusu kilichiotokea wakati wa ziara ya mkti wa wazazi (T) ktkt eneo inapojengwa hiyo hospitali ya wilaya hadi waandishi kuzuiwa kuripoti taarifa hiyo.

Pia ukiandika kwa hadhira pan epuka ubaguzi. Kwanini utumie Bugufi huku ikitaja maeneo ya Bugarama n.k huo ni ukaburu
 
Mbona kutoka nyakahora mpaka Rusumo Kuna Lami muda mrefu?. Au anaongelea kuipanua hiyo Barbara?
 
Maskini Ngara.

kwa kuwa umeamua kusifia kana kwamba hizo pesa zinatoka mfukoni mwa mtu, basi tueleze pia nani alitoa kiasi gani kujenga barabara ya lami kuelekea nyumbani kwake?

Pia atueleze kuhusu kilichiotokea wakati wa ziara ya mkti wa wazazi (T) ktkt eneo inapojengwa hiyo hospitali ya wilaya hadi waandishi kuzuiwa kuripoti taarifa hiyo.

Pia ukiandika kwa hadhira pan epuka ubaguzi. Kwanini utumie Bugufi huku ikitaja maeneo ya Bugarama n.k huo ni ukaburu
Maendeleo ni hatua. Mbunge Ndaisaba George Ruhoro anafanya kwa sehemu kutokana na bajeti anayopewa Serikalini. Muwage wavumilivu, siyo kukosoa kila Kiongozi anachoongea. In advance asanteni kwa maoni
 
Maendeleo ni hatua. Mbunge Ndaisaba George Ruhoro anafanya kwa sehemu kutokana na bajeti anayopewa Serikalini. Muwage wavumilivu, siyo kukosoa kila Kiongozi anachoongea. In advance asanteni kwa maoni
Tuwe wavumilivu na kuacha Kukosoa?
Hivi mara ya mwisho ulifika lini Ngara? Katika mchango wangu nilitaja vitu mahusus ambavyo umeamua kuvikwepa na kuja na hoja ya uvumilivu.

Kama suala ni uvumilivu kwanini huyo mbunge hakumvumilia mbunge aliyekuwepo?

Na tueleze wakatii wa kampeni alitumia lugha gani kama sio kukosoa. Au ndio Story za Nyani...

Mfikishie ujumbe kuwa huku hali sio kama anavyokudanganya kuwa alimwomba mama... mama amenipa kana kwamba ni mali ya familia.

Kuna wananchi wa Bugarama walipaswa kulipwa fidia tangu sept mwaka jana lakini hadi sasa hawajalipwa ilihali hawatakiwi kufanya chochote kwenye ardhi yao.

Hali kama hiyo iko eneo la Rusumo ambako walioathiriwa na ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme, hawajafidiwa kwa zaidi ya miaka 2 na hawatakiwi kufanya chochote kwenye ardhi yao wakisubiri fidia.
Muulize huyo unayemsifia, kwanini umeme wa Rusumo unapelekwa kwanza kigoma na kuwa eti baadaye utafanyika mradi wa kujenga line ya kuurudisha Ngara ambako umeme hukatika zaidi ya mara 10 kwa siku au wakati mwingine ukiwaka kama kibatari.
 
Back
Top Bottom