Kagame tells Kikwete "I will hit you......"

Kagame tells Kikwete "I will hit you......"

Status
Not open for further replies.
Kauli yake inanitisha kwa usalama wa Rais wetu na nchi yetu, tuna wanyarwanda wengi sana Tanzania, Zunguka Biharamulo, Ngara, Karagwe hata Chato. Sasa isije ikawa anapanga kum Hit kwa kumdhuru hata pale atakapokuwa amekwenda sehemu hizo kwa kazi za kiserikali, kagame naweza kuwatumia watu wake kumdhuru Rais wetu, Baya zaidi anawalisha Vijana wadogo sumu, hasa pale anaposema hatumuwezi kwa Anga, kwa majini hata kwa ardhini, anajivunia nini mpaka aseme hivyo?, Hebu sasa kama inawezekana hawa Raia wa Rwanda waliopo Tanzania wasakwe popote walipo na warudishwe kwao kwa usalama wa nchi yetu na rais wetu.
 
kwanza kaonyesha ujinga wake kwa kufanya kazi kama MVIZIAJI, kama mwanaume afunge mkanda akaze buti then cros Kigoma,
longolongo et oooh right time, mwehu. alaf anaongea na vijana wa rwanda. anawafundisha woga.
 
kwa hali ya kawaid tuu Kagame ni mgonjwa kabisa mtu timamu hawezi kuongea maneno kama hayo kwa mtu aliye mpa ushauri wa kutatua mgogoro alio nao.Hawezi kumtuka na Rais namna hii wakati RAIS alimpa ushauri mzuri tuu.

kagame ni mgonjwa maana yeye hatuna mgogoro nae hata kidogo maana kama ni matusi angayatoa yule mama wa Malawi amabaye tuna mgogoro nae wa ardhi, hivi jeuri hii huyu anaipata wapi kumtukana Rais wetu kiasi hiki?

Nawaone huruma sana Wanyarwnda kwa kuwa na Rais wa namna hii ambaye hana busara wala utashi, na ni wazi kuna watu au nchi zinampa kiburi huyu Kagame si bure.

Kagame anajua fika jumuiya za Kimataifa haziwezi kuruhusu rwanda kuingia kwenye vita au machafuko ndio maana anapata kichwa namna hii na kumtukana Rais wetu.

Vita haviwezi kuwa suluhu kama wengine wanavyo fikiri maana kuna marais ni vichwa vibovu kama kagame wengi sana humu duniani lakini kinacho angaliwa ni athari kwa watu wasio na hatia maana yeye Kagame atajificha na wananchi ndio wata teseka kwaajili ya huyu mgonjwa.

Kagame ni anastahili adhabu ya kupuuzwa ni mgonjwa. hatuwezi kuingia vitani na kugharimu wanyarwanda kwaajili ya huyu Kagame ni wazi amachanganyikiwa na apuuzwe.
Wala ofisi ya Rais isipoteze muda kutupiana maneno na huyu.
 
Nadhani hayo maneno siyo ya kagame kuna wahuni ambao wameyaweka, km ni ya kagame naona umefika muda muafaka wa kumuondoa madarakani kama tulivyomuondoa idi amin

Hii ni dalili ya overfeeding!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Kwanini bwana Kagame amekasirika sana kwa kauli rahisi ya JK yenye maneno ya kuleta ubinadamu? Hii spirit aliyonayo Kagame ya ugomvi, vita kukataa maridhiano ni hatari sana. Watu wenye kiongozi kama huyu hawafai kuwa na ushirika nao hata kidogo. Unabidi tujitoe kabisa hata kwenye EAC maana majirani zetu wote ndo wa namna hii hii.
 
Natamani sana maneno yake yatimie...atakuwa ametusaidia sana kama Taifa!!
Kikwete ni mzururaji na ni muhuni, huo ushauri anaojifanya kuwapatia wengine kwa nini hautekelezi nyumbani kwake???
Kiherehere tu kinamsumbua na ninaomba kwa moyo wangu wote Kagame na wenzake watekeleze maneno yao again ninaamini watakuwa wametusaidia kama Taifa.
 
Natamani sana maneno yake yatimie...atakuwa ametusaidia sana kama Taifa!!
Kikwete ni mzururaji na ni muhuni, huo ushauri anaojifanya kuwapatia wengine kwa nini hautekelezi nyumbani kwake???
Kiherehere tu kinamsumbua na ninaomba kwa moyo wangu wote Kagame na wenzake watekeleze maneno yao again ninaamini watakuwa wametusaidia kama Taifa.

Wewe ndio utakuwa wa kwanza kupelekwa mstari wa mbele kupigana dhidi ya majeshi ya Kagame!JIANDAE!
 
Ni upuuzi sana kuendelea kuendekeza kauli za .Kipumbavu. za huyu jamaa! Anaidhalilisha sana ofisi ya rais na kimsingi lazima tuoneshe kutokukubaliana nae kwa maneno na vitendo!
Anamdhalilisha kikwete na familia yake basi.
 
Siku zote ukiona mtu mzima anaongea upumbavu mbele ya media au watu dhidi ya kiongozi mwenzake ujue ana matatizo.

Rwanda ni kama sisimizi kwetu, kama anazungumzia vita Tanzania inaweza kuichukua rwanda na kuifanya wilaya kama biharamulo tu.

This idiot must be stopped now.

Kagame ni muuaji na --------, huwezi kukataa kumaliza matatizo na adui yako hata uwe nani labda tu uamini kuwa unaweza kuwaua wote ubaki peke yako. Leo tunaona marekani yenye uwezo wa kuwamaliza kabisa Taleban imekubali kukaa chini na kuongea nao sembuse Rwanda na interahamwe ambao ni wahutu na Rwanda ni nchi yao?
Kagame anarefer ku-mhit "mtu"wala sio Tanzania.
kagame wala hana kinyongo na TZ
He very well know the kind of mediocre we call our "President"
 
Haka kajamaa naona ni kagonjwa, inabidi kaondelewe madarakani...
 
Kwani tatizo ni nini hapa? Sipendi uongozi wa Jakaya kwa vipindi vyote akiwa madarakani kama Rais wa Tanzania. lakini, kutukanwa na kanchi kadogo kama Rwanda is disgusting!! Kisa Jakaya ametaka peace talks and negotiations kwa nchi zile zilizo katika vita ndani ya maziwa makuu.

Jeuri ya kagame ya kupigana vita vya mstuni, anataka kutuletea sie? Hii haikubaliki hata kidogo...


Japo ukubwa wa nchi sio uwezo wa kijeshi lakini hata mimi nimekerwa na maneno anayozungumza huyu bwana. It is so disrespectful .....nadhani angekua Mkapa vitu vingekua tofauti kidogo. Hakuna sababu ya kuwa mnyonge kwa kitu unachokiamini. Nilitegemea Kikwete arudie tena maneno yake bila kumungúnya kwamba....inabidi Kagame akae na azungumzie tofauti zake na FDLR bila kupoteza maisha zaidi ya yaliyopotea. Kama Mandela angekua na akili kama yake tusingekua na wazungu South Africa ....huyu mtu ni janga kwa nchi za maziwa makuu.
 
i recall when general Amin Dada insulted mwl Nyerere he was approaching his downfall. i predict Kagame's downfall. mfamaji haishi kutapatapa.
 
I have a feeling there is more to this story. Inawezekana Kagame amemshtukia JK ni msanii(anang'ata na kupuliza) ili aonekane mzuri kwa Kagame na vilevile mzuri kwa waasi. Kagame ni straight talker; na hapa anaonyesha jinsi alivyona msimamo kwenye kile anachokisimamia (whether he is right or wrong). JK sidhani kama anamsimamo kwenye kitu chochote; yeye anaangalia tu upepo. Soon tutasikia amebadilisha mwelekeo. Nafikiri huu ugomvi ni wa JK na Kagame; and not Tanzania na Rwanda. Hata kama Rwanda ni ndogo tusiingie kichwa kichwa kama nchi wakati hatujui who are the people/power behind Kagame. Tukubali tu nchi yetu haina leadership. Uongozi huu unategemea na upepo unaelekea wapi na wakati gani. Wacha wachapane/waviziane wenyewe, atakayepigwa atapata akili. Inawezekana kabisa JK amepeleka usanii kwenye mambo sensitive akidhani yatapita kama anavyochezea watanzania. There must be more to this story that we do not know.

tanzania tuna jeshi nzuri na vifaa vya kutosha, lakini ushauri Aliopewa kagame ni muzuri sana ni vyema kukaa chini na kuyamaliza na madui zetu,wala watanzania wasipate shoku juu ya hili tuko imara.
 
People of Africa we have to remenber that,
We're one nation, one people
and from the same place and
uterus so why to battle
so why to threaten and feel
so powerful after
the struggles empowering from
whereelse,
not to go apposite direction
of the ground of peace that our
creator happilly gave us.

WHY TO BATTLE OURSELVES THAT SHOULD BE THE TOPIC WE MUST
ASK EACH OTHER AS AFRICANS PEOPLE.
 
Kagame anarefer ku-mhit "mtu"wala sio Tanzania.
kagame wala hana kinyongo na TZ
He very well know the kind of mediocre we call our "President"

hakuna tofauti kati ya tanzania na kikwete inapokuja kwenye maswala haya.
 
if its true this is totally disrespectful, what is Kagame boast with to insult us?

Kagame hajatutukana sisi mkuu, amemkutakana KIKWETE...au wewe ndiye KIKWETE? Na hii intokana na rais wako kusoma kila ambacho kimeandikwa kwenye hotuba, HACHANGANYI NA ZAKE KWENYE ZA KUAMBIWA....!!!
 
oi huyu atakuwa hajui watu wanavyopigwa mabomu ya tumbo na kung'olewa kucha bila ganzi kwa koleo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom